"Cheche" Mitaani: Ni kama ya Ballali!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,991
toleola26.jpg


Salaam,

Kuna mambo mengi ambayo yanaendelea nchini kiasi cha kutufanya tujihoji, ni wakati gani tutapata nafasi ya kuzungumzia masuala mengine muhimu ya maana, na yenye kuhamasisha ujenzi wa taifa kama kila wiki kuna kituko kimoja kikishindana na kingine? Toleo la leo ni mfano wa maisha yetu juu ya mambo ambayo kwa hakika yanaweza hata kuchosha akili. Nimepata nafasi ya kupitia magazeti ya mitaani na yenye majina makubwa na habari ni za kusikitisha zaidi kwamba aidha sisi kama taifa tumepotea mwelekeo wetu, au tunafikiri hatujapotea!

Soma uamue mwenyewe kama kwa mtindo huu tutafika!

Kama kawaida hakikisha unatuma nakala kwa watu wengine ambao unafikiri hawajapata kijarida hiki na washauri watuandikie kupitia mhariri@klhnews.com ili waweze kukipata kila wiki pamoja na habari za kushtukiza kupitia emails zao. Tukifika watu 1000 Kufikia Juni na kila mmoja akawa anaweza kutuma kwa watu 10 ina maana kila wiki tutaweza kuwafikia watu 10,000 Sasa hivi kila wiki kutoka wasambazaji wetu 11 tunaweza kuwafikia watu wengine 100 kwa vijarida vinachochapwa kila wiki na kugawiwa bure! Hii ni kuondoa wale wanaopata kwenye emal au wanaodownload kwenye mitandao ya jamiiforums.com na mwanakijiji.com!

Na tuende na kuwa "Cheche"
 

Attachments

  • TOLEOJIPYA26.pdf
    321.1 KB · Views: 221
Last edited by a moderator:
Nilikuwa nikijiuliza cheche liko wapi?badilisha heading hiyo..ili watu walichangamkie?
 
Nilikuwa nikijiuliza cheche liko wapi?badilisha heading hiyo..ili watu walichangamkie?

True, mwenyewe nimekitafuta tangia j5 nikaenda mwanakijiji.com, katakiwa kuregister first b4 dowloading so failed, nikabakia kukisubiri hapa hapa JF......So mkuu MM kikitoka wewe weka tu heading ''Kijarida cha Cheche za fikira'' tutakichangamkia mapema sana!

Thanks kwa kazi nzuri MM
 
Mkuu MM,

Nakumbuka kwenye kijarida cha cheche toleo la 25 kulikuwa na habari ye kichwa ''UHUSIANO NA IRAN: DR.Mwinyi alificha nini?'', habari hii haikutoa details zaidi ya kilichotokea huko Tehran lakini mulituahidi kwenye toleo la wiki hii mngetupa more details- see below;

Tunaamini kuwa pasipo maelezo ya kutosha
kuna kitu kinafichwa,kijarida chako
cha Cheche kinatarajia kukupatia taarifa
wiki ijayo. Na tunaamini kitu hicho hakistahili
kufichwa kwani kinahusu TAIFA LETU


Nimepitia kijarida toleo la 26, lakini habari hii sijaiona kabisa! Vipi mkuu mmeshindwa kupata further details za hii habari? Anyway myself nilikuwa na kiu ya kujua kwa undani zaidi hii habari ya uhusiano na Iran...please advise!
 
Mkuu bila shaka haina haja ya kuprint tena mana itakuwa hasara!!!!!! Si hapo tu kwa Balali Vs Mkono?
 
