nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
na Ahmed Makongo, Kahama
WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige, ameonekana kutikiswa na maandamano yaliyofanywa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mkoani Shinyanga hivi karibuni, baada ya kuamua kukimbilia jimboni kwake kuzima moto uliowashwa na chama hicho.
Juzi na jana, Waziri Maige alilazimika kufanya mikutano katika vijiji mbalimbali vya Jimbo la Msalala analoliongoza.
Katika mikutano hiyo, Maige alitumia nafasi hiyo kuwabeza CHADEMA akisema maandamano na mikutano yao haina tija yoyote, bali ni kuzorotesha shughuli za maendeleo ya wananchi.
Wananchi wengi ambao sasa wanakabiliwa na ugumu wa maisha ikiwa ni pamoja na kupanda kwa bei za bidhaa mbalimbali waliambiwa na Maige kuwa huu ni wakati wa kutekeleza wajibu wao wa kujiletea maendeleo kuliko kutumia maandamamo ya chama hicho ambayo yana nia ya kuwapotosha.
Maige alikwenda mbali zaidi akiwataka wananchi waache kudai haki zao kwa kutumia maandamano hayo, kwa sababu wanatumia muda mwingi wa uzalishaji mali kwenye mambo yasiyo na tija.
"Uchaguzi ulisha kwisha, sasa maandamano ya nini….watu wanaacha shughuli za kuzalisha mali na maendeleo kwa ujumla wanakwenda kwenye maandamano ambayo hayana tija yoyote, wananchi tusikubali kudanganywa," alisema.
Aidha, Waziri Maige aliwataka wananchi kuelekeza nguvu zao katika kutekeleza majukumu yao ya kifamilia, sanjari na kutekeleza miradi ya maendeleo hususani katika sekta za elimu na afya. Sekta ambazo zote zimekuwa zikilaumiwa kutokana na kuwa na matatizo mbalimbali yasiyokidhi haja za wananchi. Maige ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Msalala, hata hivyo alishindwa kutetea hoja yake ya kuwataka wananchi wasiandamane kutokana na ugumu wa maisha badala yake akijikuta akitambua bayana juu ya changamoto zinazolikabili jimbo hilo katika kujiletea maendeleo. Wakati huo huo alichangia mifuko ya saruji zaidi ya 4,000 kwa ajili ya ujenzi wa zahanati, ambapo kila kijiji alikipatia jumla ya mifuko 20, na kuwataka wananchi kuwa mstari wa mbele katika ujenzi wa zahanati katika vijiji vyao.
WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige, ameonekana kutikiswa na maandamano yaliyofanywa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mkoani Shinyanga hivi karibuni, baada ya kuamua kukimbilia jimboni kwake kuzima moto uliowashwa na chama hicho.
Juzi na jana, Waziri Maige alilazimika kufanya mikutano katika vijiji mbalimbali vya Jimbo la Msalala analoliongoza.
Katika mikutano hiyo, Maige alitumia nafasi hiyo kuwabeza CHADEMA akisema maandamano na mikutano yao haina tija yoyote, bali ni kuzorotesha shughuli za maendeleo ya wananchi.
Wananchi wengi ambao sasa wanakabiliwa na ugumu wa maisha ikiwa ni pamoja na kupanda kwa bei za bidhaa mbalimbali waliambiwa na Maige kuwa huu ni wakati wa kutekeleza wajibu wao wa kujiletea maendeleo kuliko kutumia maandamamo ya chama hicho ambayo yana nia ya kuwapotosha.
Maige alikwenda mbali zaidi akiwataka wananchi waache kudai haki zao kwa kutumia maandamano hayo, kwa sababu wanatumia muda mwingi wa uzalishaji mali kwenye mambo yasiyo na tija.
"Uchaguzi ulisha kwisha, sasa maandamano ya nini….watu wanaacha shughuli za kuzalisha mali na maendeleo kwa ujumla wanakwenda kwenye maandamano ambayo hayana tija yoyote, wananchi tusikubali kudanganywa," alisema.
Aidha, Waziri Maige aliwataka wananchi kuelekeza nguvu zao katika kutekeleza majukumu yao ya kifamilia, sanjari na kutekeleza miradi ya maendeleo hususani katika sekta za elimu na afya. Sekta ambazo zote zimekuwa zikilaumiwa kutokana na kuwa na matatizo mbalimbali yasiyokidhi haja za wananchi. Maige ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Msalala, hata hivyo alishindwa kutetea hoja yake ya kuwataka wananchi wasiandamane kutokana na ugumu wa maisha badala yake akijikuta akitambua bayana juu ya changamoto zinazolikabili jimbo hilo katika kujiletea maendeleo. Wakati huo huo alichangia mifuko ya saruji zaidi ya 4,000 kwa ajili ya ujenzi wa zahanati, ambapo kila kijiji alikipatia jumla ya mifuko 20, na kuwataka wananchi kuwa mstari wa mbele katika ujenzi wa zahanati katika vijiji vyao.