palalisote
JF-Expert Member
- Aug 4, 2010
- 8,335
- 1,455
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimekiliza tena Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kuibomoa tena ngome yake baada ya kuwachomoa wanachama takriban 400, akiwamo Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana (UVCCM) Kata ya Enduleni, Cosmas Lakani.
Lakani ambaye ni mmoja wa viongozi machachari na aliyekuwa tegemeo kubwa la umoja huo katika Wilaya ya Ngorongoro, alihama na wanachama 394 kutoka kata za Ngorongoro na Enduleni juzi na kufanya idadi ya Wana CCM waliojiunga na CHADEMA ndani ya miezi miwili kufikia 3,481.
"CCM imetunyonya mpaka mwisho, walisema tuache kilimo cha kujikimu watatupa chakula, lakini wanatupa chakula kidogo, wanaona mnyama anathamani kubwa kuliko sisi tunaoishi Ngorongoro. Ndiyo maana tunawaacha na CCM yao tumekuja CHADEMA itusaidie tukadai haki yetu," alisema Ndaito Sabore.
Kada mwingine apasua vichwa viongozi wake huko Moshi, viongozi wa CCM wa Wilaya ya Moshi Vijijini, wanaumiza vichwa kujaribu kumzuia kwa kila mbinu kada wake maarufu, Ansi Mmasi, anayetajwa kuwa katika harakati za kukihama chama hicho na kujiunga na CHADEMA.
Mmasi ambaye amekuwa mpinzani mkubwa wa mbunge wa sasa wa Jimbo la Moshi Vijijini, Dk. Cyril Chami, anatajwa kuwa miongoni mwa vigogo wa CCM ambao wanatazamiwa kukihama chama hicho, ili kuwania nafasi hiyo katika uchaguzi mkuu ujao mwaka 2015.
Hata hivyo, Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Moshi Vijijini, Gabriel Masenga, alidai kuwa hajapata taarifa rasmi kutoka kwa Mmasi kama anataka kuhama, lakini akakiri kusikia fununu hizo kupitia vyombo vya habari.
Habari zaidi soma "CHADEMA yailiza tena CCM Arusha"
Lakani ambaye ni mmoja wa viongozi machachari na aliyekuwa tegemeo kubwa la umoja huo katika Wilaya ya Ngorongoro, alihama na wanachama 394 kutoka kata za Ngorongoro na Enduleni juzi na kufanya idadi ya Wana CCM waliojiunga na CHADEMA ndani ya miezi miwili kufikia 3,481.
"CCM imetunyonya mpaka mwisho, walisema tuache kilimo cha kujikimu watatupa chakula, lakini wanatupa chakula kidogo, wanaona mnyama anathamani kubwa kuliko sisi tunaoishi Ngorongoro. Ndiyo maana tunawaacha na CCM yao tumekuja CHADEMA itusaidie tukadai haki yetu," alisema Ndaito Sabore.
Kada mwingine apasua vichwa viongozi wake huko Moshi, viongozi wa CCM wa Wilaya ya Moshi Vijijini, wanaumiza vichwa kujaribu kumzuia kwa kila mbinu kada wake maarufu, Ansi Mmasi, anayetajwa kuwa katika harakati za kukihama chama hicho na kujiunga na CHADEMA.
Mmasi ambaye amekuwa mpinzani mkubwa wa mbunge wa sasa wa Jimbo la Moshi Vijijini, Dk. Cyril Chami, anatajwa kuwa miongoni mwa vigogo wa CCM ambao wanatazamiwa kukihama chama hicho, ili kuwania nafasi hiyo katika uchaguzi mkuu ujao mwaka 2015.
Hata hivyo, Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Moshi Vijijini, Gabriel Masenga, alidai kuwa hajapata taarifa rasmi kutoka kwa Mmasi kama anataka kuhama, lakini akakiri kusikia fununu hizo kupitia vyombo vya habari.
Habari zaidi soma "CHADEMA yailiza tena CCM Arusha"