nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
JUMATATU, JUNI 25, 2012 05:16
NA BENJAMIN MASESE, DAR ES SALAAM
Na Gazeti la MTANZANIA
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimewataka viongozi wa Serikali na Jeshi la Polisi nchini, kuwatambua wajumbe wa nyumba 10 wa chama hicho cha upinzani, kwa kuwa nao ni viongozi halali.
Pia kimesema kuwa, kitendo cha wajumbe hao kubaguliwa, hakiwezi kukubaliwa kwa kuwa wamechaguliwa kwa mujibu wa sheria.
Akizungumza na wandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Uchaguzi CHADEMA, Msafiri Mtemelwa, alisema hivi sasa kuna mvurugano mkubwa wa kiutawala ndani ya jamii kuhusu wajumbe wa nyumba 10.
"Sisi zamani hatukuwa na wajumbe wa nyumba 10, lakini baada ya kuona hatuwezi kuchukua nchi bila kuwa na mizizi hadi chini, tumeweka viongozi hao na wanatambuliwa kisheria.
"Pamoja na kwamba wanatambulika, jambo la ajabu ni kwamba, mtu akipata shida na kuwenda kwa mjumbe wa nyumba 10 wa Chadema kisha akapeleka barua hiyo kituo chochote cha polisi, hatapokelewa.
"Lakini mtu huyo huyo akienda kituo cha polisi na barua ya mjumbe wa nyumba 10 wa CCM, anasikilizwa vizuri na kupewa kila aina ya msaada anaotaka.
"Sasa tunahoji kwa nini mjumbe wa Chadema asitambuliwe na mjumbe wa CCM atambuliwe wakati wote hao ni wawakilishi wa vyama vya siasa?
"Huu ni ubaguzi wa hali ya juu na hatuwezi kuukubali, bila shaka hii ni mbinu ya CCM kutaka kuendelea kuwalazimisha wananchi kwamba mabalozi wa CCM, ndio wenye uhalali wanaotambulika katika maeneo husika.
"Kwa kifupi hatuwezi kukubali hali hii, wajumbe wetu wa nyumba 10 wapo kisheria na wanatambuliwa kama ilivyo kwa wajumbe wa CCM," alisema Mtemelwa.
Mtemelwa alisema kuwa, tangu Juni mosi mwaka huu, Chadema ilipoanza kuwaweka mabalozi katika maeneo mbalimbali nchini na kufanya kazi kama mabalozi wa CCM, baadhi ya wananchi wamekuwa wakikosa huduma pale wanapofika katika vituo vya polisi, ofisi za mtendaji wa kata na sehemu nyingine za Serikali, wakiwa na barua zilizotolewa na viongozi hao.
Kutokana na hali hiyo, alitoa wito kwa viongozi wasiowatambua wajumbe wa nyumba 10 wa Chadema, kutoendelea na tabia hiyo vinginevyo watachukuliwa hatua za kisheria.
NA BENJAMIN MASESE, DAR ES SALAAM
Na Gazeti la MTANZANIA
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimewataka viongozi wa Serikali na Jeshi la Polisi nchini, kuwatambua wajumbe wa nyumba 10 wa chama hicho cha upinzani, kwa kuwa nao ni viongozi halali.
Pia kimesema kuwa, kitendo cha wajumbe hao kubaguliwa, hakiwezi kukubaliwa kwa kuwa wamechaguliwa kwa mujibu wa sheria.
Akizungumza na wandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Uchaguzi CHADEMA, Msafiri Mtemelwa, alisema hivi sasa kuna mvurugano mkubwa wa kiutawala ndani ya jamii kuhusu wajumbe wa nyumba 10.
"Sisi zamani hatukuwa na wajumbe wa nyumba 10, lakini baada ya kuona hatuwezi kuchukua nchi bila kuwa na mizizi hadi chini, tumeweka viongozi hao na wanatambuliwa kisheria.
"Pamoja na kwamba wanatambulika, jambo la ajabu ni kwamba, mtu akipata shida na kuwenda kwa mjumbe wa nyumba 10 wa Chadema kisha akapeleka barua hiyo kituo chochote cha polisi, hatapokelewa.
"Lakini mtu huyo huyo akienda kituo cha polisi na barua ya mjumbe wa nyumba 10 wa CCM, anasikilizwa vizuri na kupewa kila aina ya msaada anaotaka.
"Sasa tunahoji kwa nini mjumbe wa Chadema asitambuliwe na mjumbe wa CCM atambuliwe wakati wote hao ni wawakilishi wa vyama vya siasa?
"Huu ni ubaguzi wa hali ya juu na hatuwezi kuukubali, bila shaka hii ni mbinu ya CCM kutaka kuendelea kuwalazimisha wananchi kwamba mabalozi wa CCM, ndio wenye uhalali wanaotambulika katika maeneo husika.
"Kwa kifupi hatuwezi kukubali hali hii, wajumbe wetu wa nyumba 10 wapo kisheria na wanatambuliwa kama ilivyo kwa wajumbe wa CCM," alisema Mtemelwa.
Mtemelwa alisema kuwa, tangu Juni mosi mwaka huu, Chadema ilipoanza kuwaweka mabalozi katika maeneo mbalimbali nchini na kufanya kazi kama mabalozi wa CCM, baadhi ya wananchi wamekuwa wakikosa huduma pale wanapofika katika vituo vya polisi, ofisi za mtendaji wa kata na sehemu nyingine za Serikali, wakiwa na barua zilizotolewa na viongozi hao.
Kutokana na hali hiyo, alitoa wito kwa viongozi wasiowatambua wajumbe wa nyumba 10 wa Chadema, kutoendelea na tabia hiyo vinginevyo watachukuliwa hatua za kisheria.