Katika hali ambayo haikutarajiwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo-CDM kimeingia kwa kishindo jimboni Monduli katika operesheni ya M4C Vua Gamba Vaa Gwanda.
Katika mikutano iliyofanyika juzi CDM imezoa viongozi wa vijiji,wajumbe wa serikali za mitaa na mabalozi wa nyumba kumi wapatao 25 huku wakitoa kadi kwa wanachama wapya 700.Operesheni hiyo iliongozwa na Mkiti wa mkoa Samson Mwigamba na Mkiti wa Bavicha Kamanda Ephata Nanyaro pamoja na makamanda wengjne kadhaa.
Tofauti na ilivyodhaniwa awali kwamba jimbo hilo ni la wafuasi sugu wa Lowassa lakini hali imekuwa tofauti kabisa kwani kila kata wanayofika makamanda wa CDM wanalakiwa kwa shangwe na kufungua mashina kadhaa ya chama,huku mwanachama mmoja akijitolea kulipia pango ofisi ya chama jimbo shilingi laki 6.
Source:Tanzania Daima
Katika mikutano iliyofanyika juzi CDM imezoa viongozi wa vijiji,wajumbe wa serikali za mitaa na mabalozi wa nyumba kumi wapatao 25 huku wakitoa kadi kwa wanachama wapya 700.Operesheni hiyo iliongozwa na Mkiti wa mkoa Samson Mwigamba na Mkiti wa Bavicha Kamanda Ephata Nanyaro pamoja na makamanda wengjne kadhaa.
Tofauti na ilivyodhaniwa awali kwamba jimbo hilo ni la wafuasi sugu wa Lowassa lakini hali imekuwa tofauti kabisa kwani kila kata wanayofika makamanda wa CDM wanalakiwa kwa shangwe na kufungua mashina kadhaa ya chama,huku mwanachama mmoja akijitolea kulipia pango ofisi ya chama jimbo shilingi laki 6.
Source:Tanzania Daima