Chenge huru!

Hebu jamani watu ambao ni wataalamu wa Sheria wanisaidie hapa. Mhe. Chenge ameonekana ana hatia na kahukumiwa kifungo cha Miaka mitatu (3) au kulipa faini ya Tshs laki saba [700,000/-] kwa TAFSIRI YANGU ANAITUMIKIA MIAKA 3 KWA KULIPA FAINI YA TSHS 700,000

Sasa hoja yangu:
kwa mujibu wa Ibara ya 67.-(2) (c) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 kama ilivyorekebishwa mwaka 2005 kinasema nanukuu:

"(2) Mtu hatakuwa na sifa za kustahili kuchaguliwa au kuteuliwa kuwa Mbunge-


(c) ikiwa mtu huyo amehukumiwa na Mahakama yoyote katika Jamhuri ya Muungano na kupewa adhabu ya kifo au ya kufungwa gerezani kwa muda unaozidi miezi sita kwa kukutwa na hatia ya kosa lolote, vyovyote linavyoitwa, linaloambatana na utovu wa uaminifu;"

mwisho wa nukuu.

Sasa Mhe. Chenge amehukumiwa kifungo cha Miaka 3 na badala yake amelipa faini, yaani Hakimu kasema unakwenda Miaka 3 jela ama ulipe faini, kwa maana hiyo iwapo angekosa kuwa na fedha Tshs, 700,000 angekwenda gerezani kutumikia adhabu ya miaka 3.

Sasa wanasheria na wataalamu wa Katiba hapa mnasemaje Chenge bado ni Mbunge halali wa Bariadi? au siyo Mbunge halali?

Hebu tusaidieni hapo.
 
Duuh.......ok lakini nathani sheria ndio imesema. Mana trafick kesi ndio zilivyo (fine/ kifungo)
 
Wakuu nimepata tetesi kutoka e-group moja kwamba Chenge amhukumiwa miaka mitatu jela au faini ya 700,000 pesa ya tanzania (which is less that $500)

Je ni kweli? na kama ni kweli hii ina maana gani kwake kama Mbunge na watu wa bariadi?

Is the hukumu fair?

Acid

Kwani si sheria hii ni ya nchi na ishatumika kwa wengine pia! Traffic cases huwa zinaisha kwa mitindo hiyo!

Hukumu kuwa FAIR ni vigumu kwasababu si lazima "sheria isimame kwa mwenye haki bali sheria siku zote usimamia upande wa sheria" Kesi ya Zombe si unaikumbuka mkuu!

Je wale madereva waofungwa miaka kibao, huwa wamekosa hizi faini za kishikaji AU?
 
Watu wanaolalamikia hukumu ya Mhe. Chenge wakafungue na wasome Sheria ya makosa ya barabarani na adhabu zake, suala siyo hakimu suala hapa ni sheria zinasemaje????

Nakumbuka kule Morogoro alikwepo Hakimu mmoja anaitwa Mkasimongwa aliwahi kumuhukumu Kijana aliyekuwa Dreva Taksi kwa kosa la kugonga na kusababisha majeraha ya mtembea kwa Miguu. Lakini katika hukumu ile Mhe. Mkasimongwa kipindi kile akiwa Hakimu Mkazi wa Morogoro hakusema Dreva yule alipe faini yeye alisema kutokana na ushahidi ameridhika kuwa Dreva akifanya kosa lile na iwe fundisho alimuhukumu kifungo cha Miaka 2.

Ndugu wa Dreva yule walikata rufaa na Mahakama ya juu ikaamuliwa kesi isikilizwe upya kwa sababu mtuhumia hakuelezwa kwamba anafungwa miaka 2 au faini au vyote viwili yaani kifungo na faini. Hapo baada ya kesi Review kijana alimuliwa kulipa Tshs 10,000 na akalipa na akwa nje.

Hii ni mifano michache tu mingi mnaijuwa wenzangu. Suala hapa ni sheria.

