Elections 2010 CHADEMA yatoa tamko: Hatumtambui Kikwete kama rais

Sikubaliani na uamuzi wa kutokwenda mahakamani. Katika mabandiko yangu ya nyuma nilieleza suala hili kwa urefu sana na kuonyesha kuwa Mahakama ya Rufaa ilikwisha tamka kuwa kitendo chochote kile cha Tume ambacho kimefanywa kinyume cha sheria kinapingwa. Nilijitahidi kuwasilisha maoni yangu kwa mwanasheria wao lakini inaelekea wamekataa. Inasikitisha.
Bado ninasisitiza kuwa Mahakama Kuu inabanwa na uamuzi ule wa Mahakama ya Rufaa na hapo ndio ungekuwa uwanja mzuri wa Chadema kuanika ushahidi hadharani. Lakini Wanasheria hutofautiana mbinu za kupambana.


Wanashindwa kwenda mahakamani kwa kuwa hawana ushahidi wakutosha zaidi ya maneno ya uchakachuaji tu... Nimechukizwa sana na mwenendo huu wa viongozi wetu.. Eti leo walikuwa na tafrija ya kurekea ushindi! Ushindi upi huo? Au ni huu wa viti 24 vya wa bunge?
 
Je ni hatua gani zinachukuliwa kufichua kilichofanyika?

Kamati zinakutana kutoa mchanganuo rasmi wa kilichotokea

Je, kuna precaution zozote zinafanyika ili wakuu wa Dr Slaa wasillishwe kasa na kumpatia Dr. SLAA KASA?

Ni issue ya kichama zaidi wakifanya hivyo watakuwa wametusaliti nguvu ya umma itawashukia. NINACHOJUA HAKUNA MWENYE NJAA

Je, What is the way forward?

The way foraward

1. JK hatambuliwi na CHADEMA wala na Dr. Slaa kama mgombea ingawaje watashiriki kwenye shughuli za serikali. Sababu ni NEC kupuuza kusitisha kutangaza matokeo baada ya kuelezwa kasoro
2. Kupewa nafasi ndani ya serikali haliwezekani
3. Mchakato wa Katiba ambayo ndiyo kiini cha mataizo umeanza
4, Wana Chadema wanachama na wapenzi kupitia wawakilishi wao kila ngazi waonyesha utendaji kwa maslahi ya taifa ili wananchi waone tofauti

Haya maneno nimeyasikia Star TV yakitolewa na mwenyekiti Mbowe. Mimi yamenipa matumaini makubwa kwa sababu nilitaka waseme hivyo

Umeanza vipi yani?
maana nakumbuka jk alisema kubadili katiba ni ndoto!
 
Nyie wengine mnatokea nchi gani humu duniani!? Waende mahakamani kwa lipi? Wewe unadhani peke yako ndiyo una uchungu, wenyewe hawana? Hakuna cha kuwakilisha mahakamani, maelezo yako uliyotoa yalikuwa ni null and void.

Ninatokea Tanzania ndugu yangu je wewe ndiye ambaye hujui kuwa uchaguzi ulichakachuliwa? Je, wewe una kutu ya akili kutojua kuwa Tume ya Uchaguzi ilitoa matokeo mengi yanayotofautiana na yale yaliyopatikana vituoni? Je, wewe ni miongoni mwa wale ambao hawataki ukweli ujulikane ili waliohaini matakwa ya Watanzania waadhibiwe? Je, wewe ni mchumia tumbo anayenufaika na wizi na ufisadi unaotokea nchini?

Kuhusu uchungu wa nchi yangu hilo ni suala lisilokuwa na ubishi na nenda kawaulize hao Mafisadi kuhusu mimi watakueleza kwani mimi hapa natumia jina halisi. Nina kielewa kile ninachokisema na ninaweza kukipigania. Kukurupuka kwako na kuropoka kwako kuwa eti maelezo yangu hayakuwa ya msingi au batili ni uthibitisho wazi kuwa ninazungumza na mtu ambaye uwezo wake wa kufikiria na kuchambua mambo ni mdogo sana na ingekuwa vema ukanyamaze ili usiendelee kuanika uelewa wako mdogo. Kwani wahenga walisema asiyefunzwa na mama hufunzwa na ulimwengu. Hivi ndivyo ulimwengu unakufunza kuwa wakati mwingine kunyamaza ni bora kuliko kupayuka.
 
