Chagga Restaurant

Ehud

JF-Expert Member
Feb 12, 2008
2,685
337
Wana JF nina wazo la kuanzisha Restaurant itakayouza vyakula vya Kichaga tu kama mtori,kiumbo,kishimba,machalari na kadhalika. Je hii biashara italipa kwa miji ya Dar es Salaam na Arusha? Pia kama kuna mtu anajua vyakula vingine vya kichaga ani-pm au avitaje hapa ili niviweke kwenye menu. Asanteni
 
wazo zuri lakini kwa nn visiwe vya makabila yote kama unajua mapishi yao au ukaajiri wapishi wanaoujua? bora uite jina lingine lakini sio chagga restaurant kwani dar hawaishi wachaga tu........iite Restaurant ya Kijamii au Traditional Food Restaurant
 
Wana JF nina wazo la kuanzisha Restaurant itakayouza vyakula vya Kichaga tu kama mtori,kiumbo,kishimba,machalari na kadhalika. Je hii biashara italipa kwa miji ya Dar es Salaam na Arusha? Pia kama kuna mtu anajua vyakula vingine vya kichaga ani-pm au avitaje hapa ili niviweke kwenye menu. Asanteni
Wazo zuri sana Mkuu, Siku nikiwa Dar Lazima niitafute hii Restaurant. Tuambia iko wapi ili tuwe tunaitembelea.
Mi ni mpenzi sana wa Ngande kwa hiyo nadhani itakuwepo.
 
wazo zuri lakini kwa nn visiwe vya makabila yote kama unajua mapishi yao au ukaajiri wapishi wanaoujua? bora uite jina lingine lakini sio chagga restaurant kwani dar hawaishi wachaga tu........iite Restaurant ya Kijamii au Traditional Food Restaurant

Nataka iwe ya ki-traditional zaidi lengo langu ni kutengeneza identity ya vyakula vya kichaga kama vile ambavyo Ethiopia au Chinese au India restaurant zilivyo. Vyakula vingine vinaweza kuwepo lakini nataka itambulike ni specialist wa chagga foods.
 
Wazo zuri sana Mkuu, Siku nikiwa Dar Lazima niitafute hii Restaurant. Tuambia iko wapi ili tuwe tunaitembelea.
Mi ni mpenzi sana wa Ngande kwa hiyo nadhani itakuwepo.


Usipate tabu mkuu itakuwepo ngande ya maharage na nyama wala usiwe na hofu.
 
Wana JF nina wazo la kuanzisha Restaurant itakayouza vyakula vya Kichaga tu kama mtori,kiumbo,kishimba,machalari na kadhalika. Je hii biashara italipa kwa miji ya Dar es Salaam na Arusha? Pia kama kuna mtu anajua vyakula vingine vya kichaga ani-pm au avitaje hapa ili niviweke kwenye menu. Asanteni

Kiburu (ndizi na maharage inakuwa kama mtori hivi), Ngande (ndizi na soe...magimbi flani meupeeee ndani yanaotaga mndenyi huko)... uwe serious basi sio umeandika kuongeza thread ulizoanzisha tu! wateja 'regular' tupo.
 
Wakuu nashukuru kwa maoni yenu nayafanyia kazi..
 
Mkuu we fungua tuu wateja tupo nyomi,mbona tunakulaga ng'ande hapo soccer city sinza?Ila usisaha VISHA/RLEMBWE(kunde zinapikwa halafu zinasongwa) pia NGARARIMO na KITAWA kwa asubuhi sio mbaya.
 
Back
Top Bottom