CHADEMA yataka Tanganyika irudishwe

Serayamajimbo

Senior Member
Apr 15, 2009
191
38
na Edward Kinabo


amka2.gif

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimeitaka serikali kuitikia wito wa kufanya mabadiliko makubwa ya mfumo wa utawala, ikiwa ni pamoja na kuufanyia marekebisho muundo wa sasa wa muungano ili kuirudisha nchi ya Tanganyika iliyopata uhuru wake mwaka 1961.
Hayo yalisemwa jana na Mwenyekiti wa CHADEMA wa Mkoa wa Kinondoni, John Mnyika, wakati akitoa hotuba ya ufunguzi wa kongamano la vijana wa chama hicho, lililoandaliwa mahususi kutathmini miaka 48 ya uhuru wa Tanganyika.

Nashangaa tunaposherehekea uhuru wa nchi ambayo haipo. Kimsingi uhuru tunaousherehekea wa miaka 48 ni uhuru wa nchi iitwayo Tanganyika, kwani ndiyo iliyopata uhuru mwaka 1961.
Lakini Tanganyika kikatiba haipo, nchi zilizopo ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Zanzibar. Zanzibar ipo lakini Tanganyika iliyoungana nayo haipo, tunasisitiza tena wito wetu wa kuitaka serikali kufanya mabadiliko makubwa ya mfumo wa utawala, ikiwa ni pamoja na kuufanyia marekebisho muundo wa muungano utakaoirejesha Tanganyika. alisema Mnyika.

Alisema wakati Tanganyika ikiadhimisha miaka 48 ya uhuru wake, bado haijafanikiwa kupambana na maadui wanne; ambao ni ujinga, umaskini, maradhi na rushwa.

Ujinga bado upo, serikali inajenga sekondari za kata zisizokuwa na walimu wala vifaa vya kutosha kuondoa ujinga. Maradhi yapo, leo hapa Wilaya ya Kinondoni tu tunakabiliwa na kipindupindu na mama wajawazito wanaendelea kupoteza maisha yao pale Hospitali ya Mwananyamala.

Umaskini upo, kwa mfano wakati wa Mwalimu, pato la Mtanzania lilikuwa dola mbili kwa siku (takriban sh 2,000 kwa siku), leo pato la Mtanzania ni chini ya dola moja kwa siku (chini ya sh 1,000 kwa siku). Rushwa ya kawaida iliyokuwapo wakati wa Mwalimu, sasa imeota mizizi na kuwa ufisadi unaotamalaki ndani ya mfumo mzima wa uongozi, alisema Mnyika.

Alisema wakati Tanganyika ikiadhimisha miaka 48 ya uhuru wake, hali halisi inaonyesha kuwa taifa hilo ambalo halipo kikatiba, linakabiliwa na changamoto mbalimbali, ikiwa ni pamoja na tishio la kuvunjika kwa amani na umoja uliojengwa na waasisi wake.

Waasisi walijenga amani na umoja. Leo mijadala ya kidini imekithiri na inazidi kufufua hisia za ubaguzi wa kidini kati ya waumini wa dini moja na nyingine. Leo pengo la kiuchumi kati ya matajiri na maskini linazidi. Migogoro ya kirasilimali nayo inazidi.

Tumeshuhudia mapigano kati ya wakulima na wafugaji kugombania rasilimali ya ardhi. Tumeshuhudia Watanzania wakiondolewa bila taratibu katika ardhi yao kupisha wawekezaji, mfano kule Loliondo na kwenye maeneo yenye madini. Chaguzi zetu pia zimekuwa za hatari, tumeona ya Zanzibar na tumesikia na kushuhudia umwagaji damu katika chaguzi ndogo za ubunge kwenye majimbo ya Tarime, Kiteto, Busanda na Biharamulo. Haya yote ni tishio kwa amani na umoja wa taifa letu, alisema Mnyika.

Alitoa wito kwa Rais Kikwete kukubali kufanya maamuzi magumu ya kulinusuru taifa kama ilivyopendekezwa katika maazimio ya kongamano la Mwalimu Nyerere na yale yaliyotolewa katika kikao cha Kamati Kuu ya CHADEMA kilichomalizika hivi karibuni. Katika kongamano hilo, Mnyika alizindua tuzo kwa vijana ya uhuru wa kweli ya Freeman Mbowe Freeman Mbowe Youth Real Freedom Award, itakayokuwa inatolewa kila ifikapo Desemba 9 ya kila mwaka, kwa vijana wa umri wa miaka 18 hadi 35, watakaokuwa wanashinda mashindano ya uandishi wa hotuba kuhusu uhuru wa Tanganyika, yatakayokuwa yanaandaliwa na uongozi wa CHADEMA Mkoa wa Kinondoni.
 
