Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
Salaam,
Kuna mambo mengi ambayo yanaendelea nchini kiasi cha kutufanya tujihoji, ni wakati gani tutapata nafasi ya kuzungumzia masuala mengine muhimu ya maana, na yenye kuhamasisha ujenzi wa taifa kama kila wiki kuna kituko kimoja kikishindana na kingine? Toleo la leo ni mfano wa maisha yetu juu ya mambo ambayo kwa hakika yanaweza hata kuchosha akili. Nimepata nafasi ya kupitia magazeti ya mitaani na yenye majina makubwa na habari ni za kusikitisha zaidi kwamba aidha sisi kama taifa tumepotea mwelekeo wetu, au tunafikiri hatujapotea!
Soma uamue mwenyewe kama kwa mtindo huu tutafika!
Kama kawaida hakikisha unatuma nakala kwa watu wengine ambao unafikiri hawajapata kijarida hiki na washauri watuandikie kupitia mhariri@klhnews.com ili waweze kukipata kila wiki pamoja na habari za kushtukiza kupitia emails zao. Tukifika watu 1000 Kufikia Juni na kila mmoja akawa anaweza kutuma kwa watu 10 ina maana kila wiki tutaweza kuwafikia watu 10,000 Sasa hivi kila wiki kutoka wasambazaji wetu 11 tunaweza kuwafikia watu wengine 100 kwa vijarida vinachochapwa kila wiki na kugawiwa bure! Hii ni kuondoa wale wanaopata kwenye emal au wanaodownload kwenye mitandao ya jamiiforums.com na mwanakijiji.com!
Na tuende na kuwa "Cheche"
Attachments
Last edited by a moderator: