Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
CHADEMA yatoa masharti mgogoro wa mameya
Na Reuben Kagaruki
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimetoa masharti ya kumaliza mgogoro ya uchaguzi wa mameya katika maeneo yote yenye utata vinginevyo kitaitisha maandamano ya amani nchi nzima ifikapo Januari 5, mwaka huu.Katika
masharti hayo, kimependekeza uitishwe mkutano wa majadiliano baina yake na viongozi wa juu wa serikali, ikiwezekana ahusike Waziri Mkuu, Bw. Mizengo Pinda, viongozi wa TAMISEMI na kusitishwa kwa chaguzi za wenyeviti na mameya katika maeneo yenye utata.
Maeneo yenye utata yametajwa kuwa ni pamoja na Mwanza, Arusha, Hai, Kigoma Ujiji, ambako chama ghicho kimedai uchaguizi umevurugwa katika mazingira yanayoashiria kuwapo maelekezo kutoka ngazi za juu.
Barua ya Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Willibrod Slaa kwenda kwa Msajili wa Vyama vya Siasa, Bw. John Tendwa ya Desemba 22, mwaka huu ilieleza kwamba, iwapo madai hayo hayatatekelezwa hadi Januari 4, 20211 chama kitaitisha maandamano siku inayofuata bila kujali yana kibali cha polisi au la.
Masharti ya chama hicho ni pamoja na kutaka usifanyike uchaguzi wowote wa mameya au wenyeviti wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza, Manispaa ya Kigoma/Ujiji, Manispaa ya Arusha na Hai.
"Kama unavyojua, uchaguzi wa wenyeviti na mameya hao umevurugika kwa sababu ambazo zina utata na kwa vyovyote vile kuonesha dalili ya kuwa na maelekezo kutoka ngazi za juu, jambo ambalo limeleta utata mkubwa ikiwa ni pamoja na uvunjifu wa amani," ilieleza sehemu ya taarifa hiyo na kuongeza;
"CHADEMA tumejitaidi kutuliza wapenzi wetu hata baada ya wananchi kupigwa mabomu na polisi bila sababu," alisema Dkt. Slaa
Chama hicho kimesema polisi ni watuhumiwa katika matukio ya Arusha, hivyo kama hakutakuwa na maridhiano serikali itakuwa imewalazimisha kuchukua hatua ya kuandamana.
Pia kimetaka masharti yote yaliyotolewa Arusha yaendelee, yaani Mkurugenzi wa Manispaa ajiuzulu kwa ukiukwaji wa kanuni za halmashauri na kusimamia uchaguzi kinyume na taratibu, uongozi wa TAMISEMI uliingilia uchaguzi hasa Kigoma/Ujiji, hivyo wahusika wote wachukuliwe hatua.
Chama hicho kimeitaka serikali kumchukulia hatua OCD wa Arusha kwa kuingia na kumkamata mbunge ndani ya kikao halali kinyume na kanuni za uendeshaji wa halmashauri. Kwa mujibu wa barua hiyo, chama hicho kinamtaka OCD huyo ajiuzulu au aondolewe.
"CHADEMA sasa tumefikia mahali tumechoka na unyanyasaji, serikali ijue hivyo. Ni imani yetu kama serikali inataka haki itendeke, hatua stahiki ziwe zimechukuliwa kwa wahusika kabla ya terehe 4 januari, 2011," ilieleza barua hiyo.
Katika barua yake Dkt. Slaa alieleza kuwa chama chake kinaheshimu mazungumzo yake na Bw. Tendwa na yale ya Mwenyekiti wa CHADEMA, Bw. Freeman Mbowe na Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP, Bw. Said Mwema.
"Kama tulivyokubaliana kati ya Dkt. Slaa na Bw. Tendwa, Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa itaratibu mkutano huo na kuwajulisha wahusika juu ya malalamiko ya CHADEMA," ilieleza barua hiyo.
Alisema chama hicho kitaitisha mkutano wa waandishi wa habari kuomba wananchi wa Arusha watulie hadi watakapojulishwa hatua zaidi, iwapo serikali haitakuwa imechukua hatua.
Na Reuben Kagaruki
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimetoa masharti ya kumaliza mgogoro ya uchaguzi wa mameya katika maeneo yote yenye utata vinginevyo kitaitisha maandamano ya amani nchi nzima ifikapo Januari 5, mwaka huu.Katika
masharti hayo, kimependekeza uitishwe mkutano wa majadiliano baina yake na viongozi wa juu wa serikali, ikiwezekana ahusike Waziri Mkuu, Bw. Mizengo Pinda, viongozi wa TAMISEMI na kusitishwa kwa chaguzi za wenyeviti na mameya katika maeneo yenye utata.
Maeneo yenye utata yametajwa kuwa ni pamoja na Mwanza, Arusha, Hai, Kigoma Ujiji, ambako chama ghicho kimedai uchaguizi umevurugwa katika mazingira yanayoashiria kuwapo maelekezo kutoka ngazi za juu.
Barua ya Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Willibrod Slaa kwenda kwa Msajili wa Vyama vya Siasa, Bw. John Tendwa ya Desemba 22, mwaka huu ilieleza kwamba, iwapo madai hayo hayatatekelezwa hadi Januari 4, 20211 chama kitaitisha maandamano siku inayofuata bila kujali yana kibali cha polisi au la.
Masharti ya chama hicho ni pamoja na kutaka usifanyike uchaguzi wowote wa mameya au wenyeviti wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza, Manispaa ya Kigoma/Ujiji, Manispaa ya Arusha na Hai.
"Kama unavyojua, uchaguzi wa wenyeviti na mameya hao umevurugika kwa sababu ambazo zina utata na kwa vyovyote vile kuonesha dalili ya kuwa na maelekezo kutoka ngazi za juu, jambo ambalo limeleta utata mkubwa ikiwa ni pamoja na uvunjifu wa amani," ilieleza sehemu ya taarifa hiyo na kuongeza;
"CHADEMA tumejitaidi kutuliza wapenzi wetu hata baada ya wananchi kupigwa mabomu na polisi bila sababu," alisema Dkt. Slaa
Chama hicho kimesema polisi ni watuhumiwa katika matukio ya Arusha, hivyo kama hakutakuwa na maridhiano serikali itakuwa imewalazimisha kuchukua hatua ya kuandamana.
Pia kimetaka masharti yote yaliyotolewa Arusha yaendelee, yaani Mkurugenzi wa Manispaa ajiuzulu kwa ukiukwaji wa kanuni za halmashauri na kusimamia uchaguzi kinyume na taratibu, uongozi wa TAMISEMI uliingilia uchaguzi hasa Kigoma/Ujiji, hivyo wahusika wote wachukuliwe hatua.
Chama hicho kimeitaka serikali kumchukulia hatua OCD wa Arusha kwa kuingia na kumkamata mbunge ndani ya kikao halali kinyume na kanuni za uendeshaji wa halmashauri. Kwa mujibu wa barua hiyo, chama hicho kinamtaka OCD huyo ajiuzulu au aondolewe.
"CHADEMA sasa tumefikia mahali tumechoka na unyanyasaji, serikali ijue hivyo. Ni imani yetu kama serikali inataka haki itendeke, hatua stahiki ziwe zimechukuliwa kwa wahusika kabla ya terehe 4 januari, 2011," ilieleza barua hiyo.
Katika barua yake Dkt. Slaa alieleza kuwa chama chake kinaheshimu mazungumzo yake na Bw. Tendwa na yale ya Mwenyekiti wa CHADEMA, Bw. Freeman Mbowe na Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP, Bw. Said Mwema.
"Kama tulivyokubaliana kati ya Dkt. Slaa na Bw. Tendwa, Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa itaratibu mkutano huo na kuwajulisha wahusika juu ya malalamiko ya CHADEMA," ilieleza barua hiyo.
Alisema chama hicho kitaitisha mkutano wa waandishi wa habari kuomba wananchi wa Arusha watulie hadi watakapojulishwa hatua zaidi, iwapo serikali haitakuwa imechukua hatua.