Elections 2010 Chonde Chadema nendeni Mpanda mkamlete bungeni MM/Mkiti

Quinine

JF-Expert Member
Jul 26, 2010
21,271
47,269
TUME ya Taifa ya Uchagzu (Nec) imetangaza kuwa uchaguzi wa wabunge katika majimbo saba ambayo haukufanyika Oktoba 31 mwaka huu, utafanyika Jumapili ijayo.
Kwa mujibui wa taarifa iliyolewa na Nec kwa vyombo vyahabari jana, uchaguzi huo unafanyika katika majimbo ambayo hayakufanyakia kwa sababu mbalimbali ukiwemo upungufu wa vifaa vya kupigia kura.

Mkurugenzi wa Nec, Rajabu Kiravu aliyataja majimbo yatakayofanya uchaguzi huo kuwa ni Mpanda Mjini, Mpanda vijijini, Nkenge ya Tanzania bara na Mwanakwerekwe, Mtoni, Magogoni na Wete kutoka Zanzibar.

"Watakaohusika katika kupiga kura ni wakazi wa majimbo hayo waliojiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapigakura," alieleza Kiravu.
Kiravu alifahamisha kuwa upigaji kura katika majimbo hayo utafanyika katika vituo vya kupigia kura vilivyokuwa vimepangwa kutumika wakati wa uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 30, mwaka huu.

Hata hivyo, Kiravu alifafanua kuwa watu ambao namba za kadi zao za kupigia kura zitatofautiana na namba zilizomo kwenye Daftari la Kudumu la Wapigakura, hawataruhusiwa kushiriki katika uchaguzi huo.

"Vituo vitafunguliwa saa moja asubuhi na kufungwa saa 11:00 jioni kama ilivyofanyika kwenye uchaguzi uliopita," imeeleza taaarifa hiyo na kuongeza kuwa
hakutakuwa na kampeni kabla ya uchaguzi huo kwa kuwa kipindi cha kampeni za uchaguzi mkuu kilishamalizika.
 
Slaa, Sugu, Msigwa,Mdee, Mnyika wakapige kambi Mpanda waje wote (Mpanda Mjini na Vijijini), Mwenyekiti, Zito, Wabunge wote wa kanda ya ziwa wakalilete jimbo la Nkenge. Uchaguzi wa Spika ni lini?
 
TUME ya Taifa ya Uchagzu (Nec) imetangaza kuwa uchaguzi wa wabunge katika majimbo saba ambayo haukufanyika Oktoba 31 mwaka huu, utafanyika Jumapili ijayo.
Kwa mujibui wa taarifa iliyolewa na Nec kwa vyombo vyahabari jana, uchaguzi huo unafanyika katika majimbo ambayo hayakufanyakia kwa sababu mbalimbali ukiwemo upungufu wa vifaa vya kupigia kura.

Mkurugenzi wa Nec, Rajabu Kiravu aliyataja majimbo yatakayofanya uchaguzi huo kuwa ni Mpanda Mjini, Mpanda vijijini, Nkenge ya Tanzania bara na Mwanakwerekwe, Mtoni, Magogoni na Wete kutoka Zanzibar.

"Watakaohusika katika kupiga kura ni wakazi wa majimbo hayo waliojiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapigakura," alieleza Kiravu.
Kiravu alifahamisha kuwa upigaji kura katika majimbo hayo utafanyika katika vituo vya kupigia kura vilivyokuwa vimepangwa kutumika wakati wa uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 30, mwaka huu.

Hata hivyo, Kiravu alifafanua kuwa watu ambao namba za kadi zao za kupigia kura zitatofautiana na namba zilizomo kwenye Daftari la Kudumu la Wapigakura, hawataruhusiwa kushiriki katika uchaguzi huo.

"Vituo vitafunguliwa saa moja asubuhi na kufungwa saa 11:00 jioni kama ilivyofanyika kwenye uchaguzi uliopita," imeeleza taaarifa hiyo na kuongeza kuwa
hakutakuwa na kampeni kabla ya uchaguzi huo kwa kuwa kipindi cha kampeni za uchaguzi mkuu kilishamalizika.

Na kama hizo namba ziantofautiana, ni wajibu wa mwananchi mwenye kadi au NEC? Hapa kuna harufu ya mwendelezo wa uchakachuaji kwa njia ya kuwazuia TENA baadhi ya watu wasipige kura.
 
Tunayahitaji sana Majimbo haya at least kuwa more strong bungeni. Hata kwenda tu bila kufanya kampeni yoyote pale mpanda mjini SLAA ANAWEZAKUSHAWISHI WAPIGA KURA KUMPIGIA MGOMBEA WA CHADEMA KURA
 
Nashauri baada ya kikao cha kamati kuu basi Slaa eelekee huko mpanda, wakati hawa wengine wakilazimika kusubiri bungeni ili kuapishwa, yeye akapambane huko. hivi viti vikipatikana vitaongeza na idadi ya wabunge wa viti maalum. na angepatikana kamanda mwingine kama Shibuda au Zitto akapige tafu Nkenge na ukichukulia mpango wa hawa CCM kutaka kubariki ufisadi kwa kuweka spika mdhaifu utaipa CHADEMA more credit...
 
Slaa, Sugu, Msigwa,Mdee, Mnyika wakapige kambi Mpanda waje wote (Mpanda Mjini na Vijijini), Mwenyekiti, Zito, Wabunge wote wa kanda ya ziwa wakalilete jimbo la Nkenge. Uchaguzi wa Spika ni lini?

Muda wa kampeni si umeshaisha? au kampeni zinaruhusiwa kuendelea btn NOW and Sunday?
 
Back
Top Bottom