Changamoto kwa Waandishi wa Habari: (Mwandosya & Mwakyembe Kuundiwa Mzengwe)

Mtanzania umesema kweli na ninaamini kuna mambo machache ambayo mwandishi asiyachukulie at face value au kuyakubali tu. Kwa mfano Rais aliposema "watu hawali mapanki" au pale aliposema "BAE ni kampuni ya Serikali ya Uingereza" waandishi hawana budi kuangalia kauli hizo na kuhakikisha ukweli wake. Mtu anaposema fulani ni mwanachama wa chama fulani ni bora uhakikishe anachosema ni sahihi. Nakubaliana na wewe 100% kwamba ni jukumu la wale wanaoandika habari au maoni to be as accurate as humanly possible especially ambapo ni rahisi kuverify certain information.

Nina tatizo hata hivyo na mahitimisho yako kadhaa.



Kudai kuwa habari nzima ni uongo mtupu nafikiri ni exaggeration of the first order. Nadhani umeweza kuonesha ni yapi ambayo factually are just simply wrong. Hayo yanayohusiana na facts ni rahisi kuyaweka sawa. Kama hili:





Nadhani hapa itakuwa ni maneno yako against maneno yao; kwanini tuamini kuwa vita hivyo havipo? aidha kwa sababu havipo au kwa vile umesema havipo?



Hapa inabidi watu waamini "sources" zako ambazo ni unnamed na hatujui zina maslahi gani katika pande zinazohusika. How balanced are you sources? Maana hilo gazeti na wenyewe wanasema wana "sources" zao hapo hapo Mbeya. Kwanini sources zako ziaminike zaidi ya sources zao?



Hili nadhani ni kweli kabisa; lakini it is the nature of the beast. Siasa ni moves, counter moves na moves na anti-moves! Jinsi gani waandishi wanashikiri katika michezo hii ya kisiasa? Nadhani ni sehemu yenyewe ya siasa. Kuna uhusiano wa ajabu sana kati ya vyombo vya habari na wanasiasa siyo Tanzania tu bali dunia nzima.



Wenzako wanasema kipo, wewe unasema hakipo. Mmoja wenu hayuko sahihi. Ni nani? time only will tell. Umesema Prof. hana mpango wa kugombea you might be very right, lakini ukweli wa kauli hiyo utaonekana 2010, kabla ya hapo ni jambo la probability tu. Sasa akigombea 2010 unaweza ukasema in 2008 hakuwa na mpango huo..



Of course, siasa ndivyo ilivyo. Labda kuna mambo hayapaswi kuwa hivyo (in a perfect world where personal interests are not at play) lakini katika ulimwengu ambao maslahi, matamanio, chuki, hasira, kinyongo, ushabiki, mapenzi nk vipo, utakutana na watu wa namna hiyo.

Don't be too harsh.

Mwanakijiji,
Nafikiri unajua garbage IN garbage OUT, ukijenga nyumba kwa foundation mbovu, nyumba nzima inakuwa mbovu. Hiyo makala imejengwa kwa foundation mbovu sana. Ukweli ulioko kwenye hiyo makala ni ule ambao tayari tunaujua na hakuna jipya hapo zaidi ya uzushi.

Kwanza hilo la kwamba Dr. Mwakyembe ni mjumbe wa NEC sio kweli.

Pili, nguvu ya Mwandosya kule Mbeya ni kubwa mno kiasi kwamba huyo Mwenyekiti hawezi hata siku moja kuandaa kwenye mkutano ajenda ya kumjadili prof. kwa kutumia vigezo vya mitaani. Huyo Mulla hana ubavu huo kabisa. Wanaweza kumjadili Prof. Kama kuna jambo kweli amelifanya lakini sio kwa
kutumia haya maneno ya mitaani. Kwa yeyote anayeijua Mbeya vizuri anajua hilo.

Tatu, prof. Mwandosya sio mjinga, ni mtu mwenye ueleo na ambaye anajua siasa za CCM na kikomo chake. Kama CCM waliweza kumtupa Malecela bila sababu za msingi, yeye prof. atakuwa na uwezo gani wa kupambana na rais aliyeko madarakani? Labda mwandishi angesema Prof. anataka kuhama chama lakini sio ndani ya CCM. Prof. kufanya hivyo itakuwa ni kujimaliza kisiasa
na sidhani kama yuko tayari kwa hilo.

Nne, toka uchaguzi wa NEC umeisha, prof. Mwandosya amekuwa kimya na kuweka nguvu yake kwenye uongozi wa nchi na sio siasa za ugomvi za Mbeya. Sijasikia hata mahali popote wakiandika Mwandosya anatembelea mkoa huu au wilaya hii. Sasa ataanza kampeni ofisi kwake au nyumbani kwake?

Ushauri wa bure ni kwa Wabunge kuacha kulialia na kuweka nguvu zote kwenye ku deliver kwenye majimbo yao. Magazeti yanaweza kukujenga lakini pia yanaweza kukubomoa.

Huyo Lowassa wanayemsema, kama ana nguvu si angejiokoa yeye asivuliwe kuwa PM?
 
Nakubaliana na wewe; nilichoshtuka ni wewe kusema kuwa habari nzima ni "uwongo mtupu" wakati ndani yake kuna mambo ambayo (using your own words) "Ukweli ulioko kwenye hiyo makala ni ule ambao tayari tunaujua.."

Kama kuna chembe ya ukweli katika makala hiyo then makala nzima haiwezi kuwa uongo "mtupu" isipokuwa ni uongo kwa maana ya factually wrong si kwa maana ya kulaghai.

Otherwise, nadhani kuna mitazamo miwili tofauti na sidhani kama "pseudo-obviousness" ya mambo ya Mbeya yana exclude madai yaliyotolewa kwenye makala hiyo.

Hivyo:
Kwa yeyote anayeijua Mbeya vizuri anajua hilo.

Nadhani wengine wanaoijua Mbeya vizuri wanaweza kuwa wanajua tofauti na hilo, nadhani ni mitazamo based on their own biases, experiences, prejudices etc.

Kwa hiyo mimi niko skeptical katika pande zote mbili, kwamba katika ulimwengu wa siasa, lolote lawezekana, only time will tell siwezi kupuuzia unayoyasema na yale waliyoyasema moja kwa moja.
 
Mimi sioni sababu ya kui-discount moja kwa moja habari hiyo na kusema kuwa ni uongo kwa nguvu tu ya hoja za Mtanzania ambaye na yeye anategemea habari za kuambiwa, tena kwa kutokea mbali.

hata kama ni ndugu ndio vyanzo vya kuwa na uhakika wa habari kiasi hicho, bado kuna sababu za kusita kuamini kuwa ukweli wote unasemwa hapa.
 
Nakubaliana na wewe; nilichoshtuka ni wewe kusema kuwa habari nzima ni "uwongo mtupu" wakati ndani yake kuna mambo ambayo (using your own words) "Ukweli ulioko kwenye hiyo makala ni ule ambao tayari tunaujua.."

Kama kuna chembe ya ukweli katika makala hiyo then makala nzima haiwezi kuwa uongo "mtupu" isipokuwa ni uongo kwa maana ya factually wrong si kwa maana ya kulaghai.

Otherwise, nadhani kuna mitazamo miwili tofauti na sidhani kama "pseudo-obviousness" ya mambo ya Mbeya yana exclude madai yaliyotolewa kwenye makala hiyo.

Hivyo:

Nadhani wengine wanaoijua Mbeya vizuri wanaweza kuwa wanajua tofauti na hilo, nadhani ni mitazamo based on their own biases, experiences, prejudices etc.

Kwa hiyo mimi niko skeptical katika pande zote mbili, kwamba katika ulimwengu wa siasa, lolote lawezekana, only time will tell siwezi kupuuzia unayoyasema na yale waliyoyasema moja kwa moja.

Mwanakijiji,

Hayo magazeti hivi kweli hata editors wanafanya kazi wanazotakiwa kufanya?

Maana kwa gazeti lililokuja na nguvu na lenye waandishi wengi wa maan kama Raiamwema, sikutegemea kosa la msingi kama hilo la kwamba Dr. Mwakyembe ni mjumbe wa NEC liweze kupita.

Makala ya habari kuitwa ni ya uongo sio lazima kila kitu kiwe uongo. Kama ni mahakamani, kwa kukosea mambo madogo kama hayo, tayari kila kitu kinatupwa.

Hata yale magazeti ya udaku, yanakuwa na ukweli angalau 10%, utaamini vipi habari ya mwandishi ambaye anashindwa kuchek info muhimu kama hiyo? Angeweza kuingia kwenye mtandao na kujua Mwakyembe sio mjumbe wa NEC.
 
Mwanakijiji,

Hayo magazeti hivi kweli hata editors wanafanya kazi wanazotakiwa kufanya?

Maana kwa gazeti lililokuja na nguvu na lenye waandishi wengi wa maan kama Raiamwema, sikutegemea kosa la msingi kama hilo la kwamba Dr. Mwakyembe ni mjumbe wa NEC liweze kupita.

Makala ya habari kuitwa ni ya uongo sio lazima kila kitu kiwe uongo. Kama ni mahakamani, kwa kukosea mambo madogo kama hayo, tayari kila kitu kinatupwa.

Hata yale magazeti ya udaku, yanakuwa na ukweli angalau 10%, utaamini vipi habari ya mwandishi ambaye anashindwa kuchek info muhimu kama hiyo? Angeweza kuingia kwenye mtandao na kujua Mwakyembe sio mjumbe wa NEC.

Mtanzania,

bado nasubiria majibu ya mhariri wa raia mwema kwenye hili.
 
mzee mahakamani kuna adminissable evidence na inadmissable ones. Kesi haiwezi kufutwa tu kwa sababu baadhi ya ushahidi ulikuwa tainted au haukupatikana kisheria.

Hivyo, tuondoe hilo kosa kuhusu NEC ambalo ingekuwa rahisi kwa mtu yeyote pale Raia Mwema kucheck lakini mtiririko wa hoja na madai ya sources zao zinaingia akilini na ni hoja ambazo sidhani kama ni hekima kuzitupa tu kwa sababu wamekosea kwenye kusema Mwakyembe ni member wa NEC.

Hapo nakubaliana nawewe kuhusu Wahariri wanaangalia hizo habari kweli?
 
Mimi sioni sababu ya kui-discount moja kwa moja habari hiyo na kusema kuwa ni uongo kwa nguvu tu ya hoja za Mtanzania ambaye na yeye anategemea habari za kuambiwa, tena kwa kutokea mbali.

hata kama ni ndugu ndio vyanzo vya kuwa na uhakika wa habari kiasi hicho, bado kuna sababu za kusita kuamini kuwa ukweli wote unasemwa hapa.

Kalamu,

Mimi katika conclusion yangu kwamba hiyo habari ni ya uongo, sijatumia tu sources zangu kule Mbeya, bali pia nimetumia uzoefu wangu wa zaidi ya miaka kumi juu ya siasa za huo mkoa. Nawajua players wote wanaosemwa na najua uwezo na udhaifu wa kila mtu.

Kilichoandikwa haki make sense. Nimeandika hapo juu kwanini naamini hivyo.

Mtu kama hamjui huyo Mwenyekiti anaweza kusema labda, lakini Mwenyekiti mwenyewe anajua hana uwezo wa kumvaa prof. Mwandosya kwa kutumia uvumi wa mitaani.

Ndio maana hata mkuu wa mkoa pamoja na ujinga wake, bado huwa hadiriki kumkashifu prof. Mwandosya.

Mbeya imewahi kutoa wanasiasa wengi sana. Sifa ya prof. sio matokeo ya kuwa na pesa na kutoa misaada. Ni matokeo ya jamaa kuwa muungwana na kuheshimu watu wote bila dharau na kusaidia pale anapoweza.

Mimi Prof. sio ndugu yangu wala hata yeye hanijui. Ila mimi namfahamu vizuri sana kuanzia nikiwa mwanafunzi kwenye hayo maeneo wakati yeye hata sio Mbunge. Alikuwa anatembelea shule mara nyingi na kutoa ushauri. Toka wakati huo nimekuwa nikifuatilia siasa za Mbeya na kumwelewa ipasavyo prof.
 
- Mtanzania, ni kweli Mwakyembe alitakiwa na mwenyekiti wa mkoa asishiriki mapokezi ya kumpongeza?

- Ni kweli Mwakyembe alienda kwenye mapokezi hayo kinyume na mapendekezo au ushauri wa Mwenyekiti wake wa Mkoa?

- Ni kweli alisema kwenye mkutano kuwa alishauriwa asitokee na hivyo kufanya ushauri wa siri kuwa hadharani?
 
- Mtanzania, ni kweli Mwakyembe alitakiwa na mwenyekiti wa mkoa asishiriki mapokezi ya kumpongeza?

- Ni kweli Mwakyembe alienda kwenye mapokezi hayo kinyume na mapendekezo au ushauri wa Mwenyekiti wake wa Mkoa?

- Ni kweli alisema kwenye mkutano kuwa alishauriwa asitokee na hivyo kufanya ushauri wa siri kuwa hadharani?

Mwanakijiji,

Hayo yote ni kweli lakini wananchi walipomkatalia alikubali kama ambavyo mkuu wa wilaya naye ambaye mwanzoni alipinga, baada ya kuona Mwakyembe amesema yeye atashiriki, wote walikubali na kushiriki kwenye hayo mapokezi. Hawakupeleka polisi kuzuia hayo mapokezi.

