CHADEMA yazidi kutikisa UZINI Zazibar

Molemo

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
14,534
13,225

IKIWA ni wiki ya lala salama ya kampeni za uchaguzi mdogo wa Jimbo la uwakilishi la Uzini, visiwani Zanzibar, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) tayari kimefanya mikutano 68 ya kumnadi mgombea wake, Ali Mbarouk Mshimba.
Hatua hiyo inatokana na chama hicho kufanya mikutano minane ya hadhara kila siku ili kuhakikisha jimbo hilo linatua mikononi mwake pamoja na kuwafikia wananchi wengi.Ni wazi kuwa chama hicho sasa kinatishia vyama viwili vya CCM na CUF na upo uwezekano mkubwa wa CHADEMA kunyakua jimbo hilo.
Katika mkutano uliofanyika kwenye Shehia ya Pagali, kada wa CHADEMA, Mtera Mwampamba, aliwataka vijana kujiepusha na kasumba ya kubebwa na Chama cha Mapinduzi (CCM) kwenye mikutano yake kwa ahadi ya kupatiwa ajira.
Mwampamba alisema badala yake vijana hao wanatakiwa kukumbuka walichofanyiwa katika uchaguzi mkuu uliopita baada ya kubebwa na kupelekwa kisiwani Pemba ambapo wengi wao walirudi na vilema na wengine kupoteza maisha.
Aliwataka vijana hao wasiwe na ugonjwa wa kusahau kiasi hicho, kwa kuwa hadi leo kati ya hao waliopelekwa, hakuna hata mmoja aliyepata ajira.
Naye, Ofisa Mwandamizi wa Utafiti na Sera wa CHADEMA, Mwita Waitara, aliwataka wakazi wa Uzini kutosita kuitosa CCM, kwa kuwa katika miaka 48 iliyokaa madarakani hakuna maendeleo iliyowafanyia.
Akitolea mfano alisema Uzini leo isingetakiwa kukosa huduma za maji ukizingatia kwamba Zanzibar pembe zote imezungukwa na maji, pia jimbo hilo halina shule wala zahanati, pamoja na kufahamika kuwa ndilo la pili katika harakati za kuleta mapinduzi.

SOURCE:TANZANIA DAIMA



 
Majibu kwenye sanduku la kura. Hatutaki kusikia hadithi za CDM kulalamika kuchakachuliwa na CCM/CUF safari hii. Kama ni kura kwa udogo wa jimbo lenyewe mnaweza kabisa kuzilinda na kuhakikisha zote zinahesabiwa kwa haki na kutangazwa kama zilivyo.
 
kwa zanzibar CDM wanacheza, sijui.. itakuwa ni maajabu ya Mwaka wakichukua jimbo. Hapo ndipo nitaamini sasa Maalim Seif kwisha kazi.
 
Naye, Ofisa Mwandamizi wa Utafiti na Sera wa CHADEMA, Mwita Waitara, aliwataka wakazi wa Uzini kutosita kuitosa CCM, kwa kuwa katika miaka 48 iliyokaa madarakani hakuna maendeleo iliyowafanyia.
Akitolea mfano alisema Uzini leo isingetakiwa kukosa huduma za maji ukizingatia kwamba Zanzibar pembe zote imezungukwa na maji, pia jimbo hilo halina shule wala zahanati, pamoja na kufahamika kuwa ndilo la pili katika harakati za kuleta mapinduzi.

SOURCE:TANZANIA DAIMA




Hivi huyu Mwita Waitara anajua anachoongea au na yeye analipukua tu kama Magamba?! Hivi anajua technology and cost ya kufanya DESALINATION of Ocean/sea water?

Ndiyo Zanzaibar imezungukwa na maji lakini yale ni maji ya chumvi. Hata nchi zilizoendelea kama Japan haithubutu kufanya desalination of ocean water for domestic use insteady wametafuta vyanzo vinginevyo vya kupata maji ambayo siyo ya chumvi.

Anataka kuwadanganya wana Uzini kwamba CDM ikipewa dola itaweza kufanya desalination of ocean water kuondoa tatizo la maji?

Ama kweli all politician are alike. Ujinga wa wana Siasa tuukate out right, vinginevyo hata sisi wasomi tutaonekana bogus!
 
hivi huyu mwita waitara anajua anachoongea au na yeye analipukua tu kama magamba?! Hivi anajua technology and cost ya kufanya desalination of ocean/sea water?

Ndiyo zanzaibar imezungukwa na maji lakini yale ni maji ya chumvi. Hata nchi zilizoendelea kama japan haithubutu kufanya desalination of ocean water for domestic use insteady wametafuta vyanzo vinginevyo vya kupata maji ambayo siyo ya chumvi.

Anataka kuwadanganya wana uzini kwamba cdm ikipewa dola itaweza kufanya desalination of ocean water kuondoa tatizo la maji?

