EMT
Platinum Member
- Jan 13, 2010
- 14,483
- 15,308
Tarehe 19 Julai 2011, Kamati ya Bunge la Uingereza ya Maendeleo ya Kimataifa itaanza kuchunguza kwa nini bado BAE Systems haijarudisha change ya radar kwa Watanzania. Kamati hiyo itataka kujua ni kwa nini mpaka sasa (baada ya miezi saba tokea kesi imalizike) BAE System bado haijarudisha hiyo change. Kamati ya bunge itataka kujua pia BAE Systems imehakikishaje pindi change hiyo itakaporudishwa itatumika kwa ajili ya maendeleo Tanzania. Pia kamati itataka kujua BAE System imepokea ushauri gani kutoka Wizara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza juu ya matumizi ya change pindi itakaporudishwa Tanzania.
Kamati itawahoji maafisa wa ngazi za juu wa wizara hiyo, BAE Systems and SFO. Nategemea kwenye meeting kutakuwepo na wawakilishi toka serikali ya Tanzania wakiongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje, Mh Bernard Membe na wanasheria kadhaa. Inawezekana hili ndilo limemfanya Mh Membe asiongozane na Rais Kikwete kwenye kongamano Afrika kusini? Ikumbukwe wale wabunge wetu waliokwenda London walishindwa kabisa kuishawishi serikali ya Uingereza kuilazimisha BAE Systems irudishe change kupitia serikali ya Tanzania.
Kwa sababu hiyo, serikali ya Tanzania imetishia kuishtaki BAE Systems mwezi wa tisa mwaka huu kama change itakuwa bado haijarudishwa. Ushauri wa kuchukua hatua za kisheria ulitolewa na Naibu Spika Job Ndungai. Ndungai aimeishauri serikali kuchukua hatua za kisheria dhidi ya BAE Systems hata kama change hiyo itarudishwa kupitia NGOs za Kiingereza au hata zile za Kitanzania. Hata hivyo, tayari BAE Systems imeshaandaa list inayojulikana kama "like-minded British NGOs who, through their work, witness the devastating effects of corruption on developing countries every day" kupokea hiyo change.
Akiongea na gazeti la The East African, Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma, Mh Kabwe Zitto amesema kuwa hiyo change sio "reparation" bali ni "refund" ambayo ililipwa kununua bidhaa ambayo haukuwa "fit for purpose". Mh Zitto anasema change irudishwe kupitia bunge ili isaidie ku "promote transparency". Gazeti halikufafanua Zitto anataka change hiyo itumike ku "promote transparacy" kivipi na wapi. Kwa maneno mengine, Zitto anasema kuwa tunachorudishiwa hapa sio change bali ni pesa yote tuliyolipa kununua ile radar na kwamba pesa hiyo itumike ku "promote transparency".
UPDATE: Majadiliano ya Kamati ya Bunge la Uingereza jana kuhusu malipo ya change: Credit to Mwanakijiji.
Kamati itawahoji maafisa wa ngazi za juu wa wizara hiyo, BAE Systems and SFO. Nategemea kwenye meeting kutakuwepo na wawakilishi toka serikali ya Tanzania wakiongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje, Mh Bernard Membe na wanasheria kadhaa. Inawezekana hili ndilo limemfanya Mh Membe asiongozane na Rais Kikwete kwenye kongamano Afrika kusini? Ikumbukwe wale wabunge wetu waliokwenda London walishindwa kabisa kuishawishi serikali ya Uingereza kuilazimisha BAE Systems irudishe change kupitia serikali ya Tanzania.
Kwa sababu hiyo, serikali ya Tanzania imetishia kuishtaki BAE Systems mwezi wa tisa mwaka huu kama change itakuwa bado haijarudishwa. Ushauri wa kuchukua hatua za kisheria ulitolewa na Naibu Spika Job Ndungai. Ndungai aimeishauri serikali kuchukua hatua za kisheria dhidi ya BAE Systems hata kama change hiyo itarudishwa kupitia NGOs za Kiingereza au hata zile za Kitanzania. Hata hivyo, tayari BAE Systems imeshaandaa list inayojulikana kama "like-minded British NGOs who, through their work, witness the devastating effects of corruption on developing countries every day" kupokea hiyo change.
Akiongea na gazeti la The East African, Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma, Mh Kabwe Zitto amesema kuwa hiyo change sio "reparation" bali ni "refund" ambayo ililipwa kununua bidhaa ambayo haukuwa "fit for purpose". Mh Zitto anasema change irudishwe kupitia bunge ili isaidie ku "promote transparency". Gazeti halikufafanua Zitto anataka change hiyo itumike ku "promote transparacy" kivipi na wapi. Kwa maneno mengine, Zitto anasema kuwa tunachorudishiwa hapa sio change bali ni pesa yote tuliyolipa kununua ile radar na kwamba pesa hiyo itumike ku "promote transparency".
UPDATE: Majadiliano ya Kamati ya Bunge la Uingereza jana kuhusu malipo ya change: Credit to Mwanakijiji.
Last edited by a moderator: