Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,468
- 113,583
Wanabodi,
Wakati tukiendelea kuugulia msiba wa Mwanahabari Daudi Mwangosi, kitendo cha kupigwa na polisi hadi kudondoka chini na kamera yake mkononi bila kuiachia, akamkumbatia ofisa huyo wa polisi ili kujisalimisha na kuisalimisha roho yake, akingali na kamera yake mkononi na hakuiachia mpaka kifo kilipomkuta..., ni kitendo cha ushupavu na ushujaa wa hali ya juu kwenye tasnia ya habari!. Huyu anastahili kuitwa Shujaa wa Taifa, na damu yake haitapotea bure, itakuwa ni chemchem ya ukombozi wa wanahabari kwa ujumla dhidi ya madhila mbalimbali yayowakumba na labda pia hii ndio cheche ya moto nyikani, itakayo lipua moto wa mabadiliko nchi nzima na kufikisha sio tuu mwisho wa udhalimu wa jeshi letu la polisi kupitisha hukumu ya kifo instantly without trial dhidi ya raia wasio na hatia yoyote, bali pia unaweza kuwa ndio mwanzo wa mwisho wa serikali dhalimu ambayo polisi hao dhalimu, ni sehemu ya serikali hiyo na ndio maana inawalinda polisi dhalimu hao, kwa udhalimu wao!.
Niikiangalia picha hii ya mwisho ya mpiganaji kamanda Mwangosi, imenifanya nikitafakari kituo cha televisheni cha Channel Ten na baadhi ya wanahabari wake mahiri, shupavu na vitendo vyao vya kishujaa, lakini...
Kuwakumbusha tuu, Channel Ten wakati huo ikiitwa DTV,
Kabla sijamalizia ile lakini yangu, sio vibaya nikiwataja baadhi ya watangazaji mahiri na shupavu wa Chanel Ten na vitendo vyao vya Umahiri, Ushupavu au Ushujaa.
Nimeziainisha baadhi ya sifa za kituo cha Televisheni Channel Ten na baadhi tuu ya watangazaji waliopitia kwenye mikono hiyo, sijawataja wale wote waliopo vikiwemo vichwa kama Jenerali Ulimwengu, Makwaia wa Kuhenga, Hamza Kasongo etc, sifa hizi zote na nyinginezo nyingi, zinakifanya kituo cha Televisheni cha Channel Ten, kustahili pongezi za dhati kwa mafanikio yote hayo!.
Ila kama kawaida, kile kwenye mafanikio, hapakosi changamoto, na hizo ndizo msingi mkuu wa mada yangu.
Ukiangalia safu ya vipaji vilivyo timka ni dhahiri Channel Ten kuna matatizo fulani.. na baada ya kusikia kumbe hata Marehemu Daudi Mwangosi, hakuwa mwajiriwa wa Channel Ten, he was only a correspondent!, huu ni uthibitisho wa tatizo, somewhere, some how!.
Nauomba uongozi wa Channel Ten, ufanye utaratibu mpya kabisa wa kumuenzi Daudi Mwangosi kwa kutoa "special employment" kwa "marehemu" in terms of paperwork ili kuandaa taratibu zote za mafao tangu alipojiunga nao in terms of payment ili familia yake ipate chochote kutoka Channel Ten, hata ikibidi, wamuanzishie "Daudi Mwangosi Memorial Fund" na itachangiwa na sisi wadau ili kuilinda familia yake isiadhirike na badala yake, ipate ustawi wa jasho la baba yao!.
Kiendo cha kuwa Daudi Mwangosi, hakuwa mwajiriwa rasmi wa Channel Ten, hakuiondolei Channel Ten, "full tortious liability" in an event of death!. Watanzania wengi hawajua kuwa kila mwenye chombo cha usafiri, ana liability na abiria wake in case of accident or death ndio maana bima ni muhimu!. Vivyo hivyo media zote, zina liability na waandishi wao in case of death, awe ni muajiriwa au sio muajiriwa as long as alikuwa anafanya kazi ya Channel Ten, then Channel Ten lazima ibebe resiponsiblities as if alikuwa full time employee!.
Namalizia kwa kuipa tena Channel Ten pole nyingi za msiba, hongera nyingi za kuwa vinara wa "freedom of Expression" na hongera nyingi kwa upishi wa watangazaji vipaji, mahiri na shupavu lakini ...waipokee changamoto hii...lazima mbadilike, "you have to motivate and retain the best that you have na kuanza kwa kumuenzi shujaa wetu "Daudi Mwangosi" kwa all his rights, he should have had long ago when he was alive!.
Wasalaam.
Pasco.
Wakati tukiendelea kuugulia msiba wa Mwanahabari Daudi Mwangosi, kitendo cha kupigwa na polisi hadi kudondoka chini na kamera yake mkononi bila kuiachia, akamkumbatia ofisa huyo wa polisi ili kujisalimisha na kuisalimisha roho yake, akingali na kamera yake mkononi na hakuiachia mpaka kifo kilipomkuta..., ni kitendo cha ushupavu na ushujaa wa hali ya juu kwenye tasnia ya habari!. Huyu anastahili kuitwa Shujaa wa Taifa, na damu yake haitapotea bure, itakuwa ni chemchem ya ukombozi wa wanahabari kwa ujumla dhidi ya madhila mbalimbali yayowakumba na labda pia hii ndio cheche ya moto nyikani, itakayo lipua moto wa mabadiliko nchi nzima na kufikisha sio tuu mwisho wa udhalimu wa jeshi letu la polisi kupitisha hukumu ya kifo instantly without trial dhidi ya raia wasio na hatia yoyote, bali pia unaweza kuwa ndio mwanzo wa mwisho wa serikali dhalimu ambayo polisi hao dhalimu, ni sehemu ya serikali hiyo na ndio maana inawalinda polisi dhalimu hao, kwa udhalimu wao!.
Niikiangalia picha hii ya mwisho ya mpiganaji kamanda Mwangosi, imenifanya nikitafakari kituo cha televisheni cha Channel Ten na baadhi ya wanahabari wake mahiri, shupavu na vitendo vyao vya kishujaa, lakini...
Kuwakumbusha tuu, Channel Ten wakati huo ikiitwa DTV,
- Ndio iliyokuwa TV ya kwanza kuweka msomaji wa habari zaidi ya mmoja mwaka 1994, zingine zikafuatia.
- Ndio ilikuwa TV ya kwanza kurusha matangazo yoyote ya televisheni ya moja kwa moja "live" 1995 na ndiyo ya kwanza kurusha habari "live" vituo vingine vikirekodi kwanza ndipo virushe!.
- Ndiyo ilikuwa TV ya kwanza kufanya vipindi vya mahojiano ya papo kwa papo "Vox Pop" na kipindi cha kwanza cha mahojiano ya "Vox Pop" kiliitwa "Mada Moto" Uchaguzi wa 1995!.
- Ndiyo ilikuwa TV ya kwanza kutangaza uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi live, na kutangaza jumla ya matokeo ya ukweli ya uchaguzi wa Zanzibar ambapo kiukweli CUF walishinda, ila ZEC ikaitangaza CCM ndio washindi!.
- Ndio TV ya kwanza kupigwa fine na NEC kwa kuutangaza ukweli halisi wa matokeo ya urais kituo kwa kituo na kupelekea sheria ya uchaguzi kubadishwa kuwa sasa ni marufuku kwa chombo chochote kuyatangaza jumla ya matokeo ya kura za urais toka kituo kwa kituo bali ni matokeo yaliyopikwa na NEC tuu ndio matokeo halali ya uchaguzi wa rais!.
- Kufuatia ugomvi fulani wa kibiashara, Mmiliki wa Channel Ten aliweka "detention" without trial kwa kusingiziwa ametaka kumuua mmiliki wa kituo kingine cha TV. Katibu Mkuu wa Mambo ya Ndani, akaamuru atolewe, pale pale katibu mkuu huyo alimwaga unga wake!.
- Ndicho kituo cha kwanza kuanzisha TV Talk Show iitwayo "Kiti Moto" ambayo baadae ilikuja ...
- Ndio TV ya kwanza kutangazo michuano ya kombe la dunia na kutangaza mbio za magari za langa langa (F1 grand prix) bure!, hata ulaya, huwezi kuona world cup au grand prix bure!
- Ndio TV inayoongoza kwa habari za ukweli na msisimko, vipindi vinavyoongoza kwa freedom of expression na msisimko zaidi kuliko vituo vingine vyote..lakini..
- Ndicho kituo kinachoongoza kwa kupika vipaji vya utangazaji wa Televisheni nchini, watangazaji wengi wa vituo vingine vingi, wamepikwa na Channel Ten, wengine kazi zao ni kuwasubiri, wakishaiva, kupakua tuu na kuyafaidi matunda yao!. Kwa haya yote, Channel Ten inastahili pongezi za dhati, lakini..
Kabla sijamalizia ile lakini yangu, sio vibaya nikiwataja baadhi ya watangazaji mahiri na shupavu wa Chanel Ten na vitendo vyao vya Umahiri, Ushupavu au Ushujaa.
- Betty Mkwasa ambaye kwa sasa ni mkuu wa wilaya ya Bahi, alipikwa na Channel Ten, alipohamia ITV, akashinda Tuzo ya CNN Journalist of a Year, baadae akaukwaa u-DC!.
- Ahmed Kipozi, alipikwa na Channel Ten, huyu ndiye mtangazaji wa TV wa kiume aliyeongoza kwa kuwa smart na ana sauti yenye lafudhi tamu ya ajabu!. Baadae alihamia ITV na mwishowe sauti yake kutumiwa na kurugenzi ya mawasiliano Ikulu kwenye vipindi vya JK. Kwa sasa ni Mhe. DC wa Bagamoyo.
- Bujaga Izengo Kadago, alipikwa na Channel Ten, akahamia Morogoro kwenda kuanzisha SUA TV.
- Karim Besta, (RIP) alipikwa na Channel Ten na kuhamia Morogoro kwenda kuanzisha Aboud Television.
- Ephraim Kibonde, alipikwa na Channel Ten, na kuhamia Clouds sasa ni mtangazaji mahiri wa Radio na TV
- Salim Kikeke, alipikwa na Channel Ten akahamia ITV sasa ni mtangazaji kiongozi BBC Swahili.
- Sunday Shomari, alipikwa Channel Ten akahamia ITV sasa ni Mtangazaji kiongozi VOA
- Florah Nducha, alipikwa Channel Ten, akahamia Radio One, sasa ni Mkuu wa Idhaa ya Kiswahili ya UN Radio yuko NY.
- Sakina Datoo, alipikwa Channel Ten, akaenda Sunday Citizen, then Guardian on Sunday, sasa yuko Daily Telegraph ya UK.
- Yule mtangazaji wa kile kipindi cha Kiti Moto alipikwa Channel Ten, akahamia TBC, kwa sasa ni mtangazaji wa kujitegemea akimiliki kampuni yake ya matangazo kwa jina la PPR.
Nimeziainisha baadhi ya sifa za kituo cha Televisheni Channel Ten na baadhi tuu ya watangazaji waliopitia kwenye mikono hiyo, sijawataja wale wote waliopo vikiwemo vichwa kama Jenerali Ulimwengu, Makwaia wa Kuhenga, Hamza Kasongo etc, sifa hizi zote na nyinginezo nyingi, zinakifanya kituo cha Televisheni cha Channel Ten, kustahili pongezi za dhati kwa mafanikio yote hayo!.
Ila kama kawaida, kile kwenye mafanikio, hapakosi changamoto, na hizo ndizo msingi mkuu wa mada yangu.
Ukiangalia safu ya vipaji vilivyo timka ni dhahiri Channel Ten kuna matatizo fulani.. na baada ya kusikia kumbe hata Marehemu Daudi Mwangosi, hakuwa mwajiriwa wa Channel Ten, he was only a correspondent!, huu ni uthibitisho wa tatizo, somewhere, some how!.
Nauomba uongozi wa Channel Ten, ufanye utaratibu mpya kabisa wa kumuenzi Daudi Mwangosi kwa kutoa "special employment" kwa "marehemu" in terms of paperwork ili kuandaa taratibu zote za mafao tangu alipojiunga nao in terms of payment ili familia yake ipate chochote kutoka Channel Ten, hata ikibidi, wamuanzishie "Daudi Mwangosi Memorial Fund" na itachangiwa na sisi wadau ili kuilinda familia yake isiadhirike na badala yake, ipate ustawi wa jasho la baba yao!.
Kiendo cha kuwa Daudi Mwangosi, hakuwa mwajiriwa rasmi wa Channel Ten, hakuiondolei Channel Ten, "full tortious liability" in an event of death!. Watanzania wengi hawajua kuwa kila mwenye chombo cha usafiri, ana liability na abiria wake in case of accident or death ndio maana bima ni muhimu!. Vivyo hivyo media zote, zina liability na waandishi wao in case of death, awe ni muajiriwa au sio muajiriwa as long as alikuwa anafanya kazi ya Channel Ten, then Channel Ten lazima ibebe resiponsiblities as if alikuwa full time employee!.
Namalizia kwa kuipa tena Channel Ten pole nyingi za msiba, hongera nyingi za kuwa vinara wa "freedom of Expression" na hongera nyingi kwa upishi wa watangazaji vipaji, mahiri na shupavu lakini ...waipokee changamoto hii...lazima mbadilike, "you have to motivate and retain the best that you have na kuanza kwa kumuenzi shujaa wetu "Daudi Mwangosi" kwa all his rights, he should have had long ago when he was alive!.
Wasalaam.
Pasco.