Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Chama gani kitakwenda mahakamani kupinga uteuzi wa Dr Shein?
Kufuatana na story ya kuu Mwanahalisi wiki hiiuteuzi wa Dr Ali Mohamed Shein kuwania kiti cha urais wa Visiwani ni batili.
Gazeti limesema kuwa suala hili liliibuliwa katika kikao cha NEC hivi majuzi na Nimrod Mkono ambaye alinukuu katiba ya Zanzibar na kusema kuwa Dr Shein hana sifa za kugombea urais Visiwani kwa sababu hana sifa za kuwania nafasi ya Uwakilishi kule.
Na hii inatokana na ukweli kwamba Dr Shein hakujiandikisha kama mpiga kura katika daftari la kupiga kura la Visiwani, kwani alijiandikisha kule OystyerBay, jijini Dar es Salaam.
Mkono alimtaka Dr Shein kujitoa ili kuiondoa CCM kwenye uwezekano wa kupata fedheha, iwapo atawekewa pingamizi katika ZEC au mahakamani na wapinzani.
Aidha kuna suala la ukazi wa Visiwani. Dr Shein hajakaa Visiwani kwa miaka mitatu mfululizo.
Lilipoibuliwa katika kikao cha NEC, suala hili liliborongwa-borongwa tu na baadhi ya wajumbe akiwemo mwenyekiti wa CCM, JK.
Chama kikuu cha upinzani kule Zanzibar CUF hakiwezi kumuwekea Dr Shein pingamizi kwa vile kimeshakuwa neutralized kutokana nay ale maridhiano. Habari zinasema kuwa NCCR ndiyo wanajipanga kuweka pingamizi. NCC itakuwa kweli serious?
Tujadili.
Kufuatana na story ya kuu Mwanahalisi wiki hiiuteuzi wa Dr Ali Mohamed Shein kuwania kiti cha urais wa Visiwani ni batili.
Gazeti limesema kuwa suala hili liliibuliwa katika kikao cha NEC hivi majuzi na Nimrod Mkono ambaye alinukuu katiba ya Zanzibar na kusema kuwa Dr Shein hana sifa za kugombea urais Visiwani kwa sababu hana sifa za kuwania nafasi ya Uwakilishi kule.
Na hii inatokana na ukweli kwamba Dr Shein hakujiandikisha kama mpiga kura katika daftari la kupiga kura la Visiwani, kwani alijiandikisha kule OystyerBay, jijini Dar es Salaam.
Mkono alimtaka Dr Shein kujitoa ili kuiondoa CCM kwenye uwezekano wa kupata fedheha, iwapo atawekewa pingamizi katika ZEC au mahakamani na wapinzani.
Aidha kuna suala la ukazi wa Visiwani. Dr Shein hajakaa Visiwani kwa miaka mitatu mfululizo.
Lilipoibuliwa katika kikao cha NEC, suala hili liliborongwa-borongwa tu na baadhi ya wajumbe akiwemo mwenyekiti wa CCM, JK.
Chama kikuu cha upinzani kule Zanzibar CUF hakiwezi kumuwekea Dr Shein pingamizi kwa vile kimeshakuwa neutralized kutokana nay ale maridhiano. Habari zinasema kuwa NCCR ndiyo wanajipanga kuweka pingamizi. NCC itakuwa kweli serious?
Tujadili.