Habarindiyohiyo
JF-Expert Member
- Aug 11, 2008
- 263
- 13
Mwenyekiti wa UDP John Cheyo ameisulubu CHADEMA kwa kusema kwamba falsafa yake ya Nguvu ya Umma haina maana yoyote kwa watanzania. Cheyo amesema CHADEMA watambue kuwa Kikwete ndiye Rais halali. Cheyo ameyasema hayo katika mkutano mkuu wa chama hicho unaondelea hivi sasa katika ukumbi wa Sabasaba.
Mkutano huo umemchagua kuwa mwenyekiti wa chama hicho akiwa ni mgombea pekee na kupokea majina ya wajumbe wa kamati kuu aliowateua kuendelea na nyadhifa zao. Wajumbe wa mkutano huo walitoka maeneo mbalimbali ya Dar es salaam, ambapo Cheyo amewashukuru kwa kufika kumsikiliza.
Cheyo ametumia mkutano huo kuwalaumu CHADEMA kwa kuingilia ngome zake za kisiasa katika mikoa ya kanda ya ziwa na kutaka chama hicho kichukuliwe hatua kwa kuvuruga amani ya nchi na kumpongeza Rais Kikwete kwa kubaini hila ya CHADEMA.
.........ndiyohiyo
Mkutano huo umemchagua kuwa mwenyekiti wa chama hicho akiwa ni mgombea pekee na kupokea majina ya wajumbe wa kamati kuu aliowateua kuendelea na nyadhifa zao. Wajumbe wa mkutano huo walitoka maeneo mbalimbali ya Dar es salaam, ambapo Cheyo amewashukuru kwa kufika kumsikiliza.
Cheyo ametumia mkutano huo kuwalaumu CHADEMA kwa kuingilia ngome zake za kisiasa katika mikoa ya kanda ya ziwa na kutaka chama hicho kichukuliwe hatua kwa kuvuruga amani ya nchi na kumpongeza Rais Kikwete kwa kubaini hila ya CHADEMA.
.........ndiyohiyo