Ng'wanza Madaso
JF-Expert Member
- Oct 21, 2008
- 2,268
- 333
Na Joseph Ngilisho,Arusha
MBUNGE wa Viti maalum Tanga ambaye pia ni Katibu wa CCM MKoa wa Arusha, Mary Chatanda, anazidi kuvuruga watu, sasa baada ya kuwavuruga Chadema na CCM, ameanza kuwashambulia waandishi wa habari na kuwaita wahuni, huku akiwatishia kuwapiga bastola.
Hali hiyo ya kusikitisha imetokea , wakati Katibu huyo alipoitisha mkutano na waandishi wa habari, kwenye jengo la CCM Mkoa, ili kuelezea tamko la kamati ya siasa MKoa wa Arusha, kuhusina na vurugu zilizotokea januari 5 mwaka huu.
Akitoa tamko hilo alianza kwa kusema, anaipongeza serikali kwa kutumia vyombo vya dola yaani Polisi, kudhibiti wahuni kwa kutumia jeshi la Polisi, kisha akawageukia waandishi wa habari na kuanza kuwafukuza.
Waandishi waliofukuzwa na huku akiwatamkia maneno ya kashfa kuwa wameletwa sababu ya kufuata uchumi, ni mwandishi wa gazeti la Mtanzania, Fortunata Ringo, John Shija wa radio MJ, Rose JAkson wa radio Safina na Wankyo Ghati wa radio five na gazeti la Jamb oleo.
Aidha baada ya kuwafukuza hao, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Arusha naye alilazimika kuingilia kati na kumsihi Katibu huyo awaache kwa kuwa waandishi ni kazi yao kuchukua habari.
Lakini Chatanda aliendelea kushikilia msimamo wake na kusema hapo siyo mahali pa kupata uchumi, watoke nje na waandishi hao walitoka nje ya jengo hilo.
NAye Adamu Ihucha wa gazeti la East Africa, akielezea kwa masikitiko, alisema yeye ni mmojawapo, alipoingia ndani ya kikao hicho, alimuuliza swali Mary Chatanda, kuwa kwanini wanapingana na IGP, kwa sababu IGP alisema kuna askari walitumia nguvu kubwa kupita kiasi na wewe unasema unawapongeza?
Mara baada ya swali hilo, Mary Chatanda aliingilia kati na kumkatisha huku akimkejeli mwandishi huyo kuwa, anamshangaa kuvamia mkutano ambao hakualikwa na alikuwa ametokea wapi.
Hivi wewe umetoka wapi? Maana hatukujuwi, sisi tunazungumzia mambo yetu na kunyanyuka kutoka nje ya kikao alisema Ihucha.
NAye Paul Sarwat wa gazeti la Raia Mwema, naye anasikitishw ana kauli za Katibu huyo na kusema awali, alishawahi kumfuata na kumtaka atoe ufafanuzi juu ya habari za CCM, lakini katibu huyo alimjibu kwa kejeli na kumwambia atamchapa makofi akiendelea kuandika habari za CCM.
Alisema Chatanda alimwambia kuwa yeye haoni habari za kuandika sipokuwa habari ni cCM tu, akiendelea atamchapa makofi.
Sarwat alisema kauli kama hizo zinazotolewa na kiongozi mkubwa wa ngazi ya juu ya Mkoa, zinasikitisha sana na zinapaswa kukemewa.
Akizungumzia kuhusu kauli za Mary Chatanda na kuwaukuza waandishi wa habari, MAkamu Mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari, APC, Charles Ngereza, alisema yeye amesikitishw ana udhalilishaji wa Mary Chatanda dhidi ya wanahabari.
Alisema kuwa yeye kama kiongozi amekuwa akipata malalamiko ya mara kwa mara ya waandishi kutolewa vitisho na lugha chafu na Mary Chatanda, hivyo kama waandishi wanasikitika sana na hali hiyo ikiendelea italeta mvurugano mwingine kati ya CCM na waandishi wa habari.
Ngereza alisema kuwa mbali ya kuleta mvurugano, pia itahalalisha viongozi na watu wengine kuwadhalilisha waandishi na hiyo tayari imetokea kwa Polisi kuwakamata baadhi ya waandishi kama Musa Juma wa MWananchi, ambaye alikamatw ana Polisi na kupigwa, kasha kunywanganywa Kamera na kulazimishwa kufuta Picha.
Alisema huo ni unyama na kuingilia kazi za waandhishi wa habari, ambao hawana mipaka na kazi zao, hivyo wanaomba serikali na viongozi wa juu, kuingilia kati na kuwakalisha viongozi wa Arusha, ili waheshimu uhuru wa wanahabari.
MBUNGE wa Viti maalum Tanga ambaye pia ni Katibu wa CCM MKoa wa Arusha, Mary Chatanda, anazidi kuvuruga watu, sasa baada ya kuwavuruga Chadema na CCM, ameanza kuwashambulia waandishi wa habari na kuwaita wahuni, huku akiwatishia kuwapiga bastola.
Hali hiyo ya kusikitisha imetokea , wakati Katibu huyo alipoitisha mkutano na waandishi wa habari, kwenye jengo la CCM Mkoa, ili kuelezea tamko la kamati ya siasa MKoa wa Arusha, kuhusina na vurugu zilizotokea januari 5 mwaka huu.
Akitoa tamko hilo alianza kwa kusema, anaipongeza serikali kwa kutumia vyombo vya dola yaani Polisi, kudhibiti wahuni kwa kutumia jeshi la Polisi, kisha akawageukia waandishi wa habari na kuanza kuwafukuza.
Waandishi waliofukuzwa na huku akiwatamkia maneno ya kashfa kuwa wameletwa sababu ya kufuata uchumi, ni mwandishi wa gazeti la Mtanzania, Fortunata Ringo, John Shija wa radio MJ, Rose JAkson wa radio Safina na Wankyo Ghati wa radio five na gazeti la Jamb oleo.
Aidha baada ya kuwafukuza hao, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Arusha naye alilazimika kuingilia kati na kumsihi Katibu huyo awaache kwa kuwa waandishi ni kazi yao kuchukua habari.
Lakini Chatanda aliendelea kushikilia msimamo wake na kusema hapo siyo mahali pa kupata uchumi, watoke nje na waandishi hao walitoka nje ya jengo hilo.
NAye Adamu Ihucha wa gazeti la East Africa, akielezea kwa masikitiko, alisema yeye ni mmojawapo, alipoingia ndani ya kikao hicho, alimuuliza swali Mary Chatanda, kuwa kwanini wanapingana na IGP, kwa sababu IGP alisema kuna askari walitumia nguvu kubwa kupita kiasi na wewe unasema unawapongeza?
Mara baada ya swali hilo, Mary Chatanda aliingilia kati na kumkatisha huku akimkejeli mwandishi huyo kuwa, anamshangaa kuvamia mkutano ambao hakualikwa na alikuwa ametokea wapi.
Hivi wewe umetoka wapi? Maana hatukujuwi, sisi tunazungumzia mambo yetu na kunyanyuka kutoka nje ya kikao alisema Ihucha.
NAye Paul Sarwat wa gazeti la Raia Mwema, naye anasikitishw ana kauli za Katibu huyo na kusema awali, alishawahi kumfuata na kumtaka atoe ufafanuzi juu ya habari za CCM, lakini katibu huyo alimjibu kwa kejeli na kumwambia atamchapa makofi akiendelea kuandika habari za CCM.
Alisema Chatanda alimwambia kuwa yeye haoni habari za kuandika sipokuwa habari ni cCM tu, akiendelea atamchapa makofi.
Sarwat alisema kauli kama hizo zinazotolewa na kiongozi mkubwa wa ngazi ya juu ya Mkoa, zinasikitisha sana na zinapaswa kukemewa.
Akizungumzia kuhusu kauli za Mary Chatanda na kuwaukuza waandishi wa habari, MAkamu Mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari, APC, Charles Ngereza, alisema yeye amesikitishw ana udhalilishaji wa Mary Chatanda dhidi ya wanahabari.
Alisema kuwa yeye kama kiongozi amekuwa akipata malalamiko ya mara kwa mara ya waandishi kutolewa vitisho na lugha chafu na Mary Chatanda, hivyo kama waandishi wanasikitika sana na hali hiyo ikiendelea italeta mvurugano mwingine kati ya CCM na waandishi wa habari.
Ngereza alisema kuwa mbali ya kuleta mvurugano, pia itahalalisha viongozi na watu wengine kuwadhalilisha waandishi na hiyo tayari imetokea kwa Polisi kuwakamata baadhi ya waandishi kama Musa Juma wa MWananchi, ambaye alikamatw ana Polisi na kupigwa, kasha kunywanganywa Kamera na kulazimishwa kufuta Picha.
Alisema huo ni unyama na kuingilia kazi za waandhishi wa habari, ambao hawana mipaka na kazi zao, hivyo wanaomba serikali na viongozi wa juu, kuingilia kati na kuwakalisha viongozi wa Arusha, ili waheshimu uhuru wa wanahabari.