Chatanda azua tena mvutano CCM, Chadema Arusha

Hivi karibuni kumetokea mauaji ya watu watatu huko Arusha na wengine wengi kujeruhiwa, sababu imeelezwa kuwa ni Mbunge wa Viti maalumu kupitia Jumuiya ya Wanawake (UWT) wa Mkoa wa Tanga, Mery Chatanda.

Ni huyu Marya Chatanda ambaye amewataka Maaskofu kuvua majoho yao na kuingia katika siasa na ni huyu ambaye ametinga katika uchaguzi wa Umeya huku akijua yeye ni mbunge wa mkoa wa Tanga na siyo Arusha na kupiga kura za Umeya, kama haitoshi pia ametinga katika mkutano wa ALAT Arusha na kusababisha mtafaruku huko kama ule wa Umeya na Madiwani na wabunge wa Chadema kususia mkutano huo.

Je, huyu Mary Chatanda ni nani?
Pengine ni mtoto wa Katiba, ni mtoto wa kigogo ama mke wa Kigogo gani, ni muasisi wa chama ama taifa? Naomba msaada kwa wadau.
 
Shida ya watanzania ni kwamba hao wenye uelewa wanasemewa na mambumbumbu wenye sauti ya fedha na madaraka. Hili acha tu waliendeleze ila mwisho wake unakuja
 
ndugu wana jf na wote wanaoitakia mema nchi yetu. sote tumeshuhudia malumbano makali hadi kufikia watu kutoana roho, kisa? Chatanda. mimi si mjuzi saana wa katiba lakini naweza kuisoma na kuitafisiri. suala hili linaloongelewa bila kuwa na reference za kutosha. Je chatanda anapaswa kuwakilisha wapi kwa mujibu wa sheria za nchi yetu? arusha au tanga? Naomba ninukuu maneno ya mhe.Mushashu, Bernadeta Kasabago[CCM] wakati akichangia Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Jinsia na Maendeleo ya Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) wa Mwaka 2008. alisema na hapa nanukuu

''Ibara ya 66(1)(b) na ya 78 zinazotambua kuwepo kwa affirmative action, mkakati wa makusudi wa kutambua Wabunge Viti Maalum, uendelee kuwepo kwa sababu kama nilivyoeleza haya matatizo mengine yaliyoko kwenye jamii yatakuwa hayajatoka still tunahitaji affirmative action. Kwa hiyo, napendekeza iendelee kuwepo kwenye Katiba.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini Katiba hii inamtambua Mbunge wa Jimbo, inamtambua Mbunge Viti Maalum lakini Mbunge wa Jimbo inaelezwa yeye anatakiwa kufanya kazi katika eneo lipi pamoja na kuwa Mbunge wa Viti Maalum anatambuliwa na Katiba lakini haielezi Mbunge huyu anafanya kazi katika eneo lipi. Matokeo yake ni kwamba Wabunge wa Viti Maalum wa Chama Tawala cha Mapinduzi wanawajibika katika Mkoa mzima, unakuta mtu anafanya kazi katika Majimbo 10 yaliyo katika Mkoa, unakuta mtu anafanya kazi katika Majimbo sita yaliyo katika Mkoa, hapa anafanya kidogo, hapa kidogo matokeo yake hata kazi anazofanya hazionekani, wala hazithaminiwi kwa sababu zimesambaa maeneo yote. Lakini sioni inashindikana nini Serikali kuweka sheria kwamba umeshachaguliwa Mbunge Viti Maalum eneo lako ni fulani!

Mheshimiwa Naibu Spika, Wabunge wa Viti Maalum wa Chama cha Mapinduzi tunafanyakazi kwenye Mikoa, msiniulize Wabunge wa Viti Maalum wa Vyama vingine vya Siasa maeneo yao ni yapi. Wengine labda ni Taifa au Mikoa sijui. Sasa ingekuwa ni vizuri basi ili kuleta usawa wa kijinsia tunaozungumzia hata maeneo ya kufanyia kazi yakaweza kutambuliwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napendekeza ili tuweze kutekeleza hii Itifaki kivitendo, haya yafanyike, kwanza Sheria za Uchaguzi na za Vyama vya Siasa ziwatake Vyama vya Siasa viwe na utaratibu ulio wazi wa namna gani hawa Wabunge Viti Maalum au Madiwani Viti Maalum watapatikana kwa sababu kama mlivyokwishaelezwa wengine wananyanyasika kijinsia kusudi waweze kupata nafasi hizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, Wabunge Viti Maalum baada ya Uchaguzi Mkuu watangazwe na Tume ya Uchaguzi kama Wabunge wengine na maeneo yao ya kufanyia kazi yatangazwe. Wanaweza wakapangiwa labda Wilaya kadhaa katika Mkoa lakini basi wapewe eneo ambalo liko manageable, wanaloweza kulifanyia kazi.

