ingekua ni chadema wamemmwagia ungekuta wameshakamatwa, fungua akili baba huo ni mchezo wao wenyewe, unakumbuka huko huko igunga walichoma nyumba halafu wakaacha barua eti " ni sisi chadema" kweli inakuingia akilini kuwa kweli ni chadema au ni siasa za maji taka za kubabikiziana kesi?, vipi ile kesi ya dc igunga kuvuliwa ushungi na matamko kibbao misikitini,yameishia wapi? Ccm na washirika wao waache kufanya mambo ya kinyama kwa uchu wa madaraka na waache kuchezea hela zetu kufidia maovu yao.
Acha kujidanganya ndugu! kwani mwakyembe nae kapewa sumu na upinzani? Tabia ya kudhuru na kuu ni ya watu wanoshindwa na ambao ni ccm, umesahau skendo ya meya wa mwanza aliyemuua mwanaccm mwenzake, umesahau wakina Imran kombe na kolimba nao unadhani waliuwawa na upinzani? Umemsahau kamanda wa CHADEMA alivyouwawa na CCM kule igunga? Huyo kamwagiwa na ccm wenzake ambao wamedhulumiwa. CCM ndiko mahali watu wanauwana maana hakuna mwenye dhamira ya kujitolea huko. Usiombe CHADEMA waanze mchezo huo maana kwa jinsi wanavyojua kujipanga ccm haitachukua round.Lakini wanasema ni wafuasi wa chadema ndio wanahusika na siasa hizi za kishenzi....kama kweli cdm ndugu zangu tubadilike hii sio siasa hivi ni vita!Katika hali ya kawaida ccm wasingeweza kumuumiza kada hadharani,wanao umafia lakini sio huu wa hadharani,hii wamefanya wapinzani wa ccm tu,kama c chadema basi ni nccr ama cuf,huo ndio ukweli tuache upotoshaji kwenye mabo serious!
CCM noma, hata EL afya yake nowadays si njema sana. anaonekana yuko weak kiaina. sijui ndo washa mmwakyembe?inahuzunisha sana lakini mbona............ dhuluma mauaji ftna na kila aina ya udhalilishaji VIPO NDANI YA CCM .........hebu watwambie kilicho muua DAUDI balali KILICHOMUUA ...sokoine.............kigoma malima na kinacho muangamiza........ MWAKYEMBE NA MWANDOSYA....ccm ndio serekali ccm ndio polisi ccm ndio usalama wa taifa MBONA watuhumiwa wa mauaji ya Gnr kombe wameachiwa alie waachia nani !!.........CCM ACHENI PROPOGANDA.........acheni kuuana.......hii sio siasa!!
CHADEMA wangehusika wangekuwa wamekwishakamatwa zamani sana!! Lakini watu wengi wanajua kisa na mkasa wa kijana kutokwa magamba usoni ni CCM kudhulumiana posho. Hilo ni funzo na kielelezo tosha kwa CCM kwamba ni vema ijivue magamba kikwelikweli!! Kijana ni mfano hai kwa CCM kujivua magamba, fuateni nyayo!CDM ilistahili kufutwa kwa kitendo hiki.
Amkeni watanzania.
OTIS
Hata mafuriko ya Dar es Salaam yalisababishwa na viongozi wa CHADEMA!Pole sana!!
hao hao chadema wamemlisha sumu Mwakyembe; hao hao chadema walimshughulikia kolimba; hao hao chadema walichoma nyumba wakaacha waraka; hao hao chadema walimtishia magufuli kumuuwa; hao hao chadema; ................................................... nawe ongeza mabaya yaliyowahi kutokea dhidi ya watanzania ili tuwabebeshe hawa chadema! maana angalau sasa tumepata sehemu ya kupeleka lawama zetu!!
HAKIKA NINASEMA MIAKA MICHACHE IJAYO HATA MVUA ZITAKAPOGOMA KUNYESHA AU KUNYESHA KUPITA KIASI, BASI USISHANGAE KUSIKIA INALAUMIWA CHADEMA KWA KULETA HAYO MAAFA!!!
Duu! Kafumu anaiangaliaje picha hii?Sunday, January 15, 2012
MWANA-CCM ALIYEMWAGIWA TINDIKALI IGUNGA AREJEA NCHINI BAADA YA MATIBABU INDIA
MKAZI wa Igunga, Kada wa CCM, Mussa Tesha aliyekuwa katika matibabu nchini India baada ya kumwagiwa tindikali usoni na watu wanaodaiwa kuwa wa CHADAEMA, wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo jimboni humo mwaka jana, akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam, baada ya kurejea nchini.
Kulia ni Katibu wa NEC, Uchumi na Fedha Mwigulu Nchemba ambaye alikuwa Meneja wa Kampeni za CCM jimboni humo.
