HALI katika mamlaka ya bandari [TPA] si salama kabisa, wizi umekithiri kupita kiasi makontena yanaibiwa kila kukicha, ukileta mzigo wa aina yeyote ile lazima utakuta kuna vifaa vimepunguwa,lililo baya zaidi hakuna hatua zinazochukuliwa ni mtihani kupita kiasi, wakurugenzi akina Mgawe, Mfuko na Koshuma wao wanachojua ni kuchota tu yaani chukua chako mapema hakuna lolote la maana wanalofanya kuinusuru bandari yetu ambayo ni uti wa mgongo wa taifa cha kujiuliza hivi hawa watu kwa nini wanaachwa kuendeleza kuongoza majukumu waliyoshindwa, fununu zinaonesha watetezi wao wakubwa ni katibu mkuu wa uchukuzi bwana Omar Chambo na naibu waziri wa wizara hiyo bwana Athuman Mfutakamba.
Chambo na Mfutakamba wanachotewa mamilioni na kuingiziwa katika akaunti zao na kundi la akina Mgawe ndio maana Chambo na Mfutakamba WANAHAHA KILA NAMNA kulinda uongozi mbovu wa akina Mgawe. Chambo na Mfutakamba wanajidhalilisha sana tena sana kwa viongozi wa TPA, yote sababu ya tamaa ya pesa imewafikisha pabaya na imewashushia hadhi yao kiasi kikubwa sana.
Chambo na Mfutakamba wanachotewa mamilioni na kuingiziwa katika akaunti zao na kundi la akina Mgawe ndio maana Chambo na Mfutakamba WANAHAHA KILA NAMNA kulinda uongozi mbovu wa akina Mgawe. Chambo na Mfutakamba wanajidhalilisha sana tena sana kwa viongozi wa TPA, yote sababu ya tamaa ya pesa imewafikisha pabaya na imewashushia hadhi yao kiasi kikubwa sana.