mwisho wa kunukuu.
Hitimisho: mimi kwa hili simlaumu chatanda, ila nalaumu ukimya wa katiba yetu

naomba kuwasilisha.
 
She is a stupid women ambaye amepoteza mwelekeo na awe makini sana na arusha laa sivyo ataipenda
 
Hata mimi ningependa kumfahamu, na amepata wapi ujasiri huo wa kutoka TA mpaka AR kuchakachua kura za watu.
 
chakula ya mkulu hiyo ndio maana ina kiburi hadi kwenye nywele!
 
Mkuu Polisi,

Haya ni matunda ya viraka na ukurupukaji wa wana siasa kila wanapoona kwamba sasa ni wakati wa kufanya mabadiliko fulani au kwa shinikizo kutoka nje au kwa manufaa ya Chama Tawala.

Pamoja na ukimya wa Katiba kwenye swala la eneo la kufanyia kazi la wabunge wa Viti Maalum, lakini simple logic iko wazi kutokana na utaratibu wa CCM wa kuwachagua wabunge wa Viti Maalum.

Wabunge wa Viti Maalum kupitia CCM wamegawanyika kwenye makundi yafuatayo:
1. Wawakilishi wa Mikoa - hupigiwa kura na wajumbe wa Mkutano wa UWT Mkoa
2. Wawakilishi wa UVCCM - hupigiwa kura na wajumbe Mkutano wa UVCCM wa Taifa
3. Wawakilishi wa walemavu - sijui wanavyopatikana
4. Wawakilishi wa Taasisi za Elimu ya Juu - sijui wanavyopatikana
5. Wawakilishi wa NGOs - niliona walipigiwa kura wa UWT Mkoa wa Dar

Note: Mchakato wa wabunge wa UVCCM, mpambano unaanzia ngazi ya mkoa then wanaenda ngazi ya Taifa.

Mary Chatanda alipigiwa kura na UWT mkoa wa Tanga, na hivyo kimantiki anatakiwa kuwatumikia wapiga kura wake ambao wako mkoa wa Tanga. Matatizo ya akina Mama wa Mkoa wa Arusha hayafanani na matatizo ya akina mama wa Tanga au Manyara. Hatujui aliahidi nini alipokuwa anaomba kura kwa wapiga kura wake ambao wako Mkoa wa Tanga. Je, atashughulikiaje matatizo ya akina mama wa Tanga na ili hali haingii kwenye vikao vya baraza la madiwaji wa Jiji la Tanga? Kwanini alazimishe kuwatumikia akina mama wa Arusha ambao hawakumpigia kura wakati wa uchaguzi?

Pamoja na kwamba Katiba iko kimya, kitendo cha Mary Chatanda kupewa nafasi ya Viti ya Maalum kwa kupigiwa kura na akina mama wa mkoa wa Tanga, maana yake ni kwamba anawakilisha matatizo ya akina mama wa Tanga kuanzia kwenye kata, wilaya, mkoa na hatimaye Taifa.

Mary Chatanda anatakiwa kwenda kuwatumikia akina mama wa Tanga kwa kuwatetea kwenye vikao vya baraza la madiwani huko Tanga. Angekuwa ni mwakilishi wa UVCCM, Walemavu au Taasisi za Elimu ya Juu au NGOs, angekuwa na haki, maana majimbo/maeneo yao ya kazi yamesambaa nchi nzima.

Hoja yangu hapa ni kwamba, Kama Chatanda alipigiwa kura na akina mama wa mkoa wa Tanga, maana yake ni kwamba anawajibika kwa akina mama wa CCM (UWT) mkoa wa Tanga, hapo ndipo ilipo primary responsibility yake.

manne hivi ya Wabunge wa Viti Maalum, wapo wanaowakilisha Akina Mama wewe ulemavu, wapo wanawakilisha NGOs na wapo wanaowakilisha Taasisi za Elimu ya Juu, wapo wanao
 
Viti maalum ni gharama, vm sio demokrasia, vm ni ujinga, vm havipaswi kuwepo KATIBA ijayo.
 
