Chunga Lugha yako Isilete Tafrani na Kizaazaa Ndani

DSN

JF-Expert Member
Feb 2, 2011
2,837
1,674
Kijana mmoja mmoja wa kikurya alio Mwanamke wa kabila la kisukuma akamfundisha kuzungumza kikurya hivyo mwanamke yule akawa ameifahamu vizuri luugha ya mumewe na wanawe akawa anaizungumza kwa ufasaha.Basi kunasiku mume akawa ametoka kwa matembezi kisha baada ya muda akarudi nyumbani alivyofika mlangoni mwa nyumba yake apasa sauti kubwa akimuita mke [Kitabia na jadi ya wakurya wanaume wanakuwa na sauti ya juu sana kiasi kuwa uanweza kufikilia anataka kupigna kumbe wala hasa anapokuwa katika utawala wa nyumba yake [confortable zone] au ufalme wake yaani mkewe na wanawe.

Basi akapaza sauti akimsemesha mkewe kwa sauti ya juu akisema "IYAAAA!!!!! OMAKALI NI IYAKE OBHOKIMA BHOHEYEEE!!!!!!!!!!!"

Kumbe muda aliotoka mama mkwe wake aliingia akitokea usukumani kuja kumsalimia binti yake na wajukuu zake.Kwa sauti hile ya juu ya mkwewe na maneno aliyoyasikia mama mkwe kutoka kwa mume wa binti yake mama mkwe aliondoka bila kuaga.

Tafsiri ya Maneno yale ya kikurya ni hii:"Mwanamke wewe ni vipi ugali umeivaa!!!!!!!!!!!"

Kumbe kwa mujibu wa masikio ya mama mkwe kwa lugha ya kabila ya Mama mkwe yani kisukuma alisikia neno ambalo kamwe mpaka kifo chake hapa duniani asingependa wala kutalajia kulisikia likitamkwa na mume wa binti yake yaani mkwe wake.Maneno aliyoyasema mkwe kwa lugha ya kikurya ni Ugali lakini kwa Msukuma ni tusi likimaanisha maungo ya kike.

Chunga Lugha yako isilete tafrani.

Nawasilisha
 
Back
Top Bottom