Chuo Kikuu (UDSM) Kufunguliwa na Masharti mapya!

Hii yote inatokana na kung'ang'ania hii sera iliyopitwa na wakati ya watoto wetu kusoma "BURE" au kwa "MIKOPO" kutoka serikalini. Serikali itaendelea kutudhalilisha inavyotaka. Siku zote anayemlipa mwanamziki ndiye anayechagua wimbo! Natoa wito kwa WAZAZI wenzangu tujiandae kikamilifu kuwasomesha wanetu hata kama ni kwa kuchangishana wenyewe. Mbona HARUSI, MAKANISANI, ... tunachangishana kwa mamilioni? Sadaka ya Ibada moja tu pale St. Joseph siku ya Jumapili ni shs ngapi? Fedha hizi zinawasaidia wangapi?
 
Hii yote inatokana na kung'ang'ania hii sera iliyopitwa na wakati ya watoto wetu kusoma "BURE" au kwa "MIKOPO" kutoka serikalini. Serikali itaendelea kutudhalilisha inavyotaka. Siku zote anayemlipa mwanamziki ndiye anayechagua wimbo! Natoa wito kwa WAZAZI wenzangu tujiandae kikamilifu kuwasomesha wanetu hata kama ni kwa kuchangishana wenyewe. Mbona HARUSI, MAKANISANI, ... tunachangishana kwa mamilioni? Sadaka ya Ibada moja tu pale St. Joseph siku ya Jumapili ni shs ngapi? Fedha hizi zinawasaidia wangapi?

Unayosema ni ya kweli lakini napata taabu kuamini kama umeshawahi kutoka nje ya Dar es Salaam ukaushuhudia umasikini wa Tanzania. Ndugu yangu Tanzania sio Dar es Salaam pekee. Asilimia 80 ya watanzania wanategemea kilimo na wengi wao cha jembe la mkono! Wanaweza kulima ekari ngapi ili wapate chakula na ziada ya kusomesha watoto?
 



Uongozi wa UDSM ulichelewa kuifuta hii DARUSO, to me DARUSO haikuwa ikikidhi mahitaji na matakwa ya wanachuo zaidi ya kuwa jukwaa la kuendesha siasa na kuwanyima haki wale ambayo wapo kwa nia ya kusoma. Ifike mahali wanafunzi waelewe kuwa kazi yao hapo UDSM ni kusoma na wale siyo kuendesha Chuo. Kazi za kuendesha Chuo ziachwe kwa Viongozi wa Chuo vinginevyo wanafunzi wanachukua muda mwingi kufanya yale ambayo haya wahusu kimsingi.
Bravo kwa kuifuta DARUSO

Mkuu hebu panua akili na uelewa wako kidogo.
Miaka ya nyuma sana baada ya uhuru hakukuwa na DARUSO, ARUSO, DITSO, SUASO, n.k, n.k
Miaka hiyo kulikuwa na kitu kinaitwa MUWATA.
Kuanzia UDSM,SUA,DIT,CBE hadi shule za sekondari na vyuo vya ualimu kulikuwa ni MUWATA.Baadae serikali ikaja kuifutilia mbali hiyo muwata kutokana na hisia kama hizi za udsm,tena wakati huo kulikuwa bado na mfumo wa chama kimoja cha siasa ccm, sasahivyo visingizio vya kutumiwa na wanasiasa na blabla nyingine havikuwepo.Muhimu ni kujua kuwa historia ya migomo katika vyuo vya elimu ya juu nchini haijaanza leo. miaka kadhaa baadae ilionekana jinsi ilivyokuwa vigumu kuendesha vyuo vya elimu ya juu pasipo kuwashirikisha wanafunzi hususan welfare zao, mhadhiri hawezi kuyajua mahitaji ya mwanafunzi abadani! na ndio maana kunakuwepo na vyama vya wafanyakazi mahali pa kazi, maana mtasema wafanya kazi wajibu wao ni kufanya kazi walioajiriwa kuifanay na sio kuongoza mahali husika iwe ni kampuni au shirika!!!ushirikishwaji ni jambo la lazima wala halikwepeki, na mimi natabiri kuwa DARUSO itaruhusiwa kuendelea kuwepo hivi karibuni na bila DARUSO mambo yatakuwa magumu zaidi, kinachofanywa ni vitisho tu lakini bila kutatua tatizo la mikopo itabidi chuo kifungwe milele!!!Ni vizuri kujua kuwa wanafunzi hawawezi kuziachia management za vyuo vyao kushughulikia matatizo yao, hilo halipo na halitatokea.Management za vyuo zinashindwa kushughulikia matatizo ya wafanyakazi wenzao itakuwaje kwa wanafunzi.tena hii lugha ya kwamba wanafunzi wako chuoni kusoma na sio kuongoza chuo ni ufinyu wa uelewa.utasomaje bila kuwekewa mazingira stahiki ya kusoma???hata huko vijijini tunahimiza ushirikishwaji wa wananchi katika kupanga na kutekeleza miradi yao ya maendeleo, ajabu ni kuwa mnataka kwenye chuo kikuu wasomi wakae watulie wapangiwe mambo yao.
Tangu kuanzushwa kwa sheria ya bodi ya mikopo ya elimu ya juu, wanafunzi ambao ndio wadau husika hawakushirikishwa tangu hatua za awali.Baada ya kuligundua hili, bahati nzuri nilikuwa bado niko chuoni nasoma(sio UDSM lakini)
tulifanya jitihada kubwa sana hadi tukaweza kupeleka wizarani maoni yetu kuhusu sheria ile lakini bado serikali haikutaka kutusikiliza hata kidogo.Kitu kimoja tu kilichokubaliwa na serikali ni kuwajumuisha wawakilishi wa wanafunzi kwenye bodi ya mkono ingawa jinsi wanavyoteuliwa hao wawakilishi ndipo kuna utata.Jambo lolote lile kama mlinafanywa pasipo kuwashirikisha wadau husika haliwezi kuwa na mafanikio hata kidogo. Sasa ni miaka mitano baada ya kuanzisha utaratibu wa kuchangia elimu ya juu kupitia bodi ya mikopo bado kumekuwepo na msuguano kati ya wanafunzi na serikali, hapa ndipo tunatakiwa tujiulize kwa kina na tusitafute majibu mepesi kwa maswali magumu kama wanavyofanya serikali kupitia uongozi wa udsm.
 
Unayosema ni ya kweli lakini napata taabu kuamini kama umeshawahi kutoka nje ya Dar es Salaam ukaushuhudia umasikini wa Tanzania. Ndugu yangu Tanzania sio Dar es Salaam pekee. Asilimia 80 ya watanzania wanategemea kilimo na wengi wao cha jembe la mkono! Wanaweza kulima ekari ngapi ili wapate chakula na ziada ya kusomesha watoto?

Hukohuko vijijini tembelea sehemu zao za starehe uone hiyo pesa kidogo wanayopata wanavyoitumia. Angalia wazee wanavyoongeza wanawake kila mwaka kwa mahari ya kumsomesha mtoto hadi chuo kikuu bila tatizo. Serikali za VIJIJI zikiwa na mipango na na uelewa wa kutosha wa wanavijiji hakuna mtoto ambaye hatasoma.
 
Yaani nini inakuwa shida kuchangia elimu ya juu wakati familia hutumia mamilioni kuchangia sherehe za arusi???

Tuwe na michango ya nguvu ya harambee kama Kenya ili watoto wetu wapate elimu ya juu!!

Tz kupenda vya bure bwana- we acha tu!
 
Ni mawazo hasi kusema kila siku mimi maskini basi nisaidie!!!

Tanzania na watu wake sii nchi maskini!

Mimi sikubali kuwa Tanzania ni maskini na kwa hiyo watu wake hawawezi kuchangia elimu ya juu ya watoto wao waliowazaa!
 
Ni mawazo hasi kusema kila siku mimi maskini basi nisaidie!!!

Tanzania na watu wake sii nchi maskini!

Mimi sikubali kuwa Tanzania ni maskini na kwa hiyo watu wake hawawezi kuchangia elimu ya juu ya watoto wao waliowazaa!

mkuu naona unawatania wadanganyika,
Tanzania na watu wake si maskini???kila siku JK yuko safarini kutembeza bakuli huko dunia ya kwanza kutafuta chochote kitu halafu wewe unaleta utani!!!!
Budget ya serikali ni tegemezi kwa mfano ya mwaka 2008/09 ilikuwa trgemezi kwa asilimia 38 kama sikosei.
Tusijaribu kuukwepa ukweli kwa visingizio ambavyo havipo.
Wadanganyika si masikini kinadharia kwa kuwa mnajidanganya kuwa mna rasilimali za kutosha lakini mnasahau kuwa zote ziko chini ya wageni.
 
