Ziara ya M4C iliyoongozwa na kamanda John Heche imedhirisha dhahiri kuwa ili CCM ishinde katika uchaguzi wowote hapa Njombe itafanya kazi ya ziada.Kuna kila dalili kwamba wilaya ya Njombe sasa iko chini ya CHADEMA kwa 100%.Kamanda Heche ni moja kati ya viongozi ambao amefanya kazi kubwa hapa Njombe na Makambako.Akiwa Njombe alimchana vilivyo bibi Kiroboto na pia akiwa Makambako alimfanya vibaya sana mbunge wa kuchongwa wa jimbo hilo Deo Sanga(jah people).Uchumi wa Njombe umezidi kushuka wakati ni moja ya wilaya ambayo ilipaswa kuwa na maendeleo makubwa tofauti na maeneo mengi ya Tanzania.Njombe na Makambako hakuna huduma ya maji,hakuna umeme katika vijiji nje ya miji hii,hakuna barabara za uhakika,hakuna usimamizi wa raslimali za umma na hivyo kusababisha hati chafu kila mwaka na madudu mengine mengi.
Wilaya ya Njombe ni moja ya wilaya ambayo wananchi wengi wameamua kuanza kuwekeza katika siasa tofauti na ilivyokuwa hapo awali.
Wilaya ya Njombe ni moja ya wilaya ambayo wananchi wengi wameamua kuanza kuwekeza katika siasa tofauti na ilivyokuwa hapo awali.
katika mkutano wa jana wananchi wa Njombe wamwambia John kuwa wanajisikia aibu kubwa kuwa na spika toka Njombe ambaye ni aibu ya wananjombe kutokana na kuongoza vikao vya bunge kwa ubabe usiomithilika.
CHADEMA NI MUZIKI MNENE,TUNAANZA NA MUNGU NA TUTAMALIZA NA MUNGU.