Na Mwandishi Wetu
KADA wa CCM, mkazi wa Igunga, Tabora, Mussa Tesha (24)aliyekuwa akipatiwa matibabu India, baada ya kuwagia tindikali na watu wanaodaiwa kuwa wafuasi wa Chadema wakati wa kampeni za uchagfuzi mdogo jimboni humo mwaka jana, amerejea nchini.
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa CCM, Uchumi na Fedha Mwigulu Nchemba alisema leo kwamba, Tesha amerejea juzi, akiwa amepona kiasi cha kuweza kuzungumza na kuona jicho moja huku lingine likiwa bado halioni vizuri kutokana na athari alizopata.
Akizungumza nyumbani kwake Tegeta Mwisho, Dar es Salaam, Mwigulu ambaye alikuwa Meneja wa Kampeni za CCM Igunga, alisema amemhifadhi Tesha nyumbani kwake wakati akisubiri kwenda tena India kuendelea kuendelea na matibabu madogo yaliyosalia.
Mwigulu alisema, Chama Cha Mapinduzi ambacho kiligharamia matibabu yote, hadi sasa kinaendelea kumhudumia Tesha mpaka atakapopona kabisa na kuwa na uwezo wa kufanya kazi.
"Hadi sasa tunashukuru kwamba amepona anaweza kuzungumza, kusikia na kuona walau jicho moja, tofauti na mwanzo alivyokuwa mara alipomwagiwa tindikali, hata hivyo hali yake haijaweza kuwa ya kufanya kazi mbalimbali kama za juani, hivyo CCM tunaendelea kumsaidia mpaka ajenge uwezo wa kujitegemea", alisema.
Alisema, CCM imefanya mpango wa kuwaugnanisha wabunge wa CCM kumtayarishia mtaji ambao utamsaidia Tesha kuendesha maisha yake baada ya kukumbwa na madhara hayo.
Akizungumza kwa mara ya kwanza tangu amwagiwe tindikali, Tesha amewashukuru Watanzania kwa kumuombea wakati wote alipokuwa mgonjwa na kwamba anaamini dua zao ndizo zimemwezesha kubakia hai hadi sasa.
Tesha alisema, baada ya kumwagiwa tindikali Septemba 9, mwaka jana, hakujitambua hadi alipokuwa katika hospitali ya KCMC ambako alipatiwa matibabu na baadaye kupelekwa Hospitali ya Taifa Muhimbili ambako alikaa wiki tatu kabla ya kupelekwa India.
Akiwa India kwenye Hospitali ya Apollo, Tesha alikuwa chini ya uangalizi wa baba yake mdogo, Samwel Bethwel ambaye pia gharama za kuwa huko zimebebwa na CCM. Anatarajia kwenda tena India baada ya miezi mitatu.
Pole sana!!
hao hao chadema wamemlisha sumu Mwakyembe; hao hao chadema walimshughulikia kolimba; hao hao chadema walichoma nyumba wakaacha waraka; hao hao chadema walimtishia magufuli kumuuwa; hao hao chadema; ................................................... nawe ongeza mabaya yaliyowahi kutokea dhidi ya watanzania ili tuwabebeshe hawa chadema! maana angalau sasa tumepata sehemu ya kupeleka lawama zetu!!
HAKIKA NINASEMA MIAKA MICHACHE IJAYO HATA MVUA ZITAKAPOGOMA KUNYESHA AU KUNYESHA KUPITA KIASI, BASI USISHANGAE KUSIKIA INALAUMIWA CHADEMA KWA KULETA HAYO MAAFA!!!
inahuzunisha sana lakini mbona............ dhuluma mauaji ftna na kila aina ya udhalilishaji VIPO NDANI YA CCM .........hebu watwambie kilicho muua DAUDI balali KILICHOMUUA ...sokoine.............kigoma malima na kinacho muangamiza........ MWAKYEMBE NA MWANDOSYA....ccm ndio serekali ccm ndio polisi ccm ndio usalama wa taifa MBONA watuhumiwa wa mauaji ya Gnr kombe wameachiwa alie waachia nani !!.........CCM ACHENI PROPOGANDA.........acheni kuuana.......hii sio siasa!!
Hujafa Hujaumbika...pole sana kaka...tuishie tu hapo, dah!!
Acha kujidanganya ndugu! kwani mwakyembe nae kapewa sumu na upinzani? Tabia ya kudhuru na kuu ni ya watu wanoshindwa na ambao ni ccm, umesahau skendo ya meya wa mwanza aliyemuua mwanaccm mwenzake, umesahau wakina Imran kombe na kolimba nao unadhani waliuwawa na upinzani? Umemsahau kamanda wa CHADEMA alivyouwawa na CCM kule igunga? Huyo kamwagiwa na ccm wenzake ambao wamedhulumiwa. CCM ndiko mahali watu wanauwana maana hakuna mwenye dhamira ya kujitolea huko. Usiombe CHADEMA waanze mchezo huo maana kwa jinsi wanavyojua kujipanga ccm haitachukua round.