Hukohuko vijijini tembelea sehemu zao za starehe uone hiyo pesa kidogo wanayopata wanavyoitumia. Angalia wazee wanavyoongeza wanawake kila mwaka kwa mahari ya kumsomesha mtoto hadi chuo kikuu bila tatizo. Serikali za VIJIJI zikiwa na mipango na na uelewa wa kutosha wa wanavijiji hakuna mtoto ambaye hatasoma.

Kwa Dar es Salaam ulizungumzia mamilioni. Vijijini unazungumzia shilingi ngapi? Ni kweli watanzania walio wengi wana matumizi mabaya ya fedha labda kwa makusudi tu au kwa kukosa elimu ya kutosha kuweza kuwa na vipaumbele vyenye kuleta tija kama elimu.

Lakini hata kama wakijitahidi ku-save, wananchi walio wengi hawawezi kumudu gharama za kusomesha watoto vyuo vikuu (ada za shule za msingi na sekondari ni tatizo kubwa). Amini usiamini, watanzania walio wengi ni ni hoehae. Walioendelea wanasema tunaishi kwa chini ya dola moja (roughly TShs 1,250) kwa siku! Hii ni sawa na kipato cha TShs 450,000 kwa mwaka. Ada tuu ya chuo kwa vyuo vikuu vya umma nadhani si chini ya TShs 600,000 kwa mwaka. Unaweza kuona mtanzania huyu hata kama asipokula mwaka mzima kamwe hataweza kulipa ada ya chuo kikuu hata kwa mtoto mmoja. Najua unaweza kusema hiyo dola moja kwa siku ni mahesabu ya jumla, lakini kwa hakika inatoa picha ya kiwango cha umasikini. Na hata bila hizo porojo za statistics, hata casual observation huko vijijini inatosha kukuonesha kiwango cha umasikini.

Inasikitisha kwamba kuna baadhi ya watanzania hawaelewi kiwango cha umasikini tulionao.
 
SMU,
Ukienda chuo kikuu chochote hapa nchini HAKUNA mtoto wa MASIKINI uliemuelezea hapo juu anayesoma huko. Mtoto wa masikini wa aina hiyo hatakosa msaada toka kwa ndugu, jamii au halmashauri husika. Tunaongopeana na kudanganyana sana inapofikia kueleza vipato vyetu halisi.
 
SMU,
Ukienda chuo kikuu chochote hapa nchini HAKUNA mtoto wa MASIKINI uliemuelezea hapo juu anayesoma huko. Mtoto wa masikini wa aina hiyo hatakosa msaada toka kwa ndugu, jamii au halmashauri husika. Tunaongopeana na kudanganyana sana inapofikia kueleza vipato vyetu halisi.

WildCard,

Sina haja ya kwenda chuo kikuu kupata proof. Binafsi ni mfano halisi wa umasikini ninaouelezea hapo juu. Kwa bahati lakini nilisoma katika shule za serikali (wakati huo tukipewa mpaka nauli) na chuo kikuu ilikua bure. Kama ingekuwa sasa kwa hakika mzazi wangu asingeweza!

Unazungumzia msaada kutoka kwa 'ndugu, jamii na halmashauri'. Hili ni sawa na linawezekana lakini kwa kiasi kidogo sana. Lakini umewahi kujiuliza kwa mfano hawa watoto wa mitaani wanatoka wapi? hawana ndugu? hakuna halmashauri?jamii iko wapi?
 
SMU,
Watoto wa mitaani wanatokana na sisi ambao tunafanya mapenzi bila mpangilio na kila tunayekumbana naye barabarani. Wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu wana mchango mkubwa tu kwa kuzalisha watoto hawa. Nakaa jirani na chuo kikuu kimoja hapa Dar. Nimeshindwa kukaa na housegirl mwaka ukaisha bila kupachikwa mimba na mmoja wanafunzi wa chuo hiki!
Watoto wa mitaani wanatokana pia na dada zetu kukimbilia mijini bila kujua huko wanakwenda kufanya nini. Wengine wanatokana na tabia na hulka ya baadhi ya makabila yetu kupenda kuwa OMBAOMBA.
 
Kufuta DARUSO si ufumbuzi na huwezi kuwa ufumbuzi hata siku moja. Nifikra ya mbuni kuficha kichwa kwenye mchanga na kudhani haonekani.

