Chelsea ku dominate Ligi ya Uingeleza?

ELNIN0

JF-Expert Member
Nov 26, 2009
4,161
1,460
Wakuu baada ya kubadilisha makocha wengi wa muda mfupi sasa nafikiri Chelsea ni Mwendo mdundo msimu huu na mingi ijayo. kwa sasa watu wanasema ni unbeatable yaani haifungiki kirahisi

Timu ina vipaji vingi lukuki kiasi kocha asie na akili, mbunifu hawezi kuifundisha

Vipaji hasa sehemu ya kiungo ndo CORE ya chelsea mfano Esien, Lampard, Obi na John Cole. hawa ndo viungo waliotawala mpira juzi pale emirates kwa wenzetu asenal

Pia so hapo tu Siri ya chelsea ni viungo wengi no mfano mwingine ni Michal Obi, Ballack, Decco na Maluda. ehee si unaona mziki huo?

Nikiacha viungo nije sasa kwa ma Beki, hakuna timu yenye mabeki wengi makini mno England kama chelsea kwa sasa kama vile Terry ( Captain), Carvahno, Ashley Cole na Bennet hawa wanajulikana kama solid back four, wakishirikia vizuri na kiungo Mkabaji or Holding midfider kama Essien na Obi ni hawafungiki kirahisi

Nikiwa Bako kwa mabeki mahili ya timu hii pia wapi Alex na Ivanovic, Paul Ferreira na Yury Zhirkov ( Huyu ni mrusi ambaye hucheza beki ya kushoto au mid kushoto) ukiondoa Bosingwa ambaye ni majeruhi kwa sasa

Nije kwa makipa, wapo watatu, Chec, Hiario na huyu Ross Turbull

Upande wa Strikers huko ndo hatari zaidi - manake Drogba mzee wa nyavu, Anelka, Kalou kijana wepesi sana huyu pia kuna Makinda kama watatu hatari tupu, Kakuta (18) dogo mwenye kipaji cha ajabu aliyefanya chelsea wakate rufaa kutosafiri misimu miwili), na Daniel kinda mpya toka City mwaka huu.

Unaona kuna timu 2 full ambazo akiumia mmoja huwezi hua tofauti yake na ndiyo maana nikasema ukiwa na kocha mbabaishaji timu haiwezi hii kuiongoza

Ni chelsea peke yake yenye wachezaje karibu 11 wapo loan katika vilabu vidogo duniani -

Ndo maana naamin kwamba chelsea inaweza ku dominate Ligi ya Uingeleza na ya Ulaya kwa miaka kadhaa ijayo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom