Chenge aongezewa shitaka

Mpita Njia

JF-Expert Member
Mar 3, 2008
6,997
1,163
Mods, mukiona inafaa muiunganishe na thread ile kuu.

waendesha mashitaka leo wameongeza shitaka la kuendesha gari lisilokuwa na bima katika mashitaka yanayomkabili Chenge kwenye ile kesi yake ya kuua watu wawili aliowagonga katika Bajaj.
Pia, Majid Gharib, yule mmiliki wa bajaj ambaye alikimbia, naye ameongezwa kwenye kesi hiyo
 
Mods, mukiona inafaa muiunganishe na thread ile kuu.

waendesha mashitaka leo wameongeza shitaka la kuendesha gari lisilokuwa na bima katika mashitaka yanayomkabili Chenge kwenye ile kesi yake ya kuua watu wawili aliowagonga katika Bajaj.
Pia, Majid Gharib, yule mmiliki wa bajaj ambaye alikimbia, naye ameongezwa kwenye kesi hiyo

Majid Gharib, yule mmiliki wa bajaj anakosa gani huyu?
 
Ukiangalia unaweza kubuni kuwa Chenge huenda akakwepeshwa na mauaji na kuhukumiwa kwa hili la kuendesha gari bila ya bima na yule mmiliki wa Bajaji kutolewa kafara.
 
hehehe
yule dereva anashtakiwa kwa kuokoa maisha yake kwa kuruka kutoka kwenye chombo alipoona hana njia ya kukwepa mbogo aliyecharuka.
ina maana angefariki kwenye ajali pasingekuwa na tuhuma dhidi yake. unajua ajali kama ile mtu unapagawa na inabidi kujihami sana kwani kama angepatikana nadhan mheshimiwa asingekuwa na kesi kubwa sana maana dereva wa bajaji angesulubika kirahisi mno.
 
Ukiangalia unaweza kubuni kuwa Chenge huenda akakwepeshwa na mauaji na kuhukumiwa kwa hili la kuendesha gari bila ya bima na yule mmiliki wa Bajaji kutolewa kafara.

Mwiba, Huo ndio muelekeo wa kesi, wewe sheria za bongo huzifahamu?????
 
Mimi naona kuliko kuzugana kila siku, Chenge wamwachie tuu ili aendelee na majukumu yake kama Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya Chama kitukufu na kama kuna uwezekano arudishiwe ule wadhifa wake wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali maana toka aondoke ofisi ile Michongo imepungua na visenti havipatikani kwa wingi.
Sh..xyz taip...
 
Mimi naona kuliko kuzugana kila siku, Chenge wamwachie tuu ili aendelee na majukumu yake kama Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya Chama kitukufu na kama kuna uwezekano arudishiwe ule wadhifa wake wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali maana toka aondoke ofisi ile Michongo imepungua na visenti havipatikani kwa wingi.
Sh..xyz taip...

Tehe tehe tehe....
 
Kwa asiye fuatilia mwenendo wa siasa za jamuhuri ya Danganyika atashtushwa na hili. Sisi wengine tuliisha acha lipite kama mengine mengi (mazito zaidi) yalivyopita. Sioni umuhimu wa kupoteza muda wa mahakimu kwa huyu mhe. vijicenti (wakati mwisho wa hili unajulikana), nawasihi mahakimu waendelee kusikiliza na kuhukumu kesi za walalahoi kuibiana vijisimu kariakoo na mbagala!

Huyu ndiye mwenyekiti kamati ya maadili wa CCM, vioja vitupu!!

CCM nambari one
 
Du, Bongo ni nchi nzuri sana.... hivi kesi kama hii ingemkuta mshkaji tu wa street angekuwa wapi saa hizi? Haya mambo kuna haja ya kutoyafuatilia kabisa maana saa zingine roho inauma mno inatamani ipasuke! Hapa tayari mchongo unachorwa na mzee atahukumiwa kulipa fine kwa kuendesha gari bila bima na kufungiwa leseni miezi miwili, kwisha kazi! Kwa sasa habari kuwa alikuwa amelewa hazisemwi tena, any way tunamuachia Mungu maana nae ana majibu yake, kesi ya Dito iligeuzwa ikawa bila kukusudia ili hukumu iwe kifungo cha nje lakini Mungu nadhani alichoka na ujinga huu.......
 
Ameshitakiwa kwa kushindwa kutunza kumbukumbu za dereva wake

haha, nafikiri anakimbia kujibu shitaka la kwanini aliweza kumuajiri mtu ambaye hana leseni na ndio maana dereva aliamua kutoweka baada ya tukio (mawazo yangu tuu)
 
Kwa asiye fuatilia mwenendo wa siasa za jamuhuri ya Danganyika atashtushwa na hili. Sisi wengine tuliisha acha lipite kama mengine mengi (mazito zaidi) yalivyopita. Sioni umuhimu wa kupoteza muda wa mahakimu kwa huyu mhe. vijicenti (wakati mwisho wa hili unajulikana), nawasihi mahakimu waendelee kusikiliza na kuhukumu kesi za walalahoi kuibiana vijisimu kariakoo na mbagala!

Huyu ndiye mwenyekiti kamati ya maadili wa CCM, vioja vitupu!!

CCM nambari one


Mungu atamhukumu, Ditopile yuko wapi?? RIP Ditopile
 
Chenge amrudie Mungu wake maana nina uhakika hawa mafisadi 10 yrs back hawakuwa hata na 2mil bank wamekwapua miaka hii hii...watubu,warudise pesa zote,watubu na washitakiwe mimi jamani inaniuma sana sana nashangaa hv usalama na jeshi hawapo??
 
SWALI LA MUHIMU: Kwanini awali shitaka hili halikuwepo, na wakati lilijulikana wazi. Na nini kimewafanya waliongeze sasa shitaka hilo licha ya kuwa lilipigiwa kelele na ndugu?
Hapa ndipo siri ya kesi imejificha tukibaini kilichowaogopesha kilikuwa nini tunaweza kubashiri pia kesi itaisha vipi/
 
Last edited:
Du, Bongo ni nchi nzuri sana.... hivi kesi kama hii ingemkuta mshkaji tu wa street angekuwa wapi saa hizi? Haya mambo kuna haja ya kutoyafuatilia kabisa maana saa zingine roho inauma mno inatamani ipasuke! Hapa tayari mchongo unachorwa na mzee atahukumiwa kulipa fine kwa kuendesha gari bila bima na kufungiwa leseni miezi miwili, kwisha kazi! Kwa sasa habari kuwa alikuwa amelewa hazisemwi tena, any way tunamuachia Mungu maana nae ana majibu yake, kesi ya Dito iligeuzwa ikawa bila kukusudia ili hukumu iwe kifungo cha nje lakini Mungu nadhani alichoka na ujinga huu.......

Mdogo wangu alikaa keko wiki 2,mwendesha pikipiki alimgonga ubavuni mwa gari na kuumia vibaya,kesho yake mahakamani wakadai hali ya mwenye pikipiki ni mbaya kwahiyo asipewe dhamana.
 
Mjadala huu wote wa nini?
Hamjui kwamba viongozi mliowachagua si Chenge pekee bali nina maanisha wote mliowachagua kama viongozi wenu( hapana nina maana watawala wenu) at the same time mmewapa tiketi ya kuwaueni, tena kuua yeyote kwa namna yeyote bila kesi?
Hadi pale wadanganyika tutakapokuwa tumejua kuwa tuko katika utawala mbovu sana tangu uhuru yaani utawala usiokuwa wa sheria kwa wakubwa lakini ni washeria kwa wadogo, hapo tutakapokuwa tumeamka katika usingizi huo, hapatatokea uvunjifu wa sheria wa viongozi wetu kwa dharau kubwa kama ninayoiona sasa hivi.
Lakini wasubiri tu iko siku watu wanachoka na mbaya inakuwa mbaya.
 
Mjadala huu wote wa nini?
Hamjui kwamba viongozi mliowachagua si Chenge pekee bali nina maanisha wote mliowachagua kama viongozi wenu( hapana nina maana watawala wenu) at the same time mmewapa tiketi ya kuwaueni, tena kuua yeyote kwa namna yeyote bila kesi?
Hadi pale wadanganyika tutakapokuwa tumejua kuwa tuko katika utawala mbovu sana tangu uhuru yaani utawala usiokuwa wa sheria kwa wakubwa lakini ni washeria kwa wadogo, hapo tutakapokuwa tumeamka katika usingizi huo, hapatatokea uvunjifu wa sheria wa viongozi wetu kwa dharau kubwa kama ninayoiona sasa hivi.
Lakini wasubiri tu iko siku watu wanachoka na mbaya inakuwa mbaya.

Sawa lakini wanapaswa kuelewa kuna nchi wanapaswa kuiongoza na watu wa kuwatumikia, ile ole wao siku isiyo na jina inakuja, wala haiko mbali!
 
Sawa lakini wanapaswa kuelewa kuna nchi wanapaswa kuiongoza na watu wa kuwatumikia, ile ole wao siku isiyo na jina inakuja, wala haiko mbali!
Siku akijaribu kuua ndugu yangu sikubali mambo ya kusafirisha maiti wala pesa ila nami namvaa mbaya iwe mbaya. Tena sintajali ni nani na ana wadhifa gani. Lazima nimuwinde nijilipize kisasiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii wamezoea sana sasa. Tena wameifanya fashion
 
Back
Top Bottom