Rejao
JF-Expert Member
- May 4, 2010
- 9,220
- 4,056
Rejao mkuu mawazo ya kimburukenge haya yaliyo jaa ubaguzi mbona yanakupumbaza sana .Leo unatamka Iringa unasahau Mara , Mwanza , Dar ,Singida, Shinyanga nk wewe umekalia ndoto au huamini kwamba watanzania wamesha amka
Mkuu umesahau Kigoma, mwanza, mara na simiyu pamoja na katavi.
Mpka pua itadondoka yenyewe. Suburi tu.
wewe tunakujua sana kuwa umewekwa na Nape humu ili kulinda ugali wenu.
Lengo kuu la cdm siyo kuangalia kilichofanywa na mzee wa lubambagwe.bali ni kuing'oa ccm madarakani ambayo imeoza na viongozi wake wengi wameoza ambao wanawafanya hata wale waadilifu wachache wasifanye kazi inavyotakiwa.sasa km makufuli atakuwa bado yuko ndani ya ccm sidhani km atasalimika.
ongeza na haya,
kanda ya ziwa
nyanda za juu kusini na
central zone
USIFICHE UKWELI KUHUSU COVERAGE YA CHADEMA ,KUWA MZALENDO ,KUWA MWANAMAPINDUZI.
Kikuumacho nini? Ndondo si chululu kwani wahenga walinena haba na haba hujaza kibaba.
Nadhani umeanza kuuamini uongo mliojitungia wenyewe kuhusu CHADEMA. Keep on dreaming, ya Arumeru ni cha mtoto (na kumbuka mlichosema huko).
Ushabiki wa kishenzi sana, kwa hiyo shinyanga, mwanza, Singida, Katavi, Rukwa, Dar huko kote ni ccm? ccm wamekupa nini rejeo? Au kwa sababu tu hamtungi mimba? tungeshajua nape anachowapa, bila shaka ni zaidi ya pesa? Mnatia kichefu chefu kweli.
​uuwi una ndoto za mchana mbona mapovu yanawatoka mkiwaona chadema si wanakurukupa?
haya mama Salma umesikika
So kumbe siku hizi sio wa Kaskazini? Au nimesikia vibaya?
Hata huko ulikotaja ilianza kidogo kidogo baadaye ikiwa kama ilivyo sasa, CDM walibip kwenye chaguzi za vijiji sasa wameanza kupiga CHATO
hapo nilipo bold kumbe panawauma? sasa mimi nakwambia Segerea,Iramba Magharibi,mtera,Kinondoni,Kibaha,Bumbuli ....... hapo lazima mnapoteza tuombe uzima ili 2015 nije nikukumbushe haya, halafu unasema kwamba na baadhi ya majimbo mliweka watu wasio Comptent mwaka 2010 hebu nitajie japo wbunge kumi tu ambao wapo comptent kwa sasa ndani ya CCM maana 2015 ngoma kwenu itakua ngumu maana hakuna zile propaganda mlizozoea amepita bila kupigwa
hivi hiyo avator ndiyo sura yako ilivyo?mbona mbaya hivi?kama shetani vile!:flypig:
Kila ukiandika uongo pua inazidi kuwa ndefu.
Hivi hamjishtukii kukipigania CDM, chama cha watu wachache chenye mrengo wa kigaidi, kidini, kikabila na kikanda?
Nawashangaa mpaka mnaweza kumention majimbo yenu yote hapa, imagine na mimi nianze kumention majimbo CCM iliyoshinda na inayotarajia kuyarudisha mikononi mwake, hapa JF patatosha?
Jifunzeni kutetea kinachoweza kutetewa...Losers!!!