Msiwalaumu sana hao viongozi wa mkoa na wilaya. Walikuwa under pressure kubwa. Viongozi wa taifa wenyewe hawakufanya lolote hata la kumpongeza Dr. Mwakyembe, mlitegemea kwa siasa za TZ hao viongozi wa mkoa na wilaya waseme nini?

Muhimu na ambacho wengine pia ndio tulishauri ni kuacha nguvu ya wananchi ishinde. Wananchi waliamua kumpokea mbunge wao kwa mbwembwe na yakafanyika.

Sasa hiyo tofauti sio sababu ya kuanza kuzua mambo mengine ambayo hayapo. Mara ngapi viongozi wa siasa wanatofautiana?

Pia kwenye hilo prof. Mwandosya hakuwemo kabisa.
 
I will side with Mtanzania on one thing, Raiamwema ingawa ni very credible, wana uzembe fulani wa wahariri kupitia habario kabla ya habari kuchapwa.

This is not the first time.

Kulikuwa na habari moja nafikiri ni February ambayo walipotosha maana nzima ya habari kutokana na kuchanganya mambo na kupindisha facts na hilo lilikuwa kosa la kiuhariri.

They need to check the facts including spelling.

Huu ni mfano uliopo kwenye toleo lao la 12 kwenye makala ya Joseph Mihangwa.

Lakini nani amfunge paka kengere wakati safu ya uongozi imejaa watu wenye uchafu?

What is Kengere? I have never heard of such a word in Kiswahili!
 
Sawa sawa nimekupata Mtanzania.

- Ni kweli kuwa viongozi wa dini waliingilia kati jaribio la kwanza la kuwatuhumu kina Mwandosya na Mwakyembe kwa madai hawakupewa nafasi ya kujitetea kwenye kikao cha Februari?

- Ni kweli kwamba baadhi ya watu wakimuona Dr. Mwandosya mitaani wanamuita "Rais"?

- Ni kweli kwamba Dr. Mwakyembe anajua uwepo wa tuhuma hizo dhidi yake?
 
I will side with Mtanzania on one thing, Raiamwema ingawa ni very credible, wana uzembe fulani wa wahariri kupitia habario kabla ya habari kuchapwa.

Nadhani hili ni kweli. Na haya makosa ya kiuhariri yanatokea na yatatokea. La maana ni vyombo husika kuweka utaratibu wa kuangalia habari na kuzisimamia ili zisiwe na makosa yasiyo ya lazima.
 
Kurudia swala aliloleta Kuhani hapo nyuma.

Je wanasahihisha?

Maana hata NYT, IHT na WSJ kila siku wanafanya makosa, jamaa wanasahihisha hata kama wakikosea middle initial ya mtu!
 
...........What is Kengere? I have never heard of such a word in Kiswahili!...........

hahaa..........hata kwenye keyboard herufi "L" na "R" are not that much close kutegemea hilo kosa.......au ndio influence ya kabila?.........
 
Kurudia swala aliloleta Kuhani hapo nyuma.

Je wanasahihisha?

Maana hata NYT, IHT na WSJ kila siku wanafanya makosa, jamaa wanasahihisha hata kama wakikosea middle initial ya mtu!

Hata CNN na BBC ambao ni mashirika makubwa ya habari duniani pamoja na research za hali ya juu wanazofanya bado huwa wanafanya makosa mengi tu na pia huomba samahani kwa makosa waliyoyatangaza.
 
Sawa sawa nimekupata Mtanzania.

- Ni kweli kuwa viongozi wa dini waliingilia kati jaribio la kwanza la kuwatuhumu kina Mwandosya na Mwakyembe kwa madai hawakupewa nafasi ya kujitetea kwenye kikao cha Februari?

- Ni kweli kwamba baadhi ya watu wakimuona Dr. Mwandosya mitaani wanamuita "Rais"?

- Ni kweli kwamba Dr. Mwakyembe anajua uwepo wa tuhuma hizo dhidi yake?

Mwanakijiji,

Inaelekea na wewe huujui mkoa wa Mbeya. Kisiasa huo mkoa umegawanyika sehmu kuu mbili, wale wa Kyela, Rungwe, Mbeya na kidogo na Ileje na wale wa sehemu ya Mbeya, Chunya na Mbozi.

Kundi la Kwanza lina Prof. Mwandosya kama kiongozi wao, la pili lina wapambe wengi tu lakini hakuna mtu unayeweza kusema ndio hasa kiongozi wao.

Miaka na miaka hayo makundi yana upinzani na ndani yake kuna wanasiasa, wana dini, wafanyabiashara nk. Tuhuma kati ya hayo makundi zipo na zitaendelea kuwepo.

Kusema Mulla alitaka watoe tamko la kuwatuhumu Prof. Na Mwakyembe, ni uongo. Yeye mwenyewe Mulla anajua wazi kwa kufanya hivyo angejimaliza kisiasa Mbeya. Mulla anaweza kumshambulia Mwakyembe lakini hata siku moja hatamshambulia prof. Mwandosya labda kuwe na ushahidi wazi kabisa juu ya jambo fulani.

Wanaomuita Prof rais ni makundi ya vijana sawa tu wanavyomuita Mrema, Lipumba au Mbowe. Ni ushabiki wa kisiasa ambao kwa TZ huwezi kuukwepa.

Ya Mwakyembe ni possible maana analalamika vitu vingi. Kwamimi naona hayo malalamiko hata sio muhimu, hakuna mtu anayeenda kumkwamisha kwenye juhudi za kuendeleza Kyela. Yeye ahangaike kuiletea Kyela maendeleo na wananchi watamwelewa na kumpa kipindi kingine. Haitoshi kusema anakwamishwa wakati hakuna ushahidi kuonyesha kwamba anakwamishwa. Kinachotokea ni kwamba wanasiasa wa Mbeya wanakwamishana. Kwamimi hiyo ingelikuwa motivating factor ya kumfanya atende mengi ya maana kule wilayani. yeye mwenyewe anakwamisha wengine, kwanini anashangaa wengine wakimkwamisha?

Binafsi sitaki kuongelea maungonvi ya hao viongozi, ninataka kuongelea maendeleo ya mkoa. kufanikiwa na kushindwa kwao tutaongelea mwaka 2010. Hapo
ndio itajulikana kama kweli wana ushawishi mkubwa kwenye majimbo yao. Watch this space!
 
Mtanzania, kimsingi unachosema ni kuwa kuna mambo yanaendelea huko Mbeya na ukiondoa hiyo habari ya NEC kuna mambo ambayo yanaendelea chini kwa chini huko Mbeya kutokana mgawanyiko wa siasa za Mbeya kwa kadiri ulivyozichambua. Siyo?
 
Hii habari hapa chini toka Raiamwema ni uwongo mtupu. Mwandishi ameshindwa hata kutambua jambo rahisi la kujua kwamba Dr. Mwakyembe sio mjumbe wa NEC ya CCM.

Acheni kuutumia mkoa wa Mbeya kuendeleza vita ambavyo havipo.

Sources zangu zote za huko Mbeya zinaonyesha hakuna kitu kama hicho. Baadhi ya waandishi wa habari wana sababu zao za kutaka kuona ugomvi huu unaendelea kwa cost ya wananchi wa Mbeya.

Hakuna kikao cha kuwajadili Mwandosya na Mwakyembe na wala Prof. hana mpango wa kugombea urais mwaka 2010.

Inaelekea kuna watu wanakuza hayo maneno kwa faida zao binafsi.

kwanza hoja kwamba habari hii ni uongo mtupu ni kukuza mambo.unataka kusema kwamba wanamtandao walikuwa hawamsaidii Mwang'onda dhidi ya mwandosya na pia unataka kusema kwamba wanamtandao walifurahia Mwandosya kumshinda Thom?

pia kusema vyanzo vyako vyote vimekuhakikishia kwamba habari hii ni ya kuzua ni kutokujiheshimu, hivyo vyanzo vyako ni mungu wa habari za Mbeya?kwa mfano ungetuambia umeongea na Mwandosya na Mwakyembe wakakuambia kwamba raia mwema limewazulia jambo tungeelewa

pia habari ya Mwakyembe kukatazwa kukubalia mapokezi yaliyoandaliwa na wananchi wa Kyela haikuandikwa na Raia mwema na maneno kwamba mulah alimwambia mwakyembe maagizo yametoka makao makuu ya CCM hayajawahi kukanushwa na CCM wala Mulah mwenyewe

lakini kwa faida kidogo nikumegee habari njema ya wanamtandao. wanamtandao katika kupambana na mwandosya na mkakati wa kuhakikisha kwamba viongozi wa umoja wa vijana wa CCM hawatoki kwenye mtandao wa mwandosya wemempleka mmoja wa wapiganaji wake,Rhoda George kuwa katibu wa unoja wa vijana wa mkoa.
 
Kigarama na wewe unazungumza kama unazijua siasa za Mbeya. Kwenye hiyo habari ukiondoa hilo suala la UNEC ni kitu gani kingine ambacho kina makosa, hakiwezekani kabisa, au ni cha kutunga na uzushi?
 
Back
Top Bottom