GreatConqueror
Member
- Mar 27, 2009
- 75
- 5
Kama kuna kitu kinachokera kuelekea fainali ya mabingwa ulaya mwaka huu ni matangazo yaliyotolewa na yanayotolewa na kituo cha TV cha Channel ten.
Licha ya kuonyesha unazi wa wazi kwa timu mojawapo 'MAN U' na kuitabiria ushindi hatimae kuchukua ubingwa, maneno yanayotumika katika matangazo hayo hayana ustaarabu hata kidogo!!
Mfano kusema Man U itawasambaratisha vijana "wenye sura nzuri wa arsenal". Leo hii wameibuka na tangazo linasema "baada ya kuwaoa na kuwapiga talaka tatu warembo wa arsenal mbele ya wake zao na familia zao MAN UNITED imepeleka posa BARCA".
Hivi kweli kauli hizi za matusi hazikupaswa kuepukwa na kituo kikubwa kama Channel ten? Nina imani hata kituo cha tv cha MAN TV kule UK hakiwezi kutangaza kauli kama hizi!! Nadhani hata mashabiki wastaarabu wa MAN United wameshaona tatizo la matangazo haya.
Tumesikia kuwa mafisadi papa wamekinunua kutuo hiki, nadhani hata wao wasingependa watangazaji watumie unazi na maneno machafu kwenye matangazo yanayolipiwa na wadhamini wastaarabu.
WANAHABARI MSIWE MANAZI WAZI WAZI
Licha ya kuonyesha unazi wa wazi kwa timu mojawapo 'MAN U' na kuitabiria ushindi hatimae kuchukua ubingwa, maneno yanayotumika katika matangazo hayo hayana ustaarabu hata kidogo!!
Mfano kusema Man U itawasambaratisha vijana "wenye sura nzuri wa arsenal". Leo hii wameibuka na tangazo linasema "baada ya kuwaoa na kuwapiga talaka tatu warembo wa arsenal mbele ya wake zao na familia zao MAN UNITED imepeleka posa BARCA".
Hivi kweli kauli hizi za matusi hazikupaswa kuepukwa na kituo kikubwa kama Channel ten? Nina imani hata kituo cha tv cha MAN TV kule UK hakiwezi kutangaza kauli kama hizi!! Nadhani hata mashabiki wastaarabu wa MAN United wameshaona tatizo la matangazo haya.
Tumesikia kuwa mafisadi papa wamekinunua kutuo hiki, nadhani hata wao wasingependa watangazaji watumie unazi na maneno machafu kwenye matangazo yanayolipiwa na wadhamini wastaarabu.
WANAHABARI MSIWE MANAZI WAZI WAZI