Mzee MM
hongera sana kwa kazi nzuri, yenye kufungua macho, kurudisha matumaini na kutia moyo.
Tuko bega kwa bega.
 
toleola26.jpg



Kama kawaida hakikisha unatuma nakala kwa watu wengine ambao unafikiri hawajapata kijarida hiki na washauri watuandikie kupitia mhariri@klhnews.com ili waweze kukipata kila wiki pamoja na habari za kushtukiza kupitia emails zao. Tukifika watu 1000 Kufikia Juni na kila mmoja akawa anaweza kutuma kwa watu 10 ina maana kila wiki tutaweza kuwafikia watu 10,000 Sasa hivi kila wiki kutoka wasambazaji wetu 11 tunaweza kuwafikia watu wengine 100 kwa vijarida vinachochapwa kila wiki na kugawiwa bure! Hii ni kuondoa wale wanaopata kwenye emal au wanaodownload kwenye mitandao ya jamiiforums.com na mwanakijiji.com!

Na tuende na kuwa "Cheche"

Asante kwa kazi nzuri MMM

Nimefanikiwa kukifungua na kukisoma hapa hapa bila shida. Kama inawezekana naomba uweke tena hapa hapa CHECHE toleo na. 25

Asante kwa kazi nzuri
 
Mwanakijiji,

Am I missing something? Mbona kuna utata mwingi kwenye toleo la 27 la Cheche? Kwanza kwenye sehemu ya tarehe, inasomeka Februari 11, 2008. At first I thought hii ni makala ya 2008, lakini nilipoona habari kuhusu sakata la Masha, basi nikajua kuna makosa ya kiuandishi. Pili ni kwenye picha ya "marehemu" balali. Maelezo chini ya picha yanasomeka "Mdau wa Benki M - Mhe. Nimrod E. Mkono" ilhali picha iliyotumika ni ya Balali. Nadhani hapa pia kuna tatizo la kiuandishi kidogo.
 
Mwanakijiji,

Am I missing something? Mbona kuna utata mwingi kwenye toleo la 27 la Cheche? Kwanza kwenye sehemu ya tarehe, inasomeka Februari 11, 2008. At first I thought hii ni makala ya 2008, lakini nilipoona habari kuhusu sakata la Masha, basi nikajua kuna makosa ya kiuandishi. Pili ni kwenye picha ya "marehemu" balali. Maelezo chini ya picha yanasomeka "Mdau wa Benki M - Mhe. Nimrod E. Mkono" ilhali picha iliyotumika ni ya Balali. Nadhani hapa pia kuna tatizo la kiuandishi kidogo.

Zero,

Nimeona kweli kuna makosa. Nafikiri ni shauri ya kukosa muda maana hawa wenzetu wanahangaika kubeba box kwa maisha yao ya kawaida na huku kufanikisha kuchapisha hiki kijalada kwa kujitolea. Sio kazi ndogo kabisa.

Hongera Mwanakijiji na kundi lako kwa kazi kubwa mnayofanya ya kuelemisha jamii.

Yaani hawa jamaa wajinga kweli, wanataka kutumia mbinu ile ile ambayo tayari tunajua ilikuwa ni kudanganya Wadanganyika?
 
Zero,

Nimeona kweli kuna makosa. Nafikiri ni shauri ya kukosa muda maana hawa wenzetu wanahangaika kubeba box kwa maisha yao ya kawaida na huku kufanikisha kuchapisha hiki kijalada kwa kujitolea. Sio kazi ndogo kabisa.

Hongera Mwanakijiji na kundi lako kwa kazi kubwa mnayofanya ya kuelemisha jamii.

Yaani hawa jamaa wajinga kweli, wanataka kutumia mbinu ile ile ambayo tayari tunajua ilikuwa ni kudanganya Wadanganyika?

Naelewa mazingira halisi ya kazi yenyewe ya uandishi. Sio suala la kubeba box tu, bali hata muda Mwanakijiji anaotumia hapa JF ni mkubwa vya kutosha kushangaza anapata wapi muda wa kuandaa "Cheche".

Big up guys. I really appreciate what you guys are doing!
 
Big Up kwa kijarida murua chenye kuelimisha na kuhamasisha chachu ya maendeleo na mabadiliko.

Cheers team!!!

Thanx
 
Back
Top Bottom