Moja ya tatizo la msingi huwa ni kuwa viongozi wengi wa chuo na hata serikali huwachukulia wanafunzi wa vyuo vikuu kama viumbe wasio na akili hata kidogo, ambayo upofu na ukiziwi wa uelewa. Jaribu kukumbuka pale mwanafunzi wa mwaka wa tano pale Muhimbili anagoma na unamfukuza bila kujiuliza kulikoni, maana yake umeona huyu ni mjinga tu, lakini ukimrudisha miezi tisa baadaye ni Daktari na wewe uliyemfukuza unakwenda kwake unaumwa AKUTIBU, unaweka maisha yako mikononi mwake!!!!!!!!!!!!!!!!!! sasa ghafla huyu amekuwa mtaalamu mpaka ukaridhika naye vipi. Hao wengine wa mwaka wa tatu ndio watakaoajiriwa hivi karibuni ili kujaza nafasi tunazoacha tunaozeeka!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Ikumbukwe hata akina Warioba waligoma wakachapwa viboko baadaye ndio Waziri Mkuu wa nchi n.k.

Kunahitajika utathimini wa kutosha hapa kabla ya kukurupuka kwa hasira tu kuwafukuza, kuvunja DARUSO hata kuandika kwamba ni wajinga.

Inanikumbusha mwaka fulani nikiwa UDSM, kulikuwa na mgomo UDSM, magazeti yakaandika wanafunzi wa UDSM wamegoma kwa vile hawajala mayai na kupewa maziwa WACHA WANANCHI NA WAZAZI WETU WACHARUKE!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Lakini ukweli ULIKUWA WANAFUNZI WALIKUWA WAKIMWAMBIA MAKAMU MKUU WA CHUO KUWA ILE TAARIFA YA KWAMBA WANAFUNZI WAMEKULA MAYAI ILIKUWA YA UONGO KWA SABABU HAWAKULA (KA-UFISADI KALIKUWEKPO) Bahati nzuri baadaye watu wa usalama wa taifa wakafanya uchunguzi ikagindulika kuwa taarifa za matumizi ya Cafeteria zilikuwa na wizi mkubwa (na ilikuwa kidogo tu tufukuzwe) na aliyekuwa Mkuu wa Cafeteria aliachishwa nafasi hiyo.

Hivyo tusikimbilie ufumbuzi wa haraka haraka UNAOFICHA MAMBO MAKUBWA MAHALI, TUTAKUJA JUTA!!!!!!!!!
 
SMU,
Watoto wa mitaani wanatokana na sisi ambao tunafanya mapenzi bila mpangilio na kila tunayekumbana naye barabarani. Wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu wana mchango mkubwa tu kwa kuzalisha watoto hawa. Nakaa jirani na chuo kikuu kimoja hapa Dar. Nimeshindwa kukaa na housegirl mwaka ukaisha bila kupachikwa mimba na mmoja wanafunzi wa chuo hiki!
Watoto wa mitaani wanatokana pia na dada zetu kukimbilia mijini bila kujua huko wanakwenda kufanya nini. Wengine wanatokana na tabia na hulka ya baadhi ya makabila yetu kupenda kuwa OMBAOMBA.

WildCard,
Pole kwa kupoteza housegirls kutokana na kupewa ujauzito na wanafunzi wa chuo (kama unaweza hama hiyo sehemu:)!)

Dada zetu kwa nini wanakimbilia mijini?Hawana ndugu? hakuna halmashauri? Jamii inafanya nini? Hata hivyo naona kama vile tunaelekea kutoka kwenye mada (inayohusu kufutwa kwa Daruso) - ngoja tuwatendee haki wanajamvi!

Kuna takwimu na vielelezo vingi vya kuelezea umasikini wa watanzania. Nadhani itabidi tuanzishe thread mpya ya kujadili kama watanzania walio wengi ni masikini au la (i.e. Je watanzania wanaweza kumudu gharama za kusomesha watoto wao chuo kikuu?).
 
Ama kweli Afrika inatakiwa kuamka!!Hivi haya ni mambo ya kufikiria kweli wakati huu Boresheni elimu na taaluma siyo kufikiria sheria za kumbana mwanafunzi saa hizi!!!Hivi UDSM mathalani ingekuwa na wanafunzi Millioni moja,Hiyo gharama ya kutengeneza vitambulisho tu hata ingekuwa shilling mia ingekuwa kiasi gani,Isingetosha kusomesha watoto kadhaa?Kuweni wastaarabu njooni George Washington University mjifunze!!!!
 
wito wangu ni kuwa kila mtu kwa uwezo wake na nafasi yake atoe mchango wa kuishinikiza serikai itimize wajibu wake kwa wwatu wake.

