CHADEMA yaweweseka...

sir.JAPHET

JF-Expert Member
May 18, 2012
699
133
010812.jpg

Alhamisi, Agosti 30, 2012 | Imeandikwa na Arodia Peter | Mtanzania

*Yalia polisi kuiruhusu CCM Lindi kuandamana
*Yaikataa tume ya kuchunguza mauaji Morogoro

WAKATI Jeshi la Polisi nchini, likisitisha mikutano na maandamano ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimeonekana wazi kuweweseka, baada ya wafuasi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Lindi kuandamana jana.

Habari kutoka mkoani Lindi, zinasema wafuasi wa CCM waliandamana wakati wakimsindikiza mgombea wa nafasi ya Mwenyekiti wa Wilaya wa chama hicho, Muhsin Rafi Ismail.

Kutokana na hali hiyo, Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CHADEMA, John Mnyika, aliitisha mkutano wa waandishi wa habari mjini Dar es Salaam jana na kusema maandamano hayo yameonekana wazi kukiuka maagizo ya Jeshi la Polisi.

"Tumeshangazwa sana na wenzetu wa CCM kufanya maandamano ya kumsindikiza mgombea wa nafasi ya Mwenyekiti wa Wilaya… kama tunavyokumbuka juzi polisi wamezuia vyama vyote kufanya mikutano hadi zoezi la Sensa ya Watu na Makazi litakapomalizika, jamani mbona hatutendawi haki.

"Ukiacha maandamano hayo, tunashangaa kuona Tume ya Kukusanya Maoni ya Katiba mpya, inaendelea na mikutano yake katika mikoa mbalimbali… je, suala hili haliingilii Sensa?" Alihoji Mnyika.

"Hapa hatuoni polisi wakiwazuia kwa kuwa Sensa inaendelea, zuio hilo linajitokeza wakati Chadema inapotaka kufanya shughuli zake za kisiasa kwa mujibu wa Katiba," alisema Mnyika.

Alisema wao kama chama, wanaheshimu mazungumzo na utawala wa sheria, ndiyo maana wameamua kuheshimu wito wa Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) Said Mwema, wa kusitisha mikutano na maandamano yao ili kupisha Sensa ikamilike.

Hata hivyo, alisema wanalitaka Jeshi la Polisi kutoa tamko ili umma ufahamu ni shughuli gani za kisiasa zinapaswa kuendelea ili kuepuka vikwazo.

MTANZANIA ilipomtafuta mgombea wa CCM Wilaya ya Lindi, Ismail kupata ukweli, alisema: "Ni kweli tumeandamana na wafuasi wangu wakati wa kurudisha fomu…sisi tunaona ni jambo la kawaida, hao wanaobeza wana lao jambo.

"Ni kweli maandamano yalifanyika, kimsingi ni marafiki zangu wameamua kunisindikiza, walikuwepo watembea kwa miguu, baiskeli, pikipiki na bajaji.

"Maandamano yalianzia nyumbani kwangu, Mtaa wa Uhuru, yakapita Soko Kuu, stendi ya mabasi kuelekea ofisi za chama eneo la Wailes," alisema Ismail.

Wakati huo huo, Mnyika alisema chama hicho kimeikataa tume iliyoundwa na Jeshi la Polisi kuchunguza kifo cha kijana Ally Zona, kilichotokea wakati wa kuzima maandamano yake mjini Morogoro.

Alisema, chama hicho kimefikia uamuzi wa kuikataa tume hiyo, kwa sababu tume nyingi ambazo zimeundwa na jeshi hilo, hazijawahi kutoa ripoti hadharani.

"Kama jeshi hili limeweza kumpotosha Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk. Emanuel Nchimbi, kuhusu sababu za wao kuzuia maandamano yetu, watashindwaje kuhujumu uchunguzi huo?

"Tunatoa taarifa rasmi, tunapinga na hatuitambui timu iliyoundwa na Jeshi la Polisi kuchunguza kifo hicho, kwa kuwa pia wao ni watuhumiwa wa mauaji hayo.

"Kifo hiki kinapaswa kuchunguzwa na tume huru na siyo polisi ambao ni watuhumiwa wakuu wa suala hili," alisema Mnyika.

Aidha katika hatua nyingine, Chadema kimemwomba Rais Kikwete kutumia madaraka yake ya kikatiba, kutekeleza sheria (Enquest Act), Ibara ya 33 (3), kuunda tume huru ya kuchunguza kifo chochote chenye utata.

 
CCM wapo so full of themselves... Inauma kuwa hawana busara kabisa na kutaka kuonesha kwa ubabe dhidi ya vyama vingine hasa CDM inawafanya wakose upeo wa kufikiria kuwa wananchi tunaona yote na yanatuumiza. Inakuwa kama wanachukulia Watanzania wote ni wapuuzi na wa kuendeshwa tu.

Nashangaa kwa hii habari, nilipoona habari ya kuhusu Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo mh. Amos Makalla kuendelea na shughuli zake za kisiasa katika jimbo lake tena wakati huu huu wa sensa ambapo serkali imetoa agizo shughuli kama hizo zisimame; nilichukulia kama bahati mbaya fulani hivi. Sasa hii ni dhahiri kabisa kuwa makusudi yao!

BTW Hivi vichwa vya habari naona ni wakati wa fani ya uandishi iangaliwe upya, sasa hapo CHADEMA wanaweweseka ama kueleza facts?
 
Huko sii kuweweseka Munyika amesema ukweli umwagikaji damu unao endelea ccm na selikar yake itabeba hii zambi kwakuto kuwa makini na mipango na maamzi yake

Nnchi hii ni ya watanzania wote sio ccm peke yao
 
Hapa hata mtoto mdogo wa std I ataelewa na kuwa na ufahamu wa kupambanua ukweli halisi!! na uwongo!!

Katika hali ya kawaida tungetegemea kichwa cha habari kingesomeka kiungwana!! lakini gazeti kumbe ni kati ya vijarida vilivyonunuliwa na wezi wa MABWEPANDE!!

Plain stupidity you must have a balanced information in your media!!! Wakati unatumia neno "kuweweseka" umeegemea msitu wa MABWEPANDE!!
 
WAKATI Jeshi la Polisi nchini, likisitisha mikutano na maandamano ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), upendeleo wa wazi umeonekana baada ya wafuasi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Lindi kuandamana jana.

Habari kutoka mkoani Lindi, zinasema wafuasi wa CCM waliandamana wakati wakimsindikiza mgombea wa nafasi ya Mwenyekiti wa Wilaya wa chama hicho, Muhsin Rafi Ismail.

Kutokana na hali hiyo, Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CHADEMA, John Mnyika, aliitisha mkutano wa waandishi wa habari mjini Dar es Salaam jana na kusema maandamano hayo yameonekana wazi kukiuka maagizo ya Jeshi la Polisi.

“Tumeshangazwa sana na wenzetu wa CCM kufanya maandamano ya kumsindikiza mgombea wa nafasi ya Mwenyekiti wa Wilaya… kama tunavyokumbuka juzi polisi wamezuia vyama vyote kufanya mikutano hadi zoezi la Sensa ya Watu na Makazi litakapomalizika, jamani mbona hatutendawi haki..

MTANZANIA ilipomtafuta mgombea wa CCM Wilaya ya Lindi, Ismail kupata ukweli, alisema: “Ni kweli tumeandamana na wafuasi wangu wakati wa kurudisha fomu…sisi tunaona ni jambo la kawaida, hao wanaobeza wana lao jambo.

“Ni kweli maandamano makubwa yalifanyika huku tukisindikizwa na Polisi, kimsingi ni marafiki zangu wameamua kunisindikiza, walikuwepo watembea kwa miguu, baiskeli, pikipiki na bajaji.

“Maandamano yalianzia nyumbani kwangu, Mtaa wa Uhuru, yakapita Soko Kuu, stendi ya mabasi kuelekea ofisi za chama eneo la Wailes,” alisema Ismail.

Source:Mtanzania Alhamisi
 
Niko hapa Shinyanga mjini,tangia jumatatu kuna watu wengi katika uwanja wa Kambarage kwa ajili ya chaguzi mbalimbali za CCM.Kitu ambacho kinanisikitisha ni jeshi la Polisi kusema chedema wasiendelee na mikutano yao kwa ajili ya sensa ,sasa hawa CCM wao wanaendelea na shughuli zao za kichama.Suala hili sio haki Polisi tumieni busara ili jamii nzima ya kitanzania iweze kuwaheshimu vinginevyo mnazidi kujizalilisha
 
Kila siku tunasema hapa kwamba hawa makamanda wa jeshi la polisi wanatumia nafasi zao za ukada wa ccm kukandmiza demokrasia. Lakini tunayo matumaini kwakuwa Mungu yuko upande wetu na kamwe hatutarudi nyuma hadi ukombozi wa kweli utakapopatikana.
 
Kuna upotoshaji kwenye habari hii,

Maandamano ya mgombea hayaandaliwi na Chama. Kama mgombea alichukua marafiki na watu wanaomuunga mkono wakaandamana huwezi kukilaumu chama kuwa ndicho kilichoandaa maandamano.

Kwa kanuni ya CCM hairuhusiwi kufanya maandamano wakati wa kurudisha fomu za uchaguzi wa ndani, kwa hiyo wanaofanya hivyo wanakiuka hata kanuni za CCM yenyewe.
 
Hapa hata mtoto mdogo wa std I ataelewa na kuwa na ufahamu wa kupambanua ukweli halisi!! na uwongo!!

Katika hali ya kawaida tungetegemea kichwa cha habari kingesomeka kiungwana!! lakini gazeti kumbe ni kati ya vijarida vilivyonunuliwa na wezi wa MABWEPANDE!!

Plain stupidity you must have a balanced information in your media!!! Wakati unatumia neno "kuweweseka" umeegemea msitu wa MABWEPANDE!!

mangikule,

You're very correct!

Watanzania wanatakiwa kuwa makini sana na baadhi ya media(TV,Radio,Magazeti+vijarida). Watanzania kila siku wanalishwa takataka(garbages) kutoka media mbalimbali kwa makusudi kabisa. Huu ni mkakati maalumu wa CCM na Serikali yake kuwalaghai watu ili wazidi kuwaamini! Chunguza sana habari kutoka vijarida vya udaku,magazeti na Chama na serikali kama Uhuru,Mzalendo,Daily News, Habari leo n.k. Hawajawahi kuandika habari ya ukweli hata moja!

Watu wanatakiwa wajiulize tu kwanini Rais Kiwete ameteua ma-DC wengi sana safari hii! Ni mkakati uleule wa KUTAKA KUWAHONGA NA KUWANYAMAZISHA WASIANDIKE HABARI HASI DHIDI YA CCM NA SERIKALI YAKE! Maana yake ni kwamba kama wewe utaiandika vizuri CCM na serikali yake utapewa tuzo(credit) ya u-DC au u-RC. Kama kuna ukweli wowote kuhusu vyama vya upinzani na Wabunge wake basi wewe andika uongo au kinyume chake.

Hiki ndicho kinachoendelea kwa sasa kuhusu sakata hili la mauaji ya Mwananchi asiye na hatia kule Msamvu,Morogoro. Gazeti la Mtanzania ili kupotosha ukweli limeandika kuwa CDM YAWEWESEKA! Huu si ukweli hata kidogo. Haiwezekani CDM ndiyo waweweseke wakti wao hawana tatizo lolote! Mwenye tatizo hapa ni CCM na serikali yake na hawa ndio wanaonekana kuweweseka kwa maana:

  1. Kwanza,kuzuia mikutano ya CDM kwa kisingizio cha sensa lakini wakti huohuo kuruhusu mikutano ya CCM inayoendelea kote nchini kuhusiana na kampeni za Chaguzi za chama hicho!Pia ile Tume ya kukusanya Maoni kuhusu Katiba mpya bado inaendelea na shughuli zake huku watu wakiendelea kuhudhuria mikutano ile.
  2. Pili ni kuunda tume ya uchunguzi kuhusiana na kifo cha Mwananchi wakti wa maandamano ya CDM juzi pale Morogoro. Polisi ndiyo wanatuhumiwa kuua huyo Mwananchi kwa risasi,kwa akili ya kawaida tu haiwezekani mtuhumiwa au mhalifu ajichunguze mwenyewe!Hatatenda haki hapo hata siku moja. Lazima atapindisha ukweli ili kuficha makosa yake!
  3. Tatu na mwisho ni kwamba Serikali wametoa kauli 2 tofauti zenye utata kuhusiana na kifo hicho.Kauli ya kwanza Polisi walisema marehemu aliuawa kwa risasi na kupelekea kuunda Tume ya kuchunguza mauaji hayo lakini kwa sasa wamegeuka na kutoa tamko kuwa marehemu aliuawa na kitu kizito!!!

Sasa kwa mwandishi makini hawezi kusema CDM ndio wanaweweseka. Hapa ukweli wa kichwa cha habari ni kuwa POLISI NA CCM WANAWEWESEKA! Kinachofanyika hapa ni juhudi za Polisi,Serikali na CCM kutaka kuwahadaa na kuwapotosha Watanzania wasijue ukweli wa kilichomtokea Morogoro kwa makusudi ili wasizidi kuichukia serikali ya CCM.

Mipango na style ni zilezile zilizotumika kutaka kuficha ukweli wa kilichompata Dr. Ulimboka!!!
 
Mimi nikiwaambia chdm imejaa waropokaji mnabisha, siku zote ukishindwa kufuata taratibu utaishia kulalama tu. wenzenu wanafanya maandamano ya kistaarabu, ninyi mnasababisha maafa tukiangalia arusha, singida na sasa morogoro, tunapata picha mbaya kuhusu maandamano ya cdm, na hivyo kwa polisi kuchukua tahadhari kwa wauaji ni sahihi kabisa. haya tuangalie mambo ya katiba na sensa hivi kama mtu unaakili za kutosha unaweza kufananisha na mikutano ya mvt for Chagaland>? Na iweje nyie muwe mnasababisha maafa halafu mumpe raisi kazi ya kuunda mitume isiyokuwa na tija,? haya ndo mapungufu ninayoyaona kwa wanachadema they think too little.
Akili zako finyu ndo zinakufanya uandike uliyoandika hivi katika mauaji yote ya wana CDM yanayotokea nchini yanasababishwa na CDM fikiria kabla ya kunena Polisi na CCM ndo chanzo cha vifo hivyo hakuna maandamano yaliyofanyika katika nchi hii yakawa na vurugu ila utokea vurugu pale tu polisi wanapotumwa na mabwana zako kuzuia maandamano hayo. na unaposema M4C ni movement 4 chagaland hapo ndugu yangu ni kauli ya kukata tamaa na kimbunga kinachowajia na mwaka huu mtakoma.
 
mangikule,

You're very correct!

Watanzania wanatakiwa kuwa makini sana na baadhi ya media(TV,Radio,Magazeti+vijarida). Watanzania kila siku wanalishwa takataka(garbages) kutoka media mbalimbali kwa makusudi kabisa. Huu ni mkakati maalumu wa CCM na Serikali yake kuwalaghai watu ili wazidi kuwaamini! Chunguza sana habari kutoka vijarida vya udaku,magazeti na Chama na serikali kama Uhuru,Mzalendo,Daily News, Habari leo n.k. Hawajawahi kuandika habari ya ukweli hata moja!....
Thanks Makoye This is the type of analysis we are looking for! in a government and ruling party where willingly/unwillingly, consciously/unconsciously they have decided to kill analytical minds! I hate these demons!!
 
Mimi nikiwaambia chdm imejaa waropokaji mnabisha, siku zote ukishindwa kufuata taratibu utaishia kulalama tu. wenzenu wanafanya maandamano ya kistaarabu, ninyi mnasababisha maafa tukiangalia arusha, singida na sasa morogoro, tunapata picha mbaya kuhusu maandamano ya cdm, na hivyo kwa polisi kuchukua tahadhari kwa wauaji ni sahihi kabisa. haya tuangalie mambo ya katiba na sensa hivi kama mtu unaakili za kutosha unaweza kufananisha na mikutano ya mvt for Chagaland>? Na iweje nyie muwe mnasababisha maafa halafu mumpe raisi kazi ya kuunda mitume isiyokuwa na tija,? haya ndo mapungufu ninayoyaona kwa wanachadema they think too little.
kuna watu uwezo wao wa kufikiri kweli ni mdogo sana
 
Hii miaka 5, chadema tuongeze mshikamano na maarifa ya kupambana na Serikali ya CCM yaani maadui zetu...
 
Happy sweetie umeni shangaza sana kuupambanua vizuri huwezo wako wa kufikiri.

Ikumbukwe kwamba maandamano yalizuiwa yote haijarishi, sasa sijui huko nchi gani?
Hebu jaribu kusema maandamano yapi si ya kistaarabu?
Asante pia kwa kuonesha ushabiki wako!
Pia nikwambie tumechoka na campaign zenu za kuhamasisha ukabila na wewe hizi huziwezi kabisa waachie wengine!

Yani kama umeshindwa kutambua mapungufu ya jeshi letu la polisi basi umenionesha jinsi ulivyo kuwa darasani!

Mchana mwema!


Mimi nikiwaambia chdm imejaa waropokaji mnabisha, siku zote ukishindwa kufuata taratibu utaishia kulalama tu. wenzenu wanafanya maandamano ya kistaarabu, ninyi mnasababisha maafa tukiangalia arusha, singida na sasa morogoro, tunapata picha mbaya kuhusu maandamano ya cdm, na hivyo kwa polisi kuchukua tahadhari kwa wauaji ni sahihi kabisa. haya tuangalie mambo ya katiba na sensa hivi kama mtu unaakili za kutosha unaweza kufananisha na mikutano ya mvt for Chagaland>? Na iweje nyie muwe mnasababisha maafa halafu mumpe raisi kazi ya kuunda mitume isiyokuwa na tija,? haya ndo mapungufu ninayoyaona kwa wanachadema they think too little.
 
Back
Top Bottom