Tazama kesi ya Kubaka, wanasema ili ijulikane mwanamke kabakwa lazima ule uchafu udhibitishwe na Daktari, Kijijini kwetu mwendo wa kwenda Hospitali ni siku nzima Mama Kabakwa jioni hiyo Zahanati mtakwenda wapi ili Daktari athibitishe?/

Hizi ndo zile Sheria 40 miongoni mwao zinazolalamikiwa

Nawatakia kazi njema
 
Hebu jamani watu ambao ni wataalamu wa Sheria wanisaidie hapa. Mhe. Chenge ameonekana ana hatia na kahukumiwa kifungo cha Miaka mitatu (3) au kulipa faini ya Tshs laki saba [700,000/-] kwa TAFSIRI YANGU ANAITUMIKIA MIAKA 3 KWA KULIPA FAINI YA TSHS 700,000

Sasa hoja yangu:
kwa mujibu wa Ibara ya 67.-(2) (c) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 kama ilivyorekebishwa mwaka 2005 kinasema nanukuu:

"(2) Mtu hatakuwa na sifa za kustahili kuchaguliwa au kuteuliwa kuwa Mbunge-


(c) ikiwa mtu huyo amehukumiwa na Mahakama yoyote katika Jamhuri ya Muungano na kupewa adhabu ya kifo au ya kufungwa gerezani kwa muda unaozidi miezi sita kwa kukutwa na hatia ya kosa lolote, vyovyote linavyoitwa, linaloambatana na utovu wa uaminifu;"

mwisho wa nukuu.

Sasa Mhe. Chenge amehukumiwa kifungo cha Miaka 3 na badala yake amelipa faini, yaani Hakimu kasema unakwenda Miaka 3 jela ama ulipe faini, kwa maana hiyo iwapo angekosa kuwa na fedha Tshs, 700,000 angekwenda gerezani kutumikia adhabu ya miaka 3.

Sasa wanasheria na wataalamu wa Katiba hapa mnasemaje Chenge bado ni Mbunge halali wa Bariadi? au siyo Mbunge halali?

Hebu tusaidieni hapo.

Japo mimi si mwanasheria lakini nafikiri ibara hiyo uliyoiandika haimshiki mzee Chenge. Ibara hiyo inamaana pale tu mtu kama hajachaguliwa. Wakati chenge anagombea ubunge hakuwa bado kapatikana na hatia. Na hapa ndio uone mahakama ilichofanya, ni kumkwepesha Chenge na hii Ibara ya katiba. Maana Mahakama ilikuwa na uwezo wote wa kuisikiliza na kupitisha hukumu ya kesi hii kabla ya uchaguzi, na hapo Mzee visenti angepigwa chini. Lakini walidelay makusudi ili hii Ibara isimshike. 2015 kama atagombea tena ndipo utaona hii ibara inamkamata, na utaone mwenyewe kuwa 2015 chenge hatogombea hata kama wabariadi watapenda kumpitisha tena. Labda wenye ujuzi zaidi hapa watufafanulie zaidi.
 
Kwa mtanzania yeyote aliye timamu, anaeijua Tanzania wala asingeliweza kuota kwamba Mzee wa vijisenti anaweza kufungwa ama kuhukumiwa tofauti na hivyo ilivyotokea!! Sababu yake "HAIYUMKINIKI MTU ALIYESIFIWA KWAMBA AMEITENDEA VEMA TANZANIA AHUKUMIWE KIFUNGO!!! Zingatieni mkataba wa RADA n.k. Kisha taarifa ya vile vijisenti" Ingelikuwa ni dereva wa bus au daladala ndipo ungelisikia hakimu akitoa hukumu na maneno yafuatayo: "unahukumiwa kwenda jela miaka saba na faini ya milioni mbili ili iwe fundisho kwa madereva wazembe kama wewe!!" Kwa kweli sielewi namna gani Tanzania itayaepuka matabaka. Sipati picha ya Tanzania ijayo kwa sababu ikiwa wenye nacho hukumu kwao zinalainika na maskini hukumu zao zinawashinda kipimo... Na hiyo ya Mh. Vijisenti ndiyo imekwisha itabaki hadithi. Lakini basi ikumbukwe kwamba si vibaka tu watakaoendelea kuchomwa mioto na "wananchi wenye hasira kali" bali pia inachochea ukiukwaji mkubwa wa haki na watu kukata tamaa kabisa na mahakama zetu. Na iwapo Mahakama zetu tukufu zitaendelea kuhukumu kwa mashinikizo basi ijulikane wazi mbegu tunayoipanda leo itakuwa chachu ya watu kujichukulia sheria mikononi. pata picha ya miaka ishirini ijayo, wale wahanga wa ajali ile wameacha watoto wanasimuliwa ilikuwaje wazazi wao wakauliwa na kuwasababishia maisha wanayoishi wakati huo. Imagine kwamba katika umri wao wa utoto watakuwa CHOKORAA na je nini kitatokea? Ukishayafikiri hayo basi jua wazi kwamba..

HIYO NDIYO TANZANIA TUNAYOIJENGA HII LEO
 
Duuh.......ok lakini nathani sheria ndio imesema. Mana trafick kesi ndio zilivyo (fine/ kifungo)

kapatikana na hatia ya kuendesha bila bima,kuendesha carelessly,na mauaji ya watu wawili shillingi laki saba kweli.Tena mtu mwenyewe mbunge,hiyo haki?walala hoi ndo watakaojaa segerea.
 
Adhabu nyingine haza lengo la kumkomesha mshtakiwa.
Kwanini asingepewa adhabu ya kulipa bilioni saba ili aende jela?
This country bwana!!!!!

I like! Watanzania tusilalamike haya mambo yanafanyika because we let them happen!
 
These are the two major WONDERS OF THE LAW
1. It justfy its existance by honouring lies I.e you must lie or cheat to escape. Maana yake kama umeua inabidi usema sikuua na uking'ang'anizwa sema sikukusudia. Utaadhibiwa kwa kosa la kuua bila kukusudia.

2. It always goes contrary to the majority expectation. Wengi walidhani mzee wa vijisenti ataenda jela kwa kuua lakini la! Na wengi walidhani Liyumba atapigwa faini lakini kaishia jela.

Hiyo ndiyo katiba yetu ukiua faini, ukibaka kifungo cha maisha na kutumia madaraka vibaya na kuisababishia serikali hasara unafungwa jela.
 
These are the two major WONDERS OF THE LAW
1. It justfy its existance by honouring lies I.e you must lie or cheat to escape. Maana yake kama umeua inabidi usema sikuua na uking'ang'anizwa sema sikukusudia. Utaadhibiwa kwa kosa la kuua bila kukusudia.

2. It always goes contrary to the majority expectation. Wengi walidhani mzee wa vijisenti ataenda jela kwa kuua lakini la! Na wengi walidhani Liyumba atapigwa faini lakini kaishia jela.

Hiyo ndiyo katiba yetu ukiua faini, ukibaka kifungo cha maisha na kutumia madaraka vibaya na kuisababishia serikali hasara unafungwa jela.
Maajabu makubwa ya nchi yetu Danganyika
 
Kwakuwa yupo madarakani wameamua kumlinda sababu kimsingi, kafanya mauaji kwa uzembe, kaendesha gari bila bima, Kaendesha gari kwa mwendo wa kasi!! Si sawa kwa hukumu aliyopewa!
Ila kwa kuwa hukumu ya kimungu ni ya haki, siku itafika!!
 
Sipati picha hakimu alipomwambia Chenge ama uende jela miaka mitatu au ulipe SODA (aka 700,000 tu!)
 
wandugu ktk tafakari zangu niliwahi kuandika kua mafisadi kamwe hawawezi kuhukumiwa kihalali na kwa haki ktk mahakama zetu ukizingatia pesa za mafisadi ndio zimewaweka madarakani waajiri wa mahakim na majaji kama mkwere. Pia chenge alikua mwanasheria mkuu wa serikali ki protocol ni boss wao mstaafu hivyo basi tusitaraji hukumu ya haki kwa watu hao labda tuamue kuwahukum sisi wenyewe otherwise wataendelea kula bata na sisi tutaendelea kulaum pembeni mpaka tunaingia kaburini. Mi nawasilisha inauma sana kwakweli.
 
Nashauri DPP akate rufaa kwasababu hakimu inaonekana ameshindwa kuweka maanani jambo moja; maadam amemuingiza Chenge hatihani kwa kuendesha gari hisiyokuwa na bima, hii ina maana bima haiwezi kutoa fidia yeyote kwa ndugu wa marehemu. Kutokana na hayo, naona mahakama ilitakiwa kumuhukumu Chenge kulipa mwenyewe fidia hiyo.
 
Bariadi wana mbunge batili!
Nakubaliana na wewe kwa mjibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ibara ya 67 kifungu cha pili (c) kama ninavyofukuu hapa “67.-(2) Mtu hatakuwa na sifa za kustahili kuchaguliwa au kuteuliwa kuwa Mbunge-
(c) Ikiwa mtu huyo amehukumiwa na Mahakama yoyote katika Jamhuri ya Muungano na kupewa adhabu ya kifo au ya kufungwa gerezani kwa muda unaozidi miezi sita kwa kukutwa na hatia ya kosa lolote, vyovyote linavyoitwa, linaloambatana na utovu wa uaminifu; au”.
 
Yap lazima angepewa faini tu ili atoke, jamaa anauzito wake ccm. Jela ni yetu wanyonge kina Nguza, na ss wengine.
 
Nakubaliana na wewe kwa mjibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ibara ya 67 kifungu cha pili (c) kama ninavyofukuu hapa "67.-(2) Mtu hatakuwa na sifa za kustahili kuchaguliwa au kuteuliwa kuwa Mbunge-
(c) Ikiwa mtu huyo amehukumiwa na Mahakama yoyote katika Jamhuri ya Muungano na kupewa adhabu ya kifo au ya kufungwa gerezani kwa muda unaozidi miezi sita kwa kukutwa na hatia ya kosa lolote, vyovyote linavyoitwa, linaloambatana na utovu wa uaminifu; au".

Mi nahisi tunatafsili vibayya hiki kifungu;-

Tafsili halisi ya hili jambo hukumu ni hatua mojawapo inayopelekea KUPEWA ADHABU.

Adhabu inayozungumzwa hapa NI YA KWENDA JELA au KIFO.

Kama hukumu immetoka na kukawa na option ya pili INAYOPELEKEA KUTOTUMIKIA ADHABU basi jamaa anakuwa HAJAFUNGWA NA KIFUNGU
HIKI.

Pili kwa kifungu hiki HATA KAMA ANGEHUKUMUWA KIFUNGO CHA NJE cha zaidi ya miezi sita INAONYESHA BADO ANGEENDELEA KUWA MBUNGE.

Mtazamo.

Jamaa anaendelea na ubunge wake kwa kuwa hajaenda GEREZANI/KIFO kutoana na hukumu iliyotolewa na mahakama ya Tanzania .

Hapa tuanagalie mambo mengine tu kuhusiana na mwenendo wa kesi na si kuhusu utumishi wake wa Bungeni.... ingawa nilipenda jamaa angepata hukumu YA KIFO.
 
Nakubaliana na wewe kwa mjibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ibara ya 67 kifungu cha pili (c) kama ninavyofukuu hapa “67.-(2) Mtu hatakuwa na sifa za kustahili kuchaguliwa au kuteuliwa kuwa Mbunge-
(c) Ikiwa mtu huyo amehukumiwa na Mahakama yoyote katika Jamhuri ya Muungano na kupewa adhabu ya kifo au ya kufungwa gerezani kwa muda unaozidi miezi sita kwa kukutwa na hatia ya kosa lolote, vyovyote linavyoitwa, linaloambatana na utovu wa uaminifu; au”.

Mi nahisi tunatafsili vibayya hiki kifungu;-

Tafsili halisi ya hili jambo hukumu ni hatua mojawapo inayopelekea KUPEWA ADHABU.

Adhabu inayozungumzwa hapa NI YA KWENDA JELA au KIFO.

Kama hukumu immetoka na kukawa na option ya pili INAYOPELEKEA KUTOTUMIKIA ADHABU basi jamaa anakuwa HAJAFUNGWA NA KIFUNGU
HIKI.

Pili kwa kifungu hiki HATA KAMA ANGEHUKUMUWA KIFUNGO CHA NJE cha zaidi ya miezi sita INAONYESHA BADO ANGEENDELEA KUWA MBUNGE.

Mtazamo.

Jamaa anaendelea na ubunge wake kwa kuwa hajaenda GEREZANI/KIFO kutoana na hukumu iliyotolewa na mahakama ya Tanzania .

Hapa tuanagalie mambo mengine tu kuhusiana na mwenendo wa kesi na si kuhusu utumishi wake wa Bungeni.... ingawa nilipenda jamaa angepata hukumu YA KIFO.
 
Hivi yule driver wa basi la Mohamed Trans ameishia wapi? Gari lake lilikuwa na BIMA, alikuwa na leseni, ajali ilisababishwa na tairi kupasuka, ila yeye kafungwa miaka 30!!! Hizi zote si ni trafic case? Mwenye taarifa zake atuhabarishe!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom