Chekecha ubongo kidogo

Ni chekesha bongo kweli, huyu Kijana bwana. Bado namsoma labda ntakutana na maala anapotolea mfano wa kijana aliyepata kuwa rais na kisha akaondoka madarakani akiwa bado kijana.

Nadhani haelewi vizuri asili ya roho ya udicteta huyu kijana. ngoja nirudi kule kwenye link kwanza.
 
Du nimemaliza. Huyu Jamaa anaonekana ni mkufunzi huyu sijapata nilichokikitegemea kutoka kwake "msimamo wake", hoja za namna hii zinanikumbusha nilipokuwa mwanafunzi, unapewa advantages na disadvantages alafu unaachwa mwenyewe njia panda, nadhani ndio dhana zenyewe za kudumisha uhuru wa watu, kwamba unawaacha wajichagulie wenyewe.

Nijielekeze kwenye hoja ya msingi.
Wote tunajua kwamba Mwalimu alicheza nafasi kubwa sana kwenye uandaaji wa Katiba ya nchi yetu ambamo ndimo Umri wa kugombea umeainishwa kuwa kuanzia miaka 40.

Na nikubaliane na sabatho kwamba kipengele hicho kiko vague sana.

Kisha kama alivyokumbusha sabatho kwamba wakati Mwalimu anamueleza Jakaya kwamba bado ni mdogo tayari Jakaya alikuwa na miaka 45. Hii inamaanisha kwamba neno "miaka 40" kwenye katiba liliingia kimakosa, Katiba yetu ilikuwa inamaanisha mtu awe na uwezo wa kuongoza.

Kisha nimalizie kwamba, Kwa namna tunavyoona Jakaya anavyoendesha serikali yetu basi ni wazi kwamba kuna watu ambao hata wakifikisha umri wa miaka 100 bado watakuwa ni wadogo sana kupewa majukumu ya kuongoza serikali katika nafasi ya Urais sababu wote tunashuhudia Muheshimiwa anavyojikwaa kwaa, na kudhihirisha alivyokuwa mdogo.

Mwisho, nakubaliana na hoja zake zote pia.
 
Back
Top Bottom