Elections 2010 Chama gani kitakwenda mahakamani kupinga uteuzi wa Dr Shein?

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
234
Chama gani kitakwenda mahakamani kupinga uteuzi wa Dr Shein?

Kufuatana na story ya kuu Mwanahalisi wiki hiiuteuzi wa Dr Ali Mohamed Shein kuwania kiti cha urais wa Visiwani ni batili.

Gazeti limesema kuwa suala hili liliibuliwa katika kikao cha NEC hivi majuzi na Nimrod Mkono ambaye alinukuu katiba ya Zanzibar na kusema kuwa Dr Shein hana sifa za kugombea urais Visiwani kwa sababu hana sifa za kuwania nafasi ya Uwakilishi kule.

Na hii inatokana na ukweli kwamba Dr Shein hakujiandikisha kama mpiga kura katika daftari la kupiga kura la Visiwani, kwani alijiandikisha kule OystyerBay, jijini Dar es Salaam.

Mkono alimtaka Dr Shein kujitoa ili kuiondoa CCM kwenye uwezekano wa kupata fedheha, iwapo atawekewa pingamizi katika ZEC au mahakamani na wapinzani.

Aidha kuna suala la ukazi wa Visiwani. Dr Shein hajakaa Visiwani kwa miaka mitatu mfululizo.

Lilipoibuliwa katika kikao cha NEC, suala hili liliborongwa-borongwa tu na baadhi ya wajumbe akiwemo mwenyekiti wa CCM, JK.

Chama kikuu cha upinzani kule Zanzibar – CUF – hakiwezi kumuwekea Dr Shein pingamizi kwa vile kimeshakuwa neutralized kutokana nay ale maridhiano. Habari zinasema kuwa NCCR ndiyo wanajipanga kuweka pingamizi. NCC itakuwa kweli serious?

Tujadili.
 
Wataalamu wa kaiba tusaidieni. kama ni kweli basi ccm wameula wa chuya!

Kwa scenario kama hii usitegeme tume ya uchaguzi au mahakama vina uhuru wa kufanya chochote against serikali. Serikali inaminya 'ka-kitufe' chwee... wewe uliyekimbilia mahakamani unashangaa hoja zako mahakamani zinagota.. tena watakavyofanya mambo kitaalamu litachaguliwa jopo la majaji ishirini na wanne na marafiki wa mahakama wataletwa hata kumi na tisa... na mara utasikia... oho mara hili suala ni la kisiasa blah blah.... mgombea ana sifa....
 
Hii mbona si hoja?, kwani diplomat kama Ally Karume mbona alikuwa na sifa ya kugombea na ilhali yeye si mkaazi wa Zanzibar, jibu utakalonipatia kuhusu Ally Karume ndilo hilo litakalokuwa linamfit Dr Shein. Kwa kifupi ni kwamba Dr. Shein aliondoka Zanzibar akiwa ni muwakilishi baada ya kuteuliwa kuwa makamu wa rais kufuatia kifo cha Dr Omari Ali Juma July 2001. Kwa kuwa alikuwa huku bara kikazi kama na hasa kama diplomat maana ana passport ya kidiplomasia kabla hajagombea nafasi ya urais Zanzibar kama alivyo Ali Karume basi hakuna wa kumwekea pingamizi na kama litawekwa litatupiliwa mbali kwa hoja nilizozieleza hapa na nyingine nyingi tu zitakazokuwepo huko baadae.

Hoja hii ina mpango mmoja tu nao ni kuvuruga amani na utulivu Zanzibar kwa kuwashawishi CUF kuweka pingamizi wakidhani itakuwa vinginevyo na baadae Shein atashinda na kuachana na makubaliano. Hakuna hoja hapa Dr. Shein ni Mzanzibar aliyekuwa bara kikazi za Jamhuri ya muungano kama walivyo diplomats akina Ally Karume. Case closed
 
Chama gani kitakwenda mahakamani kupinga uteuzi wa Dr Shein?

Kufuatana na story ya kuu Mwanahalisi wiki hiiuteuzi wa Dr Ali Mohamed Shein kuwania kiti cha urais wa Visiwani ni batili.

Gazeti limesema kuwa suala hili liliibuliwa katika kikao cha NEC hivi majuzi na Nimrod Mkono ambaye alinukuu katiba ya Zanzibar na kusema kuwa Dr Shein hana sifa za kugombea urais Visiwani kwa sababu hana sifa za kuwania nafasi ya Uwakilishi kule.

Na hii inatokana na ukweli kwamba Dr Shein hakujiandikisha kama mpiga kura katika daftari la kupiga kura la Visiwani, kwani alijiandikisha kule OystyerBay, jijini Dar es Salaam.

Mkono alimtaka Dr Shein kujitoa ili kuiondoa CCM kwenye uwezekano wa kupata fedheha, iwapo atawekewa pingamizi katika ZEC au mahakamani na wapinzani.

Aidha kuna suala la ukazi wa Visiwani. Dr Shein hajakaa Visiwani kwa miaka mitatu mfululizo.

Lilipoibuliwa katika kikao cha NEC, suala hili liliborongwa-borongwa tu na baadhi ya wajumbe akiwemo mwenyekiti wa CCM, JK.

Chama kikuu cha upinzani kule Zanzibar – CUF – hakiwezi kumuwekea Dr Shein pingamizi kwa vile kimeshakuwa neutralized kutokana nay ale maridhiano. Habari zinasema kuwa NCCR ndiyo wanajipanga kuweka pingamizi. NCC itakuwa kweli serious?

Tujadili.
wewe hiyo hoja umeipata wapi ati Mkono? umemnakili au ndo mambo yenu ya Kiunguja mnayaleta hapa? hamtaki Mpemba atawale sio? mtachunana ngozi muda si mrefu!
 
Naomba niulize, hivi wagombea wote wa kiti kimojawapo (urais/ubunge/udiwani) wakiwekeana pingamizi na kuondolewa katika kinyang'anyiro, ni nani sasa atashikilia wadhifa husika (urais/ubunge/udiwani) ?
 
Subiri kwanza jina lake lipitishwe na ZEC. Hujui zec wanaweza kesho kulifungua daftari na yeye akajiandikisha?
 
Hii mbona si hoja?, kwani diplomat kama Ally Karume mbona alikuwa na sifa ya kugombea na ilhali yeye si mkaazi wa Zanzibar, jibu utakalonipatia kuhusu Ally Karume ndilo hilo litakalokuwa linamfit Dr Shein. Kwa kifupi ni kwamba Dr. Shein aliondoka Zanzibar akiwa ni muwakilishi baada ya kuteuliwa kuwa makamu wa rais kufuatia kifo cha Dr Omari Ali Juma July 2001. Kwa kuwa alikuwa huku bara kikazi kama na hasa kama diplomat maana ana passport ya kidiplomasia kabla hajagombea nafasi ya urais Zanzibar kama alivyo Ali Karume basi hakuna wa kumwekea pingamizi na kama litawekwa litatupiliwa mbali kwa hoja nilizozieleza hapa na nyingine nyingi tu zitakazokuwepo huko baadae.

Hoja hii ina mpango mmoja tu nao ni kuvuruga amani na utulivu Zanzibar kwa kuwashawishi CUF kuweka pingamizi wakidhani itakuwa vinginevyo na baadae Shein atashinda na kuachana na makubaliano. Hakuna hoja hapa Dr. Shein ni Mzanzibar aliyekuwa bara kikazi za Jamhuri ya muungano kama walivyo diplomats akina Ally Karume. Case closed

Mkuu H: Hoja kubwa ya Mkono katika kikao cha NEC ilikuwa ni suala hilo a Shein kutojiandikisha kupiga kura kule Visiwani, na siyo hasa suala la ukazi. Katika hoja yako hapo juu hujazungumzia suala hili la kutojiandikisha. Katina ya Zanzibar iko wazi kabisa kuhusu hilo, na Ali Karume uliomtaja alilifahamu hili na alijiandikisha mapema kule.

Ukubali kitu kimoja tu, kwa kuwa tume ya ZEC (na NEC) siyo huru, ni outrageously pro-CCM, basi ni ubabe tu utatumika kumpitisha Dr Shein kugombea. Mara nyingi CCM hudumu kwa mtindo huu wa ubabe na uvunjifu wa Katiba ambao sasa unaonekana kukithiri. Angekuwa ni mgombea wa chama cha upinzani hawezi kupitishwa na ZEC. Au nasema uongo jamani?
 
kwani hakujiandikisha eee?

alikuwa hana nia ya kutumia haki yake ya kikatba au?

hapa labda comandoo afanye vitu vyake ampinge Shein ila kwa wenginewe hasa upinzani haiwezi kupambana na tume ya uchaguzi
 
Back
Top Bottom