Chama cha Demokrasia na Maendeleo-CHADEMA kimevunjavunja ngome ya CCM wilaya ya Ngorongoro ambapo wanachama 800 wa CCM walijitoa katika chama hicho na kujiunga na CDM.
Tukio hilo kubwa lilitokea juzi baada ya Mbunge wa Karatu Mchungaji Israel Natse kufanya mkutano mkubwa wa hadhara wilayani hapo na kutoa somo kubwa la uraia kwa wananchi wa wilaya hiyo.
Akikabidhi kadi mpya kwa wanachama hao Mchungaji Natse aliwataka wakazi hao kuwa mabalozi wa CHADEMA katika maeneo ya vijijini wanakotoka na kuwaambia sasa hivi hakuna kulala mpaka CHADEMA itakapokamata dola mwaka 2015.
Baadhi ya wanachama wa CHADEMA walimweleza Mchungaji Natse kuwa wamekuwa wakipata vitisho kutoka kwa viongozi wa serikali wilayani hapo wakilaaniwa kwa uamuzi wao wa kuipinga CCM.
Hata hivyo wanachama hao wameahidi kupambana mpaka tone la mwisho.
Source: Mwananchi Alhamisi Uk 16
Tukio hilo kubwa lilitokea juzi baada ya Mbunge wa Karatu Mchungaji Israel Natse kufanya mkutano mkubwa wa hadhara wilayani hapo na kutoa somo kubwa la uraia kwa wananchi wa wilaya hiyo.
Akikabidhi kadi mpya kwa wanachama hao Mchungaji Natse aliwataka wakazi hao kuwa mabalozi wa CHADEMA katika maeneo ya vijijini wanakotoka na kuwaambia sasa hivi hakuna kulala mpaka CHADEMA itakapokamata dola mwaka 2015.
Baadhi ya wanachama wa CHADEMA walimweleza Mchungaji Natse kuwa wamekuwa wakipata vitisho kutoka kwa viongozi wa serikali wilayani hapo wakilaaniwa kwa uamuzi wao wa kuipinga CCM.
Hata hivyo wanachama hao wameahidi kupambana mpaka tone la mwisho.
Source: Mwananchi Alhamisi Uk 16