Mkuu Polisi,

Haya ni matunda ya viraka na ukurupukaji wa wana siasa kila wanapoona kwamba sasa ni wakati wa kufanya mabadiliko fulani au kwa shinikizo kutoka nje au kwa manufaa ya Chama Tawala.

Pamoja na ukimya wa Katiba kwenye swala la eneo la kufanyia kazi la wabunge wa Viti Maalum, lakini simple logic iko wazi kutokana na utaratibu wa CCM wa kuwachagua wabunge wa Viti Maalum.

Wabunge wa Viti Maalum kupitia CCM wamegawanyika kwenye makundi yafuatayo:
1. Wawakilishi wa Mikoa - hupigiwa kura na wajumbe wa Mkutano wa UWT Mkoa
2. Wawakilishi wa UVCCM - hupigiwa kura na wajumbe Mkutano wa UVCCM wa Taifa
3. Wawakilishi wa walemavu - sijui wanavyopatikana
4. Wawakilishi wa Taasisi za Elimu ya Juu - sijui wanavyopatikana
5. Wawakilishi wa NGOs - niliona walipigiwa kura wa UWT Mkoa wa Dar

Note: Mchakato wa wabunge wa UVCCM, mpambano unaanzia ngazi ya mkoa then wanaenda ngazi ya Taifa.

Mary Chatanda alipigiwa kura na UWT mkoa wa Tanga, na hivyo kimantiki anatakiwa kuwatumikia wapiga kura wake ambao wako mkoa wa Tanga. Matatizo ya akina Mama wa Mkoa wa Arusha hayafanani na matatizo ya akina mama wa Tanga au Manyara. Hatujui aliahidi nini alipokuwa anaomba kura kwa wapiga kura wake ambao wako Mkoa wa Tanga. Je, atashughulikiaje matatizo ya akina mama wa Tanga na ili hali haingii kwenye vikao vya baraza la madiwaji wa Jiji la Tanga? Kwanini alazimishe kuwatumikia akina mama wa Arusha ambao hawakumpigia kura wakati wa uchaguzi?

Pamoja na kwamba Katiba iko kimya, kitendo cha Mary Chatanda kupewa nafasi ya Viti ya Maalum kwa kupigiwa kura na akina mama wa mkoa wa Tanga, maana yake ni kwamba anawakilisha matatizo ya akina mama wa Tanga kuanzia kwenye kata, wilaya, mkoa na hatimaye Taifa.

Mary Chatanda anatakiwa kwenda kuwatumikia akina mama wa Tanga kwa kuwatetea kwenye vikao vya baraza la madiwani huko Tanga. Angekuwa ni mwakilishi wa UVCCM, Walemavu au Taasisi za Elimu ya Juu au NGOs, angekuwa na haki, maana majimbo/maeneo yao ya kazi yamesambaa nchi nzima.

Hoja yangu hapa ni kwamba, Kama Chatanda alipigiwa kura na akina mama wa mkoa wa Tanga, maana yake ni kwamba anawajibika kwa akina mama wa CCM (UWT) mkoa wa Tanga, hapo ndipo ilipo primary responsibility yake.

manne hivi ya Wabunge wa Viti Maalum, wapo wanaowakilisha Akina Mama wewe ulemavu, wapo wanawakilisha NGOs na wapo wanaowakilisha Taasisi za Elimu ya Juu, wapo wanao

mkuu keil asante sana. Nisaidie suala moja. Mkoa wa arusha una mbunge wa viti maalum kwa tiketi ya UWT?
 
mkuu keil asante sana. Nisaidie suala moja. Mkoa wa arusha una mbunge wa viti maalum kwa tiketi ya UWT?

Waliochaguliwa na UWT Mkoa wa Arusha ni Namalok Edward Sokoine na Halima Mohamed Mamuya.
 
Hivi huyo mama ameolewa ama yuko kwa ajili ya kutumiwa na kundi fulani ndani ya CCM. Kama kuna mtu ana CV yake aiweke walau tujue akili na mawazo yake yana mwelekeo gani.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom