Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,463
- 113,532
Wanabodi,
Chuo cha Usafirishaji nchini, NIT, kimepewa changamoto ya kuukabili upungufu mkubwa wa watalaamu waliobobea kwenye taaluma ya uchukuzi na usafirishaji ili pato la sekta hiyo lichangie katika kukuza pato la taifa na mchango huo uchangie kuinua uchumi wa nchi yetui.
Changamoto hiyo, imetolewa leo na Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Eng.Omari Nundu (Mb.) wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa mitaala sita mipya ya Stashahada za Uzamili (Postgraduates Diploma), zitakazoanza kufundishwa na chuo hicho mwezi Aprili mwaka huu 2012, uliokwenda sambamba na uzinduzi wa ujenzi wa jengo jipya la chuo hicho lililopo Mabibo Dar es Salaam.
Waziri Nundu. Amesema, Tanzania imezungukwa na mataifa mengi yalifungiwa (land locked ) hivyo sekta ya usafiri na ushafirioshaji ni sekta muhimu sana kwa uchumi wa taifa, ila mpaka sasa mchango wa sekta ya uchukuzi na usafirishaji katika pato la taifa ni mdogo ukilinganisha mahitaji halisi, na kutolea mfano mwaka 2009 sekta hii ilichangia asilimia 7.1 tu ya pato la taifa kutoka asilimia 6.1 mwaka 2005.
Nae mwenyekiti wa baraza la udhamini la chuo hicho, Bibi, Prisicilla Chilipweli amesema chuo chake kimeshaanza kuzifanyia kazi changamoto hizo kwa kubuni kozi mpya zinazohitajika katika soko la ajira hivyo kuwataka Watanzania wachangamkie fursa hizo huku akizitaka taasisi mbalimbali kuwafadhili watumishi wao au kuwadhamini Watanzania kusomea fani hizo ambazo sasa zinatolewa nchini kwa gharama nafuu.
Naye Mkuu wa Chuo Hicho cha Usafirishaji, (NIT), Eng.Dr.Zacharia M.D. Mganilwa Alizitaja kozi mpya kuwa ni
1. Postgraduate Diploma in Air Transport Management
2. Postgraduate Diploma in Shipping and Port Management
3. Postgraduate Diploma in Logistics and Transport Management
4. Postgraduate Diploma in Travel and Tourism Management
5. Postgraduate Diploma in Procurement and Logistics Management na;
6. MBA - Logistics and Transport Management
Chuo cha Taifa cha Usafirishaji kilianzishwa mwaka 1975, chini ya lililokuwa shirika la uchukuzi la Taifa (NTC), kwa madhumuni ya kutoa huduma za kitaalamu kwa makampuni tanzu yaliyokuwa chini ya shirika hilo. Baadaye kupitia sheria ya bunge Na. 24 ya mwaka 1982 serikali ilikipandisha hadhi na kuwa taasisi ya elimu ya juu na kukipa majukumu ya kufundisha, kufanya utafiti na kutoa ushauri wa kitalaamu katika sekta ya usafirishaji na uchukuzi. Kwa sasa Chuo kipo chini ya Wizara ya Uchukuzi. Chuo kina usajili na ithibati ya Baraza la Taifa la Ufundi (NACTE).
MY Take.
Kwa vile hizi ni kozi adimu haswa kwa wanaopenda kupata ajira mashirika ya kimataifa, nawashauri wenzetu haswa wanaomaliza form six msikimbilie vyuo vikuu kichwa kichwa huku huna uhakika wa ajira kwa unachokwenda kusomea, fikiria kujiunga na chuo kama NIT, ukimaliza hapo ni ajira nje nje na starting salary zake, take home sio chini ya Dola 2,000 kwa mwezi!.
Pasco.
Chuo cha Usafirishaji nchini, NIT, kimepewa changamoto ya kuukabili upungufu mkubwa wa watalaamu waliobobea kwenye taaluma ya uchukuzi na usafirishaji ili pato la sekta hiyo lichangie katika kukuza pato la taifa na mchango huo uchangie kuinua uchumi wa nchi yetui.
Changamoto hiyo, imetolewa leo na Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Eng.Omari Nundu (Mb.) wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa mitaala sita mipya ya Stashahada za Uzamili (Postgraduates Diploma), zitakazoanza kufundishwa na chuo hicho mwezi Aprili mwaka huu 2012, uliokwenda sambamba na uzinduzi wa ujenzi wa jengo jipya la chuo hicho lililopo Mabibo Dar es Salaam.
Waziri Nundu. Amesema, Tanzania imezungukwa na mataifa mengi yalifungiwa (land locked ) hivyo sekta ya usafiri na ushafirioshaji ni sekta muhimu sana kwa uchumi wa taifa, ila mpaka sasa mchango wa sekta ya uchukuzi na usafirishaji katika pato la taifa ni mdogo ukilinganisha mahitaji halisi, na kutolea mfano mwaka 2009 sekta hii ilichangia asilimia 7.1 tu ya pato la taifa kutoka asilimia 6.1 mwaka 2005.
Nae mwenyekiti wa baraza la udhamini la chuo hicho, Bibi, Prisicilla Chilipweli amesema chuo chake kimeshaanza kuzifanyia kazi changamoto hizo kwa kubuni kozi mpya zinazohitajika katika soko la ajira hivyo kuwataka Watanzania wachangamkie fursa hizo huku akizitaka taasisi mbalimbali kuwafadhili watumishi wao au kuwadhamini Watanzania kusomea fani hizo ambazo sasa zinatolewa nchini kwa gharama nafuu.
Naye Mkuu wa Chuo Hicho cha Usafirishaji, (NIT), Eng.Dr.Zacharia M.D. Mganilwa Alizitaja kozi mpya kuwa ni
1. Postgraduate Diploma in Air Transport Management
2. Postgraduate Diploma in Shipping and Port Management
3. Postgraduate Diploma in Logistics and Transport Management
4. Postgraduate Diploma in Travel and Tourism Management
5. Postgraduate Diploma in Procurement and Logistics Management na;
6. MBA - Logistics and Transport Management
Chuo cha Taifa cha Usafirishaji kilianzishwa mwaka 1975, chini ya lililokuwa shirika la uchukuzi la Taifa (NTC), kwa madhumuni ya kutoa huduma za kitaalamu kwa makampuni tanzu yaliyokuwa chini ya shirika hilo. Baadaye kupitia sheria ya bunge Na. 24 ya mwaka 1982 serikali ilikipandisha hadhi na kuwa taasisi ya elimu ya juu na kukipa majukumu ya kufundisha, kufanya utafiti na kutoa ushauri wa kitalaamu katika sekta ya usafirishaji na uchukuzi. Kwa sasa Chuo kipo chini ya Wizara ya Uchukuzi. Chuo kina usajili na ithibati ya Baraza la Taifa la Ufundi (NACTE).
MY Take.
Kwa vile hizi ni kozi adimu haswa kwa wanaopenda kupata ajira mashirika ya kimataifa, nawashauri wenzetu haswa wanaomaliza form six msikimbilie vyuo vikuu kichwa kichwa huku huna uhakika wa ajira kwa unachokwenda kusomea, fikiria kujiunga na chuo kama NIT, ukimaliza hapo ni ajira nje nje na starting salary zake, take home sio chini ya Dola 2,000 kwa mwezi!.
Pasco.