Tuandike makalla nyingi kwenye vyombo vya habari za kulaani na kukemea ukaburu dhidi ya watoto wwa maskini tanzania

ikiwezekana tuandae maadamano ya kualaani na kudai utawala uondolewe kuokoa chuo
Tetesi. wanataka kuua UDSM ili waikuze Dodoma University kuandaa legacy ya mkuu wwa kaya na pili kupunguza watu wanaohoji utawala.UDSM inaonekana haina adabu kwa sababu inajengea wanafunzi utamaduni wwa kuhoji mambo
Elimu ni haki na sio
 
Serikali wasomeshe watu bure harafu wafute hiyo DARUSO.
Tanzania ni masikini acheni matusi hapa,kitendo cha mzee wangu kule kwenda kufua na kuoga kule motoni ni kielelezo tosha hata basic needs zake hawezi tosheleza.

Acheni propagada hapa eti anatumia pesa vibaya wanazitowa wapi hizo fedha za kutumia vibaya kama NESI analipwa elfu 70 kwa mwezi kwa mwaka anakuwa na laki 8 na unamtaka mtu huyu alipe laki 5 kwa mwaka atazitowa wapi na mda wote yupo kazini?

Tena huyu Nesi kwa Tz eti ndiye anaishi maisha yale STD,Acheni matusi kabisa Tanzania ni masikini acheni matusi kabisa.
Kama serikali yenyewe imefanya ile ada ya shule za msingi bure eti kwa kigezo kuna watoto wanashindwa pata ile ada je? unategemea huyu mtoto ataipata hii ya chuo?

Anatumia fedha vibaya wapi kwa ile chupa ya gongo ya USD 0.015 na kiasi hicho cha fedha kulewesha watu 10 hiyo ndiyo matumiza mabaya?

Hivi wewe ulishawahi kuona mtu amevaa nguo ambayo imepigwa viraka hadi nguo inapoteza rangi yake kutokana na kuwa viraka ni seheemu kubwa kuliko nguo original?

Hayo matumizi mabaya ya fedha ,hizo fedha wanazipata kwa kilimo cha mkono? ama uvuvi wa kutumia kasia?
 
R.I.P. DARUSO! Ila nitawashangaa wanafunzi na UDASA kama wata succumb
 
huu ndio mchemko....they have failed to address the root of the problem!!!
 
Date::1/15/2009
Wabunge: Wanafunzi wote vyuo vikuu warejeshwe
Jackson Odoyo
Mwananchi​

WABUINGE wameitaka serikali isimamie zoezi la kuwarejesha wanafunzi wa vyuo vikuu waliofukuzwa na kuhakikisha kwamba wote wanarudishwa masomoni.

Akizungumza na waandishi wa habari jana kwa niaba ya wabunge wa Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii, mwenyekiti wa kamati hiyo, Omary Kwaang’ alisema serikali inatakiwa iwe makini katika suala hilo la kurejesha wanafunzi hao chuoni.

Mwenyekiti huyo alitoa kauli hiyo siku moja baada ya vyuo vikuu mbalimbali nchini, kutangaza utaratibu mpya wa kuwarejesha wanafunzi waliofukuzwa mapema mwaka jana kwa sababu za mgomo vyuoni.

Moja ya taratibu hizo ni suala la kujaza fomu na kujiandikisha upya huku wakitakiwa kulipa madeni yote wanayodaiwa chuoni hapo.

Sababu kubwa iliyofanya wanafunzi hao kuanzisha migomo hiyo ni kupinga sera ya uchangiaji wa elimu, wakidai kuwa inawapa upendeleo wanafunzi wanaotoka katika familia zenye uwezo na kuwabana wale wanaotoka katika familia zisizokuwa na uwezo.

"Tunaomba serikali iwe makini katika suala hili la kurudisha wanafunzi vyuo vikuu na kuhakikisha kwamba, hakuna mwanafunzi atakayeachwa katika zoezi hili la kuwarejesha," alisema Kwaang' na kuongeza:

"Hatuoni sababu ya baadhi ya wanafunzi kurejeshwa na wengine kukataliwa. Hiyo si halali hata kidogo".


Kwaang' pia alisema hakuna sababu ya nchi kuendelea kubeba mzigo wa kusomesha watoto wanaotoka familia zenye uwezo wakati kuna watoto wanaohitaji msaada wa serikali.

"Watoto wote wenye uwezo wa kuchangia wanapaswa kuchangia masomo yao, ili serikali iendelee kuwasaidia watoto wasiokuwa na uwezo," aliongeza Kwaang'.

"Ingawa sera ya kuchangia huduma ni jambo la msingi katika jamii, kitendo cha Bodi ya Mikopo kuwagawa wanafunzi katika makundi sita kinaigawa nchi katika makundi mawili na inawaongezea wazazi mzigo."

Naye Mkurugenzi wa Bodi ya Mikopo, George Nyatega alisema ili kukuza kiwango cha fedha zinazotolewa wakati wa mikopo, inapaswa fedha hizo zitozwe riba.

“"Fedha zinazokopeshwa zinapungua thamani yake kila siku, kwa sababu hazitozwi riba, sasa basi ili hali hiyo isiendelee kuwepo inabidi wanafunzi wote wanaopewa mikopo watozwe riba," alisema Nyatega na kuongeza:

"Mikopo inatolewa bila kutoza riba na urejeshwaji wake huchukua muda mrefu (hadi miaka 10) ni dhahiri kwamba thamani yake inapungua."

"Njia pekee ya kulinda thamani ya mikopo hiyo ni kutoza riba inayolingana na mfumuko wa bei".

"Pamoja na kwamba wazo la kutoza riba halikubaliki kwa wadau, bodi itaendelea kulielezea ili liweze kueleweka," alizidi kusisitiza.

Hata hivyo Kwaang' alifafanua kwamba sera ya kuchangia iko katika sekta zote, lakini tatizo ni namna ya kuitekeleza kwani utekelezaji wake inachangia kuwagawa wanafunzi na kwamba, hali hiyo ikiachwa iendelee itawagawa watoto wa Kitanzania kwa maana kwamba kutakuwa na tabaka la watu wenye elimu na wasiokuwa na elimu ndani ya nchi moja.

"Haya makundi ya wanafunzi wanaopewa mikopo yanaongeza mzigo kwa wazazi na pili yanaleta tabaka la elimu ndani ya nchi kiasi ambacho kinatufanya tujiulize maswali mengi," alisema.

"Sera ya uchangiaji haiepukiki, lakini tatizo linalokuja hapa ni utaratibu wa kuwagawa wanafunzi hawa katika makundi sita ya uchangiaji, sasa swali la kujiuliza katika hili ni je, utaratibu huo hauwaachi wanafunzi wanaostahili ? alihoji mwenyekiti huyo.

Katika hatua nyingine, Kwaang' alisema utaratibu huo haustahili hata kidogo kwa sababu inawaongezea wazazi mizigo ambayo haistahili na kwamba inawafanya washindwe kuwasomesha watoto.

Mfumo unaotumiwa kuchambua uwezo wa kiuchumi wa wazazi wa wanafunzi hao (means testing) huwagawa wanafunzi katika makundi sita. Kundi la kwanza "A", mwanafunzi hupata mkopo kwa asilimia mia, wakati katika kundi "B", mwanafunzi hupata mkopo kwa asilimia 80 na katika kundi la tatu, mwanafunzi hupata mkopo kwa asilimia 60.

Katika kundi la tatu, mwanafunzi hupata mkopo kwa asilia 40 na kundi la mwisho linahusu wanafunzi ambao hawapati mkopo kabisa.

"Tunazingatia uwezo wao kiuchumi wa mwombaji ikiwa pamoja na historia ya elimu ya mwombaji, kiwango cha elimu ya wazazi ama walezi wake, shughuli za kiuchumi za mwombaji na wazazi au walezi," alisema Nyatega.


Hili angalau linatia moyo. Lakini tunataka wakaliseme na kulitolea maelekezo bungeni - lisiishie kwenye magazeti tu! Nitashangaa kama bunge litakaa kimya ikiwa watoto wa masikini zaidi ya 2000 wanaelekea watakosa elimu ya juu kwa sababu ya kushindwa kuchangia.
 
Hii inaweza ikapeleka msukumo utakaowazibua masikio hao beaurocrats. Wamekuwa kama viziwi..hawasikilizi kilio cha hawa watoto.
Wasiishie hapo, waakikishe hili swala linamalizwa kabisa kwa kuupeleka huu mzozo bungeni.
 
Back
Top Bottom