Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,988
Kuna habari ambazo nilikuwa nazifuatilia kwa siku kadhaa sasa na zilitokana kwanza na suala la Prof. Baregu na sasa limewagusa baadhi ya watu pale Mlimani. Uchunguzi wangu umedokeza kuwa wale wasomi ambao wamekuwa vocal kwenye vyombo vya habari kama kina Kitila wanaanza kurukwa kupewa nafasi za juu za kuweza kuinfluence policies za chuo. Nimetaarifiwa kuwa kulikuwa na promotions ambazo zimefanyika pale mlimani ambazo huwa zinatokea kwa kupigiana kura -sijui kura zinapigwaje - baadhi ya watu ambao walishinda kura kwenye idara zao na wakawa lined up for promotion wamerukwa.
Sasa, sijui kama UDSM inataka maprofesa wanaoimba sifa za serikali na CCM tu au kama chuo kikuu kinahitaji kupromote wide views za kisiasa, kijamii na kiuchumi bila kufanya maamuzi ya kisiasa. Sasa najiuliza kama ni kweli watu kama kina Kitila ambao ni wasomi na wamekubali kutumikia nchi katika academia wanaweza kurukwa kwa sababu tu ni "opposition figures" kuna tatizo gani kutangaza vyuo vikuu kama DSM kuwa ni vyuo vya CCM?
Lakini ninachojiuliza sana ni kuwa ni lini UDSM kama chuo maarufu zaidi nchini kilianza kuogopa mawazo tofauti wakati kwa wanaokumbuka kiliwahi kupata sifa miaka ya sabini kuwa ni kitovu cha academic thinking katika africa? What happened? Je kukataza siasa kabisa kwenye vyuo vikuu tunasaidia wasomi wetu kukua na kuappreciate controversial ideas and alternative theoretical propositions?
Sasa, sijui kama UDSM inataka maprofesa wanaoimba sifa za serikali na CCM tu au kama chuo kikuu kinahitaji kupromote wide views za kisiasa, kijamii na kiuchumi bila kufanya maamuzi ya kisiasa. Sasa najiuliza kama ni kweli watu kama kina Kitila ambao ni wasomi na wamekubali kutumikia nchi katika academia wanaweza kurukwa kwa sababu tu ni "opposition figures" kuna tatizo gani kutangaza vyuo vikuu kama DSM kuwa ni vyuo vya CCM?
Lakini ninachojiuliza sana ni kuwa ni lini UDSM kama chuo maarufu zaidi nchini kilianza kuogopa mawazo tofauti wakati kwa wanaokumbuka kiliwahi kupata sifa miaka ya sabini kuwa ni kitovu cha academic thinking katika africa? What happened? Je kukataza siasa kabisa kwenye vyuo vikuu tunasaidia wasomi wetu kukua na kuappreciate controversial ideas and alternative theoretical propositions?