Jamani hiki kisa kimenifanya niwaze sana! Kuna bishost mmoja (tupo nae ofisi moja) yamemkuta makubwa! Bidada alikua na boyfriend hapa ofisini. Mambo yalionekana kuwa sawa baina yao mpaka majuzi mkaka alipopigiwa simu na mtu aliedai kuwa ni boyfriend wa mdada na amepata number yake ya simu toka kwenye simu ya mdada. Kwa hiyo nadhani kwenye mazungumzo wakakubaliana wakutane (Yaani hawa wanaume wawili).Basi walipokutana, of course huyu boyfriend wa hapa ofisini akawa haamini kama kweli binti alikua na mtu mwingine. Basi wakakubaliana wamtafute huyu bint ili wajue msimamo wake. Binti akakimbilia kwao, kina kaka hao wakaenda mpaka home kwa kina binti. Binti akagoma kabisa kutoka nje akidai anaumwa pressure! Sasa katika kukaa kaa pale yule jamaa ambaye alimpigia simu mwenzie akaanza kufunguka kwamba huyu bidada anawachanganya, na pia ana jamaa mwingine ambaye wamezaa nae na kamnunulia gari na kiwanja (kweli mdada ameanza ku drive sio siku nyingi)! Mara ghafla wakati wale kina kaka wanaendelea kumsubiri binti, akatoakea mshkaji mwingine ambaye ni wa ofisini pia na akadai kwamba yeye ni boy frend wa mdada muda mrefu! Basi kwa hasira hawa kina kaka watatu wakaamua kwenda zao baa ya karibu wakanywa pombe weee na kuendelea kushare story za binti! binti bila aibu akawa anawatumia msg kila mmoja kwa wakati wake! Chonde chonde kina dada na kina kaka, hii lifestyle ya kuchanganya wapenzi sio kabisa! mwisho wa siku ni kuumbuka tu sio ujanja wala nini!