Mundali
JF-Expert Member
- Sep 16, 2010
- 749
- 164
Wana JF salaam.
Najua wengi mtashangazwa na thread yangu, lakini kwa kusukumwa na utashi na hisia za mabadiliko ya kifikra, kisiasa na kiuchumi wa taifa letu, na ili kujibu hoja dhaifu za wafuasi wa CCM. Kwa mtazamo wangu chama cha mapinduzi (CCM) hakipo.
Kwa tafsiri isiyo rasmi, chama cha kisiasa ni muungano wa watu wenye nia na lengo moja la kisiasa. Muungano huu huwezesha wanachama kutengeneza mkataba ambao watauamini na kuutekeleza katika kutimiza malengo yao. Mkataba huo huitwa KATIBA. Hivyo chama kinaishi kwa kutokana na uwepo wa wanachama na katiba (mtazamo wangu).
Turejee mambo muhimu na ya msingi katika katiba ya CCM (Toleo la14 la mwaka 2010).
IMANI YA CCM (Ibara ya 4)Ibara ya 4(1) Binadamu wote ni sawa.
Ibara ya 4(2) Kila mtu anastahili heshima ya kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake.
Ibara ya 4(3) Ujamaa na kujitegemea ndio njia pekee ya kujenga jamii ya watu walio sawa na huru.
MALENGO NA MADHUMUNI YA CCM (Ibara ya 5)
Ibara ya 5(3) Kuhimiza ujenzi wa ujamaa na kujitegemea kwa mujibu wa Azimio la Arusha.
Ibara ya 5(9) Kuona kwamba nchi yetu inatawaliwa kwa misingi ya kidemokrasia na ya kijamaa.
SEHEMU YA PILI
WANACHAMA
Ibara ya 7. Raia yoyote wa Tanzania mwenye umri usiopungua miaka 18, anaweza kuwa mwanachama wa CCM iwapo anakubali Imani, Malengo na Madhumuni ya CCM.
WAJIBU WA MWANACHAMA (Ibara ya15)
Ibara ya 15(5) Kukiri kwa imani na kutekeleza kwa vitendo siasa ya CCM ya ujamaa na kujitegemea.
Pia katiba ya CCM imeweka ahadi za mwana CCM, zipo 9. Hapa ntaongelea ahadi tano tu.
Ahadi ya 4: Rushwa ni adui wa haki, sitapokea wala kutoa rushwa.
Ahadi ya 5: Cheo ni dhamana, sitatumia cheo changu wala cha mtu mwingine kwa faida yangu.
Ahadi ya 6: Nitajielimisha kwa kadiri ya uwezo wangu na kuitumiaelimu yangu kwa faida ya wote.
Ahadi ya 8: Nitasema kweli daima fitina kwangu mwiko.
Ahadi ya 9: Nitakuwa mwanachama mwaminifu wa CCM na raia mwema wa Tanzania na Afrika.
Kwa mujibu wa vipengele hivyo vya katiba ya CCM, mambo yafuatayo yanakitokea CCM haina viongozi (kwa sababu hawaamini katika katiba yao), ama haina wanachama, kama isemavyo ibara ya 7. Vinginevyo wanachama wa CCM na viongozi wake wanatekeleza malengo na madhumuni ambayo hawakujiwekea kwa mujibu wa katiba yao, hivyo wanakiuka katiba. Chama kinachopingana na katiba yake kimekufa.
Uwezekano wa pili ni kwamba CCM haina katiba, ama wana katiba ya nyuma ya pazia. Sababu CCM kupitia kwa viongozi wake wameikana katiba ya sasa na wameukana wajibu wao kama isemavyo ibara ya 15.
Hivyo basi CCM haipo kwa mujibu wa katiba yao, na haistahili kuongoza nchi.
Nawasilisha.
Najua wengi mtashangazwa na thread yangu, lakini kwa kusukumwa na utashi na hisia za mabadiliko ya kifikra, kisiasa na kiuchumi wa taifa letu, na ili kujibu hoja dhaifu za wafuasi wa CCM. Kwa mtazamo wangu chama cha mapinduzi (CCM) hakipo.
Kwa tafsiri isiyo rasmi, chama cha kisiasa ni muungano wa watu wenye nia na lengo moja la kisiasa. Muungano huu huwezesha wanachama kutengeneza mkataba ambao watauamini na kuutekeleza katika kutimiza malengo yao. Mkataba huo huitwa KATIBA. Hivyo chama kinaishi kwa kutokana na uwepo wa wanachama na katiba (mtazamo wangu).
Turejee mambo muhimu na ya msingi katika katiba ya CCM (Toleo la14 la mwaka 2010).
IMANI YA CCM (Ibara ya 4)Ibara ya 4(1) Binadamu wote ni sawa.
Ibara ya 4(2) Kila mtu anastahili heshima ya kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake.
Ibara ya 4(3) Ujamaa na kujitegemea ndio njia pekee ya kujenga jamii ya watu walio sawa na huru.
MALENGO NA MADHUMUNI YA CCM (Ibara ya 5)
Ibara ya 5(3) Kuhimiza ujenzi wa ujamaa na kujitegemea kwa mujibu wa Azimio la Arusha.
Ibara ya 5(9) Kuona kwamba nchi yetu inatawaliwa kwa misingi ya kidemokrasia na ya kijamaa.
SEHEMU YA PILI
WANACHAMA
Ibara ya 7. Raia yoyote wa Tanzania mwenye umri usiopungua miaka 18, anaweza kuwa mwanachama wa CCM iwapo anakubali Imani, Malengo na Madhumuni ya CCM.
WAJIBU WA MWANACHAMA (Ibara ya15)
Ibara ya 15(5) Kukiri kwa imani na kutekeleza kwa vitendo siasa ya CCM ya ujamaa na kujitegemea.
Pia katiba ya CCM imeweka ahadi za mwana CCM, zipo 9. Hapa ntaongelea ahadi tano tu.
Ahadi ya 4: Rushwa ni adui wa haki, sitapokea wala kutoa rushwa.
Ahadi ya 5: Cheo ni dhamana, sitatumia cheo changu wala cha mtu mwingine kwa faida yangu.
Ahadi ya 6: Nitajielimisha kwa kadiri ya uwezo wangu na kuitumiaelimu yangu kwa faida ya wote.
Ahadi ya 8: Nitasema kweli daima fitina kwangu mwiko.
Ahadi ya 9: Nitakuwa mwanachama mwaminifu wa CCM na raia mwema wa Tanzania na Afrika.
Kwa mujibu wa vipengele hivyo vya katiba ya CCM, mambo yafuatayo yanakitokea CCM haina viongozi (kwa sababu hawaamini katika katiba yao), ama haina wanachama, kama isemavyo ibara ya 7. Vinginevyo wanachama wa CCM na viongozi wake wanatekeleza malengo na madhumuni ambayo hawakujiwekea kwa mujibu wa katiba yao, hivyo wanakiuka katiba. Chama kinachopingana na katiba yake kimekufa.
Uwezekano wa pili ni kwamba CCM haina katiba, ama wana katiba ya nyuma ya pazia. Sababu CCM kupitia kwa viongozi wake wameikana katiba ya sasa na wameukana wajibu wao kama isemavyo ibara ya 15.
Hivyo basi CCM haipo kwa mujibu wa katiba yao, na haistahili kuongoza nchi.
Nawasilisha.