Viongozi wa Chadema siku za hivi karibuni wamekuwa watu wasio eleweka kutokana na kutokuweka huo wanaosema uchakachuwaji wa kura adharani, kila siku wanasema wanakusanya data tu hatimaye tutafika 2011 pasipo kupatikana hizo data kamili...

Naona hizi ni dalili za kutufanya tusahau mambo ya uchanguzi na kubaki tukiamini kuwa uchanguzi ulitawaliwa na wizi ..

Nawataka viongozi wachadema kutoa hilo tamko lao mapema iwezekanavyo ili tutambue huo uchakachuwaji wanaousema, wakishindwa kufanya hivyo hakuna sababu ya kutokumtambua JK.

Sasa unataka wakurupuke ili useme kuwa sio watu makini au?imekula kwako,hawa kurupuki ng'o
 
Wanashindwa kwenda mahakamani kwa kuwa hawana ushahidi wakutosha zaidi ya maneno ya uchakachuaji tu... Nimechukizwa sana na mwenendo huu wa viongozi wetu.. Eti leo walikuwa na tafrija ya kurekea ushindi! Ushindi upi huo? Au ni huu wa viti 24 vya wa bunge?

kumbe we unadhani wameshindwa?
wanajua wananchi wangapi wamepigia chadema kura,hata kama raisi wetu hakutangazwa mshindi,kinacho tambulika kwetu ni kimoja tumeshinda na wana wa nchi wanatukubali,tunapo sherehekea tuna jiandaa kwa kuwafanyia yale waliyo tutuma kufanya na kuonesha kuwa hawakukosea kutuchagua.

sasa wewe unadhani wameshindwa nini?
toka viti 5 hadi 24 ni kushindwa?
ulitaka wakae kulia badala yake au?
 
Ninatokea Tanzania ndugu yangu je wewe ndiye ambaye hujui kuwa uchaguzi ulichakachuliwa? Je, wewe una kutu ya akili kutojua kuwa Tume ya Uchaguzi ilitoa matokeo mengi yanayotofautiana na yale yaliyopatikana vituoni? Je, wewe ni miongoni mwa wale ambao hawataki ukweli ujulikane ili waliohaini matakwa ya Watanzania waadhibiwe? Je, wewe ni mchumia tumbo anayenufaika na wizi na ufisadi unaotokea nchini?

Kuhusu uchungu wa nchi yangu hilo ni suala lisilokuwa na ubishi na nenda kawaulize hao Mafisadi kuhusu mimi watakueleza kwani mimi hapa natumia jina halisi. Nina kielewa kile ninachokisema na ninaweza kukipigania. Kukurupuka kwako na kuropoka kwako kuwa eti maelezo yangu hayakuwa ya msingi au batili ni uthibitisho wazi kuwa ninazungumza na mtu ambaye uwezo wake wa kufikiria na kuchambua mambo ni mdogo sana na ingekuwa vema ukanyamaze ili usiendelee kuanika uelewa wako mdogo. Kwani wahenga walisema asiyefunzwa na mama hufunzwa na ulimwengu. Hivi ndivyo ulimwengu unakufunza kuwa wakati mwingine kunyamaza ni bora kuliko kupayuka.

Wewe, katika nchi ambayo ina watu kama wewe, kutofautina matokeo ni kitu cha kawaida kabisa. Huwezi ukapata exact figures za Kigoma,mwanza, mbeya, Tanga na mikoa yote nchini na zile zitakazokuwa tume. Isitoshe tume inaweza kufanya masahihisho kurekebisha yale makosa yaliyotokea vituoni. Hicho kitu kiko all over the world, si TZ tu. Hii ni tatizo la miundo mbinu. Kama kuna wizi vituoni, hilo ni suala lingine litatokana na uzembe wa vyama vya siasa kubweteka na ni funzo kwa 2015.
Ninapokuambia maelezo yako ni upupu nina maana kuanza kuchachamaa sasa hivi ati matokeo yamechakachuliwa na ili hali ulijua uwezekano huo hata kabla ya uchaguzi ni upuuzi mkubwa sana.
Sijajua wewe uchungu wako ni upi? Kwamba ulikuwa ni lazima upate unachokitegemea na hukubali kilichopo au ni mkereketwa kama mashabiki wa mpira wa simba na yanga ambao siku zote wanajua team zao zinatakiwa zishinde na zikishindwa anafukuzwa mwenyekiti?! Na ushindwe ulegee mpaka ufe.
 
watanzania wote wenye akili timamu wasio wanafiki, wazalendo na wacha Mungu, hawamtaki Jk, achana na kumtambua. Mungu si mchakachuaji, si mwongo, si mnafiki, ana kila sifa njema....
 
Kipenzi chako? ni padri huyo soma thread ya habari mchanganyiko kuwahusu watu hao, na Tz wameanza
 
By FLORENCE MUGARULA, Daily Nation
Monday, November 15 2010


In Summary: Chadema says it will not recognise the president elected at what it says were fraudulent elections

Chama Cha Demokrasia Na Maendeleo on Monday announced that it would not to recognise President Jakaya Kikwete as a President because of several weaknesses that were recorded during the past general election.

The former Chadema Presidential candidate, Dr Wilbrod Slaa told the Press that President Kikwete was the product of fabricated election results, which Chadema does not recognise.


Dr Slaa added that the Presidential results were not allowed to be questioned anywhere after being released by the National Electoral Commission and that his party has no grounds to say anything in the line of the law.


“I said this before NEC announced the results and we wrote to them trying to explain our complaints but they did not even respond, therefore the only way was to reject the results and not to recognise the President,” said Dr Slaa.


According to Dr Slaa, Chadema has decided not to recognise President Kikwete because the results were fabricated and thus there was no reason to accept him as a President.


The former Karatu MP added that it was difficult to accept election results which were recorded without adhering to the principles of democracy.


Another reason behind rejecting the results and not recognising President Kikwete is that the general election was not free and fair.


“The whole election process was not conducted under conducive environments, we have been warning NEC on this matter but no important measures have been taken on the matter,” said Dr Slaa.


According to Dr Slaa, the matter has been officially handed over to the party (Chadema) so that important measures can be taken for future betterment of wananchi.


“I am using this opportunity to tell all Tanzanians that I was not satisfied by the results and therefore I do not recognize Mr Jakaya Kikwete as a President, I want Tanzanians to understand this,” said Dr Slaa.


But, when reached for the comments, the Attorney General, Judge Fredrick Werema said the new election Act demands that all complaints be filed in court.


“I think the law is open on all complaints about election issues, everything is supposed to be filed in court,” said the AG.


On the Chadema’s stand over President Kikwete’s win, Judge Werema said Chadema’s decision was ‘nonsense’. (Ni mawazo na msimamo wa kijinga na kipumbavu kutomkubali Rais)


Commenting to the matter, the Chadema national chairman, Mr Freeman Mbowe said the party will pressurise for the independence committee to probe the violation of elections principles all over the country.


Source: Daily Nation
 
I concur when the electoral process is rigged recognizing those results is to condone impunity. But I still insist that going to Court is an option that should be deployed. Let the Court come clean on this and not to be thwarted by constitutional provisions that purport to take away that right. The Court of Appeal was clear on this in the case of Kaborou.
 
I concur when the electoral process is rigged recognizing those results is to condone impunity. But I still insist that going to Court is an option that should be deployed. Let the Court come clean on this and not to be thwarted by constitutional provisions that purport to take away that right. The Court of Appeal was clear on this in the case of Kaborou.

What are the constitutional limitations on exercising this legal option with regard to presidential elections?
 
I concur when the electoral process is rigged recognizing those results is to condone impunity. But I still insist that going to Court is an option that should be deployed. Let the Court come clean on this and not to be thwarted by constitutional provisions that purport to take away that right. The Court of Appeal was clear on this in the case of Kaborou.

I'm scared of getting into the war again with you on the issue of The Court of Appeal. Why don't you discuss with your fellow lawyers as to the meaning of the Constitution on this matter and on the fact that even CHADEMA interpret it that the Constitution does not allow any proceedings/inquiries on the Presidential results announced by NEC.
 
What are the constitutional limitations on exercising this legal option with regard to presidential elections?

There is a clear line in the Constitution (74(12)) which forbids any legal actions on this. I quote the constitution:

74(12) "Hakuna mahakama yoyote itakayokuwa na mamlaka ya
kuchunguza jambo lolote lililotendwa na Tume ya Uchaguzi katika
kutekeleza madaraka yake kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii.
(13) Katika utekelezaji wa madaraka yake kwa mujibu wa katiba hii"
 
“I think the law is open on all complaints about election issues, everything is supposed to be filed in court,” said the AG.

On the Chadema’s stand over President Kikwete’s win, Judge Werema said Chadema’s decision was ‘nonsense’. (Ni mawazo na msimamo wa kijinga na kipumbavu kutomkubali Rais)

Huyu ni AG kweli ?
 
• Ataka tume huru iundwe kuchunguza wizi wa kura

na Salehe Mohamed, Dodoma


HATIMAYE Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimetoa tamko zito la kutomtambua Rais Jakaya Kikwete, kwa madai kuwa ameingia madarakani kwa wizi wa kura (uchakachuaji).

Msimamo huo ulitangazwa jana mkoani hapa na viongozi wa chama hicho wakiongozwa na Mwenyekiti wao, Freeman Mbowe na Katibu Mkuu Dk. Willibrod Slaa, ambapo walisema utakuwa ni unafiki kumhalalisha kiongozi aliyeingia madarakani kwa uchakachuaji wa kura.

Akizungumza na waandishi wa habari, Dk. Slaa, ambaye alikuwa mgombea urais wa CHADEMA, alisema wakati wa utangazaji wa matokeo, CHADEMA waliiandikia barua Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuwataka kusitisha zoezi hilo, kwa sababu lilikuwa na kasoro nyingi, ikiwamo ya wizi wa kura, lakini NEC haikuwasikiliza.

Alibainisha kuwa NEC ilifanya kazi kwa uzembe na usiri na ilishiriki kuiba kura zake na kubadilisha matokeo kwa lengo la kumsaidia mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kikwete kupata ushindi mwembamba wa asilimia 61.

Alisema wananchi wamekoseshwa fursa ya kuongozwa na kiongozi waliyemtaka, kwa sababu Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 31, mwaka huu haukuwa huru na wa haki, hivyo hawaoni sababu ya kumtambua kiongozi aliyetokana na matokeo ya uchakachuaji.

“Nawashukuru Watanzania kwa kunipa kura zile zilizotangazwa na NEC, lakini leo napenda kuutangazia umma kuwa simtambui Rais Jakaya Kikwete kwa sababu kura zilizompa ushindi zilipatikana kwa msaada wa wizi na si matakwa ya wananchi,” alisema.

Dk. Slaa ambaye hii ni mara yake ya kwanza kuzungumza na vyombo vya habari tangu kutangazwa kwa matokeo ya urais, alisema lengo la demokrasia ni kupatikana kwa kiongozi aliyetokana na matakwa ya wananchi, lakini NEC na vyombo vya usalama viliamua kumpendelea mgombea wa CCM, Jakaya Kikwete.

Alibainisha kuwa wamefikia hatua ya kutomtambua Rais Kikwete, kwa sababu utaratibu uliopo hivi sasa wa kisheria na kikatiba, hautoi nafasi kupinga matokeo ya uchaguzi katika mahakama au chombo kingine kinachoundwa kikatiba.

Alisema NEC inalindwa kisheria na hata kama inachakachua matokeo ya uchaguzi kwa makusudi kwa lengo la kumnufaisha Rais Kikwete na chama chake.

Alibainisha kuwa katika mazingira hayo ya kisheria na kikatiba, njia pekee waliyonayo kuonyesha kutoridhika na ukiukwaji wa makusudi wa nguzo kuu za uchaguzi huru na wa haki, ni kuheshimu dhamiri zao kwa kutoyatambua matokeo ya uchaguzi wa rais yaliyotangazwa na NEC hivi karibuni.

Aidha, alisema Usalama wa Taifa ni mafisadi wa kutumia rasilimali za taifa kwa kusaidia wizi wa kura kwenye Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 31, mwaka huu.

Alisema anao ushahidi wa kutosha kuwa Usalama wa Taifa walifanya kazi hiyo ili kumnufaisha mgombea wa CCM, Kikwete ambaye alitangazwa mshindi katika nafasi ya urais kwa kupata kura milioni tano.

Dk. Slaa alisema matokeo ya uchaguzi yalibadilishwa kwa lengo la kumbeba Kikwete na kuongeza kuwa ushahidi huo hawezi kuupeleka Usalama wa Taifa kama alivyotakiwa na Kaimu Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa, Jacky Zoka, bali ataupeleka mahakamani kama akifunguliwa kesi ya kuikashifu idara hiyo nyeti.

Alibainisha kuwa hawezi kuupeleka ushahidi huo kwa chombo hicho kwa sababu chenyewe ndicho kilichoshiriki kufifisha demokrasia kwa kuchakachua matokeo ya urais, ili Kikwete aibuke na ushindi dhidi ya yeye (Slaa).

“Wanataka niwapelekee ushahidi, nifanye hivyo kwa nini wakati wao ndio ninao watuhumu? Wasijidanganye kuwa nitafanya wanachokitaka, kama wanaona wao si mafisadi, wakanishitaki mahakamani, huko ndiko nitawaonyesha,” alisema.

Alibainisha kuwa kitendo cha Usalama wa Taifa kuwasambaza vijana wao mikoani kwa lengo la kuisaidia CCM na mgombea wake ni kosa la jinai, kwa sababu wao wamepewa jukumu la kuangalia usalama wa raia wote na wala si kutetea masilahi ya chama fulani.

Aliongeza kuwa CHADEMA haimuogopi yeyote, hivyo Usalama wa Taifa wasijidanganye kuwa wanao uwezo wa kuwatisha, ili wasiibue vitendo viovu vinavyofanywa na taasisi za umma kwa lengo la kulinda masilahi ya watu fulani.

Alisema CHADEMA walishawahi kutangaza orodha ya mafisadi ambayo ilikuwa na vigogo kadhaa wa CCM na serikali, akiwamo Rais Kikwete, hivyo hawawezi kuogopa kuwataja watendaji wa Usalama wa Taifa walioshiriki kwenye vitendo vya wizi wa kura.

Alisema katika wizi wa EPA, walizitaja baadhi ya kampuni zinazomilikiwa na watendaji wa Usalama wa Taifa ambao walitishia kwenda mahakamani lakini hadi sasa hawajakwenda.

Hivi karibuni Dk. Slaa, alitoa malalamiko kuwa Usalama wa Taifa walishiriki kuiba kura ili kumsaidia Rais Kikwete, lakini madai hayo yalipingwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa, Jack Zoka.

Naye Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, alisema msimamo wao hauwezi kubadilisha matokeo hayo wala kumzuia aliyetangazwa na kuapishwa kuwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kufanya kazi zake lakini hawapo tayari kuhalalisha matokeo yaliyotokana na ukiukwaji wa makusudi wa katiba, sheria za uchaguzi na kanuni za uchaguzi huru na wa haki.

Alisema hivi sasa CHADEMA inataka iundwe tume ya uchunguzi wa mchakato mzima wa uchaguzi pamoja na kutaka kuwapo kwa katiba mpya na tume huru ya uchaguzi, ambayo haitapendelea chama chochote cha siasa.

Aliongeza kuwa watapeleka hoja bungeni kutaka mabadiliko ya katiba na wanaamini hoja hiyo itapata uungwaji mkono na wabunge wa chama tawala na wale wa upinzani, kwa sababu haitakuwa ikisimamia masilahi ya chama bali inalenga kustawisha maendeleo ya nchi.

“Hatudai mambo haya kwa nguvu, vurugu na fujo, kwani tukifanya hivyo tutakuwa tunaathiri amani na utulivu tulionao, sisi ni wadumisha amani, tutalitumia Bunge na majukwaa mbalimbali kudai tume huru ya uchaguzi pamoja na katiba mpya,” alisema.

Alisema pamoja na kutomtambua Rais Kikwete, wabunge, madiwani na watendaji kwenye halmashauri mbalimbali hapa nchini, hawataacha kazi zao, bali wataendeleza utumishi wa umma ndani ya vyombo husika huku wakitanguliza mbele masilahi ya taifa, ikiwamo kupambana na ufisadi.

Alisema hata kama wabunge wake watateuliwa na rais, CHADEMA haitakuwa tayari kuingia serikalini, kwani yenyewe inajiandaa kuongoza serikali ijayo.

Mbowe alitumia fursa hiyo kuwataka Watanzania na waandishi wa habari kutolazimisha ndoa ya wapinzani na wanasiasa, bali walazimishe fikra zinazokubaliana kushirikiana.

Alisema vipo vyama vya upinzani ambavyo vimekuwa vikivaa ngozi ya kondoo wakati vyenyewe ni chui ambao hawapendi kuona maendeleo ya CHADEMA.

“Sisi tupo tayari kushirikiana na chama chochote makini, nasisitiza makini kwa sababu kuna vingine ni wakala wa CCM. Leo hii kuna vyama vya siasa vimetupeleka mahakamani vikitaka tuvilipe fidia na wabunge wetu wavuliwe nyadhifa zao, sasa unataka tushirikiane navyo?” alihoji.
Alisema CHADEMA iliwasiliana na Chama cha Wananchi (CUF) kuhusu kuunganisha nguvu na kuunda kambi ya upinzani lakini kwa bahati mbaya walipewa jibu kuwa chenyewe kimejiunga na vingine kuanzisha kambi ndogo.
 
There is a clear line in the Constitution (74(12)) which forbids any legal actions on this. I quote the constitution:

74(12) "Hakuna mahakama yoyote itakayokuwa na mamlaka ya
kuchunguza jambo lolote lililotendwa na Tume ya Uchaguzi katika
kutekeleza madaraka yake kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii.
(13) Katika utekelezaji wa madaraka yake kwa mujibu wa katiba hii"

Ebu nielimishe zaidi. Kifungu hicho hapo juu hakisemi ni uchaguzi upi, wa raisi au wa wabunge. Inaoenekana unaweza kwenda mahakamani ku challenge uchaguzi wa wabunge ingawa sijui ni wapi katiba inasema specifically kuhusu wabunge. Swali langu kuhusu uchaguzi wa raisi ni hili:

Is there a constitutional provision that explicitly states that the results of a presidential election - as opposed to parliamentary elections - are final, and can not be challenged in court, after they are announced by the electoral commission?
 
Wanashindwa kwenda mahakamani kwa kuwa hawana ushahidi wakutosha zaidi ya maneno ya uchakachuaji tu... Nimechukizwa sana na mwenendo huu wa viongozi wetu.. Eti leo walikuwa na tafrija ya kurekea ushindi! Ushindi upi huo? Au ni huu wa viti 24 vya wa bunge?
Hii issue ni sensitive kwa hiyo ni bora Chadema wakachukua muda na kukusanya evidence na facts zote kuliko wakakurupuka na kuonekana hamnazo kama hao wanao wapigia kelele.

**Mtu akifanya vizuri lazima umpongeze.
 
Back
Top Bottom