Mwisho wataomba na mangi wao arudishwe... wamefulia hao na kugombana kama wake wenza!!!
 
Hii ni sera ya CUF kuwepo kwa serikali tatu tangu mwanzo..kama chadema wanafikiri the same...then hakuna sababu ya kutoungana
 
..idea ya kurudisha serikali ya Tanganyika bila kuuvunja muungano sikubaliano nayo.

..ningependelea CUF na CHADEMA waende hatua moja mbele kwa kupendekeza MUUNGANO UVUNJWE.
 
..idea ya kurudisha serikali ya Tanganyika bila kuuvunja muungano sikubaliano nayo.

..ningependelea CUF na CHADEMA waende hatua moja mbele kwa kupendekeza MUUNGANO UVUNJWE.
Muungano uvunjwe? mzima kweli wewe?

Kuna matatizo kwenye muungano lakini kama vile nimeshazoea kuishi Tanzania

Nafikiri wanatakiwa waende mbele zaidi kuwe na serikali moja yenye nguvu na heshima..vunja mabunge mengi yasiyo na maana na kufaidi synergies mbalimbali za ku-merge
 
Kwa nini Zanzibar bado ipo hata baada ya muungano na Tanganyika haipo, Je kungekuwa na serikali tatu(serikali ya Tanganyika, Serikari ya Zanzibar na Serikali ya Muungano) toka enzi ya muungano ingekuwaje, Julius angechagua kuwa rais wa Tanganyika au rais wa Muungano, kuna mchezo mkali sana hapa..sugueni vichwa mtanielewa tuu.
 
Muungano uvunjwe? mzima kweli wewe?

Kuna matatizo kwenye muungano lakini kama vile nimeshazoea kuishi Tanzania

Nafikiri wanatakiwa waende mbele zaidi kuwe na serikali moja yenye nguvu na heshima..vunja mabunge mengi yasiyo na maana na kufaidi synergies mbalimbali za ku-merge
Tumain,
Kwa muungano tupo pamoja kabisa.
 
Tumain said:
Muungano uvunjwe? mzima kweli wewe?

Kuna matatizo kwenye muungano lakini kama vile nimeshazoea kuishi Tanzania

Nafikiri wanatakiwa waende mbele zaidi kuwe na serikali moja yenye nguvu na heshima..vunja mabunge mengi yasiyo na maana na kufaidi synergies mbalimbali za ku-merge.

Tumain,

..I am serious kwamba Muungano uvunjwe.

..Wazanzibari hawataki kuacha utaifa wao na kujiunga na wenzao wa Tanganyika kuunda nchi moja, yenye serikali moja, Tanzania.

..bado kutakuwa na uwezekano kwa Watanganyika na Wazanzibari kushirikiana kwa namna mbalimbali kama majirani. kwa msingi huo you wont miss that much "Utanzania" wako.
 
Muungano uvunjwe? mzima kweli wewe?

Kuna matatizo kwenye muungano lakini kama vile nimeshazoea kuishi Tanzania

Nafikiri wanatakiwa waende mbele zaidi kuwe na serikali moja yenye nguvu na heshima..vunja mabunge mengi yasiyo na maana na kufaidi synergies mbalimbali za ku-merge
Sometimes you speak points
 
Tumain,

..I am serious kwamba Muungano uvunjwe.

..Wazanzibari hawataki kuacha utaifa wao na kujiunga na wenzao wa Tanganyika kuunda nchi moja, yenye serikali moja, Tanzania.

..bado kutakuwa na uwezekano kwa Watanganyika na Wazanzibari kushirikiana kwa namna mbalimbali kama majirani. kwa msingi huo you wont miss that much "Utanzania" wako.
jokaKuu,
Mwungano uvunjwe ili iweje? Una hakika gani kuwa ukivunjwa Tumain hatamiss Utanzania wake? Kwanza mkiuvunja kutakuwepo uhasama na sidhani utakubali kumwona Tumain akiwa na Utanzania. Mtawaambia rudini kwenu Zanzibar na hamtaishia hapo. Mtawafukuza Wapemba na dhambi hiyo ikianza kuwatafuna hamtaishia hapo. Baadaye mtaanza kujiangalia ni nani Mtanganyika halisi na sisi ambao tunaunga mwungano mtatujengea zengwe.
 
