Chuo Kikuu (UDSM) Kufunguliwa na Masharti mapya!

Hii ni sawa na kufagia taka na kuzifunika chini ya zulia. Lakini wahenga walisema "Kuvunjika kwa Koleo sio mwisho wa uhunzi".
 
Hii imekaa vizuri na inatia moyo kuona kuna baadhi ya viongozi wanakuwa na mtizamo tofauti na sera zilizowekwa ambazo zinaonyesha wazi kuwabagua watu.

Sulihisho la hili tatizo ni kuwa na kigezo kimoja tu cha kupata mkopo na sio huu utaratibu wa kuwa na asilimia 100,80,60... hii ni uzushi wa wazi kabisa kwani kwa nchi kama TZ hauwezi kupima kipato halisi cha mtu na mtu anaweza kujaza hizo form kwa namna yeyote ile. Pili kwani hata hao wenye uwezo sio kwamba wazazi wao wameokota tu hizo pesa .. wamezinfanyia kazi so nao pia hauwezi kusema serikali iwatenge.
Suluhisho ni moja tu.. kuweka grade... yeyote atakayepata division I ukipata hiyo basi unapata mkopo asilimia 100 bila kujali unatoka familia masikini ama tajiri. Hiyo ndio njia ya kuondoa ubishi wote huu.

Mwisho najiuliza serikali ni nani??? mbona huyu jamaa kiongozi mkubwa bungeni akiwa kama mwenyekiti wa kamati na yeye anasema serikali iwe makini... nilitarajia angetoa kauli yake akiwa yeye kama hiyo serikali... hii inasikitisha kuona kwamba hata hao viongozi nao wenyewe wanajiona sio serikali sasa serikali ni nani..????
 
Ni kosa kubwa kwa mkusanyiko mkubwa wa wanafunzi pale UDSM kutokuwa na chombo chao kinachowaongoza katika mambo mbali mbali ndani na nje ya chuo hicho. Wanafunzi wanaweza kabisa kuunda DARUSO yao ya chini meza na kutaarifiana mambo mbali mbali kuhusiana na yale yanayowapa karaha mbali mbali katika muda ambapo wapo pale kama wanafunzi.


Kweli kabisa. Inatia huzuni na ni ngumu kuamini kuwa Profesa wa mambo ya Siasa na Demokrasia anaweza kupitisha maamuzi kama haya. Potelea mbali vijana nao wanakosea wakati mwingine. Hebu jamani tafuteni chanzo, siyo DARUSO, ni sera ya uchangiaji, jadilini na amueni. Kuifuta DARUSO ni kama kufunika bomu tu, litalipuka siku moja. You cant stop people from organizing and mobilizing themselves. Tujifunze kwa wale wazee wa Afrika Mashariki, walijilaza tena pale Selender bridge mbele ya kituo cha polisi, itakuwa hao vijana.

Hawa wanaopata percent ya ada ya mkopo adha yake mnaijua lakini? Kila siku wadogo zetu wanatulilia shida. Jambo hili limechangia wengine kuwa wezi, na hata wengine changudoa mradi tu wapate ada iliyobaki wasome.

Wasomi wote mliopo humu ndani, tunawasidiaje hawa vijana?
 
.....kuzuia migomo/lawama kama hizi naona serikali itoe 100% ya loan kwa wanafunzi wote watakaofanikiwa kupata hizo sponsorship ,lakini disadvantage yake ni kukata idadi ya wanafunzi,na waweke category mbili za full/partial sponsorship(loan),nina uhakika kuna wengi tuu watakuwa more than happy kuchukua hiyo half na nyingine kusaidiwa na familia zao/kazini/mikopo ya bank etc,tukubali ile nchi nayo njaa kali na serikali haiwezi kusomesha kila mtu na lazima tuwe na njia nyingine za kusaidia la sivyo migomo na kufukuzwa itakuwa order of the day!
 
Serikali wasomeshe watu bure harafu wafute hiyo DARUSO.
Tanzania ni masikini acheni matusi hapa,kitendo cha mzee wangu kule kwenda kufua na kuoga kule motoni ni kielelezo tosha hata basic needs zake hawezi tosheleza.

Acheni propagada hapa eti anatumia pesa vibaya wanazitowa wapi hizo fedha za kutumia vibaya kama NESI analipwa elfu 70 kwa mwezi kwa mwaka anakuwa na laki 8 na unamtaka mtu huyu alipe laki 5 kwa mwaka atazitowa wapi na mda wote yupo kazini?

Tena huyu Nesi kwa Tz eti ndiye anaishi maisha yale STD,Acheni matusi kabisa Tanzania ni masikini acheni matusi kabisa.
Kama serikali yenyewe imefanya ile ada ya shule za msingi bure eti kwa kigezo kuna watoto wanashindwa pata ile ada je? unategemea huyu mtoto ataipata hii ya chuo?

Anatumia fedha vibaya wapi kwa ile chupa ya gongo ya USD 0.015 na kiasi hicho cha fedha kulewesha watu 10 hiyo ndiyo matumiza mabaya?

Hivi wewe ulishawahi kuona mtu amevaa nguo ambayo imepigwa viraka hadi nguo inapoteza rangi yake kutokana na kuwa viraka ni seheemu kubwa kuliko nguo original?

Hayo matumizi mabaya ya fedha ,hizo fedha wanazipata kwa kilimo cha mkono? ama uvuvi wa kutumia kasia?

Hakuna NESI hospitali serikali analipwa 70,000 p.m angalia vema record zako. Mishahara Afya imeboreshwa kuliko sekta zinyine 2006 kima cha chini ni 150,000 hadi 200,000.
Wengi mnakaa Ughaibuni na hatufanyi utafiti wa kutosha kwanza...kwa kifupi to some sektas life and pay is better now than before!

Utashangaa unakaa Ulaya ukifika Tz peers wako wako mbali na wamekuzidi kimaendeleo mbali!

Karibuni nyumbani tujenge taifa!
 
Hakuna NESI hospitali serikali analipwa 70,000 p.m angalia vema record zako. Mishahara Afya imeboreshwa kuliko sekta zinyine 2006 kima cha chini ni 150,000 hadi 200,000.
Wengi mnakaa Ughaibuni na hatufanyi utafiti wa kutosha kwanza...kwa kifupi to some sektas life and pay is better now than before!

Utashangaa unakaa Ulaya ukifika Tz peers wako wako mbali na wamekuzidi kimaendeleo mbali!

Karibuni nyumbani tujenge taifa!

Wee acha propaganda
Huu mtazamo wako wa kushindana kimaisha sijui peers na kitu gani ,ni propaganda zinahusiana nini na umasikini wetu.wewe unafanya kushindana na aliye ulaya ili uje umzidi hapo ndipo tatizo la ufisadi lipoanzia ,kwanza umemzidi kwa lipi? kielimu,kimali za kufisadi wananchi ,kimtazamo ama kinini?

Wewe huoni aibu kwa serikali ya Poland kunipa mimi elimu bure toka bachala hadi masters wakati serikali yetu yenyewe inanyima watanzania elimu ni Upuuzi kabisa.
Hawa wapolish mbona wameweza kunimpa mimi msaka nyoka elimu ya bure yumkini si raia wao ni vipi serikali yetu inashindwa kulipia watu wake???
kwanza ni aibu tupu.

Jamani mwenye data nzuri ya fungu wanalopata wafanyakazi wa serikali kwa ngazi zote watuwekee hapa.

watu wana entertain atoms za kipuuzi kabisa
Samahani kwa maneno makali
 
Hii imekaa vizuri na inatia moyo kuona kuna baadhi ya viongozi wanakuwa na mtizamo tofauti na sera zilizowekwa ambazo zinaonyesha wazi kuwabagua watu.

Sulihisho la hili tatizo ni kuwa na kigezo kimoja tu cha kupata mkopo na sio huu utaratibu wa kuwa na asilimia 100,80,60... hii ni uzushi wa wazi kabisa kwani kwa nchi kama TZ hauwezi kupima kipato halisi cha mtu na mtu anaweza kujaza hizo form kwa namna yeyote ile. Pili kwani hata hao wenye uwezo sio kwamba wazazi wao wameokota tu hizo pesa .. wamezinfanyia kazi so nao pia hauwezi kusema serikali iwatenge.
Suluhisho ni moja tu.. kuweka grade... yeyote atakayepata division I ukipata hiyo basi unapata mkopo asilimia 100 bila kujali unatoka familia masikini ama tajiri. Hiyo ndio njia ya kuondoa ubishi wote huu.

Mwisho najiuliza serikali ni nani??? mbona huyu jamaa kiongozi mkubwa bungeni akiwa kama mwenyekiti wa kamati na yeye anasema serikali iwe makini... nilitarajia angetoa kauli yake akiwa yeye kama hiyo serikali... hii inasikitisha kuona kwamba hata hao viongozi nao wenyewe wanajiona sio serikali sasa serikali ni nani..????

....ni kweli mkuu technical know how ya kujua income ya watu wengi TZ inaweza kuwa ngumu sana,na ninaunga mkono 100% loan kwa wanao qualify kwenye hiyo list,lakini realistically ujue serikali itakata number of sponsorship/loan, kama wanatoa 10000 loan kila mwaka,jee zikishuka 7500 mko tayari au kilio ni kile kile,hapa lazima kuwe na give & get katika deal yeyote itakayofikiwa btn serikali na wananchi,na kumbe hizo loan ni interest free? na collection mechanism yake nasikia iko very poor...lazima wawe seriuos na waache mizaha kama wanataka na vizazi vijavyo viendelee kupata hiyo loan privilege,interest ni muhimu at least the rate to keep up with inflation na lazima waweke njia za kupata hizo loan back la sivyo hii kitu serikali itashindwa.
 
Wee acha propaganda
Huu mtazamo wako wa kushindana kimaisha sijui peers na kitu gani ,ni propaganda zinahusiana nini na umasikini wetu.wewe unafanya kushindana na aliye ulaya ili uje umzidi hapo ndipo tatizo la ufisadi lipoanzia ,kwanza umemzidi kwa lipi? kielimu,kimali za kufisadi wananchi ,kimtazamo ama kinini?

Wewe huoni aibu kwa serikali ya Poland kunipa mimi elimu bure toka bachala hadi masters wakati serikali yetu yenyewe inanyima watanzania elimu ni Upuuzi kabisa.
Hawa wapolish mbona wameweza kunimpa mimi msaka nyoka elimu ya bure yumkini si raia wao ni vipi serikali yetu inashindwa kulipia watu wake???
kwanza ni aibu tupu.

Jamani mwenye data nzuri ya fungu wanalopata wafanyakazi wa serikali kwa ngazi zote watuwekee hapa.

watu wana entertain atoms za kipuuzi kabisa
Samahani kwa maneno makali

Wacha porojo zisizo na msingi, nani aone aibu sasa badala ya we kuona aibu unapewa elimu free alafu unataka wenzako waone aibu kweli ni sawa?? Suala la uchangiaji katika Elimu na Afya haliepukiki, unakosea sana kuifananisha poland na nchi ambayo ipo kwenye orodha za nchi kumi masikini zaidi duniani, kwa mawazo yako finyu unaona ni sahihi kuifananisha Tanzania na Poland kweli?? Unategemea serikali itoe elimu free kwa pesa ipi?? hao wapoland wanaokupa wewe elimu bure wamedonate nini kwenye budget ya Tanzania?? Ni vyema ukafikiria kwanza then uje hapa na kutoa comments zako kuliko kuanza kuropoka while hujafanyia analysis ya kitu unachotaka kukiongelea,, Chuo kimesema kimeondoa sheria inayotambua society zote za wanafunzi mpaka hapo watakaporejesha tena hiyo sheria, mwanafunzi unapaswa kutambua kilichokupeleka chuoni si kwenda kucreate migomo kushinikiza utimiziwe unachokitaka, unaenda chuo kusoma na si kwenda kusimamia bar na sehemu za kukaangia chips ilimradi tu unufaishe tumbo lako.. umekwenda mwenyewe pale na hujaenda na mwenzako.... pili jiulize hawa wanafunzi wa vyuo vingine ambavyo hawajagoma wenyewe wanafurahia hii hali au wanachukia?? kwa kiasi kikubwa wametambua nini kimewapeleka na wakashituka mapemaaa wala haajajiingiza kwenye hiyo migomo njaaa ambayo wameripuka kuianzisha baaada ya kuona pesa za Epa zinarudishwa kwa kufikiria watapewa wao,, hakuna mwanafunzi ambaye hajaingiziwa pesa kutoa loan board, wote wamepewa pesa sasa jiulize kwa nini wameshindwa kulipa hata hiyo nusu ada while pesa wamepewa mapemaaaa?? na pesa za maladhi pia wamepewa mapemaaaa why ushindwe kulipa ada angalau nusu? kwa kukusaidia tu nenda kwenye hii link [media]http://www.udsm.ac.tz/TanzaniansStudentsDebtsStatus.pdf[/media] uangalie the way hawa wanafunzi wanavyojitakia mambo mengine yasiyo na msingi, mtu una udhamini wa A, ada yako unayotakiwa kulipa ni 72,000/= hutaki kulipa unasingizia wazazi wangu masikini kweli?? wewe umefika chuo kikuu huna uwezo wa kupata 70,000/= kweli?? hata ukiamua kufundisha tuition kwa watoto wa primary unakamata hiyo pesa kiulainii na ya kwenda kunywa bia inabakia, na hawa watoto wengi wa wazazi wao wamewapa ada kamili lakini kwa kutaka ufahari na kujisahau wameamua kuikamua wakitegemea watasoma tu bure mpaka watamaliza..... NO WAY UCHANGIAJI KATIKA ELIMU NI LAZIMA
 
Wabunge: Wanafunzi wote wa Vyuo Vikuu Warejeshwe:

Mheshimiwa Kwaang', Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge inayoshughulikia Maswala ya Jamii anastahili kupongezwa kwa msimamo huu. Ni lazima awasilishe hoja hii Bungeni katika kikao kijacho ili Bunge liweze kulazimisha Serikali kutekeleza agizo hilo la Bunge.

Serikali imejenga shule nyingi za sekondari katika kipindi cha miaka miwili ambazo sasa hazina waalimu. Hospitali nyingi nchini hazina madaktari au wauguzi wa kutosha. Wataalam Kilimo hawatoshelezi. Hali kadhalika wahandisi wa kutosha hakuna. Wataalamu katika kila nyanja ni wachache, na kilio cha Watanzania ni kukosa wataalamu. Hawa hawawezi kupatikana kama Wizara yetu ya Elimu na vyuo vikuu watasahau kwamba jukumu la Serikali ni kuongeza wataalamu kwa haraka iwezekanavyo. Kama inawezekana basi Serikali isomeshe wanafunzi wote bure na hii Bodi ya Mikopo ifutwe.

Sera ya Serikali iwe ni kuongeza bajeti ya elimu ili wanafunzi wasome bure na waalimu walipwe mishahara na marupurupu mengine kuwavutia. Hata katika nchi kama Kenya bajeti ya elimu ni asilimia marudufu ya kwetu. Maendeleo yetu yatasuasua hadi hapo tutakapoamua kutoa kipaumbele cha dhati kwa sekta ya elimu.

Inanishangaza kuona viongozi wa Wizara na Vyuo Vikuu ambao walisoma bure zama za Mwalimu Julius Nyerere, sasa wamesahau na wanataka watoto wao na wa ndugu zao maskini, wasome kwa mikopo.

Inashangaza zaidi pale afisa wa Bodi ya Mikopo anaposhauri kwamba mikopo iwe inatozwa riba ambayo itawezesha urejeshwaji usipungue thamani kutokana na mlipuko wa bei. Inaonekana huyu afisa haelewi kwamba elimu hutolewa kama huduma ya kijamii (social services) kama vile matibabu na dawa hospitalini. Ukitoa elimu kwa kukopesha mikopo kama benki ya biashara, kamwe nchi haitaendelea.


Kilasara (JF Junior Member)
 
Walimfukuza yule Mganda wakasema ndio chanzo cha migomo sasa wamehamia DARUSO
Wanafunzi lazima wawe na chombo chao cha kuwawakilisha
Tatizo kubwa la wanachuo ni kuhusu kutaka serikali kuwakopesha mikopo 100% hilo ndio tatizo na sio DARUSO naamini hata wakiifuta hiyo DARUSO bado hwajatatua tatizo
 
Kwa:
Wanachuo na Wafanyakazi Wote,
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

UTARATIBU WA KUINGIA NA KUTOKA ENEO LA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM 18 – 23 JANUARI 2009

Uongozi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam unawaarifu wakazi wa Chuo Kikuu na wafanyakazi, wote kuwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kitafunguliwa tarehe 19/01/2009.
Ili zoezi la kusaili wanafunzi waliotimiza masharti na kuruhusiwa kurudi Chuo lifanyike kwa ufanisi na kwa usalama, uongozi wa Chuo umeweka utaratibu maalumu wa kuingia na kutoka Chuoni hapa kutoka tarehe 18 mpaka 23 Januari 2009. Utaratibu huo ni kama ifuatavyo:
•Kuingia Chuo – Lango la Ubungo karibu ya Chuo cha Maji cha Rwegarulila tuu.
•Kutoka Chuo – Lango la Upande wa Chuo Kikuu cha Ardhi tuu.
•Milango mingine yote itafungwa na haitatumika kwa kuingia au kutoka, na hii ni pamoja na
oLango la kutoka Changanyikeni/ Msewe/ Makongo
oKupita Hall VI
oKupitia Savei.
•Njia nyingine zote ambazo sio rasmi zitadhibitiwa ipasavyo.
•Wale wote wanaotoka Changanyikeni, Jeshini, na Chuo cha Takwimu wanaombwa watumie njia ya Msewe na kuelekea Ubungo au Makongo kuelekea Mwenge.
•Wafanyakazi wa Chuo wanaombwa kutembea na vitambulisho vyao vya kazi, ili wavitumie kuingilia langoni. Kwa wafanyakazi wake/waume na watoto wakubwa wa wafanyakazi wasio na vitambulisho wanaombwa wawasiliane na Wakuu wa vitengo vya wafanyakazi husika ili wawapatie barua za utambulisho.
•Watoto wa shule za Sekondari na Msingi wanaruhusiwa kupita sehemu za Chuo wakiwa na sare za shule tu.
•Huduma za daladala zitaishia langoni. Kwa wanachuo na wafanyakazi, kutakuwa na usafiri wa ndani ya Chuo kutoka lango la maji mpaka lango la Chuo Kikuu cha Ardhi.
•Ramani iko nyuma.

Chuo kinawaomba uvumilivu na radhi kwa usumbufu wowote utakaotokea.

IMETOLEWA NA MENEJIMENTI
CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM
Januari 16, 2009

KAZI IPO
 
kwa wale ambao hawajaiona hii(utaratibu wa kusajiliwa upya)

UNIVERSITY OF DAR ES SALAAM

PROCEDURES FOR REGISTRATION OF READMITTED STUDENTS
All students who have satisfied all the conditions for readmission to the University of Dar es Salaam and whose names have been published are called for registration at the University in strict adherence to the following procedures.
Important cautions
1 All students were deregistered upon the closure of the University. Hence none of those who have been published for readmission and registration shall have the studentship status of the University of Dar es Salaam before they are registered in accordance with the procedures hereunder.
2 The leadership of all students organizations ceased upon the deregistration of students, hence it shall be unlawful for any student to purport acting or representing students under the auspices of the students’ organizations.
3 The whole of the area comprising the University of Dar es Salaam shall be restricted for entry to only those students whose names have been published and only on the dates and time specified under these procedures. Any person entering the University without express permission shall be committing breach of order and peace and subject to immediate prosecution.
4 Readmitted students shall only proceed to those areas to which they are instructed to go and present themselves to the relevant authorities as they shall be instructed. Infringement of the procedures for readmission shall constitute the breach of University Rules and appropriate disciplinary measures shall be taken including the immediate withdrawal of the culprit’s readmission.
5 Remember to bring with you originals and photocopies of your birth certificate, certificate of secondary education examination and advanced certificate of secondary education examination for registration purposes.

Procedures for Readmission and Registration
All students whose names have been published for readmission at the University of Dar es Salaam shall strictly abide by these procedures. No readmission or registration shall take place during the readmission week except by strict adherence to these procedures.
1. Students whose names have been published for readmission shall report to the University of Dar es Salaam Main Campus at Mlimani in accordance with the following timetable
rd th
(a) All published finalist students (whether 3year finalists or 4year
th
finalists) shall report for readmission and registration on Monday 19January 2009;
(b)All published third year non-finalist students shall report for readmission
th
and registration on Tuesday 20January 2009;
(c) All published second year students shall report for readmission and registration on Wednesday 21st January 2009; and
(d)All published first year students shall report for readmission and
nd
registration on Thursday 22January 2009
1 All qualifying students coming to report for readmission shall check their names outside the University of Dar es Salaam Gate adjacent to the Rwegarulila Water Institute where a checkpoint shall be situated. It shall be unlawful for any person purporting to be a student to enter the University area without obtaining a special pass.
2 All qualifying students whose names will be ascertained at the checkpoint shall surrender their respective previous student identity cards and shall be issued with registration documents and be instructed to proceed to their respective Faculties.
3 Readmission of students shall strictly take place between 8.00am and 4.00pm of each designated date and shall be strictly for those who have been listed for readmission on that date. Hence any student who shall default to appear for readmission on the designated date shall not be readmitted during the readmission week. Such students shall have to wait for a special procedure after the said week and shall remain outside the University area at their own expenses. It is therefore emphasized that those who have been published for readmission must strictly observe these procedures.
5. Every student who will have been issued with the special pass shall be required to proceed to his/her Faculty Dean’s office for registration. No person shall be permitted to visit any other place within the University
without wearing his/her new student identity card. Any person found within the University and who is not wearing a student identity card shall have committed breach of order and peace and subject to immediate prosecution measures.
4 Every student who fulfils the registration requirements shall be issued with a new identity card and be instructed to proceed for residential allocation. No person shall be allowed to be present within the perimeters of the Halls of Residence without having and wearing his/her student identity card.

Resumption of Lectures
Lectures for each year shall resume immediately after registration as follows
th
(a) Lectures for finalist students shall commence on Tuesday 20 January 2009. Only students wearing the new student identity cards will be permitted to attend lectures;
(b)Lectures for non-finalist third year students shall commence on Wednesday 21st January 2009. Only students wearing the new student identity cards will be permitted to attend lectures;
nd
(c) Lectures for second year students shall commence on Thursday 22 January 2009. Only students wearing the new student identity cards will be permitted to attend lectures; and
rd
(d)Lectures for first year students shall commence on Friday 23 January 2009. Only students wearing the new student identity cards will be permitted to attend lectures.
Student Affairs
Until such time the Council approves new students’ organizations leadership all students affairs shall be dealt with in accordance with such rules and procedures to be issued by the Dean of Students. It shall be unlawful for any person to assume leadership over students’ affairs except in accordance with the directions and instructions of the Dean of Students.
PROFESSOR MAKENYA MABOKO
DEPUTY VICE CHANCELLOR (ACADEMIC)
 
Kuna taarifa za kuaminika kwamba njia zote za kuingia na kutokea chuoni zitafungwa kuanzia tarehe 18/01/2009 hdi 23/01/2009, siku ambayo usajili wa wanafunzi waliotimiza masharti utafanyika. Kwa mujibu wa habari katika mabao za matangazo chuoni hapo, njia ya kuingilia itakuwa moja tu ya geti la chuo cha Maji aka Getimaji, na ya kutokea itakuwa moja tu ya Chuo Kikuu cha Ardhi aka ARU. Njia hizi zinawahusu watu wote, wanafunzi na wafanyakazi. Raia waishio Msewe na Changanyikeni, ikiwa pamoja na wanajeshi wa kambi ya kule Changanyikeni hawaruhusiwi kabisa kupita chuoni. Wakati wanafunzi na wafanyakazi wenye vitambulisho tu ndio watakao ruhusiwa kuingia na kutoka chuoni, wengine waliobaki hawaruhusiwi kabisa !! Wafanyakazi wanaoishi changanyikeni watalazimika kwenda Ubungo ili waingie chuoni, na watalazimika kwenda Mwenge ili warudi manyumbani kwao Changanyikeni (hebu jaribu kupata picha hiyo). Kwa wale mnaoishi maeneo hayo anzeni kutafakari route zenu ziweje!!

Pia si vibaya kuuunganisha na tangazo hili lililopo kwenye webusaiti ya chuo:


UNIVERSITY OF DAR ES SALAAM
PROCEDURES FOR REGISTRATION OF READMITTED STUDENTS

All students who have satisfied all the conditions for readmission to the University of Dar es Salaam and whose names have been published are called for registration at the University in strict adherence to the following procedures.
Important cautions
1. All students were deregistered upon the closure of the University. Hence
none of those who have been published for readmission and registration
shall have the studentship status of the University of Dar es Salaam before
they are registered in accordance with the procedures hereunder.
2. The leadership of all students organizations ceased upon the deregistration
of students, hence it shall be unlawful for any student to purport acting or
representing students under the auspices of the students’ organizations.
3. The whole of the area comprising the University of Dar es Salaam shall be
restricted for entry to only those students whose names have been published
and only on the dates and time specified under these procedures. Any person
entering the University without express permission shall be committing
breach of order and peace and subject to immediate prosecution.
4. Readmitted students shall only proceed to those areas to which they are
instructed to go and present themselves to the relevant authorities as they
shall be instructed. Infringement of the procedures for readmission shall
constitute the breach of University Rules and appropriate disciplinary
measures shall be taken including the immediate withdrawal of the culprit’s
readmission.
5. Remember to bring with you originals and photocopies of your birth
certificate, certificate of secondary education examination and advanced
certificate of secondary education examination for registration purposes.

Procedures for Readmission and Registration

All students whose names have been published for readmission at the University of Dar es Salaam shall strictly abide by these procedures. No readmission or registration shall take place during the readmission week except by strict adherence to these procedures.
1. Students whose names have been published for readmission shall report to
the University of Dar es Salaam Main Campus at Mlimani in accordance
with the following timetable-
(a) All published finalist students (whether 3rd year finalists or 4th year
finalists) shall report for readmission and registration on Monday 19th
January 2009;
(b) All published third year non-finalist students shall report for readmission
and registration on Tuesday 20th January 2009;
(c) All published second year students shall report for readmission and
registration on Wednesday 21st January 2009; and
(d) All published first year students shall report for readmission and
registration on Thursday 22nd January 2009
2. All qualifying students coming to report for readmission shall check their
names outside the University of Dar es Salaam Gate adjacent to the
Rwegarulila Water Institute where a checkpoint shall be situated. It shall be
unlawful for any person purporting to be a student to enter the University
area without obtaining a special pass.
3. All qualifying students whose names will be ascertained at the checkpoint
shall surrender their respective previous student identity cards and shall be
issued with registration documents and be instructed to proceed to their
respective Faculties.
4. Readmission of students shall strictly take place between 8.00am and
4.00pm of each designated date and shall be strictly for those who have been
listed for readmission on that date. Hence any student who shall default to
appear for readmission on the designated date shall not be readmitted during
the readmission week. Such students shall have to wait for a special
procedure after the said week and shall remain outside the University area at
their own expenses. It is therefore emphasized that those who have been
published for readmission must strictly observe these procedures.
5. Every student who will have been issued with the special pass shall be
required to proceed to his/her Faculty Dean’s office for registration. No
person shall be permitted to visit any other place within the University
without wearing his/her new student identity card. Any person found within
the University and who is not wearing a student identity card shall have
committed breach of order and peace and subject to immediate prosecution
measures.
6. Every student who fulfils the registration requirements shall be issued with a new identity card and be instructed to proceed for residential allocation. No
person shall be allowed to be present within the perimeters of the Halls of
Residence without having and wearing his/her student identity card.

Resumption of Lectures

Lectures for each year shall resume immediately after registration as follows-
(a) Lectures for finalist students shall commence on Tuesday 20th January 2009. Only students wearing the new student identity cards will be permitted to attend lectures;
(b) Lectures for non-finalist third year students shall commence on Wednesday 21st January 2009. Only students wearing the new student identity cards will be permitted to attend lectures;
(c) Lectures for second year students shall commence on Thursday 22nd January 2009. Only students wearing the new student identity cards will be permitted to attend lectures; and
(d) Lectures for first year students shall commence on Friday 23rd January 2009.Only students wearing the new student identity cards will be permitted to attend lectures.

Student Affairs

Until such time the Council approves new students’ organizations leadership all
students affairs shall be dealt with in accordance with such rules and procedures to be issued by the Dean of Students. It shall be unlawful for any person to assume leadership over students’ affairs except in accordance with the directions and instructions of the Dean of Students.

DEPUTY VICE CHANCELLOR (ACADEMIC)
 
Hapo ndo ujue kuwa watu wazima wapo serious sasa na kwa wale ambao walikuwa wanaona watarudi chuo bila kumaliza ada haya sasa nafikiri mmeshaanza kusoma ishara za nyakati.... Kushindana na serikali ni issue jamani madogo kuweni wapole tu waungwana wameshaawaambia kuwa sera ya uchangiaji haiwezi kubadilika kamwe nyie bado hataki kukubali sasa nini mnachokitafuta?? subirini tu labda nchi ikiongozwa na viongozi wengine wanaweza kuwafikiria
 
Jamani ifike wakati tutofautishe vyuo vikuu na secondali.
Watu wanafundishwa wapevuke alafu walimu wao hawataki wapevuke iki si kichina?
 
Hiki chuo sasa kinaendeshwa na maprofessor uchwara. Ndio maana nchi haisongi mbele. Badala ya kutatua matatizo, sisi tunafunika tukidhani ndio suluhisho. Waafrika ndivyo tulivyo....we are doomed.
 
Hatimaye Chuo kikuu cha Dar es Salaam katika mkakati wa kuhakikisha kwamba wanaingia chuoni wale tu wanaostahili, kuanzia tarehe 18--23, Menejimenti ya Chuo imetoa ilani kwa watumiaji wa njia zinazopita chuoni hapo kutotumia njia hizo! kwa maana nyingine kwa mjibu wa ilani hiyo ambayo nimebahatika kuiona milango miwili ama geti mbili tu zitatumika, kuingia chuo italazimika kupita geti maji na kutoka itakuwa geti la Chuo cha ardhi, mageti mengineyo kama Changanyikeni nk hakuna ruksa hata kidogo! katika kipindi hicho! sisi wakaazi wa Changanyikeni nk tunashauriwa kutumia njia ya msewe kuelekea Ubungo na kama tunahitaji kwenda Mwenge basi njia ni Makongo juu! wanafunzi wa shule za msingi wataruhusiwa kupita katika lango la chuo kama tu watakuwa na sare zao za shule, na kwa wafanyakazi wote wa chuo watalazimika katika kipindi chote hicho kutumia vitambulisho vyao na kuwaonyesha walinzi wa chuo auxiliaries vitambulisho vyao! na kwa kada nyinginezo kama Wanajeshi wote watalazimika kutii utaratibu huo uliowekwa na Chuo, mh! ndiyo mambo hayo ya private roads nk wana exercise jurisdiction yao! Ilani haijasema kwasisi wengine ambao makulaji yetu na masuala ya chinywaji tunategemea UDASA club, Hillpark nk status yetu ni vipi? lakini pia kwa wengineo tulio na marafiki na ndugu wa karibu malekchara hapo mlimani ilani haijasema kabisa inakuwa vipi? ama kama ninashida yoyote itakayonilazimu nifike chuo itakuwa vipi? Je uamuzi uliochukuliwa umezingatia kabisa mibadala yote ambayo ingewezekana kuchukuliwa? ama ndio haya mambo ya kumeneji ki makenika? Je kulikuwa na ulazima wowote wa kutupa adhabu sisi wakazi wa pembezoni mwa chuo? ama wananchi wengine wa kawaida? ama tunapata adhabu kimtindo kwasababu ya ndugu na wadogo zetu 'jeuri'?
 
Hatimaye Chuo kikuu cha Dar es Salaam katika mkakati wa kuhakikisha kwamba wanaingia chuoni wale tu wanaostahili, kuanzia tarehe 18--23, Menejimenti ya Chuo imetoa ilani kwa watumiaji wa njia zinazopita chuoni hapo kutotumia njia hizo! kwa maana nyingine kwa mjibu wa ilani hiyo ambayo nimebahatika kuiona milango miwili ama geti mbili tu zitatumika, kuingia chuo italazimika kupita geti maji na kutoka itakuwa geti la Chuo cha ardhi, mageti mengineyo kama Changanyikeni nk hakuna ruksa hata kidogo! katika kipindi hicho! sisi wakaazi wa Changanyikeni nk tunashauriwa kutumia njia ya msewe kuelekea Ubungo na kama tunahitaji kwenda Mwenge basi njia ni Makongo juu! wanafunzi wa shule za msingi wataruhusiwa kupita katika lango la chuo kama tu watakuwa na sare zao za shule, na kwa wafanyakazi wote wa chuo watalazimika katika kipindi chote hicho kutumia vitambulisho vyao na kuwaonyesha walinzi wa chuo auxiliaries vitambulisho vyao! na kwa kada nyinginezo kama Wanajeshi wote watalazimika kutii utaratibu huo uliowekwa na Chuo, mh! ndiyo mambo hayo ya private roads nk wana exercise jurisdiction yao! Ilani haijasema kwasisi wengine ambao makulaji yetu na masuala ya chinywaji tunategemea UDASA club, Hillpark nk status yetu ni vipi? lakini pia kwa wengineo tulio na marafiki na ndugu wa karibu malekchara hapo mlimani ilani haijasema kabisa inakuwa vipi? ama kama ninashida yoyote itakayonilazimu nifike chuo itakuwa vipi? Je uamuzi uliochukuliwa umezingatia kabisa mibadala yote ambayo ingewezekana kuchukuliwa? ama ndio haya mambo ya kumeneji ki makenika? Je kulikuwa na ulazima wowote wa kutupa adhabu sisi wakazi wa pembezoni mwa chuo? ama wananchi wengine wa kawaida? ama tunapata adhabu kimtindo kwasababu ya ndugu na wadogo zetu 'jeuri'?

Shy si nasikia Udasa club ni kwa members wa udasa only? sasa wewe ufuate nini huko while si member wa udasa? na hapo hillpark unaposema kwani ni lazima ukale hapo?? au ndo kujiamini kwako kwa kutaka kuwapima polisi kama wana ubavu au la?? hahahaha haya bwana lakini kumbuka KUNGURU MJANJA..............................??
 
Shy si nasikia Udasa club ni kwa members wa udasa only? sasa wewe ufuate nini huko while si member wa udasa? na hapo hillpark unaposema kwani ni lazima ukale hapo?? au ndo kujiamini kwako kwa kutaka kuwapima polisi kama wana ubavu au la?? hahahaha haya bwana lakini kumbuka KUNGURU MJANJA..............................??

ARISA pako wazi siku zote na hadhi ya misosi ni zaidi ya UDASA.
 
Back
Top Bottom