Channel Ten: Mchungaji Antony Lusekelo azungumzia Kuchinja!

Status
Not open for further replies.
1-Mkaribisheni kwenu mtu aliye dhaifu, lakini msibishane naye juu ya mawazo yake binafsi.-
2-Watu huhitilafiana: mmoja imani yake inamruhusu kula kila kitu; lakini mwingine ambaye imani yake ni dhaifu, hula tu mboga za majani.-
3-Mtu ambaye hula kila kitu asimdharau yule ambaye hawezi kula kila kitu; naye ambaye hula tu mboga za majani asimhukumu anayekula kila kitu, maana Mungu amemkubali.-
4-Wewe ni nani hata uthubutu kumhukumu mtumishi wa mwingine? Akisimama au akianguka ni shauri la Bwana wake; naam, atasimama imara, maana Bwana anaweza kumsimamisha.
5-Mtu anaweza kufikiria siku fulani kuwa ya maana zaidi kuliko nyingine; mtu mwingine aweza kuzifikiria siku zote kuwa sawa. Kila mmoja na afuate msimamo wa akili yake.-

6-Anayeadhimisha siku fulani anaadhimisha siku hiyo kwa ajili ya kumtukuza Mungu; naye anayekula chakula fulani anafanya hivyo kwa kumtukuza Bwana maana anamshukuru Mungu. Kadhalika naye anayeacha kula chakula fulani anafanya hivyo kwa ajili ya kumtukuza Bwana, naye pia anamshukuru Mungu.-

7-Maana hakuna mtu yeyote miongoni mwetu aishiye kwa ajili yake mwenyewe, wala hakuna anayekufa kwa ajili yake mwenyewe-

8-maana tukiishi twaishi kwa ajili ya Bwana; tukifa, tunakufa kwa ajili ya Bwana. Basi, kama tukiishi au tukifa, sisi ni mali yake Bwana.-

9-Maana Kristo alikufa, akafufuka ili wapate kuwa Bwana wa wazima na wafu.

10-Kwa nini, basi wewe wamhukumu ndugu yako? Nawe,

kwa nini wamdharau ndugu yako? Sisi sote tutasimama mbele

ya kiti cha hukumu cha Mungu.

11-Maana Maandiko yanasema: "Kama niishivyo, asema Bwana kila mtu atanipigia magoti,

na kila mmoja atakiri kwamba

mimi ni Mungu."

12-Kwa hiyo, kila mmoja

wetu atatoa

hoja yake mbele

ya Mungu.

13-Basi, tuache kuhukumiana, bali tuazimie kutokuwa kamwe kikwazo

kwa ndugu yetu au kumsababisha aanguke katika dhambi.-

14-Katika kuungana

na Bwana Yesu, nina hakika kwamba hakuna kitu chochote kilicho najisi

kwa asili yake; lakini, mtu akidhani kwamba kitu fulani

ni najisi, basi, kwake huwa najisi
.-

15-Kama ukimhuzunisha ndugu yako

kwa sababu

ya chakula unachokula, basi mwenendo wako hauongozwi

na mapendo. Usikubali hata kidogo chakula chako kiwe sababu

ya kupotea

kwa mtu mwingine ambaye Kristo alikufa

kwa ajili yake
!
-

16-Basi, msikubalie kitu mnachokiona

kuwa kwenu

ni kitu chema kidharauliwe.-

17-Maana Utawala

wa Mungu si shauri la kula

na kunywa, bali unahusika

na kuwa na uadilifu, amani

na furaha iletwayo

na Roho Mtakatifu.-

18-Anayemtumikia Kristo namna

hiyo humpendeza Mungu,

na kukubaliwa

na watu.-

19-Kwa

hiyo tuyazingatie daima mambo yenye kuleta amani,

na yanayotusaidia kujengana.-

20-Basi, usiiharibu kazi

ya Mungu

kwa sababu

ya ubishi juu

ya chakula. Vyakula vyote

ni halali,

lakini haifai kula chakula ambacho kitamfanya mtu aanguke katika dhambi
.-

21-Afadhali kuacha kula nyama, kunywa divai, au kufanya chochote ambacho chaweza kumsababisha ndugu yako aanguke.-

22-Basi, shikilia unachoamini kati yako

na Mungu wako. Heri mtu yule ambaye, katika kujiamulia la kufanya, haipingi dhamiri yake.-

23-Lakini mtu anayeona shaka juu

ya chakula anachokula, anahukumiwa

kama akila,

kwa sababu msimamo

wa kitendo chake haumo katika imani. Na, chochote kisicho

na msingi wake katika imani

ni dhambi.

?


UPOTOSHAJI. Nionyeshe aya moja inayoongelea chakula kilichotolewa kwa miungu mingine. Hapa inafafanuliwa tofauti ya chakula kati ya wafuasi wa Kristo:

naye anayekula chakula fulani anafanya hivyo kwa kumtukuza Bwana maana anamshukuru Mungu. Kadhalika naye anayeacha kula chakula fulani anafanya hivyo kwa ajili ya kumtukuza Bwana, naye pia anamshukuru Mungu


Tena wakristu wanafundishwa kutohukumiana kwa habari ya tofauti ya vyakula, mfano wale walao kiti moto na wale wanaodhani si sawa. HAKUNA HABARI YA CHAKULA KILICHOTOLEWA KWA MIUNGU WA KIGENI HAPA!

Usikubali hata kidogo chakula chako kiwe sababu

ya kupotea

kwa mtu mwingine ambaye Kristo alikufa

kwa ajili yake
!

Hii ni dhahiri kuwa wanazungumziwa wale walioamini tayari kuwa Kristu ni Bwana. Hebu tazama hii aya inayofuata, je ni kweli kwamba Roho Mtakatifu alikuwa akinena kwa habari ya Ibada za miungu mingine? Shetani ni mjanja sana hata kubadili maandiko!

20-Basi, usiiharibu kazi

ya Mungu

kwa sababu

ya ubishi juu

ya chakula. Vyakula vyote

ni halali,

lakini haifai kula chakula ambacho kitamfanya mtu aanguke katika dhambi
.-

21-Afadhali kuacha kula nyama, kunywa divai, au kufanya chochote ambacho chaweza kumsababisha ndugu yako aanguke.

Je, ewe mkristu uliyeamini, unadhani ukila nyama iliyochinjwa na mwislamu utamsaidia asianguke dhambini?
 
Warumi 14: 1-23, hakuna mstari wa 31

Kwenye kipindi kilicho rushwa na chaneli ten mzee wa Upako ameonyesha kushangazwa na viongozi wa kikristo wanao ng'ang'ania kuchinja. Amesema ""nawashangaa sana wachungaji wenye hoja za kipumbavu eti nani achinje"

"Wanamsumbua waziri mkuu eti kujadili nani achinje wakati nchi ina matatizo lukuki, kwani waislamu walipo kuwa wana chinja ilikuwaje?"

Akaendelea kusema "Tuombee amani tuache hoja za kijinga eti nani achinje nani asichinje".

Aliongea mengi kuonyesha namna ambavyo amani yetu inaweza kutoweka kwa ajili ya mawazo ya kijinga! Amewaomba wakristo kusoma Warumi 14 mstari 1 na 31.

Naomba mwenye biblia atuweke mstari huo unasemaje.
 
Waislamu wengi tunafuatilia kwa karibu mafundisho yenu. Kuna wachungaji wanaohubiri mafundisho mema kwenu kama Mzee wa Upako na Mchungaji Kakobe!

unamaanisha nini kusema mafundisho yenu? nachokiona ni kwamba unasema mafundisho mema kwa sababu yanakubaliana na interests zako, lakini swala la kuchinja kwa namna waislamu mnavyolichukulia ni katika namna inayokandamiza uhuru wa watu wote bila kujali dini zao? kwa sababu kuna watu hawana dini nchi hii na labda hawajali nani anachinja nyama, kwa vyovyote vile hawa hawategemei kuingiliwa na mtu wakati wanachinja vitoweo wao...

Ndio maana mimi kila wakati nasema kwamba, mwenye uwezo wa kumaliza hizi chokochoko ni serikali na ni kwa kusimamia katiba, ambayo inaruhusu mtu kufanya jambo lolote lile isipokuwa asivunje katiba na sheria za nchi. lakini kwa vile wameingia kwenye mtego wa kidini ndio maana sintofahamu imetapakaa.
 
Kwa hiyo umemkubali kwa kuwa amesupport waislamu wachinje au umemkubali kwa sababu maandiko ndivyo yanavyosema? au umemkubali kwa lipi?
 
