samirnasri
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 1,388
- 213
Kuna taarifa kuwa watumishi walioajiri katika ofisi za halmashauri ya jiji la mwanza wamekuwa katika wakati mgumu tangu chadema waanze kuiongoza halmashauri hiyo ambayo ni miongoni mwa halmashauri zinazokusanya mapato mengi zaidi hapa nchini. Watumishi hao wamekuwa katika wakati mgumu baada ya baraza la madiwani linaloongozwa na chadema kudaiwa kufuta malupulupu mbalimbali waliyokuwa wakijigawia watumishi hao wakiongozwa na mkurugenzi wa jiji. Taarifa zinazohitaji uchunguzi zaidi zinasema kuwa hapo nyuma watumishi wa halmashauri walikuwa wakipigana vikumbo hadi siku za jumamosi na jumapili kwenda ofisini kufanya kazi huku wakiambulia malupulupu yanayokadiriwa kufikia sh. Laki mbili na nusu za kitanzania kila mwisho wa wiki pamoja na malipo ya overtime. Baada ya chadema kuongoza halmashauri inasemekana malipo ya overtime yamefutwa pamoja na yale malupulupu ya kila mwisho wa wiki. Tangu uamuzi huo uchukuliwe watumishi wengi wamekua wakitoka ofisini sa tisa na wamekuwa wakionekana mara chache sana siku za jumamosi na jumapili. Taarifa zinazidi kusema kuwa kuna watumishi sasa wanatamani kuuza magari yao kwa kuwa pesa za kuyagharamikia zimekuwa ngumu. Chanzo: kutoka halmashauri ya jiji-mwanza.