Hii yote inatokana na kung'ang'ania hii sera iliyopitwa na wakati ya watoto wetu kusoma "BURE" au kwa "MIKOPO" kutoka serikalini. Serikali itaendelea kutudhalilisha inavyotaka. Siku zote anayemlipa mwanamziki ndiye anayechagua wimbo! Natoa wito kwa WAZAZI wenzangu tujiandae kikamilifu kuwasomesha wanetu hata kama ni kwa kuchangishana wenyewe. Mbona HARUSI, MAKANISANI, ... tunachangishana kwa mamilioni? Sadaka ya Ibada moja tu pale St. Joseph siku ya Jumapili ni shs ngapi? Fedha hizi zinawasaidia wangapi?