Naanza kwa kusema mimi sio mshabiki wa mzee wa upako.
Wakristo sasa tunataka kuanza kuendekeza mambo ya kimwili. Hili suala la kuchinja sidhani kama linamjenga mkristo kiroho. Kama tukifikia muafaka kwamba nyama ya mkristo ichinjwe na mkristo na nyama ya muislamu ichinjwe na muislamu ina maana hili litakuwa anguko kubwa sana katika amani ya nchi yetu na kazi ya kuwafikia watu waache dhambi na waje kwa Kristo Yesu aliyesulubishwa kwa ajili yao itakuwa ngumu.
Pata picha, ina maana shughuli (mf. harusi, msiba, n.k ambayo itahusu na kula) ya mkristo itabidi ihudhuriwe na wakristo tu na hivyo kwa upande wa waislamu. Tukitoka hapo, tutafuata na mambo mengine kama wimbo wa taifa n.k.
Walioanzisha huu mjadala wa nani achinje walitakiwa wajue pia madhara yake ya muda mrefu.
Na wale wanaoona kwamba hawawezi kula nyama ilichinjwa na mwislamu wajichinjie wenyewe kimya kimya na sio kuhamasisha wengine katika suala litakalotenganisha Taifa letu. Na tena kwa kuwa wamegundua ni dhambi, basi wanatakiwa watubu kwa ajili ya zile nyama walizokula siku za nyuma (hata kama walikuwa hawajui kwamba ni dhambi) pamoja na dhambi nyingine kama kuzini, kudanganya, kuiba, kufanya uasherati, kusengenya, kumatamani mtu kimapenzi, n.k. Hapo ndio wataonekana wapo makini na sio kung'ang'ania kuchinja tu.

Kwa hiyo basi, tufanye kila juhudi tutimize yale yaletayo amani na kujengana. Usiiharibu kazi ya Mungu kwa ajili ya chakula. Vyakula vyote vinafaa, lakini ni kosa kula kitu ambacho kinamfanya mwenzako kujikwaa. Ni afadhali usile nyama wala kunywa divai au kufanya jambo lingine lo lote litakalomfanyandugu yako aanguke. Unavyoamini kuhusu mambo haya, iwe ni siri yako na Mungu. Amebarikiwa mtu ambaye hajisikii kuhukumiwa afanyapo jambo analoamini kuwa ni sawa. Lakini mtu mwenye mashaka kuhusu anachokula, amehukumiwa ikiwa atakula, kwa sababu kula kwake hakutokani na imani. Kwa maana jambo lo lote ambalo halito kani na imani, ni dhambi (Warumi 14:19-23)
 
Naanza kwa kusema mimi sio mshabiki wa mzee wa upako.
Wakristo sasa tunataka kuanza kuendekeza mambo ya kimwili. Hili suala la kuchinja sidhani kama linamjenga mkristo kiroho. Kama tukifikia muafaka kwamba nyama ya mkristo ichinjwe na mkristo na nyama ya muislamu ichinjwe na muislamu ina maana hili litakuwa anguko kubwa sana katika amani ya nchi yetu na kazi ya kuwafikia watu waache dhambi na waje kwa Kristo Yesu aliyesulubishwa kwa ajili yao itakuwa ngumu.
Pata picha, ina maana shughuli (mf. harusi, msiba, n.k ambayo itahusu na kula) ya mkristo itabidi ihudhuriwe na wakristo tu na hivyo kwa upande wa waislamu. Tukitoka hapo, tutafuata na mambo mengine kama wimbo wa taifa n.k.
Walioanzisha huu mjadala wa nani achinje walitakiwa wajue pia madhara yake ya muda mrefu.
Na wale wanaoona kwamba hawawezi kula nyama ilichinjwa na mwislamu wajichinjie wenyewe kimya kimya na sio kuhamasisha wengine katika suala litakalotenganisha Taifa letu. Na tena kwa kuwa wamegundua ni dhambi, basi wanatakiwa watubu kwa ajili ya zile nyama walizokula siku za nyuma (hata kama walikuwa hawajui kwamba ni dhambi) pamoja na dhambi nyingine kama kuzini, kudanganya, kuiba, kufanya uasherati, kusengenya, kumatamani mtu kimapenzi, n.k. Hapo ndio wataonekana wapo makini na sio kung'ang'ania kuchinja tu.

