Abuu Kauthar
JF-Expert Member
- Jul 10, 2011
- 3,950
- 5,692
Chanzo cha vurugu zilizotokea mwishoni mwa wiki iliyopita katika eneo la Mbagala kizuiani Wilaya ya Temeke jijini Dar-es-Salaam imeelezwa kusababishwa na mama mzazi wa Emmanuel Josephat (14) anayetuhumiwa kukojolea Qur'an kutoa lugha ya kejeli na kashfa dhidi yatukio hilo.
Mama huyo ambaye jina lake halikufahamika mara moja imeelezwa kwamba alikejeli tukio hilo na kugoma kumsikiliza mzazi mwenzie ambaye mwanae alinyang'anywa Qur'an na kusema kwamba yeye alidhani ni jambo la kutisha kama kuua kumbe suala lenyewe ni dogo na lisilo na maana,"nilidhani mwanangu kaua kumbe jambo lenyewe ni hili dogo" alisema mama huyo.
Imeelezwa kwamba mama huyo alikuwa tatizo hadi hapo baba mzazi wa mtoto alinyang'anywa Qur'an Hamis Saluum Mbonde kufika nyumbani kwa mama huyo kutaka kufanya mazungumzo katika kupata ufumbuzi.
Kisiwa limebainishwa kuwa tukio hilo lilitokea siku ya Jumatano Oktoba 10 saa 12 jioni, ambapo vijana hao walianza kubishana juu ya kitabu hicho ndipo Emmanuel aliamua kukikojolea.
Mabishano hayo yalianza baada ya Emmanuel kumuuliza Zakaria maana ya kitabu hicho na alipojibiwa alimweleza kwamba anaweza akafanya chochote na asipatwe lolote.
Baada ya mabishano hayo, walifika katika uwanja wa mpira na kisha Zakaria akatoa mpira wake na kuwapa vijana waliokuwa uwanjani hapo na kuanza kucheza.
Taarifa ziliendelea kusema kuwa baada ya Zakaria kuweka kitabu chake mahala alipoona panafaa aliingia uwanjani na kuanza kucheza mpira na wenzake na mara Emmanuel akaonekana akifungua zipu na kukojolea kitabu hicho.
Akizungumza na Kisiwa wakati vurugu zinaendelea maeneo yote yaliyozunguka kizuiani sambamba na mabomu kirindima kila kona Hamis alisema tukio hilo lisingeweza kuwa kubwa kiasi hiki ama kufikia hivi, bali kilichopelekea kufikia hapo ni kutokana na kauli ya ya mama mzazi wa Emmamuel ambayo ilionekana kizidisha hasira za Waislam.
Hamisi alisema chanzo cha hasira hizo ziliibuka saa chache kabla kijana huyo kupelekwa kituoni wakati baba mzazi wa Zakaria alipokuwa akimsihi mzazi huyo wa Emmanuel ampeleke mwanae police kwa usalama wake.
Hamis aliendelea kusema wakati akihojiwa mama huyo aliwakebehi waliomuuliza na kusikika akisema 'Nilifikiri labda mwanangu kaua!kumbe kakojolea msahafu tu'alisema mama huyo.
Kauli hiyo inatajwa kuwa ndio chanzo cha hasira za waislamu ambapo wwngine walisikika wakilia na kusema 'Mtoeni huyo tumpe adhabu yetu' haiwezekani audhalilishe uislamu namna hii' Hicho ndicho chanzo cha vurugu hizo alisema Hamis.
Hata hivyo alisema kinachotakiwa ni kufanywa sasa ni kuviacha vyombo vya dola vilishughulikie na kuonya kwamba kauli zakejeli dhidi ya Imani ya mtu mwingine hazifai na zisipoangaliwa zinaweza kuleta madhala.
Source: Kisiwa
Mama huyo ambaye jina lake halikufahamika mara moja imeelezwa kwamba alikejeli tukio hilo na kugoma kumsikiliza mzazi mwenzie ambaye mwanae alinyang'anywa Qur'an na kusema kwamba yeye alidhani ni jambo la kutisha kama kuua kumbe suala lenyewe ni dogo na lisilo na maana,"nilidhani mwanangu kaua kumbe jambo lenyewe ni hili dogo" alisema mama huyo.
Imeelezwa kwamba mama huyo alikuwa tatizo hadi hapo baba mzazi wa mtoto alinyang'anywa Qur'an Hamis Saluum Mbonde kufika nyumbani kwa mama huyo kutaka kufanya mazungumzo katika kupata ufumbuzi.
Kisiwa limebainishwa kuwa tukio hilo lilitokea siku ya Jumatano Oktoba 10 saa 12 jioni, ambapo vijana hao walianza kubishana juu ya kitabu hicho ndipo Emmanuel aliamua kukikojolea.
Mabishano hayo yalianza baada ya Emmanuel kumuuliza Zakaria maana ya kitabu hicho na alipojibiwa alimweleza kwamba anaweza akafanya chochote na asipatwe lolote.
Baada ya mabishano hayo, walifika katika uwanja wa mpira na kisha Zakaria akatoa mpira wake na kuwapa vijana waliokuwa uwanjani hapo na kuanza kucheza.
Taarifa ziliendelea kusema kuwa baada ya Zakaria kuweka kitabu chake mahala alipoona panafaa aliingia uwanjani na kuanza kucheza mpira na wenzake na mara Emmanuel akaonekana akifungua zipu na kukojolea kitabu hicho.
Akizungumza na Kisiwa wakati vurugu zinaendelea maeneo yote yaliyozunguka kizuiani sambamba na mabomu kirindima kila kona Hamis alisema tukio hilo lisingeweza kuwa kubwa kiasi hiki ama kufikia hivi, bali kilichopelekea kufikia hapo ni kutokana na kauli ya ya mama mzazi wa Emmamuel ambayo ilionekana kizidisha hasira za Waislam.
Hamisi alisema chanzo cha hasira hizo ziliibuka saa chache kabla kijana huyo kupelekwa kituoni wakati baba mzazi wa Zakaria alipokuwa akimsihi mzazi huyo wa Emmanuel ampeleke mwanae police kwa usalama wake.
Hamis aliendelea kusema wakati akihojiwa mama huyo aliwakebehi waliomuuliza na kusikika akisema 'Nilifikiri labda mwanangu kaua!kumbe kakojolea msahafu tu'alisema mama huyo.
Kauli hiyo inatajwa kuwa ndio chanzo cha hasira za waislamu ambapo wwngine walisikika wakilia na kusema 'Mtoeni huyo tumpe adhabu yetu' haiwezekani audhalilishe uislamu namna hii' Hicho ndicho chanzo cha vurugu hizo alisema Hamis.
Hata hivyo alisema kinachotakiwa ni kufanywa sasa ni kuviacha vyombo vya dola vilishughulikie na kuonya kwamba kauli zakejeli dhidi ya Imani ya mtu mwingine hazifai na zisipoangaliwa zinaweza kuleta madhala.
Source: Kisiwa