Serikali kutafuta dawa ya kansa ya kizazi

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,319
33,125
jk%20kampeni2.jpg
Jakaya Mrisho Kikwete

Burhani Yakub,
Tanga

SERIKALI imesema katika kipindi cha miaka mitano
ijayo, Serikali yake itaelekeza nguvu zake kupambana na tatizo la kansa ya shingo ya kizazi ili kuokoa vifo vingi kwa wanawake.

Hayo yalisemwa na Rais Jakaya Kikwete wakti akitoa ahadi hiyo jana alipokuwa akizungumza na wakazi wa Jiji la Tanga wakati wa mkutano wake wa kampeni uliofanyika katika uwanja wa Mkwakwani.

Alisema kutokana na kansa ya shingo ya kizazi kwa kuwa ni tatizo kubwa, Serikali imeamua kuelekeza nguvu zake katika
kutafuta chanjo ya uhakika ili kuonda kabisa tatizo hilo.

“Chanjo ya kansa ya shingo ipo,katika nchi za wenzetu,hivyo na sisitumeona hatuwezi kuachia wanawake wazidi kuteketea tutaifuata iliko ili tatizo hilo baadaye liweze kutoweka nchini,”alisema Kikwete.

Alisema matayarisho ya kutoa chanjo hiyo, imeanza na kwamba ifikapo mwakani wanawake wataanza kuchanjwa ili wasiweze kupata maradhi hayo.
Rais Kikwete alidokeza kuwa Serikali imejenga maabara kubwa na ya kisasa katika hospitali ya Mkoa wa Tanga ya Bombo ambayo ina uwezo wa kupima aina mbalimbali za magonjwa.

“Maabara ya Bombo ni kubwa na ya kisasa yenye uwezo wa kupima magonjwa mbalimbali,”alisema.
Alisema maabara hiyo imetolewa kwa msaada wa taaisi ya ABBOT ya Marekani na Serikali kuamua ijengwe katika Hosptaliya Bombo.

Kuhusu ugonjwa wa malaria, Rais Kikwete alisema tayari serikali imepokea idadi ya vyandarua 14,000,000 na
kwamba itahakikisha kila kaya inapewa ili kutokomeza ugonjwa wa
malaria.

chanzo : Serikali kutafuta dawa ya kansa ya kizazi
 
"alisema.
Alisema maabara hiyo imetolewa kwa msaada wa taaisi ya ABBOT ya Marekani na Serikali kuamua ijengwe katika Hosptaliya Bombo.

Hili jamaa ongo sana! Jamaa wa Abbot waliamua kujenga hiyo maabara Tanga sababu wana kazi zao na NIMR Tanga, wasingekubali kujenga sehemu nyingine yeyote (Bagamoyo) kwa shinikizo la serikali. Wanamaabara nyingine nzuri tu pale Muhimbili kule Bacteriology, sababu kuna tafiti za Wamarekani kutoka Havard. Wananchi wamedanganywa eti serikali iliamua, this is very low again from Kikwete! Siajabu kwa kauli hii ya uwongo wananchi walishangilia
 
Hili jamaa ongo sana! Jamaa wa Abbot waliamua kujenga hiyo maabara Tanga sababu wana kazi zao na NIMR Tanga, wasingekubali kujenga sehemu nyingine yeyote (Bagamoyo) kwa shinikizo la serikali. Wanamaabara nyingine nzuri tu pale Muhimbili kule Bacteriology, sababu kuna tafiti za Wamarekani kutoka Havard. Wananchi wamedanganywa eti serikali iliamua, this is very low again from Kikwete! Siajabu kwa kauli hii ya uwongo wananchi walishangilia
mkuu kuna long term strategy ya supplies and services contracts let alone philanthropic deed.... abbott is not only building hizi lab tanga, hata mnh wamefanya hivyo na kama unakumbuka prof lema alidai hawawezi tumia baadhi ya mashine... hii si siasa mazee
 
mkuu kuna long term strategy ya supplies and services contracts let alone philanthropic deed.... abbott is not only building hizi lab tanga, hata mnh wamefanya hivyo na kama unakumbuka prof lema alidai hawawezi tumia baadhi ya mashine... hii si siasa mazee

Jamaa hana mpya ameamua kuingiza kwenye ahadi zake kisiasa! Kule CPL (Central Pathology Lab) jamaa wa Abbott wametengeneza maabara ya kisasa sana pale Muhimbili hospital nadhani ni miongoni mwa maabara nzuri nchini. Wanafanya serology tests nyingi tu,bacteriology tests na hata molecular assays. Jamaa kila kitu kizuri wanaweka kisiasa. Nakumbuka sana Prof Lema na hadithi zake, kinachotakiwa pale ni kuwapa vijana ajira na malipo ya kueleweka wafanye kazi. Nadhani Dir wa ile maabara ni dada mmoja wa South Afrika.
 
Akiwa kwenye ziara yake ya kanda ya ziwa na kwingineko, nimemsikia jk akiahidi kutoa chanjo ya saratani ya shingo ya kizazi kwa akina mama wote. Hii nayo ni kati ya zile ahadi zisizotekelezeka za mheshimiwa huyu kwa sababu:

1) chanjo hii hutolewa kwa watu ambao hawajapata maambukizi ya virusi vya HPV ambavyo ndio husababisha saratani hii na virusi hivi huenezwa kwa njia ya zinaa, kwa hiyo hutolewa kwa wasichana/wanawake ambao hawajaanza mahusiano ya kimapenzi. Umri unaopendekezwa ni kati ya miaka 9 - 16, kwa hiyo kusema akina mama wote watapatiwa chanjo hii si sahihi. Na hawa si wapiga kura (9 - 16), so akina mama wanadanganywa. Kama umeshakuwa na mahusiano haikusaidii kwa kuwa asilimia 90% ya akina mama tayari huwa na maambukizi wanapokuwa kwenye mahusiano.

2) chanjo hii ni gharama sana, kwa tanzania inapatikana chanjo ambayo ni 'bivalent' ambayo dose moja ni sh 45,000/- na mtu mmoja anahitaji dose tatu kila miaka mitatu, kwa matumizi haya ya serikali ya jk ya anasa kuliko maendeleo na afya hawataweza kuafford, labda waniambie kama bush or sorry obama ameahidi kutoa chanjo hii bure, vinginevyo hiki nacho ni kiini macho.

Ningependa kumshauri mh. Jk, aahidi ku-raise awareness juu ya saratani ya shingo ya kizazi ambayo ndiyo saratani inayoongoza kwa kuua akina mama wengi tanzania kuliko saratani nyingine yoyote na kwamba akina mama wawe na tabia ya kucheck afya zao, hii inaweza kusaidia kugundulika viashiria vya saratani hii au saratani yenyewe katika hatua za awali ambazo zinaweza kutibika tena kwa gharama ndogo kuliko hiyo chanjo.

Jk asitumie ignorance ya watanzania kuomba kura, najua hili la chanjo ya kizazi labda kashauriwa lakini kwa mara nyingine tena kaingizwa chaka.
 
Mkuu nadhani kama ulivyosema JK akiongea huwa haelewi vyema anachokisema. Kwa mara nyingine tena tunawalaumu washauri wake! Alichotakiwa ni kuhamasisha na kutoa fursa ya wanawake kupima hii saratani. Na labda kwa kuwa kuna ofa ya kampeni angesema wanawake watapimwa hii saratani bure kwa mwaka mara moja. Atenge fungu kwa ajili hivyo. Pili, kuhusu hiyo ya chanjo inawezekana tukiacha anasa na pale tunapoangalia kuwa taifa linaanzia hapo kwenye kizazi.
Pamoja na mateso mengine, ni kweli kabisa hii saratani inawatesa sana wanawake wa Tanzania
 
Ugomvi wangu ni kwamba hivi hakuna watu ambao huwa wanamshauri kabla ya muheshimiwa huyu kuongea kuuza chai na kahawa jukwaani kwa bei ambayo hata mtu wa "Kariakoo" ataielewa.???
 
Kapotolo unachosema ni kweli. Chanjo, japo kuna ubishi hata nchi za nje jinsi ya kuigharimia, ni ghali. Kinachotakiwa ni kuwataka wanaume pia wapime uwepo wa vimelea vyake, kwa kuwa ngono ndio inayoambukiza ugonjwa huu!!
 
Inawezekana wanamweleza vitu sahihi ila anasahau, haiwezekani kila kitu tuwasingizie wasaidizi wake.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom