Byendangwero
JF-Expert Member
- Oct 24, 2010
- 871
- 56
Kulingana na mfumo unaotumika katika mabunge ya "commonwealth", mwenyekiti wa kamati ya matumizi ya serikali anapashwa kutoka kwenye chama kilichoshika nafasi ya pili nyuma ya kile kinachounda serikali, ambacho ni CDM. Katika hali hiyo kumteua mtu kama Cheyo, ambaye idadi ya kura zilizopigwa kwa chama chake hazifikii hata asilimia moja, ni sawa na kuinyima sauti ya umma fursa ya kusimamia serikali katika matumizi ya rasilimali ya umma.