Bunge lakwamisha kesi ya Chenge
Dar Leo Alhamisi Juni 11 2009
Na Rehema Maigala, Kinondoni
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kinondoni leo imelazimika kuahirisha kesi inayomkabili Waziri wa zamani Wizara ya Miundombinu, Andrew Chenge kutokana na vikao vya Bunge vinavyoendelea Mkoani Dodoma.
Mshitakiwa Chenge anashtakiwa pamoja na mwenzake Majid Ghalib (26), mbele ya HakimuEmilius Mchauro wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni ambapo kesi yao imesomwa na Mwendesha Mashitaka David Mafwimbo.
Akiahirisha kesi hiyo Hakimu Mchauro amesema kuwa, Mahakama imelazimika kuahirisha kesi hiyo kutokana na mshitakiwa Chenge kuiomba Mahakama ifanye hivyo kwakuwa anahudhuria vikao vya Bunge mjini Dodoma.
Alisema kuwa mshitakiwa huyo ameomba pia apewe ruhusa baada ya kumaliza vikao hivyo aende nchini Afrika Kusini kwa ajili ya matibabu.
Kutokana na sababu hizi nalazimika kuahirisha kesi hii hadi Agosti 13 mwaka huu amesema Hakimu Mchauro.
Mwendesha Mashitaka Mafwimbo awali amedai kuwa, mshitakiwa Chenge anashitakiwa kwa makosa manne ambapo mshitakiwa Ghalib Ghalib anadaiwa kutotunza kumbukumbu za mwajiri wake.
Wakati mshitakiwa Chenge anadaiwa kuendesha gari kwa uzembe na kusababisha vifo vya Victoria George na Beatrice Costantino pia kuendesha gari bila ya bima ambao ni uendeshaji wa kizembewa gari na kusababisha uharibifu wa bajaji.
Ajali hiyo ilitokea saa 10 alfajiri baada ya gari T 512 ACE Toyota Pick Up Hilux alilokuwa akiendesha Chenge kuigonga pikipiki aina ya Bajaji yenye namba za usajili T 736 AXE waliyokuwa wamepanda wanawake wawili waloikuwa wakitoka Maisha Club.
Wanawake hao Victoria George na Beatrice Costantine walipoteza maisha muda mfupi kutokana na kuumia kichwani na kutokwa damu.
Dar Leo Alhamisi Juni 11 2009
Na Rehema Maigala, Kinondoni
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kinondoni leo imelazimika kuahirisha kesi inayomkabili Waziri wa zamani Wizara ya Miundombinu, Andrew Chenge kutokana na vikao vya Bunge vinavyoendelea Mkoani Dodoma.
Mshitakiwa Chenge anashtakiwa pamoja na mwenzake Majid Ghalib (26), mbele ya HakimuEmilius Mchauro wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni ambapo kesi yao imesomwa na Mwendesha Mashitaka David Mafwimbo.
Akiahirisha kesi hiyo Hakimu Mchauro amesema kuwa, Mahakama imelazimika kuahirisha kesi hiyo kutokana na mshitakiwa Chenge kuiomba Mahakama ifanye hivyo kwakuwa anahudhuria vikao vya Bunge mjini Dodoma.
Alisema kuwa mshitakiwa huyo ameomba pia apewe ruhusa baada ya kumaliza vikao hivyo aende nchini Afrika Kusini kwa ajili ya matibabu.
Kutokana na sababu hizi nalazimika kuahirisha kesi hii hadi Agosti 13 mwaka huu amesema Hakimu Mchauro.
Mwendesha Mashitaka Mafwimbo awali amedai kuwa, mshitakiwa Chenge anashitakiwa kwa makosa manne ambapo mshitakiwa Ghalib Ghalib anadaiwa kutotunza kumbukumbu za mwajiri wake.
Wakati mshitakiwa Chenge anadaiwa kuendesha gari kwa uzembe na kusababisha vifo vya Victoria George na Beatrice Costantino pia kuendesha gari bila ya bima ambao ni uendeshaji wa kizembewa gari na kusababisha uharibifu wa bajaji.
Ajali hiyo ilitokea saa 10 alfajiri baada ya gari T 512 ACE Toyota Pick Up Hilux alilokuwa akiendesha Chenge kuigonga pikipiki aina ya Bajaji yenye namba za usajili T 736 AXE waliyokuwa wamepanda wanawake wawili waloikuwa wakitoka Maisha Club.
Wanawake hao Victoria George na Beatrice Costantine walipoteza maisha muda mfupi kutokana na kuumia kichwani na kutokwa damu.