Jasusi,

..Wazanzibari hawautaki huu Muungano. they simply do not want to be identified as Tanzanians. sasa ya nini kuwalazimisha?

..Watanganyika kule vijijini hawana habari nao kabisaaa.

..vurugu zitatokea kama tutaendelea kungangania huu Muungano mpaka Wazenj watakapoamua kufanya vurugu na maasi. sasa kabla hawajafika huko bora tuwarudishie mamlaka kamili ya nchi yao.

..kuna taratibu zinazopaswa kufanyika ktk kuvunja muungano huu. tunaweza kutafuta msaada na ushauri on how to proceed.

..tunapaswa kuzingatia hayo hapo juu ili kuondoa uwezekano wa kutoa vurugu na uhasama unaouzungumzia.
 
jokaKuu,
Mwungano uvunjwe ili iweje? Una hakika gani kuwa ukivunjwa Tumain hatamiss Utanzania wake? Kwanza mkiuvunja kutakuwepo uhasama na sidhani utakubali kumwona Tumain akiwa na Utanzania. Mtawaambia rudini kwenu Zanzibar na hamtaishia hapo. Mtawafukuza Wapemba na dhambi hiyo ikianza kuwatafuna hamtaishia hapo. Baadaye mtaanza kujiangalia ni nani Mtanganyika halisi na sisi ambao tunaunga mwungano mtatujengea zengwe.

Mkuu. Inategemea itakavyofanyika. Tuige kutoka kwa former Czechoslovakia na si Yugoslavia! Mimi naamini kuna haja ya kufanya referendum ya kweli na wazi kuhusu huu Muungano na kama wengi katika kila upande wakitaka uendelee, uendelee. Moja ya upande ukikataa uendelee, basi tupeana talaka na kila mmoja achukue zake hamsini. Tunahitaji legitimacy ili hao ambao kila siku wanawabeza watanganyika kuwa wanalazimisha muungano wasiwe na la kufanya. Hatuwezi kuendelea hivi tulivyo.

BTW, mimi nilidhani mambo yatakuwa vice versa? Wazanzibari hawafichi kuwa hawataki watanganyika nchini kwao wakati sijasikia mtanganyika akisema kuwa wafunge virago. nadhani kitakachotokea ni wale wenye asili ya bara walio Zanzibar watafukuzwa na wale wazanzibari walio bara watapewa chaguo la uraia. Wakitaka utanganyika watakubalika na wasipotaka basi aidha wabaki kwa residency permit au waondoke waende kwengine wanakotaka ( si lazima Zanzibar)!

Amandla.........
 
Nafikiri Huku ni kumfukua Mwalim Nyerere...!!!

Chadema nafikiri huu mtizamo wenu juu ya Muungano usiwe wa kificho uwe wa Wazi. Isije akatokea Kiongozi Mwingine akasema ule ulikuwa msimamo wa Mnyika na si Chadema.

Wakati Wenzetu wa Europe wanafikiria kuungana ili kuwa na Power kama US, sisi twafikiria tofauti. Sie tumeungana lkn bado twafikiria Kunyonyana.
 
CHADEMA oyee....mie kama mzenji sitaki muungano kabisa, kama kulazimishwa basi ziwe hizo tatu...but I prefer the first one!!!

Sitaki mapaspoti ya kijani kibichi!!!:rolleyes:
 
CHADEMA oyee....mie kama mzenji sitaki muungano kabisa, kama kulazimishwa basi ziwe hizo tatu...but I prefer the first one!!!

Sitaki mapaspoti ya kijani kibichi!!!:rolleyes:
Wengi bado wanahitaji Muungano... tena kwa nia ya kuwa na muungano bora zaidi kuliko huu!
 
Kwa nini Zanzibar bado ipo hata baada ya muungano na Tanganyika haipo, Je kungekuwa na serikali tatu(serikali ya Tanganyika, Serikari ya Zanzibar na Serikali ya Muungano) toka enzi ya muungano ingekuwaje, Julius angechagua kuwa rais wa Tanganyika au rais wa Muungano, kuna mchezo mkali sana hapa..sugueni vichwa mtanielewa tuu.
Katika kusugua vichwa, haya ni miongoni mwa maswali ya kujiuliza;
Serikali ni nini?
Tanganyika ni nini?
 
Back
Top Bottom