CHADEMA yamshitaki Mkuchika kwa AG

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,885
6,885
Mkuchika(17).jpg

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu,
Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), George Mkuchika


Chadema wamfikisha Mkuchika kwa AG

Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimemwandikia barua Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) kumtaka atoe ufafanuzi wa kisheria kuhusu uamuzi wa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), George Mkuchika, wa kuruhusu madiwani watano, kuendelea na nyadhifa zao, kuhudhuria vikao vya halmashauri na kulipwa posho, licha ya kuvuliwa uanachama na chama hicho.

Mkuchika alitoa maamuzi hayo kupitia barua yenye kumbukumbu namba HA.23/235/01/06 aliyomwandikia Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Estomih Chang’ah ya Agosti 23, mwaka huu, akiwaruhusu kuendelea na vikao vya halmashauri hiyo hadi hapo mahakama itakapotoa uamuzi juu ya kufukuzwa kwao uanachama.

Akizungumza na NIPASHE jana, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alisema wanataka ufafanuzi huo kutoka kwa AG kwa vile wanaamini maamuzi yaliyofikiwa na Mkuchika ni kinyume cha sheria. “Tumemwandikia Mwanasheria Mkuu wa Serikali atoe ufafanuzi wa kina wa kinachofanyika ndani ya serikali yake, kama hiyo ni misingi ya sheria, au atoe ushauri wa kisheria kurekebisha udhaifu uliojitokeza,” alisema Mbowe. Alisema madiwani waliofukuzwa katika chama, kamwe hawawezi kuhudhuria vikao vya halmashauri, kwani hawana sifa hiyo.

Mbowe alisema wananchi wa Jiji la Arusha hawatakuwa tayari kuwaruhusu ‘madiwani’ hao kuhudhuria vikao hivyo, badala yake watawazuia. Alisema watu waliowachochea na kuwadanganya ‘madiwani’ hao kukisusia chama chao kwa sababu ya kufukuzwa, walishawaahidi kuwa wangewalinda. Hata hivyo, alisema hawawezi kuwalinda bila kufuata sheria.

IPPMedia
 
Nduguzanguni chadema hapo haki aitatendeka ni kama ( kesi ya ngedere upeleke kwa nyani) shitakini kwa wananchi wa Arusha peoples poweeeer
 
Nduguzanguni chadema hapo haki aitatendeka ni kama ( kesi ya ngedere upeleke kwa nyani) shitakini kwa wananchi wa Arusha peoples poweeeer

Pamoja na haki kutotendeka, cha msingi hatua waliyochukua ni nzuri ili tuendelee na hii video ya viongozi wa Kikwete kugongana kikauli, tumsikie na mwanasheria wa Serikali anatuambia nini kwa mtazamo wake. Hapo tutaweza kugundua pia kauli zao watoka kwa aliyewaweka madarakani au ni zao binafsi.
 
  • Thanks
Reactions: FJM
walidanganywa kuwa watalindwa.. nani atawalinda .. bila kufuata misingi ya sheria? serikali inataka kupindisha sheria?
 
Majibu ya AG yataibua ukweli au uongo wa umakini wake ukizingatia Werema ni mmoja wa waudhuriaji wa semina elekezi iliyotolewa na J.K kwa mawaziri.

Umenikumbusha kitu, kwani yanayojilia sasa tusishangae sana ni matokeo ya semina elekezi ambayo hata mwanasheria wa serikali na Jaji Mkuu walikkuwa wajumbe wa semina hiyo.
 
Sisi huku Arusha tunasubiri hatima ya kamati iliyo chini ya msajili wa vyama. Na ameshasema kwamba Mkuchika kavunja sheria. Huo upuuzi wa Mkuchika kuingilia maamuzi ya vyama vingine hatuwezi kuuvumilia. Tutamwonyesha kwamba hao madiwani tumeshawakataa na hakuna wa kutulazimisha tuendelee nao. Ufisadi wa kuendelea kula posho na kutuwakilisha wakati tumewakataa utamfanya aje kujuta!
 
Sisi huku Arusha tunasubiri hatima ya kamati iliyo chini ya msajili wa vyama. Na ameshasema kwamba Mkuchika kavunja sheria. Huo upuuzi wa Mkuchika kuingilia maamuzi ya vyama vingine hatuwezi kuuvumilia. Tutamwonyesha kwamba hao madiwani tumeshawakataa na hakuna wa kutulazimisha tuendelee nao. Ufisadi wa kuendelea kula posho na kutuwakilisha wakati tumewakataa utamfanya aje kujuta!
well said!
 
Sijawahi ona serikali legelege kama hii na isiyoona mbali, najua ingekuwa serikali makini tatizo la umeya wa Arusha lingekuwa limeisha.
 
Chondechonde CCM mnataka kuichafua nchi yetu.Nyie ndio chama tawala mnatakiwa kuilinda katiba ya nchi sasa kwanini mnaivunja?Sasa ngoja sisi huko Arusha tuandae maandamano mje kutuua tena, ila nawahakikishieni nyie CCM hao madiwani hawatahudhuria kikao chochote na mkilazimisha Arusha itawaka moto.Kama mnawataka itisheni uchaguzi wagombee kupitia chama chenu au muidhinishe sheria ya mgombea binafsi kabla ya uchaguzi mtakaoupanga hapa Arusha.Achani ujanjaujanja umepitwa na wakati,huo ndio ushauri wangu kwenu CCM na Serikali yenu.
 