Kwa hiyo basi, tufanye kila juhudi tutimize yale yaletayo amani na kujengana. Usiiharibu kazi ya Mungu kwa ajili ya chakula. Vyakula vyote vinafaa, lakini ni kosa kula kitu ambacho kinamfanya mwenzako kujikwaa. Ni afadhali usile nyama wala kunywa divai au kufanya jambo lingine lo lote litakalomfanyandugu yako aanguke. Unavyoamini kuhusu mambo haya, iwe ni siri yako na Mungu. Amebarikiwa mtu ambaye hajisikii kuhukumiwa afanyapo jambo analoamini kuwa ni sawa. Lakini mtu mwenye mashaka kuhusu anachokula, amehukumiwa ikiwa atakula, kwa sababu kula kwake hakutokani na imani. Kwa maana jambo lo lote ambalo halito kani na imani, ni dhambi (Warumi 14:19-23)

Ndugu, umesoma hoja ili kujua ni nini hasa ambacho wakristu hawataki? Unaonaje kama Quran ikapitishwa kuwa katiba ya nchi ili kudumisha umoja wetu na kuondoa mikanganyiko?
 
Ndugu, umesoma hoja ili kujua ni nini hasa ambacho wakristu hawataki?
Naelewa wana hoja ya msingi, ila sio kipaumbele cha muhimu kwa sasa na sioni sababu ya kuhasisha wakristo wote katika suala kama hili. Yaani mwisho wa siku, kama ikiamuliwa kuwe na mabucha ya kikristo na kiislamu utakuwa ni mwanzo wa utengano wa kudumu. Haya mambo hayataaishia hapa jamani
 
Naelewa wana hoja ya msingi, ila sio kipaumbele cha muhimu kwa sasa na sioni sababu ya kuhasisha wakristo wote katika suala kama hili. Yaani mwisho wa siku, kama ikiamuliwa kuwe na mabucha ya kikristo na kiislamu utakuwa ni mwanzo wa utengano wa kudumu. Haya mambo hayataaishia hapa jamani

Tujifunze kwa nchi nyingine. Hili si jambo geni ila hapa kwetu tu. Mungu atakuwa kipaumbele cha kwanza daima kuliko mawazo binafsi. Ni kwa sababu hizo leo hii kuna mashahidi wa imani. Tofauti ya waislamu na wakristu baadhi ni kuwa waislamu husimamia kile wanachokiamini wakati baadhi ya wakristu hupima upepo hata kama ni kwa gharama ya kumkana Mungu wanayemwamini. Siko tayari kuwa sehemu ya ibada ya Allah ili tu kuwaridhisha wanadamu na kumwasi Mungu.
 
Ukiniona MZIMU nimemkubali Mtu, jua huyo mtu anastahili. Jamani kwa watu wenye akili, hakuna suluhu nyengine itakayo linda Amani ya Nchii hii zaidi ya hiyo alioitoa Mchungaji Antony Lusekelo. Kwani hayo hayo ndio anayo yaongelea Mzee Pinda na Mzee Steven Wasira.

Kama kuna mkristo yoyote anapingana na huyu mchungaji, hakika huyo ndio asie itakia Mema Nchi hii.
Kwa hiyo mzee wa upako ndo umemwona anawakilisha imani sahihi ya kikristo? na kwa nini unataka wakristo peke yao ndo waridhie kila kitu ila isiwe waislamu. Kama waislamu wanaona wakristo wakichinja inawaathiri imani yao, vivo hivyo na kwa wakristo kwani wamekatazwa kutumia vyakula vilivyotolewa sadaka kwa miungu wasioijua.
 
1-Mkaribisheni kwenu mtu aliye dhaifu, lakini msibishane naye juu ya mawazo yake binafsi.-
2-Watu huhitilafiana: mmoja imani yake inamruhusu kula kila kitu; lakini mwingine ambaye imani yake ni dhaifu, hula tu mboga za majani.-
3-Mtu ambaye hula kila kitu asimdharau yule ambaye hawezi kula kila kitu; naye ambaye hula tu mboga za majani asimhukumu anayekula kila kitu, maana Mungu amemkubali.-
4-Wewe ni nani hata uthubutu kumhukumu mtumishi wa mwingine? Akisimama au akianguka ni shauri la Bwana wake; naam, atasimama imara, maana Bwana anaweza kumsimamisha.
5-Mtu anaweza kufikiria siku fulani kuwa ya maana zaidi kuliko nyingine; mtu mwingine aweza kuzifikiria siku zote kuwa sawa. Kila mmoja na afuate msimamo wa akili yake.-

6-Anayeadhimisha siku fulani anaadhimisha siku hiyo kwa ajili ya kumtukuza Mungu; naye anayekula chakula fulani anafanya hivyo kwa kumtukuza Bwana maana anamshukuru Mungu. Kadhalika naye anayeacha kula chakula fulani anafanya hivyo kwa ajili ya kumtukuza Bwana, naye pia anamshukuru Mungu.-

7-Maana hakuna mtu yeyote miongoni mwetu aishiye kwa ajili yake mwenyewe, wala hakuna anayekufa kwa ajili yake mwenyewe-

8-maana tukiishi twaishi kwa ajili ya Bwana; tukifa, tunakufa kwa ajili ya Bwana. Basi, kama tukiishi au tukifa, sisi ni mali yake Bwana.-

9-Maana Kristo alikufa, akafufuka ili wapate kuwa Bwana wa wazima na wafu.

10-Kwa nini, basi wewe wamhukumu ndugu yako? Nawe,

kwa nini wamdharau ndugu yako? Sisi sote tutasimama mbele

ya kiti cha hukumu cha Mungu.

11-Maana Maandiko yanasema: "Kama niishivyo, asema Bwana kila mtu atanipigia magoti,

na kila mmoja atakiri kwamba

mimi ni Mungu."

12-Kwa hiyo, kila mmoja

wetu atatoa

hoja yake mbele

ya Mungu.

13-Basi, tuache kuhukumiana, bali tuazimie kutokuwa kamwe kikwazo

kwa ndugu yetu au kumsababisha aanguke katika dhambi.-

14-Katika kuungana

na Bwana Yesu, nina hakika kwamba hakuna kitu chochote kilicho najisi

kwa asili yake; lakini, mtu akidhani kwamba kitu fulani

ni najisi, basi, kwake huwa najisi.-

15-Kama ukimhuzunisha ndugu yako

kwa sababu

ya chakula unachokula, basi mwenendo wako hauongozwi

na mapendo. Usikubali hata kidogo chakula chako kiwe sababu

ya kupotea

kwa mtu mwingine ambaye Kristo alikufa

kwa ajili yake!-

16-Basi, msikubalie kitu mnachokiona

kuwa kwenu

ni kitu chema kidharauliwe.-

17-Maana Utawala

wa Mungu si shauri la kula

na kunywa, bali unahusika

na kuwa na uadilifu, amani

na furaha iletwayo

na Roho Mtakatifu.-

18-Anayemtumikia Kristo namna

hiyo humpendeza Mungu,

na kukubaliwa

na watu.-

19-Kwa

hiyo tuyazingatie daima mambo yenye kuleta amani,

na yanayotusaidia kujengana.-

20-Basi, usiiharibu kazi

ya Mungu

kwa sababu

ya ubishi juu

ya chakula. Vyakula vyote

ni halali,

lakini haifai kula chakula ambacho kitamfanya mtu aanguke katika dhambi.-

21-Afadhali kuacha kula nyama, kunywa divai, au kufanya chochote ambacho chaweza kumsababisha ndugu yako aanguke.-

22-Basi, shikilia unachoamini kati yako

na Mungu wako. Heri mtu yule ambaye, katika kujiamulia la kufanya, haipingi dhamiri yake.-

23-Lakini mtu anayeona shaka juu

ya chakula anachokula, anahukumiwa

kama akila,

kwa sababu msimamo

wa kitendo chake haumo katika imani. Na, chochote kisicho

na msingi wake katika imani

ni dhambi.

?

hili ndilo neno
 
Unaezungumzia maandaki,shari au vita!!
Nikuhakikishie kikinuka apa TZ hutotoa pua yako nje ya kizingit cha mlango wako,watu wapo vzuri sio kelele masaa 24.
Prove Ilunga,Ponda(mrundi) sio magaid?
Dini imekosa Hekima na Elimu ndani yake,kila m2 mjuaji.
:(
 
Kwa ujumla post yenyewe imekaa ki-udini udini...sijaipenda! Unapozungumzia Mch.A.Lusekelo amefafanua sana, ulitakiwa ueleze alichofafanua ni nini na si kueleza mitazamo yake ya kisiasa na kutaka kuitunza amani kwa kuvunja sheria, binafsi siku zote huwa naamini 'Sheria ni haki' so kama Wakristo ... sheria zetu zipo kwenye BIBLIA na tungependa kusikia kutoka kwake BIBLIA inasemaje kuhusu kuchinja na si vinginevyo ... Kazi yake kubwa ni kutufundisha BIBLIA inasemaje kuhusu kuchinja na si kutoa maoni yake binafsi kuhusu amani na kuchinja.

Siamini kama Waislamu wanahitaji upendeleo wa kuchinja, la hasa, wanapigania haki yao iliyoandikwa kwenye vitabu vyao vya dini hivyo kusema waachwe wachinje ni kuwadharau huku wengine tukijifanya ni mambumbumbu, je, sheria za dini zenu (Ukristo, Buddha e.t.c) zinasemaje kuhusu kuchinja? Vipi kuhusu uchinjaji wa kibiashara wa 'mkuu wa meza' nao ubaki kwa waislamu?! Ningefurahi kuona na watu wa dini nyingine wakichangia kwa kushabikia uzi huu na si tu Mwamakula MZIMU Mohamedi Mtoi

Kwa uliyoyaandika, Mch.A.Lusekelo seem to be bias, myopia, selfish na pengine anawakilisha mawazo yake binafsi .... tunahitaji kujua vitabu vya dini nyingine vinasemaje that all. Msisahau, 'Two wrongs, dont make it right'.
 
Last edited by a moderator:
nimewahi kusikia haya kwenye mahubiri ya wa Upako kupitia channel ten "nina magari sita siyo ya japan, nina Range Rover sport, nina BMW X5, nina Landrover Discovery....nikiamka asubuhi naangalia kwenye parking niendeshe lipi!!! halafu nilivyo na mkwara kwenye gari nakua peke yangu, kama wewe unakuja kanisani kwangu na haujafanikiwa umekaa mwaka wa kwanza,wa pili na haujanunua usafirii! basi wewe hutoi dhaka, hutoi fungu la kumi ndo maana hufanikiwi, Yesu hakutembea na malofa...."~Mzee wa upako aka SMG, ha ha haaaa.

Hii niliisikia bana!!

Mzimu, hili suala alilozungumza ndugu yangu hapo juu uliisikia?
 
Namsikiliza Mchungaji Antony Lusekelo Chanel Ten sasa hivi. Nimemkubali huyu kweli ni kiongozi sahihi katika Imani ya Kikristo. Tukiwa na Viongozi wa kama hawa Amani yetu ya inchi haiwezi kutetereka.

Heshima kwako Mchungaji. Natamani Wachungaji, Mapdre na Maaskofu pamoja na Makidanali wote Muwe na upeo mkubwa wa kufikiria kama huyu Mchungaji. Huyu ni Tunu ya nchi.

Kwa ufupi tu, Mchungaji Antony Lusekelo Ameshangaa kulikoni leo Mashekhe na Maaskofu au Mapadre au Wachungaji wagombane wakati waliishi kwa amani tangu zamani. Kama ni suala la kuchinja, mbona suala hilo tangu enzi ya wazee wetu, walikua wanachinja waislamu wanakula wote. "Kama tukichinja sisi waislamu hawali, basi wachinje waislamu tule wote. Kuchinja isiwe ndio sababu ya kuvunja amani ya nchi yetu".

Ameeleza kwa kirefu suala hilo. Hiyo ndio ilikua mada ya kipindi.

Huyu nimekua nikifuatilia mahubiri yake, huyu kweli anawakilisha imani sahihi ya kikristo. Mimi sio Mkristo mimi ni Muislamu, ila hua tuna wapenda viongozi kama hawa katika jamii. Sio vizuri sisi watanzania kutengana kimisingi ya dini. Ni vibaya na hatari sana. Familia nyingi ni mchanganyiko.

Huyu jamaa ni kati ya wachungaji wazuri tulionano, inabidi tuwatumie vizuri. Nampenda, na ana upeo mkubwa. Hata linapokuja swala la kuongelea issue zisizokuwa za dini, huwa anaongea anakuja ana-link na maandiko matakatifu halafu anamaliza kila kitu. Zaidi ya yote, ni mpenda amani sana, kila inapotokea issue ambayo ni burning, lazima ataiongelea.
 
Nyama nyama tu achinje mkristu au mwislam ni nyama tu, Mabucha yote tuanayo nunua nyama hata hatuulizi zimechinjwa na nai na wapi .
Au zinakuwa na alama?
 
Kila mmoja amepewa karama, wengine karama ya kuimba, wengine karama ya kucheza, wengine karama ya kufundisha, wengine karama ya kujifunza na hawa wengine karama ya KUCHINJA.
Acheni wachinje na wale kwa madhabahu yao, kitoweo kitolewacho kama ibada kilihitimishwa pale Yesu alipotundikwa juu ya Msalaba Mtakatifu kilichobaki hakuna tena IBADA HIYO.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom