Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Endapo hakutakuwa na mgombea wa Urais ambaye amepata kura zaidi ya asilimia hamsini basi wagombea wawili waliopata kura nyingi zaidi wataenda kwenye mzunguko wa pili ndani ya siku arobaini baada ya uchaguzi. Kwa minajili hiyo tunaweza kuona kuwa yawezekana Prof. Lipumba ndiye anashikilia ufunguo wa ushindi wa aidha Kikwete au Dr. Slaa. Je, tuko tayari kwa mzunguko wa pili ukitokea kama ilivyotokea Brazili jana Jumapili baada ya mgombea wao wa Urais kuongoza saana kwenye kura za maoni lakini siku ya kura ameshindwa kupata asilimia zaidi ya 50?
Mwanzoni nilifikiria kuwa sheria yetu inaruhusu mshindi kushinda kwa kura za wingi tu hata kama ni chini ya asilimia 50 kumbe mabadiliko ya sheria ya Uchaguzi ya 1985 mwaka 1995 yameweka utaratibu wa raundi ya pili ya kura za rais.
Mwanzoni nilifikiria kuwa sheria yetu inaruhusu mshindi kushinda kwa kura za wingi tu hata kama ni chini ya asilimia 50 kumbe mabadiliko ya sheria ya Uchaguzi ya 1985 mwaka 1995 yameweka utaratibu wa raundi ya pili ya kura za rais.