Chambo na Mfutakamba wanalinda uozo TPA

kalanjadd

Member
Oct 16, 2011
39
16
HALI katika mamlaka ya bandari [TPA] si salama kabisa, wizi umekithiri kupita kiasi makontena yanaibiwa kila kukicha, ukileta mzigo wa aina yeyote ile lazima utakuta kuna vifaa vimepunguwa,lililo baya zaidi hakuna hatua zinazochukuliwa ni mtihani kupita kiasi, wakurugenzi akina Mgawe, Mfuko na Koshuma wao wanachojua ni kuchota tu yaani chukua chako mapema hakuna lolote la maana wanalofanya kuinusuru bandari yetu ambayo ni uti wa mgongo wa taifa cha kujiuliza hivi hawa watu kwa nini wanaachwa kuendeleza kuongoza majukumu waliyoshindwa, fununu zinaonesha watetezi wao wakubwa ni katibu mkuu wa uchukuzi bwana Omar Chambo na naibu waziri wa wizara hiyo bwana Athuman Mfutakamba.

Chambo na Mfutakamba wanachotewa mamilioni na kuingiziwa katika akaunti zao na kundi la akina Mgawe ndio maana Chambo na Mfutakamba WANAHAHA KILA NAMNA kulinda uongozi mbovu wa akina Mgawe. Chambo na Mfutakamba wanajidhalilisha sana tena sana kwa viongozi wa TPA, yote sababu ya tamaa ya pesa imewafikisha pabaya na imewashushia hadhi yao kiasi kikubwa sana.
 
Nasikia kati ya miaka 4 iliyopita kuna tume 3 ziliundwa na Wizara kuchunguza utendaji mbovu wa TPA chini ya Mgawe lakini mpaka leo hakuna hata tume moja ambayo mapendekezl yao yamewahi kufanyiwa. Halafu wafanyakazi wa TPA ni waoga sana hata kutoa taarifa kwa hizo tume zilizoundwa kwa sababu wanahisi Mgawe akigundua basi ana deal na individual perpendicularly.
 
Sio TPA tuu mashirika karibuni yote yaliyo chini ya serikali yanaboronga
 
Naomba ufafanue hayo makontena yanaibiwa kule ticts au kule general cargo terminal? Nijuavyo ticts wana walinzi wao, na tpa wana auxiliary police. Ticts walikataa kutumia walinzi wa tpa walinzi wa ticts wana njaa kali sababu mishahara midogo.
 
Back
Top Bottom