Chuo kipya cha NELSON MANDELA

Bluray,

..watetezi wa hoja kwamba chuo hicho kijengwe ktk mikoa ya pembezoni wanaamini kwamba kitatoa fursa za kiuchumi kwa wananchi wa maeneo hayo.

..vilevile wanaamini kwamba kujengwa kwa chuo ktk maeneo hayo kutalazimisha kujengwa kwa supporting infrastructures kama hospitali,shule,barabara,uwanja wa ndege etc.

..wengine pia wanaamini wananchi wa sehemu hizo ambazo tunasema "zimesahauliwa" watajisikia "vizuri" and part of a "larger Tanzanian-family" kwa mradi kama huo kupelekwa karibu na maeneo yao. wanadai hii itajenga umoja wa kitaifa.

..nakubaliana na approach yako kuhusu suala hili, but sometimes it is hard not to empathise na wananchi wa hii mikoa ya pembezoni.

..wasiwasi wangu ni kwamba unaweza kujenga chuo hicho huko pembezoni halafu wananchi wa maeneo ya karibu wakabaki kuwa watazamaji tu wakati wanaosoma hapo ni vijana toka maeneo ya mbali.

NB:

..leo hii ukiwapa wananchi wa Kigoma/Lindi/Mtwara/Tabora hayo mabilioni yaliyopangwa kujenga chuo cha Mandela watumie kwa ajili ya elimu, je watatumia pesa hizo kujenga shule za sekondari kadhaa au kujenga chuo kikuu kimoja?

Inabidi tuwe na "from the ground up approach", badala ya top down approach.Inabidi miradi na huduma ziende kwenye proven demand, siyo ku speculate kuwa tutapata demand. Haya mambo ya top down ni part and parcel ya command system, vijiji vya ujamaa, ma hudro electric project makubwa ambayo tunakuwa bilked "Confesion of An Economic Hitman" style.

Tengeneza mazingira ya wananchi kuwa na proven demand ya chuo, kwa kuanzisha shule za sekondari nyingi, then ukiwa na demand, au hata projection nzuri ya demand, unajenga chuo.Sio unajenga chuo kikuu sehemu inayohitaji shule za msingi na sekondari.
 
Ni pale ilipokuwa Arusha Tech? Maana hata mbeya tech kimekuwa chuo kikuu. Na nia ni kuendeleza pale walipokuwa.Kwangu mimini habari njema

Mkuu Ndahani kwa ufahamu wangu Chuo Kikuu cha Mandela kinajengwa Tengeru nje kidogo ya mji wa Arusha,kinachukua ardhi na miundombinu yote ya CARMATEC.

Sina hakika sana lakini nadhani masharti ya kujenga chuo kikuu cha Nelson Mandela ilikuwa ni pamoja na kuwa na miundombinu iliyo tayari na ndiyo sababu kubwa iliyoifanya serekali kukubali miundombino yote ya CARMATEC ichukuliwe na Mandela University.

CARMATEC wamepewa kilipokuwa kiwanda cha pareto kinachotazamana na kilichokuwa kiwanda cha kutengeneza magurudumu [General Tyre ea Ltd].

Haya mambo ya Pemba na Kigoma sidhani kama yana nafasi hasa hili suala la kuwa na miundombinu iliyotayari.
 
Ndiyo mkuu,wangelifanya utaratibu kijengwe pengine-kila kitu Arusha?
Naomba utupe details za hicho chuo kinatoa kozi zipi?
 
Tumefanikiwa kupata nafasi ili chuo hiki kiwe Tanzania. Lakini for some unknown reasons WATAWALA na washauri wao wameamua kiwe ARUSHA!

Swali kwa nini kisijengwe Pemba hiki chuo ?..if not KIGOMA for that matter?

Ni taarifa njema lakini inaonekana baadhi ya wachangiaji ni wabaguzi sana. Kijengwe wapi kama imeamuliwa na watawala si hoja, tufarijike kwamba Watanzania watapata chuo cha uhandisi kitakachozalisha wataalamu wengi watakaosaidia katika kubuni vitu mbalimbali na kuharakisha maendeleo ya Tanzania. Ikumbukwe Tanzania ina uhaba wa Wahandishi. Tusiwe jamii ya walalamaji.
 
Tumefanikiwa kupata nafasi ili chuo hiki kiwe Tanzania. Lakini for some unknown reasons WATAWALA na washauri wao wameamua kiwe ARUSHA!<br />
<br />
Swali kwa nini kisijengemba hiki chuo ?..if not KIGOMA for that matter?
<br />
<br />
akili yako finyu sana. Chuo ni kimoja, mikoa ni zaidi ya 20, ulitaka iwaje? Tugawe madarasa?
 
Ni pale ilipokuwa Arusha Tech? Maana hata mbeya tech kimekuwa chuo kikuu. Na nia ni kuendeleza pale walipokuwa.Kwangu mimini habari njema
HAPANA. kipo njia ya chini, kupitia usa river, ilikokuwa CARMATEC. KIZURI SANA HIKO CHUO.
 
mi naona niwape mji nashukuru kwa ubishi wenu nimepata kuelewa vivutio mbalimbali vya mikoa nimekuwa mtalii ghafla! dodoma hawajasema ngoja niwasemee. kijengwe dodoma kwanza ni katikati kuna zabibu mibuyu inayoleta mvuto mzuri wa mji. kuna uzoefu wa vyuo vingi kwa sasa vyenye watu wengi. serikali hupanga mambo yake hapa. uchumi wetu na pato la mkoa lipo chini tunaupita mkoa mmoja hivyo wakileta hiki chuo kinaweza kuleta mabadiliko bila kusahau tupo karibu na dar ukilinganisha na kigoma. jamani watani zangu si mjitokeze na nyie mn'gan'ganie nyie vipi?
 
Ni pale ilipokuwa Arusha Tech? Maana hata mbeya tech kimekuwa chuo kikuu. Na nia ni kuendeleza pale walipokuwa.Kwangu mimini habari njema

Nope, ni eneo iliyokuwa zamani taasisi ya zana za kilimo (carmatec), nje kidogo ya usa river (old moshi-arusha road)
 
ni moja kati ya vyo vya Engineering vi3 vitakavyojengwa Africa.
Sio vitakavyojengwa,kimeshajengwa already,kwenye eneo lililokua carmatec zamani,kiko kwenye final finishing touches na walimu wameshaanza ajiriwa,kitasave south countries of Africa.
 
Back
Top Bottom