Bazobonankira
Senior Member
- Jan 18, 2007
- 120
- 61
Wadau wa Forum,
Heshima kwenu nyote!! Sina uhakika kuwa kwa kuwasilisha swali langu hapa nitaweza kupata ufafanuzi ama nitakwaza maslahi ya baadhi ya watu fulani fulani. Pamoja na wasisasi nilio nao, dhamira yangu inanituma kuweka swali hili mahala hapa na kutarajia michango yakinifu.
Katika pita pita zangu hapa na pale, nimepata kukutana na mtu aliyejitambulisha kuwa anaitwa John Chikomo. Sikupata kumjua kabla, mpaka hapo nilipokutana naye.
Kisha akaendelea kujitambulisha ya kwamba anaongoza taasisi/chama kinachojihusisha na mazingira hapa nchini.
Baada ya utambulisho huo nilibaki na maswali kadhaa, ambayo nilipojaribu kumdadisi hakupenda kuzungumzia katu! Kati ya maswali ya msingi niliyojiuliza ni kuwa:
Je, Chikomo ni jina kutoka maeneo gani hasa hapa Tanzania? Kwa maana Chikomo kadhaa niliopata kuwasikia wote wanatoka kati ya Zimbabwe na Malawi.
Kama ni kweli ninavyohisi (inategemea na wadau watasema nini kuhusu majina haya), ni kwa vipi raia wa kigeni kuongoza harakati za taasisi ya mazingira yenye kutetea maslahi yetu?
Naomba kuwasilisha hoja!
Heshima kwenu nyote!! Sina uhakika kuwa kwa kuwasilisha swali langu hapa nitaweza kupata ufafanuzi ama nitakwaza maslahi ya baadhi ya watu fulani fulani. Pamoja na wasisasi nilio nao, dhamira yangu inanituma kuweka swali hili mahala hapa na kutarajia michango yakinifu.
Katika pita pita zangu hapa na pale, nimepata kukutana na mtu aliyejitambulisha kuwa anaitwa John Chikomo. Sikupata kumjua kabla, mpaka hapo nilipokutana naye.
Kisha akaendelea kujitambulisha ya kwamba anaongoza taasisi/chama kinachojihusisha na mazingira hapa nchini.
Baada ya utambulisho huo nilibaki na maswali kadhaa, ambayo nilipojaribu kumdadisi hakupenda kuzungumzia katu! Kati ya maswali ya msingi niliyojiuliza ni kuwa:
Je, Chikomo ni jina kutoka maeneo gani hasa hapa Tanzania? Kwa maana Chikomo kadhaa niliopata kuwasikia wote wanatoka kati ya Zimbabwe na Malawi.
Kama ni kweli ninavyohisi (inategemea na wadau watasema nini kuhusu majina haya), ni kwa vipi raia wa kigeni kuongoza harakati za taasisi ya mazingira yenye kutetea maslahi yetu?
Naomba kuwasilisha hoja!