Chanzo cha vurugu mbagala hiki hapa

Abuu Kauthar

JF-Expert Member
Jul 10, 2011
3,950
5,692
Chanzo cha vurugu zilizotokea mwishoni mwa wiki iliyopita katika eneo la Mbagala kizuiani Wilaya ya Temeke jijini Dar-es-Salaam imeelezwa kusababishwa na mama mzazi wa Emmanuel Josephat (14) anayetuhumiwa kukojolea Qur'an kutoa lugha ya kejeli na kashfa dhidi yatukio hilo.
Mama huyo ambaye jina lake halikufahamika mara moja imeelezwa kwamba alikejeli tukio hilo na kugoma kumsikiliza mzazi mwenzie ambaye mwanae alinyang'anywa Qur'an na kusema kwamba yeye alidhani ni jambo la kutisha kama kuua kumbe suala lenyewe ni dogo na lisilo na maana,"nilidhani mwanangu kaua kumbe jambo lenyewe ni hili dogo" alisema mama huyo.
Imeelezwa kwamba mama huyo alikuwa tatizo hadi hapo baba mzazi wa mtoto alinyang'anywa Qur'an Hamis Saluum Mbonde kufika nyumbani kwa mama huyo kutaka kufanya mazungumzo katika kupata ufumbuzi.
Kisiwa limebainishwa kuwa tukio hilo lilitokea siku ya Jumatano Oktoba 10 saa 12 jioni, ambapo vijana hao walianza kubishana juu ya kitabu hicho ndipo Emmanuel aliamua kukikojolea.
Mabishano hayo yalianza baada ya Emmanuel kumuuliza Zakaria maana ya kitabu hicho na alipojibiwa alimweleza kwamba anaweza akafanya chochote na asipatwe lolote.
Baada ya mabishano hayo, walifika katika uwanja wa mpira na kisha Zakaria akatoa mpira wake na kuwapa vijana waliokuwa uwanjani hapo na kuanza kucheza.
Taarifa ziliendelea kusema kuwa baada ya Zakaria kuweka kitabu chake mahala alipoona panafaa aliingia uwanjani na kuanza kucheza mpira na wenzake na mara Emmanuel akaonekana akifungua zipu na kukojolea kitabu hicho.
Akizungumza na Kisiwa wakati vurugu zinaendelea maeneo yote yaliyozunguka kizuiani sambamba na mabomu kirindima kila kona Hamis alisema tukio hilo lisingeweza kuwa kubwa kiasi hiki ama kufikia hivi, bali kilichopelekea kufikia hapo ni kutokana na kauli ya ya mama mzazi wa Emmamuel ambayo ilionekana kizidisha hasira za Waislam.
Hamisi alisema chanzo cha hasira hizo ziliibuka saa chache kabla kijana huyo kupelekwa kituoni wakati baba mzazi wa Zakaria alipokuwa akimsihi mzazi huyo wa Emmanuel ampeleke mwanae police kwa usalama wake.
Hamis aliendelea kusema wakati akihojiwa mama huyo aliwakebehi waliomuuliza na kusikika akisema 'Nilifikiri labda mwanangu kaua!kumbe kakojolea msahafu tu'alisema mama huyo.
Kauli hiyo inatajwa kuwa ndio chanzo cha hasira za waislamu ambapo wwngine walisikika wakilia na kusema 'Mtoeni huyo tumpe adhabu yetu' haiwezekani audhalilishe uislamu namna hii' Hicho ndicho chanzo cha vurugu hizo alisema Hamis.
Hata hivyo alisema kinachotakiwa ni kufanywa sasa ni kuviacha vyombo vya dola vilishughulikie na kuonya kwamba kauli zakejeli dhidi ya Imani ya mtu mwingine hazifai na zisipoangaliwa zinaweza kuleta madhala.
Source: Kisiwa
 
النّظير إلى رقميّ =Analog to Digital
 
Chanzo cha vurugu zilizotokea mwishoni mwa wiki iliyopita katika eneo la Mbagala kizuiani Wilaya ya Temeke jijini Dar-es-Salaam imeelezwa kusababishwa na mama mzazi wa Emmanuel Josephat (14) anayetuhumiwa kukojolea Qur'an kutoa lugha ya kejeli na kashfa dhidi yatukio hilo.
Mama huyo ambaye jina lake halikufahamika mara moja imeelezwa kwamba alikejeli tukio hilo na kugoma kumsikiliza mzazi mwenzie ambaye mwanae alinyang'anywa Qur'an na kusema kwamba yeye alidhani ni jambo la kutisha kama kuua kumbe suala lenyewe ni dogo na lisilo na maana,"nilidhani mwanangu kaua kumbe jambo lenyewe ni hili dogo" alisema mama huyo.
Imeelezwa kwamba mama huyo alikuwa tatizo hadi hapo baba mzazi wa mtoto alinyang'anywa Qur'an Hamis Saluum Mbonde kufika nyumbani kwa mama huyo kutaka kufanya mazungumzo katika kupata ufumbuzi.
Kisiwa limebainishwa kuwa tukio hilo lilitokea siku ya Jumatano Oktoba 10 saa 12 jioni, ambapo vijana hao walianza kubishana juu ya kitabu hicho ndipo Emmanuel aliamua kukikojolea.
Mabishano hayo yalianza baada ya Emmanuel kumuuliza Zakaria maana ya kitabu hicho na alipojibiwa alimweleza kwamba anaweza akafanya chochote na asipatwe lolote.
Baada ya mabishano hayo, walifika katika uwanja wa mpira na kisha Zakaria akatoa mpira wake na kuwapa vijana waliokuwa uwanjani hapo na kuanza kucheza.
Taarifa ziliendelea kusema kuwa baada ya Zakaria kuweka kitabu chake mahala alipoona panafaa aliingia uwanjani na kuanza kucheza mpira na wenzake na mara Emmanuel akaonekana akifungua zipu na kukojolea kitabu hicho.
Akizungumza na Kisiwa wakati vurugu zinaendelea maeneo yote yaliyozunguka kizuiani sambamba na mabomu kirindima kila kona Hamis alisema tukio hilo lisingeweza kuwa kubwa kiasi hiki ama kufikia hivi, bali kilichopelekea kufikia hapo ni kutokana na kauli ya ya mama mzazi wa Emmamuel ambayo ilionekana kizidisha hasira za Waislam.
Hamisi alisema chanzo cha hasira hizo ziliibuka saa chache kabla kijana huyo kupelekwa kituoni wakati baba mzazi wa Zakaria alipokuwa akimsihi mzazi huyo wa Emmanuel ampeleke mwanae police kwa usalama wake.
Hamis aliendelea kusema wakati akihojiwa mama huyo aliwakebehi waliomuuliza na kusikika akisema 'Nilifikiri labda mwanangu kaua!kumbe kakojolea msahafu tu'alisema mama huyo.
Kauli hiyo inatajwa kuwa ndio chanzo cha hasira za waislamu ambapo wwngine walisikika wakilia na kusema 'Mtoeni huyo tumpe adhabu yetu' haiwezekani audhalilishe uislamu namna hii' Hicho ndicho chanzo cha vurugu hizo alisema Hamis.
Hata hivyo alisema kinachotakiwa ni kufanywa sasa ni kuviacha vyombo vya dola vilishughulikie na kuonya kwamba kauli zakejeli dhidi ya Imani ya mtu mwingine hazifai na zisipoangaliwa zinaweza kuleta madhala.
Source: Kisiwa

acha uongo, chuki na fitina na kutaka kupanua ugonvi , awali walisema"amenyanganywa qurani", na wewe unasema "emanuel alikifuata kitabu" mahali klipo hifadhiwa, you can fool some people sometimes buta you cant fool all the people all the times.
 
Ajenti wa ibilisi tena huyu. Yaani unataka kusema kwamba kichaa akikimbia na nguo zako wakati unaoga umkimbize ukiwa uchi? mbona wewe utaonekana kichaa kuliko huyo kichaa mwenyewe. Na hilo amini usiamini ndilo linawapata waislamu sio Tanzania tu bali dunia nzima na kuonekana magaidi tu.
 
What if kama yule dogo angejichizika baada ya kukojolea hiko kitabu, hizo vurugu zingetokea?
 
What if kama yule dogo angejichizika baada ya kukojolea hiko kitabu, hizo vurugu zingetokea?

ndiyo, vurugu zingetokea, tena zaidi ya hizi, wangefanya maandamano ya kusherehekea maajabu ya Kitabu chao na Mungu wao.
 
Penda kuongozwa na hekima ya MUNGU (Hekima ya kiroho).huna

budi kama MUISLAM/Mkristo utofautishe kati ya hekima ya kidunia na Hekimaya kiroho.



· Hekima ya kidunia huambatana na wivu,ubnafsi,chuki,hila na udanganyifu.(Yak 3:14-16 Lakini mkiwa na wivu wenye uchungu na ugomvi mioyoni mwenu,msijisifu,wala msiseme uongo juu ya kweli,hekima hiyo siyo ile ishukayokutoka juu,bali ni ya dunia,ya tabia ya kibinaadamu na shetani,maana hapo palipo wivu na ugomvi ndipo palipo na machafuko,na kila tendo baya).



· Hekima ya kiroho (Yak 3:17-18 Lakini hekima itokayo juu,kwanza ni safi,tena ni ya amani,ya upole,tayari kusikiliza,maneno ya watu,imejaa rehema na matunda mema,haina fitina,haina unafiki,Na tunda la haki hupandwa katika amani na wale wafanyao amani.), huambatana na kuizingatia hali njema ya wengine,kabla ya kujifikiria mwenyewe.Mfano; Mkulima apandaye mbegu nzuri hutegemea mavuno mazuri.Hali kadhalika wakristo/waislam wapandao amani katika uhusiano wao na wenzao wanaweza kutazamia mavuno ya haki katika maisha yao.
 
Wakristo tumezulumiwa na kuonewa tangu mawazo wa ukristo hata sasa tunazulumiwa lakini tupo wala hatujibu mapigo, kwasababu sisi hatupigni vita vya kimwili bali vita vya kiroho.
 
Thread zingine hata unashindwa what to comments coz they are full of s.......
 
Bado haileti maana kwenda kuchoma makanisa na magari ambayo hayakuhusika katika huo ugomvi/mabishano.
 
matunda ya university of morogoro hayo,hivi huyo hapo mtoa mada anaweza akawa na masters kabisa kwa umbumbumbu wa aina hii. wanapanda miti ya machungwa wanavuna minyaanyaaa na miputuputu.
 
Believe me or not in just no days kutaletwa hapa story nyingine tofauti na hii inayodai ndiyo ya ukweli kabisa kuhusu kilichotokea Mbagala
 
Umetumwa si bure maana hizi habari ni za kupika ili kuhalalisha unyama ulofanywa na waislam. Hakika umefel mapema katika hatua ya kwanza wewe na kisiwa. Wakristo ni easoni hawawezi kudanganyika kirahisi hivi. Lol!
 
Back
Top Bottom