Nduguzanguni chadema hapo haki aitatendeka ni kama ( kesi ya ngedere upeleke kwa nyani) shitakini kwa wananchi wa Arusha peoples poweeeer
<br />
<br />Unasema ukweli mkuu,tujaribu kukumbuka yaliyojili kwenye mkutano wa nne wa bunge!Werema huyu huyu alimtukana Lisu,kuwa anaongea ili aonekane kwenye tv,ili ilikuwa ni hali ya kiitikadi zaidi!lakini pia alibaliki hoja ya kuhamisha pesa za bajeti kutoka wizara ya Ujenzi kwenda uchukuzi bila kufata taratibu!baada ya wabunge wa chadema kuomba utaratibu ufatwe!Kwa ujumla huwa anapendelea serikali zaidi!
 
Dawa ya serekali legelege kama ya kikwete ni maandamano tu,wana arusha tusipoandamana hii serekali kiziwi haitatuelewa tunachotaka! Wataendelea na maamuzi yanayokizina kila kukicha, AG ana jipya.
 
Dawa ya serekali legelege kama ya kikwete ni maandamano tu,wana arusha tusipoandamana hii serekali kiziwi haitatuelewa tunachotaka! Wataendelea na maamuzi yanayokizina kila kukicha, AG ana jipya.
 
Hivi AG ni nani vile? CDM inahaha tu, waende wakaandamane tuone tena sinema ya Arusha.
 
Kweli Kiwete hana Mawaziri kabsaaa!

Hivi hii Miwaziri ya Kiwete aliitoa wapi hasa na mingi ni mijizee na imechoka ile mbaya. Mijiwaziri inaongea kana kwamba ina mtindio wa ubongo!Mkuchika jinga kabisa,ina maana Waziri mzima hajui KATIBA YA NCHI? Hawa MADIWANI waliotimuliwa uanachama toka CDM analazimisha waingie kwenye vikao KWA TIKETI NA SERA YA CHAMA GANI?

Baraza lote la Kiwete is just a bunch of Fools! Pinda anasema alisha kubaliana na viongozi waandamizi wa CDM wakae meza moja chini ya John Tendwa-Msajili wa Vyama vya Siasa ili wamaliza mgogoro wa Umeya Jiji la Arusha,na Tendwa alishakubali kuwa arbitrator between CDM and CCM.

Hapa anatokea kibabu mmoja aliyechoka kufikiri anasema Madiwani waliofukuzwa na CDM waendelee na udiwani mpaka kesi yao ya msingi waliyofungua Mahakamani itolewe hukumu. Yaani mpaka hapo Waziri mzima anakuwa HAJAONA KUWA AMEEINGILIA UHURU WA MAHAKAMA!!!

Kama Mkuchika anaona hao Madiwani 5 wana akili zinazofanana na Wana Magamba BASI ANGELIITISHA UCHAGUZI haraka iwezekanavyo ili wagombee kwa tiketi ya Chama Cha Magamba-CCM NA AHAKIKISHE WANASHINDA kwa maslahi ya chama chake au la BASI AFUATILIE KESI YA MTIKILA MAHAKAMA KUU YA MGOMEA BINAFSI ILI HAWA MADIWANI wa Mkuchika wawanie kama Wagombea binasfi,
 
hivi AG anayepindisha sheria kila cku na kutuambia hakuna haja ya katiba mpya ataweza mamba ya arusha?
 
Kwa kuwa kamanda yupo Arusha tutapata taarifa na maelekezo zaidi ya nini cha kufanya
 
Dawa ya serekali legelege kama ya kikwete ni maandamano tu,wana arusha tusipoandamana hii serekali kiziwi haitatuelewa tunachotaka! Wataendelea na maamuzi yanayokizina kila kukicha, AG ana jipya.

Mkuchika amepotoka hata kama AG atapindisha ukweli kwani Msajili Tendwa keshasema sheria imekiukwa. Mbona CCM wakiwafukuzaga wanachama wao hatupambani kuwarudisha? Wanajidai kuwapigania akina Mallah kwa maslahi ya nani?. Hapa inatakiwa akina Mallah kuwapigia wakazi wa Arusha magoti watubu na kuonyesha remorse na siyo kuomba support kutoka Magamba waliowatukana tu Octoba mwaka 2010.
 
Mkuchika amepotoka hata kama AG atapindisha ukweli kwani Msajili Tendwa keshasema sheria imekiukwa. Mbona CCM wakiwafukuzaga wanachama wao hatupambani kuwarudisha? Wanajidai kuwapigania akina Mallah kwa maslahi ya nani?. Hapa inatakiwa akina Mallah kuwapigia wakazi wa Arusha magoti watubu na kuonyesha remorse na siyo kuomba support kutoka Magamba waliowatukana tu Octoba mwaka 2010.

Ukisikia kinogaubaga tokana na mkoroga uliokolea ndo isue hii.

  • Mkuchika awakumbatia Madiwani kinyume cha sheria
  • Chadema wanamshtaki kwa Mwanasheria wa Serikali
  • Mahakama hata haijaanza kusikiliza kesi mkuchika kishatoa hukumu dhidi ya Chadema
  • Pinda alipindisha kauli bungeni dhidi ya maongezi yake na Chadema juu ya suluhisho la Arusha
  • Msajili wa vyama vya siasa atoa kauli ya kupingana na Mkuchika na kwamba katiba imekiukwa
  • Msajili wa Vyama vya siasa kushughulikia usuluhishi wa mgogoro wa Arusha.
Tukiangalia yote hayo ni vurugu mechi ya nguo kuchanika
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom