Dr Lizzy
Platinum Member
- May 25, 2009
- 30,801
- 59,274
Nazitamani chapati. . .chapati za kusukumwa wala so za mayai. . .
Za kupika mwenyewe. . .wala so za jirani hata kama zimepikiwa chai. .
Bwana akishaenda shamba. . nami nifunge kibwebwe. .
Nende lilipo duka. . . .
Ahhhhh vina haviji ila nazitamanije. Natamani ningekaa chini nikande unga lainiiiii ulotiwa chumvi kidogo na maji ya uvugu vugu tu basi. Niuchanganye mpaka niridhike.
Nitie mafuta kwenye bakuli na kijiko ndo nianze kukata kipande kimoja kimoja na kusukuma, nikimaliza nikipake mafuta king'ae. Nikisukuma yasimwagike mwagike maana sijazidisha. Nivipange vipande vilosokotwa kwenye sahani au sinia lilonyunyuziwa unga kwa mbali.
Nikishasokota zote niandae chakugeuzia pia chakuwekea na kufunikia. Niwashe jiko langu kisha niweke frying pain yangu juu yake. .
Nianze kusukuma tena na kuziweka jikoni moja moja. Zikianza kupata rangi nizipake na mafuta. . .nizigeuze mara mbili mpaka rangi ipendeze. Niziweke kwenye chombo kisha nifunike kwa muda. Zilainike vizuri ndio nijisevie kwa mchuzi wa nyama au maharage yaloungwa kwa nazi. Nikizikata zichambuke mpaka nione raha.
Haki ningekua sijajikata kidole leo ningezikaanga hata usiku.
Wapi wapenzi wa chapati. . . . . .?
Za kupika mwenyewe. . .wala so za jirani hata kama zimepikiwa chai. .
Bwana akishaenda shamba. . nami nifunge kibwebwe. .
Nende lilipo duka. . . .
Ahhhhh vina haviji ila nazitamanije. Natamani ningekaa chini nikande unga lainiiiii ulotiwa chumvi kidogo na maji ya uvugu vugu tu basi. Niuchanganye mpaka niridhike.
Nitie mafuta kwenye bakuli na kijiko ndo nianze kukata kipande kimoja kimoja na kusukuma, nikimaliza nikipake mafuta king'ae. Nikisukuma yasimwagike mwagike maana sijazidisha. Nivipange vipande vilosokotwa kwenye sahani au sinia lilonyunyuziwa unga kwa mbali.
Nikishasokota zote niandae chakugeuzia pia chakuwekea na kufunikia. Niwashe jiko langu kisha niweke frying pain yangu juu yake. .
Nianze kusukuma tena na kuziweka jikoni moja moja. Zikianza kupata rangi nizipake na mafuta. . .nizigeuze mara mbili mpaka rangi ipendeze. Niziweke kwenye chombo kisha nifunike kwa muda. Zilainike vizuri ndio nijisevie kwa mchuzi wa nyama au maharage yaloungwa kwa nazi. Nikizikata zichambuke mpaka nione raha.
Haki ningekua sijajikata kidole leo ningezikaanga hata usiku.
Wapi wapenzi wa chapati. . . . . .?