Walimu watangaza mgogoro na chama chao
By Thobias Mwanakatwe | 16th June 2012
Walimu nchini wametangaza mgogoro dhidi ya Chama cha Walimu Tanzania (CWT) ambao unaweza kusababisha mgomo wa nchi nzima kutokana na kutoridhishwa na mambo kadhaa ya ukandamizaji yanayoendelea ndani ya chama hicho.
Kwa mujibu wa taarifa waliyoisambaza kwa vyombo vya habari, walimu wa mkoa wa Kigoma walisema kutokana na hali ilivyo ndani ya chama hicho kuna haja kwa serikali kuingilia kati mgogoro huo unaoendelea kufukuta ambao umeanza kusababisha walimu kukosa ari na moyo wa kufundisha na usumbufu mwingi wa kwenda kwenye Mahakama ya Usuluhishi.
"Wanachama wamenyimwa fursa na demokrasia ya kutoa mawazo na kutatua matatizo yao kwa njia ya mikutano katika vituo vyao vya kazi kwa sababu katiba mbaya ya CWT, toleo la Desemba 18, 2009 kifungu cha 11 ( a) – (c), haiwapi madaraka wawakilishi kuitisha mikutano katika sehemu zao za kazi,"imeeleza sehemu ya taarifa hiyo.
Walimu hao walisema wamekuwa wakikatwa asilimia mbili ya mishahara yao ya kila mwezi kama ada ya uanachama hata wale ambao hawajajiunga uanachama jambo ambalo limekuwa likiwashangaza walimu wapya kutokana na kuwepo kwa utaratibu huo kandamizi.
Walisema chama kimekuwa hakina uwazi katika matumizi ya pesa za wanachama na wasio wanachama wake kwa mfano makato ya ada ya uwakala ya wasio wanachama yanapaswa kuwekwa katika akaunti tofauti na ile ya wanachama wake kutokana na kifungu cha 72 (3) (e) cha Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini Na.6/ 2004;
Walimu hao walisema kinachowashangaza ni kutokuwepo na sheria inayoruhusu mwalimu kujiondoa ndani ya chama na asiendelee kukwatwa ada ya uanachama na kuhoji suala la sheria ipi inayowaingiza kwenye makampuni ambayo yameanzishwa na CWT.
Aidha, wamelalamikia chama kuendeshwa kibiashara bila wanachama kujulishwa kama kampuni hiyo ni ya nani na ipo kwa faida ya nani na pia zipo taarifa za kuanzishwa kwa benki wakati katiba ya CWT haisemi lolote kuhusu benki hiyo.
Walisema kama mambo hayo yanayoendelea ndani ya chama hicho hayatapatiwa ufumbuzi na viongozi wa CWT watalazimika kutumia vyombo vya sheria kudai haki yao.
Rais wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Grasian Mkoba, akizungumzia malalamiko hayo alisema walimu ambao siyo wanachama wa chama hicho wanakatwa ada ya uanachama kutokana na sheria iliyoanzishwa na vyama vya wafanyakazi.
"Sheria iliyoanzisha vyama vya wafanyakazi inasema kuwa wanachama watarajiwa wakijiunga na chama zaidi ya nusu yao waliobaki wanakatwa ada ya chama hata kama hawajajiunga,"alisema Mkoba.
Mkoba alisema kwa walimu ambao wanataka kujiondoa ndani ya chama wanaweza wakafanya hivyo kwa kuandika barua lakini sheria inasema kama waliobaki ndani ya chama ni zaidi ya nusu waliojiondoa wataendelea kukatwa ada ya uachama hata kama wamejiondoa.
SOURCE: NIPASHE
By Thobias Mwanakatwe | 16th June 2012
Walimu nchini wametangaza mgogoro dhidi ya Chama cha Walimu Tanzania (CWT) ambao unaweza kusababisha mgomo wa nchi nzima kutokana na kutoridhishwa na mambo kadhaa ya ukandamizaji yanayoendelea ndani ya chama hicho.
Kwa mujibu wa taarifa waliyoisambaza kwa vyombo vya habari, walimu wa mkoa wa Kigoma walisema kutokana na hali ilivyo ndani ya chama hicho kuna haja kwa serikali kuingilia kati mgogoro huo unaoendelea kufukuta ambao umeanza kusababisha walimu kukosa ari na moyo wa kufundisha na usumbufu mwingi wa kwenda kwenye Mahakama ya Usuluhishi.
"Wanachama wamenyimwa fursa na demokrasia ya kutoa mawazo na kutatua matatizo yao kwa njia ya mikutano katika vituo vyao vya kazi kwa sababu katiba mbaya ya CWT, toleo la Desemba 18, 2009 kifungu cha 11 ( a) – (c), haiwapi madaraka wawakilishi kuitisha mikutano katika sehemu zao za kazi,"imeeleza sehemu ya taarifa hiyo.
Walimu hao walisema wamekuwa wakikatwa asilimia mbili ya mishahara yao ya kila mwezi kama ada ya uanachama hata wale ambao hawajajiunga uanachama jambo ambalo limekuwa likiwashangaza walimu wapya kutokana na kuwepo kwa utaratibu huo kandamizi.
Walisema chama kimekuwa hakina uwazi katika matumizi ya pesa za wanachama na wasio wanachama wake kwa mfano makato ya ada ya uwakala ya wasio wanachama yanapaswa kuwekwa katika akaunti tofauti na ile ya wanachama wake kutokana na kifungu cha 72 (3) (e) cha Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini Na.6/ 2004;
Walimu hao walisema kinachowashangaza ni kutokuwepo na sheria inayoruhusu mwalimu kujiondoa ndani ya chama na asiendelee kukwatwa ada ya uanachama na kuhoji suala la sheria ipi inayowaingiza kwenye makampuni ambayo yameanzishwa na CWT.
Aidha, wamelalamikia chama kuendeshwa kibiashara bila wanachama kujulishwa kama kampuni hiyo ni ya nani na ipo kwa faida ya nani na pia zipo taarifa za kuanzishwa kwa benki wakati katiba ya CWT haisemi lolote kuhusu benki hiyo.
Walisema kama mambo hayo yanayoendelea ndani ya chama hicho hayatapatiwa ufumbuzi na viongozi wa CWT watalazimika kutumia vyombo vya sheria kudai haki yao.
Rais wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Grasian Mkoba, akizungumzia malalamiko hayo alisema walimu ambao siyo wanachama wa chama hicho wanakatwa ada ya uanachama kutokana na sheria iliyoanzishwa na vyama vya wafanyakazi.
"Sheria iliyoanzisha vyama vya wafanyakazi inasema kuwa wanachama watarajiwa wakijiunga na chama zaidi ya nusu yao waliobaki wanakatwa ada ya chama hata kama hawajajiunga,"alisema Mkoba.
Mkoba alisema kwa walimu ambao wanataka kujiondoa ndani ya chama wanaweza wakafanya hivyo kwa kuandika barua lakini sheria inasema kama waliobaki ndani ya chama ni zaidi ya nusu waliojiondoa wataendelea kukatwa ada ya uachama hata kama wamejiondoa.
SOURCE: NIPASHE