Ama kweli all politician are alike. Ujinga wa wana siasa tuukate out right, vinginevyo hata sisi wasomi tutaonekana bogus!

kila kitu ni mipango wewe!hakuna kinachoshindikana!
 
Hivi huyu Mwita Waitara anajua anachoongea au na yeye analipukua tu kama Magamba?! Hivi anajua technology and cost ya kufanya DESALINATION of Ocean/sea water?

Ndiyo Zanzaibar imezungukwa na maji lakini yale ni maji ya chumvi. Hata nchi zilizoendelea kama Japan haithubutu kufanya desalination of ocean water for domestic use insteady wametafuta vyanzo vinginevyo vya kupata maji ambayo siyo ya chumvi.

Anataka kuwadanganya wana Uzini kwamba CDM ikipewa dola itaweza kufanya desalination of ocean water kuondoa tatizo la maji?

Ama kweli all politician are alike. Ujinga wa wana Siasa tuukate out right, vinginevyo hata sisi wasomi tutaonekana bogus!

Acha kudanganya watu kwa kukariri mambo, Japan hawajashindwa bali hawajaamua, haiingii akilini Japan washindwe and then Cyprus waweze.
 
Zanzibar ina wenyewe chadema ipate umaarufu kutoka wapi? propaganda inapendeza kama inakaribiana na ukweli.
 
IKIWA ni wiki ya lala salama ya kampeni za uchaguzi mdogo wa Jimbo la uwakilishi la Uzini, visiwani Zanzibar, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) tayari kimefanya mikutano 68 ya kumnadi mgombea wake, Ali Mbarouk Mshimba.
Hatua hiyo inatokana na chama hicho kufanya mikutano minane ya hadhara kila siku ili kuhakikisha jimbo hilo linatua mikononi mwake pamoja na kuwafikia wananchi wengi.Ni wazi kuwa chama hicho sasa kinatishia vyama viwili vya CCM na CUF na upo uwezekano mkubwa wa CHADEMA kunyakua jimbo hilo.
Katika mkutano uliofanyika kwenye Shehia ya Pagali, kada wa CHADEMA, Mtera Mwampamba, aliwataka vijana kujiepusha na kasumba ya kubebwa na Chama cha Mapinduzi (CCM) kwenye mikutano yake kwa ahadi ya kupatiwa ajira.
Mwampamba alisema badala yake vijana hao wanatakiwa kukumbuka walichofanyiwa katika uchaguzi mkuu uliopita baada ya kubebwa na kupelekwa kisiwani Pemba ambapo wengi wao walirudi na vilema na wengine kupoteza maisha.
Aliwataka vijana hao wasiwe na ugonjwa wa kusahau kiasi hicho, kwa kuwa hadi leo kati ya hao waliopelekwa, hakuna hata mmoja aliyepata ajira.
Naye, Ofisa Mwandamizi wa Utafiti na Sera wa CHADEMA, Mwita Waitara, aliwataka wakazi wa Uzini kutosita kuitosa CCM, kwa kuwa katika miaka 48 iliyokaa madarakani hakuna maendeleo iliyowafanyia.
Akitolea mfano alisema Uzini leo isingetakiwa kukosa huduma za maji ukizingatia kwamba Zanzibar pembe zote imezungukwa na maji, pia jimbo hilo halina shule wala zahanati, pamoja na kufahamika kuwa ndilo la pili katika harakati za kuleta mapinduzi.

SOURCE:TANZANIA DAIMA
[/QUO




Kumbe source ni gazeti la uhuru la CDM
 
Suala la Uzini na chadema linakuzwa wakati chadema haina jeuri ya kutamba znz, siasa za maji taka.
 
Hivi huyu Mwita Waitara anajua anachoongea au na yeye analipukua tu kama Magamba?! Hivi anajua technology and cost ya kufanya DESALINATION of Ocean/sea water?

Ndiyo Zanzaibar imezungukwa na maji lakini yale ni maji ya chumvi. Hata nchi zilizoendelea kama Japan haithubutu kufanya desalination of ocean water for domestic use insteady wametafuta vyanzo vinginevyo vya kupata maji ambayo siyo ya chumvi.

Anataka kuwadanganya wana Uzini kwamba CDM ikipewa dola itaweza kufanya desalination of ocean water kuondoa tatizo la maji?

Ama kweli all politician are alike. Ujinga wa wana Siasa tuukate out right, vinginevyo hata sisi wasomi tutaonekana bogus!

tuambie kiwango chako cha usomi...
 
Ili kuipenya zanzibar chadema wanahitaji propaganda ya juu sana na hii ni kati ya propaganda hiyo kwamba inakubarika zanzibar wakati ukweli haikubariki.
 
Back
Top Bottom