Changia CHADEMA; M4C

Wewe mkubwa, unaye jiita "Tume ya Katiba" ni lini,na wapi,saa ngapi ukaichangia CHADEMA?......huo ndio unafiki wa mchana kweupe
 
CHADEMA ni freemasons?
sasa tumejua,
WASABATO TUKO WAPI?

Lengo lako ni kuwafitinisha Wasabato na CDM au kutangaza ujumbe wa malaika wa tatu. Wazo zuri limetolewa kutekeleza nia mbaya. Kwa hili tunaomba Wasabato uwaache kwani wanajua wito wao nadhani si huu.
 
mimi natuma hela hata kama watazipigia bia sijali wala sitaki kujua matumizi.
Mapato na matumizi ni kuiangusha ccm.
 
kama kuna hela tume ya katiba amechangia naomba aseme ni shilingi ngapi bora arudishiwe hili gamba
 
Ukombozi wa nchi hii utafanywa na Watanzania wenyewe,wenye moyo. Ukiona mtu anahojihoji hivyo wakati anaona kazi inayofanyika tambua huyo kaathiriwa na kofia na T-shirt za kijani. Wengi wamejengewa tabia mbaya ya kupewa....... Na hao NYINYI.M, na siyo wao kuchangia chama.
 
Najua wewe sio chadema! Au hauko serious!

Ndugu yangu warea; hata kama mimi sio CHADEMA, tunachokitaka hapa ni mabadiliko. Kodi zetu zinatumika vibaya, rasilimali zetu zinaibiwa mchana kweupe, twiga wanapakia ndege, viwanja vya ndege migodini, watanzania tumeendelea kubaki maskini. Leo hii Chadema kimedhihirisha pasipo na shaka kwamba kinaweza kuisimamia na kuiwajibisha serikali endapo tu wananchi/walalahoi tutakiunga mkono. Shime tuungane pamoja. Vita yetu ni dhidi ya udhalimu na ufisadi, umaskini kwenye nchi yenye maliasili, dhahabu, alamasi na Tanzanite nyingi. Itoshe kusema sasa hatudanganyiki
 
i have just sent my contribution to CHADEMA and hope this small contribution will help in bringing change in my country
 
Changia CHADEMA kupitia M-PESA kufanikisha Vuguvugu la Mabadiliko nchi nzima

Chadema ina takribani wanachama milioni mbili. Kila mmoja akichangia angalau shs 1,000/- kwa mwezi, M4C inapata Bilioni 2. Hii ni mara 10 ya ruzuku inayopata Chadema kwa mwezi. Mara 10!
Kuwa sehemu ya mabadiliko na kuwa upande sahihi wa historia. Waweza kuchangia kiasi chochote kile mara nyingi kadri unavyopenda. Wajulishe wengine pia kuhusu habari hii

Jinsi ya kuchangia:

Bonyeza *150*00#
Chagua 4. Lipa bili yako
Chagua 1. Ingiza namba ya kampuni
Ingiza namba ya kampuni (111 333)
Ingiza namba ya kumbukumbu. (Namba yako ya simu)
Ingiza kiasi (Kiasi chochote kuanzia 1,000 mpaka 1,000,000)
Ingiza namba ya siri (Namba yako ya siri)
Thibitisha kwa kubonyeza 1 au batilisha kwa kubonyeza 2.




mkuu sisi tumeshachangia sana na hatuchoki. Pamoja sana!
 
Changia CHADEMA kupitia M-PESA kufanikisha Vuguvugu la Mabadiliko nchi nzima

Chadema ina takribani wanachama milioni mbili. Kila mmoja akichangia angalau shs 1,000/- kwa mwezi, M4C inapata Bilioni 2. Hii ni mara 10 ya ruzuku inayopata Chadema kwa mwezi. Mara 10!
Kuwa sehemu ya mabadiliko na kuwa upande sahihi wa historia. Waweza kuchangia kiasi chochote kile mara nyingi kadri unavyopenda. Wajulishe wengine pia kuhusu habari hii

Jinsi ya kuchangia:

Bonyeza *150*00#
Chagua 4. Lipa bili yako
Chagua 1. Ingiza namba ya kampuni
Ingiza namba ya kampuni (111 333)
Ingiza namba ya kumbukumbu. (Namba yako ya simu)
Ingiza kiasi (Kiasi chochote kuanzia 1,000 mpaka 1,000,000)
Ingiza namba ya siri (Namba yako ya siri)
Thibitisha kwa kubonyeza 1 au batilisha kwa kubonyeza 2.



[ shukran sana ndugu, nadodosha kitu sasa hv, nilijaribu sana nikawa nashindwa]
 
Back
Top Bottom