Mzee wa Kale
Member
- Feb 7, 2009
- 44
- 0
Na Mwinyi Sadallah,
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Zanzibar, kimeitisha maandamano makubwa kushinikiza viongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar(SMZ) warejeshe huduma ya umeme haraka au watangaze kujiuzulu, kabla ya maadhimisho ya Mapinduzi ya Zanzibar Januari 12, mwakani.
Tamko hilo lilitolewa jana na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Zanzibar, Hamad Mussa Yussuph, alipokuwa akizungumzia athari za kukosekana umeme kwa wananchi wa visiwa vya Zanzibar.
Alisema juhudi zinazochukuliwa na Serikali ya Zanzibar tangu kukosekana kwa umeme Desemba 10, mwaka huu, haziridhishi na wananchi wamekuwa wakiambulia ahadi hewa.
Alisema maandamano hayo yataanzia katika viwanja vya Maisara mjini Unguja na kumalizia katika viwanja vya Kibandamaiti mjini Unguja, ambapo pia wataalikwa wawakilishi wa asasi zisizokuwa za kiserikali na vyama vya siasa.
Alisema maandamano hayo yatafanyika Januari 10, mwaka huu ikiwa ni siku mbili kabla ya maadhimisho ya Mapinduzi Zanzibar.
Tunataka hadi Januari 12, mwaka huu umeme uwe umerejea Zanzibar au viongozi wawe wamewajibika kwa kushindwa kuwatumikia wananchi kama walivyoahidi, alisema.
Kukosekana kwa umeme kumesababisha matumizi makubwa ya jenereta, ambapo tayari yameanza kuleta athari baada ya mtu mmoja, Mahmuni Ali Abdallah, kulipukiwa na jenereta na kujeruhiwa vibaya na kulazimika kukimbizwa Hospitali ya Taifa Muhimbili, jijini Dar es Salaam kwa matibabu.
Hata hivyo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Kiongozi, Hamza Hassan Juma, alisema siyo kweli kwamba serikali haichukui hatua, lakini juhudi mbalimbali zinachukuliwa hivi sasa kutatua tatizo hilo.
Alisema hivi sasa serikali imeweka mipango ya muda mfupi na mrefu ili kuhakikisha huduma hiyo inapatikana haraka iwezekanavyo na kupunguza athari kwa wananchi.
CHANZO: NIPASHE
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Zanzibar, kimeitisha maandamano makubwa kushinikiza viongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar(SMZ) warejeshe huduma ya umeme haraka au watangaze kujiuzulu, kabla ya maadhimisho ya Mapinduzi ya Zanzibar Januari 12, mwakani.
Tamko hilo lilitolewa jana na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Zanzibar, Hamad Mussa Yussuph, alipokuwa akizungumzia athari za kukosekana umeme kwa wananchi wa visiwa vya Zanzibar.
Alisema juhudi zinazochukuliwa na Serikali ya Zanzibar tangu kukosekana kwa umeme Desemba 10, mwaka huu, haziridhishi na wananchi wamekuwa wakiambulia ahadi hewa.
Alisema maandamano hayo yataanzia katika viwanja vya Maisara mjini Unguja na kumalizia katika viwanja vya Kibandamaiti mjini Unguja, ambapo pia wataalikwa wawakilishi wa asasi zisizokuwa za kiserikali na vyama vya siasa.
Alisema maandamano hayo yatafanyika Januari 10, mwaka huu ikiwa ni siku mbili kabla ya maadhimisho ya Mapinduzi Zanzibar.
Tunataka hadi Januari 12, mwaka huu umeme uwe umerejea Zanzibar au viongozi wawe wamewajibika kwa kushindwa kuwatumikia wananchi kama walivyoahidi, alisema.
Kukosekana kwa umeme kumesababisha matumizi makubwa ya jenereta, ambapo tayari yameanza kuleta athari baada ya mtu mmoja, Mahmuni Ali Abdallah, kulipukiwa na jenereta na kujeruhiwa vibaya na kulazimika kukimbizwa Hospitali ya Taifa Muhimbili, jijini Dar es Salaam kwa matibabu.
Hata hivyo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Kiongozi, Hamza Hassan Juma, alisema siyo kweli kwamba serikali haichukui hatua, lakini juhudi mbalimbali zinachukuliwa hivi sasa kutatua tatizo hilo.
Alisema hivi sasa serikali imeweka mipango ya muda mfupi na mrefu ili kuhakikisha huduma hiyo inapatikana haraka iwezekanavyo na kupunguza athari kwa wananchi.
CHANZO: NIPASHE